Sunday, June 07, 2015
Friday, June 05, 2015
IDADI YA WALIOFARIKI GHANA YAFIKIA 175
Takriban
watu 175 wamefariki kufiakia sasa kufuatia moto uliotokea katika kituo
kimoja cha mafuta katika mji mkuu wa Ghana Accra.
Moto huo
uliozuka siku ya jumatano usiku ulianza wakati wakaazi wa mji huo
walipokuwa wakikabiliana na siku mbili za mvua kubwa ambayo imewaacha
raia wengi bila makaazi pamoja na stima.
Mafuriko hayo yaliathiri juhudi za uokozi na huenda yalisababisha moto kulingana na mwandishi wa BBC Sammy Darko mjini Accra. Tayari Ghana imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kufuatia vifo hivyo.
Mlipuko huo ulitokea hapo jana
wakati mamia ya watu walipokuwa wamejihifadhi katika kituo hicho cha
mafuta kutokana na mvua kubwa zinazonyesha. Rais wa Ghana, John Mahama amesema janga hilo halitajirudia tena.
RAHEEM STRLING KUELEKEA OLD TRAFFORD
Mshambuliaji
wa Liverpool Raheem Sterling huenda akaelekea katika kilabu ya
Manchester United ,hatahivyo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 ana
wasiwasi kuhusu athari za uhamisho huo hususan kutokana na ushindani
mkali uliopo kati ya klabu hizo mbili.
Sterling amekataa ombi la kitita cha pauni laki moja kutoka kwa Liverpool akisema kuwa anataka kuondoka na kukichezea kilabu ambacho kina uwezo wa kushinda mataji. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.
SERENA ATINGA FAINALI FRENCH OPEN 2015
Serena
Williams amefanikiwa kutinga fainali za michuano ya tenis ya French
Open. Licha ya kujisikia kuumwa Serena aliweza kupambana vikali na
kumbwaga mpinzani wake Timea Bacsinszky kwa seti 4-6 6-3 6-0 na kufuzu
kucheza fainali za mwaka huu.
Serena nambari moja duniani kwa wanawake sasa atapambana na Lucie Safarova katika mchezo wa fainali kesho, Jumamosi. Serena amekuwa akiumwa kipindi chote cha michuano hiyo, kiasi kwamba anasema hakutarajia kushinda katika mchezo huo.
Serena anajaribu kushindi taji la tatu la michuano hiyo ya French Open na taji la ishirini la michuano mikubwa. Mapema
katika uwanja wa Philippe Chatrier, Safarova wa 13 kwa ubora alimtupa
nje MSerbia Ana Ivanovic na kuwa mwanamke wa kwanza wa Czech kufika
fainali za michuano hiyo katika uwanja wa Roland Garros katika kipindi
cha miaka 34.
Kwa upande wa Wanaume, fainali zitafanyika Jumapili hii. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.
Tuesday, June 02, 2015
AL-SHABAAB WADAIWA KUVITEKA VIJIJI KENYA
Hofu
kubwa imetanda Kaskazini mwa nchi ya Kenya,baada ya kuwepo kwa taarifa
kwamba kundi la wapiganaji wa Al shabaab Limeviteka vijiji kadhaa katika
mpaka wa Kenya na somalia.
Mamia ya wakaazi wameyatoroka makaazi yao kufuatia taarifa za kuwepo kwa wapiganaji wa Alshabaab wapatao thelathini.
Shule nne zinaripotiwa kufungwa.
Naibu
kamishna wa kaunti ya Mandera amenukuliwa akisema kwamba wamepokea
ripoti za kuwepo kwa wapiganaji hao na watawaandama na kulidhibiti eneo
hilo. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.
MLIPUKO WA BOMU WAUA WATU 20 NIGERIA
Takriban watu 20 wamefariki kutokana na mlipuko wa bomu katika mji wa kaskazini mashariki wa Maiduguri nchini Nigeria.
Mji huo ulikuwa umeshambuliwa saa za alfajiri siku ya jumanne na washukiwa wa kundi la Boko haram .
