Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Monday, April 20, 2015
SOMA MAGAZETI YA LEO JUMATATU APRILI 20, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
LOWASSA ATHIBITISHA UBORA WA AFYA YAKE
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowasa akiwa katika matembezi ya kupinga mauaji ya albino.
WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowasa, jana alithibitisha kwa vitendo kuwa afya yake iko safi baada ya kutembea umbali wa kilomita tano kwa miguu kwenye matembezi ya kupinga mauaji ya albino nchini.
Kwa muda mrefu, Lowassa ambaye ni mmoja wa makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaotajwa kuwania nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu, amekuwa akidaiwa kuwa na matatizo ya afya na kuwa hawezi kuhimili mikimiki ya kampeni na shughuli nyingine zinazohitaji nguvu.
Lakini matembezi ya jana yaliyoongozwa na Lowassa kuanzia Uwanja wa Taifa wilayani Temeke mpaka viwanja vya TCC Chan’gombe na kutumia dakika 25, yamedhihirisha vinginevyo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
UCHINA KUWEKEZA MABILIONI PAKISTAN
Rais wa China Xi Jinping ameanza ziara ya siku mbili nchini Pakistan hii leo.
Bwana
Xi atazindua mpango wa uwekezaji wa kichina wa gharama ya dola bilioni
50 ambao Pakistan ina matumaini kuwa utasuluhisha tatizo lake ya
nishati.
Mpango huo unaofahamika kama barabara ya uchumi ya China
na Pakistan ni pamoja na barabara , reli na mabomba ya jumla ya umbali
wa kilomita 3000 kutoka mji wa bandari wa Gwadar nchini Pakistan hadi
mji wa ulio mashariki mwa China wa Kashgar.
Waandishi wa habari
wanasema kuwa lengo la China ni kuongeza ushawishi wake wa kiuchumi kwa
Pakistan ili kulegeza ule wa Marekani na India. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
SULUHU YATAKIWA KUHUSU WAHAMIAJI
Waziri
mkuu wa Italia Matteo Renzi ametoa wito wa kufanyika kikao cha dharura
cha viongozi wa umoja wa ulaya kujadili swala la wahamiaji wanaoangamia
kwenye bahari ya Meditarenean wakijaribu kuingia ulaya. Inafuatia ajali
ya hivi punde ambao karibu watu 700 wanahofiwa kufa maji baada ya boti
kuzama baharini kaskazini mwa Libya, kilomita 200 kutoka kisiwa cha
Lampedusa, nchini Italia.
Manusura 28 wa janga la hivi punde
kwenye bahari ya Meditaranean walitarajiwa kufikishwa kisiwani Sicily
alfajiri ya Jumatatu. Hadi kufikia usiku, ni miili 24 iliyokuwa
imeopolewa, na maafisa wa usalama kwenye pwani ya Italia, wakaipeleka
kisiwani Malta.
Ni vigumu kuhakikisha idadi ya watu walioanza
safari kwenye boti hiyo kutoka pwani ya Libya. Lakini walionusurika
wanasema walikuwa kati ya watu 500 na 700 kabla ya kupinduka kilomita
mia mbili kutoka Lampedusa, kwenye maji ya Libya. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA BARA
Rnk | Team | MP | W | D | L | GF | GA | +/- | Pts | |||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
1 | Young Africans | 21 | 14 | 4 | 3 | 39 | 12 | 27 | 46 | |||
2 | Azam | 22 | 11 | 9 | 2 | 29 | 15 | 14 | 42 | |||
3 | Simba SC | 22 | 9 | 8 | 5 | 27 | 17 | 10 | 35 | |||
4 | Kagera Sugar | 23 | 8 | 7 | 8 | 22 | 22 | 0 | 31 | |||
5 | Ruvu Shooting | 23 | 7 | 8 | 8 | 16 | 21 | -5 | 29 | |||
6 | Mtibwa Sugar | 23 | 6 | 10 | 7 | 22 | 23 | -1 | 28 | |||
7 | Mbeya City | 23 | 6 | 10 | 7 | 19 | 21 | -2 | 28 | |||
8 | Mgambo JKT | 22 | 8 | 4 | 10 | 18 | 21 | -3 | 28 | |||
9 | Stand United | 22 | 7 | 7 | 8 | 19 | 24 | -5 | 28 | |||
10 | Coastal Union | 23 | 6 | 9 | 8 | 16 | 23 | -7 | 27 | |||
11 | JKT Ruvu | 23 | 6 | 7 | 10 | 17 | 23 | -6 | 25 | |||
12 | Ndanda | 23 | 6 | 7 | 10 | 18 | 26 | -8 | 25 | |||
13 | Polisi Morogoro | 23 | 5 | 9 | 9 | 15 | 22 | -7 | 24 | |||
14 | Tanzania Prisons | 23 | 3 | 13 | 7 | 15 | 22 | -7 | 22 |
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
LOOO...!!! SIMBA NOMA "INA WAGANGA WENGI WA KIENYEJI KULIKO WATAALAMU WA BENCHI LA UFUNDI"
Simba waligoma kuingia kwenye vyumba vya kubadilishia nguo walipocheza na Mbeya City jumamosi iliyopita uwanja wa Sokoine
MTANDAO wa SHAFFIH DAUDA kwa muda mrefu sasa
umekuwa ukifanya tafiti na kufuatilia mwenendo wa klabu ya Simba katika
mechi za ligi kuu soka Tanzania bara msimu huu.
