Thursday, December 18, 2014

POLISI WAZUIA MAZISHI YA AISHA MADINDA HADI KESHO


Jeshi la polisi limezuia mazishi ya aliyekuwa mnenguaji wa Twanga Pepeta na Extra Bongo, Aisha Madinda hadi hapo mwili wake utakapofanyiwa uchunguzi kutokana na utata wa kifo chake.
Akizungumza na Mwananchi, dada wa marehemu, Hamida Mbegu alisema Polisi waliwaambia kuwa mwili huo unahitaji kufanyiwa vipimo ili kubaini sababu za kifo chake, japokuwa familia haikuwa tayari kwa jambo hilo.
Alisema Polisi walisisitiza kuwa ni lazima mwili ufanyiwe vipimo kutokana na kuwapo kwa utata wa kifo hicho.
Hamida amesema kwa mujibu wa polisi vipimo vitafanyika asubuhi, hivyo baada ya vipimo kumalizika mwili utapelekwa Kigamboni ambako ndiyo familia imekusanyika na baada ya swala ya Ijumaa utazikwa kwenye makaburi ya familia yaliyopo Kibada, Kigamboni.
Akizungumzia suala hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Camilius Wambura, alisema kuwa kutokana na mazingira ya kifo hicho ni lazima Polisi wajiridhishe kwa kuufanyia mwili vipimo.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

WABUNGE WARUSHIANA NGUMI BUNGENI...!!!

Wabunge wakiwa katika vikao bungeni 
Wabunge wa Kenya wametofautiana vikali bungeni na kuvuana mashati huku wakirushiana ngumi kufuatia mjadala kuhusu mswada tatanishi wa usalama ambao wabunge wa upinzani wanasema unakiuka uhuru wa wakenya.
Bunge lililazimika kuahirisha vikao vyake kwa dakika 30 badala ya kujadili mswada tatanishi kuhusu usalama wa nchi. Kikao cha leo kilikuwa kikao maalum ambacho kilipaswa kupitisha mswada huo ambao baadaye utaidhinishwa na Rais kuwa sheria.
Wabunge wa upinzani walipinga mswada huo na kuanza kurusha karatasi sakafuni huku wakitatiza shughuli bungeni humo.


Seneta Johnston Muthama alijipata pabaya kwani long'i yake iliraruliwa katika mvutano bungeni humo.
 
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year. 

NAIBU SPIKA AMWAGIWA MAJI BUNGENI

 Naibu spka Joyce Laboso ambaye amemwagiwa soda 
 
 Kikao cha adhuhuri cha wabunge nchini Kenya, kinaendelea kuzua hisia kali huku wabunge wakiendelea kuvurugana humo.
Wabunge hao wanajadili mswada tatanishi wa usalama ambao upande wa upinzani unasema unakwenda kinyume na katiba na kuwanyima wakenya haki yao ya kujieleza.
Mmoja wa wabunge hao wa upinzani amemwagia soda naibu spika Joyce Laboso ambaye alikuwa anasimamia kikao hicho cha kufanyia mswada huo mabadiliko kabla ya kupitishwa.
Spika wa bunge hilo sasa amechukua usukani na kuamuru kutimuliwa kwa wabunge wawili waliokuwa wamezidi vurugu. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