Saa
chache baadaye ,mlipuaji wa kujitolea muhanga alijilipua katika soko la
kuuza ngombe la Gamboru ndani ya mji huo kulingana na walioshuhudia.
Wakati
wa kuapishwa kwake rais mpya wa Nigeria Muhammadu Buhari alisema kuwa
anayahamisha makao makuu ya kijeshi katika vita dhidi ya wapiganaji hao
kutoka mji mkuu wa Abuja hadi Maiduguri. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.
Thursday, May 28, 2015
MWANASHERIA KENYA AJITOSA KUMUOA MTOTO WA OBAMA...!!!
Mwanasheria kijana nchini ametuma ombi la kumuoa mtoto wa Rais Barack Obama anayeitwa Malia.
Mwanasheria Felix Kiprono alisema jana kwamba yupo
tayari kutoa ng’ombe 50, kondoo 70 na mbuzi 30 ikiwa ni mahari ya
kumposa mtoto huyo.
Alisema kuwa analazimika kufanya hivyo ili kutimiza ndoto yake ya muda mrefu ya kumuoa mtoto wa Rais Obama.
“Nimevutiwa kumchumbia Malia tangu mwaka 2008,” alisema Kiprono baada ya kuhojiwa na gazeti la The Nairobian. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.
ODAMA: NAOGOPA MSAADA WA MASHARTI...!!!
MWIGIZAJI mwenye mvuto katika filamu za Bongo, Jennifer Kyaka ‘Odama’,
amesema anaogopa marafiki wa kiume kwa kuwa huwa na masharti magumu
pindi wanapotoa msaada.
“Wasanii wa kiume kwangu sipendi kwa kuwa huwa na masharti kuliko marafiki wa kike ambao husaidia bila masharti ya ajabu,” alisema.
Aliongeza kwamba, marafiki wa kike anakuwa huru kuwaeleza shida na matatizo yake kuliko wa kiume ndiyo maana hiyo ni sababu yake nyingine ya kutopenda marafiki wa kiume kama anavyopenda marafiki wa kike. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.
“Wasanii wa kiume kwangu sipendi kwa kuwa huwa na masharti kuliko marafiki wa kike ambao husaidia bila masharti ya ajabu,” alisema.
Aliongeza kwamba, marafiki wa kike anakuwa huru kuwaeleza shida na matatizo yake kuliko wa kiume ndiyo maana hiyo ni sababu yake nyingine ya kutopenda marafiki wa kiume kama anavyopenda marafiki wa kike. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.
"NATAKA KUWA MCHEKESHAJI" INSPEKTA HAROON
UNALIKUMBUKA kundi la Gangwe Mobb, hapo lazima utamtaja Haruna Kaena
‘Insepkta Haroun’ na Luten Kalama, wawili hao baada ya kutengana kila
mmoja akawa anafanya kazi binafsi lakini sasa Inspekta Haroun ameibuka
na kudai kwamba anataka kuwa mwigizaji wa vichekesho.
Inspekta Haroun aliyetamba na wimbo wa ‘Mtoto wa Geti Kali’ aliendelea kueleza kwamba fani anazozipenda ni muziki na kuigiza vichekesho.
“Mimi msanii hivyo natakiwa niwe mbunifu, nisibweteke na kazi, fani moja na kwa sasa napenda kuwa mwigizaji wa vichekesho kwa kuwa napenda kazi hiyo na ninaiweza,” alijinadi.
Msanii huyo aliwahi kushirikishwa katika vipengele vya uigizaji katika kipindi cha vichekesho kilichokuwa kikirushwa na televisheni ya Clouds. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.
Inspekta Haroun aliyetamba na wimbo wa ‘Mtoto wa Geti Kali’ aliendelea kueleza kwamba fani anazozipenda ni muziki na kuigiza vichekesho.
“Mimi msanii hivyo natakiwa niwe mbunifu, nisibweteke na kazi, fani moja na kwa sasa napenda kuwa mwigizaji wa vichekesho kwa kuwa napenda kazi hiyo na ninaiweza,” alijinadi.
Msanii huyo aliwahi kushirikishwa katika vipengele vya uigizaji katika kipindi cha vichekesho kilichokuwa kikirushwa na televisheni ya Clouds. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.