Mwishoni mwa juma lililopita,
Simba ilifungwa magoli 2-0 na Mbeya City fc katika uwanja wa Sokoine,
Mbeya na kuifanya klabu hiyo kongwe nchini kuendelea kukaa nafasi ya
tatu kwa pointi 35 walizokusanya baada ya kushuka dimbani mara 22.
Machi 18 mwaka huu walifungwa
magoli 2-0 na Mgambo JKT katika uwanja wa CCM Mkwakwani Tanga, lakini
wakashinda 2-1 ugenini dhidi ya Kagera Sugar uwanja wa CCM Kambarage,
Shinyanga na ilikuwa aprili 6 mwaka huu (jumatatu ya pasaka).
Katika mechi hizo tatu, mtandao huu ulikuwa unachunguza mwenendo wa Simba na namna wanavyoiandaa timu kwa ajili ya mechi. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
MBWANA AWATAKA MASHABIKI WA PRISONS KUISAPOTI HADI MWISHO
Mbwana Makata, kocha mkuu wa Tanzania Prisons.
MBWANA Makata, kocha mwenye
uzoefu wa kufundisha timu za majeshi safari hii amepewa jukumu la
kuibakisha Tanzania Prisons ligi kuu Tanzania bara msimu ujao.
Makata, kocha wa zamani wa JKT
Ruvu na JKT Oljoro jana ameiongoza Prisons kupata sare nyumbani ya goli
1-1 dhidi ya Wakata miwa wa Mtibwa Sugar katika mechi ya ligi kuu
iliyopigwa uwanja wa CCM Kumbukumbu ya Sokoine, Mbeya.
Baada ya sare hiyo, Makata
amesema: “Mechi ilikuwa ni muhimu kwetu kuweza kupata matokeo ya
ushindi, lakini mechi ilikuwa ngumu na tumeweza kutapa sare ya goli 1-1.
Kikubwa niwapongeze vijana wangu kwasababu ratiba kwetu ilibana wiki
hii, tulicheza jumatano, tukawa safarini na kucheza tena leo (jana),
muda wa maandalizi haukuwepo."
"Cha msingi niwaombe wakazi wa Mbeya,
mashabiki wa Prisons waisapoti timu yao, tupambane mpaka dakika za
mwisho tuone nini kitatokea” Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Sunday, April 19, 2015
ALIYENUSURIKA AJALI MBEYA ASIMULIA..!!!
Mmoja wa manusura wa ajali iliyotokea eneo la Mto Kiwira, Rungwe mkoani Mbeya, Mariam Manfredy akiwa amelazwa kwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa Mbeya.
Mmoja wa majeruhi wa ajali iliyoua watu 19, Mariam Manfredy (28) aliyevunjika mguu wa kushoto, anasimulia ajali hiyo na kusema chanzo ni mwendo kasi na kuungua kwa breki.
Gari hilo lilikuwa ‘limeshona’ abiria, lilikuwa
likitoka jijini Mbeya kwenda Kiwira wilayani Rungwe kabla ya kuanguka
eneo la Mto Kiwira na kuua watu 18 palepale na mmoja alifia Hospitali ya
Igogwe huku wengine watatu wakijeruhiwa.
Mariam aliyelazwa katika Hospitali ya Rufaa Mbeya
(MRH), alisema alipanda basi hilo katika Kijiji cha Simambwe akienda
Kiwira kununua bidhaa za biashara. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
MADEREVA WA MABASI KAMA WA BODABODA...!!!
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga, akitoa takwimu za vifo vilivyotokana na ajali za barabarani kati ya January Mosi hadi Aprili 12 mwaka huu, sawa na siku 102 vifo 969.
WAKATI ajali za barabarani zikiendelea kumaliza nguvu kazi ya Taifa
na kuumiza vichwa vya Watanzania kuhusu suluhisho la ajali hizo,
imefahamika moja ya tatizo sugu ni kukosekana kwa madereva wenye taaluma
stahiki, ingawa wana leseni.
Wiki hii peke yake, ajali tatu za mabasi zilizotokea Mbeya, Morogoro
na maeneo ya Mwanza, zimesababisha vifo vya watu 40 ndani ya siku sita.
Tayari Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga,
ametoa takwimu za vifo vilivyotokana na ajali za barabarani kati ya
Januari Mosi mwaka huu hadi Aprili 12, sawa na siku 102 vifo 969. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
SOMA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI APRILI 19, 2015 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
UWT ARUSHA WAWAKATAA WALIMU KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU
Wanawake wa UWT wakishangilia.
