Sunday, April 19, 2015

UWT ARUSHA WAWAKATAA WALIMU KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU

Wanawake wa UWT wakishangilia.
Wanawake wa UWT wakishangilia.

JUMUIYA ya Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Mkoa wa Arusha, imetangaza wazi kuwakataa walimu kusimamia uchaguzi wa madiwani, wabunge na rais, kutokana na tabia ya kufanya hujuma kwa chama hicho wakati wanasaidiwa mambo mengi ya msingi na serikali ya CCM.
Mbali ya walimu, pia UWT imewanyooshea kidole baadhi ya polisi mkoani Arusha kwa kuwa na mapenzi yaliyopitiliza dhidi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), hali inayowafanya kushindwa kutenda haki katika maamuzi mbalimbali.

Msimamo huo umetangazwa kwa nyakati tofauti na Mwenyekiti wa jumuiya hiyo mkoa wa Arusha, Flora Zelote alipokuwa akizungumza katika kata mbalimbali za wilaya ya Arusha katika ziara yake ya kikazi ya kukagua uhai wa jumuiya hiyo na chama kwa ujumla. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Alisema kutokana na hali hiyo, jumuiya yake ina mpango wa kufikisha mapendekezo yao kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na makao makuu ya CCM ya namna ya kuwapata wasimamizi wengine wa uchaguzi mbadala wa walimu hao.

Alisema CCM imeonekana kama mpangaji katika nyumba yake, kutokana na mabaya yanayofanywa dhidi yake na watumishi wanaowalipa mishahara huku chama hicho kikiendelea kukaa kimya.

“Polisi na walimu wanaolipwa mishahara na serikali ya CCM wanakihujumu chama chetu, hii ni sawa na mwenye nyumba kugeuka kuwa mpangaji au mke anayebaki kung’ang’ania cheti cha ndoa wakati nje ‘nyumba ndogo’ amemdhibiti mumewe.

Hii haiwezekani,” alisema Zelote. Alitumia nafasi hiyo kuwatahadharisha viongozi wa Taifa wa CCM, kurejesha majina yale yale ya wagombea watakayoyapendekeza mikoani, vinginevyo wakirejesha majina mengine tofauti, watakuja kuwanadi wao katika kampeni.

Zelote alisema hali ilivyo sasa, chama kinapaswa kuheshimu matakwa ya wananchi ya nani wanamtaka, badala ya kuendelea na tabia ya kuwapendekeza watu kwa utashi wa kikundi cha watu, jambo ambalo linasababisha ugumu katika kuwanadi wagombea hao.

“Mimi naomba nitoe msimamo wa jumuiya yangu mkoa wa Arusha, sisi tutapendekeza wagombea kwa matakwa ya wananchi watakaowachagua na tutawafikisha kwao ili wafanye maamuzi sahihi, wakifanya vinginevyo, wakawaleta wa kwao, tutawapa taarifa waje kuwafanyia kampeni,” alisema Zelote.

Alisema maamuzi hayo, pia yatafutwa katika ngazi ya wilaya, ambapo vilevile kama wataacha mapendekezo ya kata zao na wakafanya vinginevyo, nao watapewa taarifa kwenda kuwanadi wagombea waliowarejesha kwa utashi wao. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...