WABUNGE WAMKAANGA MAGUFULI
Waziri wa Ujenzi, Dk John Pombe Magufuli amekuwa hapati wakati mgumu anapowasilisha bajeti ya wizara hiyo, lakini hali ilikuwa tofauti jana wakati wabunge walipoungana kueleza hofu yao katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa barabara kutokana na madeni ya makandarasi.
Wabunge hao walidiriki kueleza kuwa kuna ufisadi
katika ununuzi wa kivuko cha Bagamoyo na wengine kueleza kuwa miradi
iliyotajwa kwenye hotuba ya bajeti ilishatekelezwa miaka ya 80 na 90.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kamati ya Miundombinu
kuhusu bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2015/2016 iliyosomwa na
Makamu Mwenyekiti, Profesa Juma Kapuya, deni linalodaiwa na makandarasi
ni kati ya Sh850 bilioni na Sh900 bilioni.
“Kamati haijaridhishwa kabisa na hali hii kwani
deni hili sasa ni kubwa kuzidi hata bajeti inayotengwa kwa ajili ya
miradi ya maendeleo ya wizara hii, jambo ambalo linafanya bajeti hii
kuonekana ni kiini macho tu,” alisema Profesa Kapuya.
Kambi ya Upinzani
Katika taarifa yake, Kambi ya Upinzani Bungeni
(KUB) ilimshutumu Waziri Magufuli kwa kuandika hotuba ndefu ili
kuwachanganya wabunge, huku hotuba hizo zikitaja hata miradi ya barabara
zilizojengwa miaka ya 80 na 90.
Friday, May 22, 2015
UCHAGUZI FIFA, WAWILI WAJITOA
Wagombea
wawili kati ya wanne waliojitokeza kuwania nafasi ya urais wa
shirikisho la vyama vya soka Duniani FIFA wamejitoka katika
kinyang'ang'anyiro hicho.
Nyota wa zamani wa soka huko Ureno ,
Luis Figo ambaye ni mmoja wa waliojitoa kuwania nafasi hiyo,amelalamikia
mfumo wa uendeshaji wa uchaguzi huo na kuiita kuwa ni wakinafiki.
Amesisitiza
kuwa kwa mtazamo wake anaona kuwa taratibu zilizowekwa zililenga
kumnufaisha mgombea mmoja tu na si kuelta usawa wa wote waliojitokeza
kuwania nafasi hiyo,ambapo inaonekana kuwa ni mpango uliowekwa kumpatia
nafasi ya ushindi Rais wa sasa Sepp Blatter ambaye anawania nafasi hiyo
kwa kipindi cha tano.
Hata hivyo Rais wa chama cha soka huko
Uholanzi , Michael van Praag , akijitoa. Huku wapinzani waliosalia ni Bw
Blatter ambaye ni Jordan Prince Ali Al Hussein ambaye ni mwanachama wa
kamati ya utendaji ya FIFA.
Mgombea mwingine aliyejitoa pia ni
Rais wa chama cha soka cha Uholanzi Michael van Praag na hivyo kuwaacha
Blatter na mtu anayedaiwa kuwa mpinzani wake wa karibu Prince Ali Al
Hussein ambaye ni mjumbe wa kamati ya utendaji ya FIFA. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Wednesday, May 20, 2015
MICHUANO YA COSAFA YAANZA AFRIKA KUSINI
Michuano ya COSAFA,nchini Afrika Kusini Michuano ya kumi na tano ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu kusini mwa Afrika,COSAFA imezikutanisha timu za ukanda huo nchini Afrika Kusini. Michuano hiyo ilianza kutimua vumbi Jumapili mei 17 na itakamilika mei 30 .
Timu 12 kati ya 14 kutoka nchi wanachama wa COSAFA tayari zipo nchini Afrika Kusini kuchuana katika mashindano hayo.
Angola na Comoro ambazo ni wanachama wa COSAFA hazikuweza kushiriki mwaka huu.
Nafasi zao zimechukuliwa na Ghana iliyofikia fainali za michuano ya Caf ya mwaka huu na Tanzania kutoka ukanda wa Afrika mashariki na kati ikiwa mwanachama wa CECAFA.