JUMUIYA ya Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Mkoa wa Arusha,
imetangaza wazi kuwakataa walimu kusimamia uchaguzi wa madiwani, wabunge
na rais, kutokana na tabia ya kufanya hujuma kwa chama hicho wakati
wanasaidiwa mambo mengi ya msingi na serikali ya CCM.
Mbali ya walimu, pia UWT imewanyooshea kidole baadhi ya polisi mkoani
Arusha kwa kuwa na mapenzi yaliyopitiliza dhidi ya Chama cha Demokrasia
na Maendeleo (Chadema), hali inayowafanya kushindwa kutenda haki katika
maamuzi mbalimbali.
Msimamo huo umetangazwa kwa nyakati tofauti na Mwenyekiti wa jumuiya
hiyo mkoa wa Arusha, Flora Zelote alipokuwa akizungumza katika kata
mbalimbali za wilaya ya Arusha katika ziara yake ya kikazi ya kukagua
uhai wa jumuiya hiyo na chama kwa ujumla. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
USALAMA WAIMARISHWA AFRIKA KUSINI
Maafisa zaidi wa polisi wametumwa katika maeneo yenye mashambulio dhidi ya raia wa kigeni nchini Afrika Kusini. Yamkini
watu sita wameuawa na makundi yenye silaha, ambayo yanawalaumu
wahamiaji wa kiafrika kwa kuchukua kazi zao nchini Afrika Kusini.
Rais
Jacob Zuma amewatembelea watu hao walioathirika na ghasia hizo, mauwaji
pamoja na kuibwa kwa mali zao huku akiahidi kukabiliana vilivyo na
wimbi la mashambulio hayo.
Bwana Zuma alifutilia mbali ziara yake nchini Indonesia, ili kukabiliana na vurumai hizo zilizoanza majuma mawili yaliyopita.
Yamkini
watu sita wameuawa na makundi yenye silaha, ambayo yanawalaumu
wahamiaji wa kiafrika kwa kuchukua kazi zao nchini Afrika Kusini. Nchini Harare Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, alilaani ghasia hizo.
Ghasia
hizo zilianza baada ya mfalme mmoja wa Kizulu, Goodwill Zwelethini,
kusema kuwa raia wa kigeni sharti waondoke Afrika Kusini. Akiongea
katika kambi hiyo iliyoko mjini Durban kiongozi mkuu wa jimbo la
Gauteng, David Makhura, anasema kuwa uhasama na ghasia hizo
zinazoshuhudiwa, haundamani na uhuru wa miaka mingi ambayo Afrika Kusini
ilipigania. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Saturday, April 18, 2015
WATU 38 WAFARIKI KATIKA AJALI
Basi dogo aina ya Hiace likiwa limetumbukia kwenye Mto Kiwira eneo maarufu kwa jina la Uwanja wa Ndege, wilayani Rungwe mkoani Mbeya.
Msiba mwingine mzito umelikumba
taifa baada ya watu 38 kupoteza maisha katika matukio mawili tofauti,
likiwamo la ajali ya basi dogo aina ya Toyota Hiace iliyoua watu 19
wakati ikifanya safari ya wizi mkoani Mbeya.
Tukio jingine limetokea mkoani Shinyanga ambako
wachimbaji wadogo 19 wa dhahabu waliokuwa katika mgodi mdogo wa Kalole,
wilayani Kahama wamekufa baada ya kufunikwa na kifusi usiku wa kuamkia
jana kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.
Polisi wakiwa katika machimbo ya dhahabu ya Kalole wilayani Kahama jana baada ya machimbo hayo kuporomoka na kuua watu 19.
Polisi wakiwa katika machimbo ya dhahabu ya Kalole wilayani Kahama jana baada ya machimbo hayo kuporomoka na kuua watu 19.
Matukio hayo ni mwendelezo wa majanga ya ajali
ambazo zimekuwa zikitokea kwa takriban wiki mbili mfululizo na kuua
mamia ya watu. Zaidi ya watu 980 wamefariki dunia katika ajali za
barabara katika muda wa zaidi ya miezi mitatu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
MENGI ATUHUMIWA KWA UHAINI, MWENYEWE AIBUKA NA KUNENA...!!!
MWENYEKITI wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi, ametuhumiwa kutaka kuiangusha Serikali ya Rais Jakaya Kikwete na kumshughulikia baada ya kumaliza uongozi wake Oktoba, mwaka huu.
Baada ya tuhuma hizo kuelekezwa kwake na gazeti la Taifa Imara lililochapishwa Machi 23, mwaka huu likiwa na kichwa cha habari kinachosema, ‘Zitto amchongea Mengi kwa JK? Mwenyewe ameibuka Dar es Salaam jana na kuzikanusha mbele ya waandishi wa habari akisema zimemshtua na kumuogopesha.
“Tuhuma zilizotolewa na gazeti la Taifa Imara la Machi 23-29, mwaka huu kwamba nina nia ya kutaka kuiangusha Serikali ya Rais Kikwete na kumshughulikia baada ya kumaliza muda wake wa uongozi, zimenishtua sana,” alisema Mengi. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
SOMA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRILI 18, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Subscribe to:
Posts (Atom)