WATU 33 WAUAWA, 100 WATEKWA NIGERIA

Wapiganaji wa kundi la Boko Haram  

Wanamgambo wamevamia kijiji kimoja kazkazini mashariki mwa Nigeria na kuwaua takriban watu 33 na kuwateka wengine 100,mmoja ya waathiriwa amesema.
Amesema kuwa washukiwa wa kundi la Boko haram waliwakamata vijana wadogo,wanawake na watoto kutoka kijiji cha Gumsuri.
Shambulizi hilo lilitokea siku ya jumapili lakini habari hizo zilibainika baada ya waathiriwa kufika mji wa Maiduguri.
Wakati huohuo,jeshi la Cameroon limesema kuwa limewaua wanamgambo 116 ambao walikuwa wameshambulia kambi moja ya kijeshi kulingana na AFP.
Moja ya vijiji vilivyoavamiwa na wanamgambo wanaodaiwa kutoka kwa kundi la Boko haram
Wakaazi wameiambia BBC kwamba wanamgambo waliojihami na silaha walishambulia eneo la mpakani la Amchide siku ya jumatano,walipowasili kwa magari mawili huku wengine wakitembea.
Walivamia eneo la soko na kuchoma maduka na zaidi ya nyumba 50.
Hakuna kundi lililokiri kutekeleza mashambulizi hayo lakini maafisa wamelaumu wapiganaji wa Boko Haram.
Zaidi ya watu 2000 wameuawa katika ghasia za makundi yaliojihami na silaha mwaka huu pekee,hususan kazkazini mwa Nigeria karibu na mpaka na Cameroon. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Wednesday, December 17, 2014

AJALI ZAUA WATU 8 TABORA NA MOROGORO

Kamanda wa Polisi Tabora, Suzan Kaganda


 Kamanda wa Polisi mkoani Tabora, Suzan Kaganda. PICHA|MAKTABA

WATU wanane wamekufa papo hapo, huku wengine 50 wakijeruhiwa vibaya katika ajali mbili tofauti zilizotokea Tabora na Morogoro jana.

Katika ajali ya Tabora, basi la Kampuni ya Mohammed Trans likitoka Mwanza kwenda Dar es Salaam lilipinduka mara nne katika kijiji cha Makomero, kata na wilaya ya Igunga na kuua watu 5 na kujeruhi 50.

Kamanda wa Polisi mkoani humo, Suzan Kaganda alikiri kutokea kwa ajili hiyo na kusema jeshi hilo bado linaendelea na uchunguzi wa kujua chanzo cha ajili hiyo iliyotokea majira ya saa 5:30 asubuhi.

Alilitaja basi hilo kuwa ni aina ya Scania lenye namba za usajili T 738 AAP ambalo lilikuwa na zaidi ya abiria 55. Akizungumza katika eneo la tukio, mmoja wa majeruhi, Maimuna Mussa (27) aliyekuwa akielekea Dodoma na mtoto wake mwenye umri wa miaka miwili, alisema walikuwa kwenye mwendo kasi na alishitukia gari likiacha njia na kupinduka mara nne.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.  

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI AJIUZULU...!!!

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema 

WAKATI Watanzania wakisubiri kusikia uamuzi wa Rais Jakaya Kikwete juu ya maazimio manane yaliyotolewa na Bunge kuhusu sakata la uchotaji wa zaidi ya Sh bilioni 300 katika akaunti ya Tegeta Escrow ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema amejiuzulu wadhifa huo.
Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, iliyotolewa jana na Mkurugenzi wake, Salva Rweyemamu kwa vyombo vya habari imethibitisha kujiuzulu kwa Werema kuanzia jana.
Amekuwa kwenye wadhifa huo tangu mwaka 2009, alipochukua nafasi ya Johnson Mwanyika aliyestaafu. Taarifa hiyo iliongeza kuwa Rais Jakaya Kikwete amekubali ombi la kujiuzulu kwa mwanasheria huyo.
Kabla ya kugeukia taaluma ya sheria, Werema alikuwa mwalimu katika Shule ya Sekondari ya Shaaban Robert jijini Dar es Salaam kati ya mwaka 1979 na 1980.

Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO DESEMBA 17, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA WAMWAGA DAMU

Kamanda wa Polisi mkoani Tabora, Suzan Kaganda. PICHA|MAKTABA 

Wakati tukio la Bukombe likihusisha mtu kuchinjwa katika sherehe za ushindi wa mkewe kuwa mwenyekiti wa mtaa, huko Nzega kijana moja alipigwa risasi na polisi wakati wa kusubiri matokeo ya uchaguzi huo.
Bukombe
Mume wa mshindi wa kiti cha mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kapela, wilayani Bukombe ameuawa baada ya kuchinjwa katika hafla ya ushindi wa mkewe.
Mtu huyo, Bundara James (56), aliuawa usiku wa kuamkia juzi katika Mtaa wa Kapela ulioko kwenye Kata ya Igulwa wilayani Bukombe muda mfupi baada ya kumalizika kwa hafla ya kusherehekea ushindi huo.
Mke wa marehemu ambaye sasa ni mwenyekiti wa mtaa huo, Lusia Samwel alisema mumewe ambaye ni mtumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe, alikutwa amechinjwa na watu wasiojulikana ambao walitoweka baada ya tukio hilo wakiacha panga walilofanyia uhalifu kwenye eneo la tukio.

Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

NAPE: KAKOSA YA CCM YAMEINUFAISHA UKAWA

 
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye. PICHA|MAKTABA 

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kilifanya makosa katika baadhi ya maeneo ambayo yamekigharimu na kusababisha wananchi kupiga kura za hasira kukiadhibu katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu matokeo ya uchaguzi huo ambao umeonyesha kuvinufaisha vyama vya upinzani kupitia umoja wao wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Nape alisisitiza kwamba makosa hayo ndiyo yaliyosababisha wapinzani kujinyakulia mitaa kadhaa kwa wepesi. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

PAKISTAN YAOMBOLEZA MAUAJI YA WAATOTO

Raia wa Pakistan wakiwaombea watoto 140 waliouawa katika shambulizi la kigaidi katika shule moja nchini humo. 
Raia nchini Pakistan wanaadhimisha siku tatu za maombolezo kuwakumbuka zaidi ya watu 140 waliouwawa,karibia wote wakiwa watoto katika shambulio lililotekelezwa na kundi la Taliban.
Waziri mkuu Nawaz Shariff ameitisha mkutano wa vyama vyote vya kisiasa nchini humo kujadili vile watakavyoweza kujibu shambulizi hilo la Peshawar.
Ameelezea shambulizi hilo kuwa janga la kitaifa lililotekelezwa na wakatili.
Mkuu wa jeshi Jenarali Raheel Shariff ameahidi kulipiza kisasi kwa kila tone la damu linalomwagika.
Nchini India ,shule zimenyamaza kwa dakika mbili ili kutoa heshima kwa wale waliouawa.
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year. 

HAITI WAANDAMANA KUMNG'OA RAIS WAO

Rais wa Hait mICHAEL Martelly
Mamia ya raia wa nchini Haiti wameandamana katika mitaa ya Port-au-Prince wakishinikiza Rais Michel Martelly kuondoka madarakani.
Hata hivyo maandamano hayo yamegeuka vurugu baada polisi kutumia mabomu ya mchozi kuwatawanya waandamanaji hao. polisi wamepambana na waaandamanaji hao ambao wamekuwa wakirusha mawe na kuchoma moto matairi mitaani.
Madai ya raia hao ni kumtaka Rais Martelly kuitisha uchaguzi na kuunda serikali,ambapo uchaguzi ulitakiwa kuitishwa miaka mitatu iliyopita.
Waziri mkuu wa Haiti Laurent Lamothe, siku ya jumapili aliamua kuachia ngazi baada ya shinikizo la siku mbili.Maoni kutoka vyama vya upinzani ni kwamba wanamtaka rais Martelly kujiuzulu. Awali Waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry ameitaka Hait kuitisha uchaguzi mara moja.
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.  

Na BBC

PLUIJM ATUA YANGA, MAXIMO ATIMULIWA MAZOEZINI

Kocha Hans van Pluijm akiwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam juzi, kuchukua mikoba ya Marcio Maximo aliyetupiwa virago Yanga. (Na Mpigapicha Wetu).

Kocha Hans van Pluijm akiwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimatafa wa Julius Nyerere Dar es Salaam juzi.

UONGOZI wa Klabu ya soka ya Yanga jana asubuhi ulilazimika kumwondoa mazoezini Kocha Mkuu, Marcio Maximo na kumrudisha klabuni ili kumalizana naye kabla ya kuanza safari ya kurudi kwao Brazil, huku akiiacha timu hiyo ikifundishwa na kocha anayetarajiwa kuchukua nafasi yake, Hans van Pluijm.