Monday, May 18, 2015
NKURUNZIZA AWAFUKUZA KAZI MAWAZIRI WATATU
Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza .
Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza, amewafuta kazi mawaziri watatu, huku maandamano yakiendelea katika mji mkuu kufuatia jaribio la mapinduzi, juma lililopita.
Mawaziri walioachishwa kazi ni wa Ulinzi, mashauri ya nchi za kigeni na biashara.
Mapema hii leo, polisi walifyatua risasi hewani katika mji mkuu Bujumbura, kujaribu kuutawanya umati wa vijana uliokuwa ukifanya ghasia.
IS WAUTEKA MJI WA RAMADI
Wapiganaji wa Islamic State
Baada ya mapigano makali kwa siku kadhaa katika mji wa Ramadi nchini Iraq, hatimaye mji huo kwa sasa unashikiliwa na wapiganaji wa kundi la IS.
Makundi ya wanajeshi wa serikali wamekimbia kutoka katika eneo hilo na Islamic State wamejitangazia ushindi dhidi ya mji huo na kwamba wanaushikilia.
Mapema msemaji wa Gavana wa jimbo hilo amesema kuwa wapiganaji hao wanayashikilia baadhi ya majengo mhimu ya serikali katika jimbo hilo.
Hata hivyo umoja wa Mataifa umelaani hatua hiyo ya IS, ambapo pia Waziri Mkuu wa Iraq Haider al-Abadi amesema kuwa kwa sasa wanajipanga kwa kushirikiana na majeshi ya Shia ili kukabiliana na wapiganaji hao. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
MAN CITY YAICHAPA SWANSEA 4-2
Yaya Toure mshambuliaji wa Man City
Matokeo ya Mechi mbili za ligi kuu ya England zilizochezwa hapo jana,Manchester City iliwachabanga Swansea mabao 4-2 .
Ni Wilfried Bony ambaye mnamo dakika ya 90 lililopigilia msumali wa moto kwa Swansea baada ya kufunga bao la nne.
Lakini Yaya Toure yeye alizifumania nyavu mara mbili dakika 21 na 74. , James Milner naye akifunga mnamo dakika ya 36.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Huku katika mechi ya pili Arsenal wakitoa sare ya bao 1-1 dhidi ya Man united,ambapo kwa matokeo hayo sasa Arsenal wanaendelea kujiimarisha katika nafasi ya tatu. Leo West Brom watakipiga na Chelsea katika dimba la The Hawthons.
Sunday, May 17, 2015
'SI IKULU ILIYOWASAFISHA MAWAZIRI' PINDA
Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda amewajibu wabunge waliokosoa kitendo cha mawaziri watano waliotajwa kwenye kashfa za Operesheni Tokomeza na akaunti ya escrow, akisema Ikulu haikuhusika kuwasafisha bali ilitangaza matokeo ya uchunguzi wa tume.
Mtendaji huyo mkuu wa Serikali pia amesema mawaziri hao bado wanachunguzwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Jeshi la Polisi, kuhusu kuhusishwa kwao na operesheni hiyo iliyotekelezwa kwa kukiuka haki za binadamu, na sakata la escrow lililohusisha uchotwaji wa Sh306 bilioni zilizokuwa Benki Kuu.
Wakichangia hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu wiki iliyopita, baadhi ya wabunge walihoji kitendo cha Ikulu kuwasafisha mawaziri wachache na kuwaacha wengine waliojiuzulu kisiasa kutokana na wizara zao kukumbwa na kashfa na kumtaka Waziri Mkuu atoe majibu wakati akifanya majumuisho ya mjadala.
RAIA WAPYA WAKUTWA NA NYARA ZA SERIKALI...!!!
Kamanda wa Polisi mkoa wa Katavi.
POLISI mkoani Katavi imewakamata raia wapya watatu waliokuwa wakimbizi kutoka Burundi kwa kujihusisha na biashara haramu ya meno ya tembo.
Watu hao walikamatwa na nyara za Serikali zenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 1.2.
Nyara hizo za Serikali ni vipande vitatu vya meno ya tembo vikiwa sawa na jino moja la mnyama huyo vikiwa tayari kusafirishwa kwenda mjini Tabora.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi , Dhahiri Kidavashari amewataja watuhumiwa hao kuwa ni pamoja na Frank Hamis (18) , Steven Jonas (22) na Jackson Erasto ambao karibuni wamepewa uraia wa Tanzania.
Kidavashari alibainisha kuwa watuhumiwa hao walikutwa juzi saa 3:00 asubuhi katika chumba alichopanga mwanafunzi wa kidato cha Nne katika shule ya sekondari Katumba, Ernest John (19) katika eneo la Mnyasi kijijini Katumba wilayani Mlele.
“Mwanafunzi huyo ana uhusiano nao wa kindugu hivyo aliwakaribisha kulala chumbani kwake alimokuwa amepanga katika nyumba ambayo ni mali ya Felix Gado iliyopo eneo la Mnyasi kijijini Katumba.
GIZA NENE MAKADA URAIS CCM
Katibu mwenezi CCM Nape Nnauye.
Hali bado ni tete kwa makada sita waliofungiwa na CCM kujihusisha na masuala ya uchaguzi baada ya chama hicho tawala kueleza kuwa mchakato wa kuwachunguza haujakamilika na adhabu yao inaweza kuendelea hata baada ya vikao vya juu vitakavyofanyika mwishoni mwa wiki.
CCM pia imebadili tarehe za vikao vya Halmashauri Kuu na Kamati Kuu ambavyo awali vilipangwa kufanyika Mei 20, 21 na 22 na badala yake sasa vitafanyika Mei 22,23 na 24.
Akizungumza na waandishi wa habari jana kwenye ofisi za chama hicho jijini, Katibu Mwenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema hafahamu lini adhabu ya viongozi hao itakwisha kwani bado mchakato wa kuwachunguza haujafika mwisho.
Wednesday, May 13, 2015
RAIS NKURUNZIZA APINDULIWA...!!!
Meja Generali Niyombareh amesema wamechukua hatua hiyo baada ya watu
wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa
Nkurunziza.
Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi
februari anasema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani
mbali na sheria za kimataifa.
Jenerali Niyombareh alikuwa ameandamana na viongozi wengine wa jeshi la Burundi.
Tayari wanajeshi wameshika doria nje ya makao makuu ya runinga ya taifa.
JACQUELINE WOLPER: ANAETOKA NA NAY WA MITEGO AMESHAJULIKANA
Jacqueline Wolper
Muigizaji wa filamu zabkibongo, Jacqueline Wolper amewaweka njiapanda mashabiki wake kwa kaul yake kuwa msichana aliye katika uhusiano wa kimapenzi na msanii wa bongo flava Emmanuel Elibariki 'Nay wa Mitego' amekwishafahamika tofauti na alivyokuwa akihisiwa yeye.
"Watu hawana dogo, ukiwa na ukaribu na mtu unaambiwa ni mpenzi wako, Nay hakuwahi kuwa mpenzi wangu kwa kuwa ni zaidi ya rafiki kwangu, ila watu wasio waelewa ndiyo waliokuwa wakivumisha kuwa tuna uhusiano kwa maslahi yao, lakini sasa ukweli umejulikana kama mnavyoona na mnavyosikia Nay ni wa nani" alieleza Jacqueline bila kuweka wazi ni nani anatoka na mwana hip hop huyo.
Wolper aliongeza kuwa taarifa hizo ziliposanbaa alipata tabu ambapo alitumia muda mwingi kutolea maelezo kwa watu wake wa karibu.
BARCELONA YATINGA FAINALI
Messi, Suarez na Neymar wakishangilia bao
Miamba ya soka Hispania, Barcelona wamefanikiwa kutinga fainali baada ya kuibwaga Bayern Munich kwa jumla ya mabao 5-3 waliyokusanya katika mikondo yote miwili waliyokutana katika hatua ya nusu fainali.
Katika mchezo wa usiku wa kuamkia leo ambao ulipigwa katika dimba la Allinza Arena, Bayern walipaswa kushinda bao nne bila ili wapate tiketi ya kusonga mbele.