Maximo aliondolewa mazoezini na kupakiwa kwenye basi dogo la timu hiyo aina ya Toyota Hiace lililokuwa likiendeshwa na meneja wa timu hiyo, Hafidh Salehe.
Aliambana na msaidizi wake, Leonard Neiva na kiungo Emerson de Oliveira Roque aliyesajiliwa hivi karibuni akitokea nchini Brazil.
Kitendo hicho kilitokana na uongozi huo kufikia makubaliano ya kumtimua kazi kocha huyo pamoja na msaidizi wake Neiva, kutokana na kushindwa kuipa mafanikio tangu alipoanza kuifundisha timu hiyo katika kipindi cha miezi minne.

Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MLIBERIA APATAITC, MUSHEED ASUBIRI SIMBA

Kpah Sherman

Kpah Sherman
MSHAMBULIAJI mpya wa Yanga, Kpah Sherman sasa ni ruksa kucheza katika Ligi Kuu baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kuthibitisha kwamba hati yake ya uhamisho kumruhusu kucheza soka nchini tayari imeshafika.

Aidha, wakati Sherman akiwa na uhakika wa kuitumikia klabu hiyo, TFF imethibitisha kuchelewa kwa hati ya uhamisho ya kiungo mpya wa Yanga, Emerson de Oliviera Roque ambaye aliombewa ITC ili kuitumikia timu hiyo.
Licha ya kuwepo kwa taarifa za kukatwa kwa mchezaji huyo na nafasi yake kupewa aliyekuwa mchezaji wa Simba, Amisi Tambwe, Mkurugenzi wa Mashindano wa TFF, Boniface Wambura alisema jana kuwa ITC hiyo haijafika.

Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

KLABU BINGWA DUNIA MADRID YATINGA FAINALI

Raha ya goli ni shamra shamra, wanapongezana.
Wakicheza katika dimba la Stade de Marrakech. Mjini Marrakech Nchini Morocco, Mabingwa wa Ulaya Real Madrid wamepata ushindi mnono wa goli 4-0 dhidi ya Cruz Azul na kutinga Fainali ya Mashindano ya FIFA ya Kombe la Dunia kwa Klabu.
Real Madrid walianza kupata magoli yake dakika ya kumi na 15 kupitia kwa beki Sergio Ramos mshambuliaji Karim Benzema akaongeza la pili dakika ya 36,
Kipindi cha Pili, Gareth Bale, alifunga bao la 3 na Isco, kuhitimisha kwa goli la 4 na kuipelea Madrid fainali.
Azul walikosa penati dakika ya 40 iliyopigwa na Gerardo Torrado, na kuokolewa na kipa Iker Casillas.
Real wanasubiri mshindi wa mchezo wa leo kati ya San Lorenzo ya Argentina na Auckland City ya New Zealand.
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

CHELSEA NUSU FAINALI CAPITAL CUP

Chelsea wakipasha
Chelsea, wakicheza katika uwanja wa iPro Stadium waliwachabanga timu ya Derby County, Bao 3-1 kwenye Kombe la Ligi maarufu kama Capital One Cup, na kutinga Nusu Fainali.
Eden Hazard, ndie alianza kuipatia Chelsea, goli la kwanza dakika ya 33 kabla ya Filipe Luis, kufunga goli la pili dakika ya 56 huku Andre Schurrle, akihitimisha ushindi kwa goli la dakika ya 82.
Bao la kufutia machozi kwa Derby lilifungwa na Craig Bryson, Dakika ya 71.
Kwenye Mechi nyingine ya Robo Fainali Sheffield United, waliwashangaza Southampton kwa kuwabanjua Bao 1-0.
Bao la ushindi la Sheffield lilifungwa na McNulty, Dakika ya 63. Southampton walibaki 10 baada ya Gardos kupewa Kadi Nyekundu.
Leo Usiku zitachezwa Robo Fainali nyingine mbili ambapo Liverpool, watakuwa Wageni wa Bournemouth.
Huku katika uwanja wa white Hart Lane Tottenham Hotspur watawakaribisha Newcastle United. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...