Lakini mpaka kipyenga kinapulizwa the Bavarian 3,Barcelona wakajipatia mabao mawili.
Leo usiku kutakuwa na mchezo kati ya Real Madrid dhidi ya Juventus katika dimba la Banabeu.
NGASSA ASAINI KUCHEZA AFRIKA KUSINI
Mrisho Ngassa
Mshambuliaji hodari wa timu ya Yanga, Mrisho Ngassa amemwaga wino wa kuichezea timu ya Free State Stars ya ligi kuu Afrika Kusini kwa miaka minne.
Ngassa ameripotiwa kufurahia mkataba huo mnono na kuanza maisha yake mapya baada ya kucheza nyumbani kwa miaka kadhaa.
"Nataka kuitumia fursa hii kutangaza soka la Tanzania na nitajituma ili kufanya vizuri zaidi" alisema mchezaji huyo.
Katika mitandao mbalimbali ya kijamii Ngassa ameonekana akiwa na kocha wa timu hiyo mara baada ya kusaini mkataba.
Friday, May 01, 2015
UKAWA WAKUNA VICHWA SAA 48
Mwenyekiti mwenza wa Ukawa, Freeman Mbowe akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari, Dar es Salaam jana. Wengine ni wenyeviti wenza, James Mbati, Profesa Ibrahim Lipumba na Dk Emmanuel Makaidi.
Saa 48
zilizotumika kikaoni kutafuta muafaka wa majimbo yenye utata ndani ya
umoja wa vyama vya upinzani vilivyo chini ya Ukawa, zimekatika bila
mafanikio na mvutano unaonekana kubakia kwenye majimbo 12 kati ya 239
waliyopanga kugawana.
Vyama hivyo vinavyounda Umoja wa Katiba ya
Wananchi vimekubaliana kusimamisha mgombea mmoja kuanzia kiti cha urais
hadi udiwani, lakini kazi ya kugawana majimbo imekuwa ikivisumbua na
ilitarajiwa kuwa ingemalizika juzi baada ya viongozi kukutana kwa siku
mbili kuanzia Jumanne.
Lakini habari kutoka ndani ya kikao hicho
kilichofanyika jijini Dar es Salaam zinaeleza kuwa wajumbe walishindwa
kufikia muafaka kwenye majimbo 12.
Hata hivyo, viongozi hao wa vyama hivyo walikataa kutaja majimbo hayo yaliyosalia. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
SOMA MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 01, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
SUMATRA KIINI CHA AJALI BARABARANI...!!!
Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta
WAZIRI wa Uchukuzi, Samuel Sitta amesema ajali za barabarani
zinachangiwa na uzembe wa taasisi inayosimamia sekta ya usafiri jambo
linalogharimu maisha ya watu wasio na hatia, na kuitaka taasisi hiyo
kuchukua hatua na kuhakikisha nidhamu inarejea kwenye sekta hiyo.
Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) ndiyo
yenye dhamana ya kusimamia na udhibiti wa sekta ya usafiri katika nchi
kavu na majini.
Sitta aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam alipozungumza na
waandishi wa habari wakati Kamati ya Bunge ya Miundombinu ilipokuwa
ikizungumza na viongozi wa wizara hiyo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
BAN KI-MOON ASIKITISHWA NA MAPIGANO YEMEN
Katibu
mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ameelezea tahadhari yake kuhusiana
na hatari ya raia kuendelea kupigana, Nchini Yemen. Anasema kuwa
zaidi ya watu elfu moja mia tano wameuwawa na wengine laki tatu
wametoroka makazi yao, katika kipindi cha majuma sita yaliyopita.
Mashambulizi katika majumba ya raia zikiwemo hosptali na maghala ya vifaa vya misaa ya kibinadamu yamekuwa yakiendelea.
Kumekuwa na taarifa watu wenye silaha wamekuwa wakiwateka raia katika mitaa ya Aden.
Shirika
la Umoja wa mataifa la misaada ya chakula limesema halina jinsi zaidi
ya kusitisha mipango yake ya kusambaza misaada kutoka na tatizo la
mafuta.
Kwa sasa mapigano makali yanaendelea katika mipaka ya eneo la Yemen na Saudia Arabia. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
MAANDAMANO MAPYA BALTIMORE MAREKANI
Kumetokea maandamano mapya
nchini Marekani katika mji wa Baltimore kufuatia kifo cha kijana mweusi
Freddie Gray aliyekufa kutokana na majeraha akiwa mikononi mwa polisi. Mamia ya watu wameandamana katika mitaa, wakionyesha ujasiri licha ya
hali mbaya ya hewa iliyokuwepo.
Mtetezi wa haki za binadamu,
Mchungaji Al Sharpton, ameitisha mkutano mjini Baltimore ili kuimarisha
uhusiano baina ya polisi na wanajamii. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
YANGA INA MATUMAINI YA USHINDI
Kocha
mkuu wa Yanga, Hans Pluijm amesema wana ari ya kushinda mechi yao ya
mwishoni mwa wiki hii dhidi ya Etoile du Sahel licha ya kuwaacha
wachezaji wake tegemezi katika msafara wao wa Tunisia.
Yanga
imeondoka Dar es Salaam Jumatano usiku huku wachezaji wake tegemezi,
wakiwemo Hassan Dilunga, Salum Telela na Danny Mrwanda, aliyekuwa
akicheza soka la kulipwa nchini Vietnam wakiachwa kutokana na sababu
mbalimbali zikiwemo za kifamilia. “Yanga imesajili zaidi ya wachezaji 20, wote ni muhimu katika timu”.
“Ni
kweli niliwahitaji katika mechi yetu ngumu dhidi ya Etoile, lakini
sababu mbalimbali zimepelekea kuachwa kwao”, amesema Pluijm. Yanga
itacheza na wenyeji wao, Etoile du Sahel katika mechi ya marudiano ya
raundi ya 16 bora ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika.
Katika
mechi iliyochezwa wiki mbili zilizopita jijini Dar es Salaam, Yanga
ililazimishwa sare ya 1-1 hivyo kuwa na kibarua kigumu cha kushinda
ugenini huku wenyeji wao wakililia sare ili kucheza hatua inayofuata. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
TAZAMA PICHA ZA YANGA WAKIWA KATIKA MAZOEZI NCHINI TUNIS
Katika mazoezi ya jana usiku kocha mkuu
wa Yanga, Hans van der Pluijm amewaambia vijana wake kujiamini na
kucheza soka la kushambulia ili kufunga magoli ya mapema na
kuwachanganya Etoile du Sahel katika mechi ya leo usiku kuanzia majira
ya saa 3:00 usiku kwa saa za Tanzania.
Mkuu wa Idara ya habari na Mawasiliano wa
Yanga, Jerry Muro naye kama kawaida yupo Tunisia kufuatilia mambo
yanavyokwenda. Yanga wanahitaji ushindi au sare ya angalau magoli 2-2
ili kusonga mbele moja kwa moja kwasababu mechi ya kwanza jijini Dar es
salaam timu hizi zilitoka sare ya 1-1.
Maelekezo ya hapa na pale kabla ya kuanza mazoezi.
Mrisho Ngassa (kushoto) na Simon Msuva (kulia) wanatarajia kuongoza safu ya ushambuliaji leo
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
BEN DAVIES APASULIWA BEGA
Beki wa kulia wa Tottenham Ben Davies ameenguliwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Wales baada ya kufanyiwa upasuji wa bega. Mlinzi huyu aliumia wakati wa mchezo wa ligi kati ya timu yake na Southampton uliofanyika wiki iliyopita.
Davies hatojumuika na wenzake katika mchezo wa kuwania kuzufu kwa michuno ya ulaya ya mwaka2016. Ambapo
Wales watakua na mchezo dhidi ya Ubelgiji , tayari kocha wa timu hiyo
Chriss Coleman amemuita kikosini beki wa Swansea City's Neil Taylor
kuziba pengo hilo.
Hii inasababisha mchezaji huyu kukosa michezo iliyobaki ya ligi ya England. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Subscribe to:
Posts (Atom)