Sunday, June 23, 2013
ASKOFU AITAKA SERIKALI KUWABANA WASIOTAKA NCHI ITAWALIKE.
RAIS
Jakaya Kiwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa
serikali na dini wakati alipohudhuria sherehe za miaka 25 ya Askofu wa
jimbo kuu la Morogoro Telesphol Mkude wa pili kulia kwa rais katika
viwanja vya shule ya ST Peter mkoani Morogoro jana.
SIKU
chache baada ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutaka Serikali iachwe ifanye
kazi yake katika kudhibiti vurugu zinazoibuka kila kukicha, Askofu wa
Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro, Mhashamu Telesphor Mkude naye
ameitaka Serikali kuwadhibiti wote wasiotaka nchi itawalike.Askofu huyo amesema kuonya pekee hakusaidii, bali inawajibu wa kuwachukulia hatua kali ili kukomesha vitendo vinavyotishia amani nchini.Askofu
Mkude aliyasema hayo jana wakati wa maadhimisho ya Jubilei ya miaka 25
ya uaskofu wake kwenye viwanja vya Seminari ya Mtakatifu Petro mjini
hapa ambapo Rais Jakaya Kikwete alikuwa miongoni mwa wageni mashuhuri
waliohudhuria.
RIHANNA AMPIGA SHABIKI WAKE NA KIPAZA SAUTA BAADA YA SHABAKI HUYO KUMKERA...!!!

MWIMBAJI nyota wa muziki wa R&B, Robyn Rihanna Fenty, anayefahamika zaidi kwa jina la Rihanna, amenaswa na kamera akimpiga shabiki ‘mic’ usoni alipokuwa akifanya shoo huko Birmingham, Uingereza Jumatatu iliyopita.
Rihanna alifanya tukio hilo la kushtua alipojichanganya kwenye umati wa mashabiki, huku akiimba kwenye shoo hiyo ambayo ni sehemu ya ziara yake ya dunia inayojulikana kama ‘Diamond World Tour’ akiitangaza albamu yake ya saba ya ‘Unapologetic’ iliyotoka mwaka jana.
Ilidaiwa kuwa Rihanna mwenye umri wa miaka 25 alishindwa kudhibiti hasira zake baada ya shabiki huyo asiyefahamika kumng’ang’ania mkono wake.
Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo aliandika kwenye ukurusa wake wa Twitter: "Rihanna amempiga mtu mmoja na mic yake katika ajali haha oops."
Na Rihanna alijibu akisema kuwa alikusudia kumpiga shabiki huyo kwa sababu alikuwa akimzuia.
TAMASHA LA KILI MUSIC AWARDS NDANI YA UWANJA WA JAMHURI DODOMA.....OMMY DIMPOZ APIGWA CHUPA NA MASHABIKI JUKWAANI..!!
Ommy
dimpoz arushiwa chupa na mawe jukwaaani dodoma na kushindwa kufanya
show ya kilimanjaro muzik award dodoma. Wadau wa dom wasema kamwe msanii
yoyote atakaye mdisi msanii wa dodoma awatamkubari kufanya show dom na
watamshusha jukwaani kama walivyo fanya leo

Msanii
wa Muziki wa Kizazi Kipya,Linex akiwasalimia mashabiki na wapenzi wa
Muziki waliofurika kwa wingi ndani ya Uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma
leo,ambapo usiku huu kulikuwa na bonge moja la Show ya Kilimanjaro
Tanzania Music Tour 2013.

Msanii Ben Pol akighani moja ya nyimbo zake.

POLISI 7 WAFUNGWA JELA MIAKA 5 KWA KOSA LA MAUAJI HUKO KIGOMA
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Tabora imewahukumu kifungo cha miaka mitano jela askari saba wa Jeshi la Polisi mkoani Kigoma ambao walikuwa wakishtakiwa kwa mauaji.
Akitoa
hukumu yake katika kikao cha Mahakama Kuu kilichokuwa kikifanyika
mkoani Kigoma Jaji wa mahakama hiyo, Sam Mpaya Rumanyika alisema kuwa
baada ya kupitia ushahidi mbalimbali Mahakama hiyo imewatia hatiani
askari hao kwa kosa la kuua bila kukusudia.
Katika
kesi hiyo namba 35 ya mwaka 2012 washitakiwa hao walifikishwa
mahakamani hapo na kusomewa shitaka la kumuua Festo Stephano, mkulima wa
kijiji cha Rungwe Mpya Wilaya ya Kasulu mkoani hapa katika tukio
lililotokea Agosti 6, mwaka 2011.
Askari
hao waliohukumiwa ni pamoja na Baraka Hongdi, Koplo Mawazo, Koplo
Swahib, D/C Charles, D/C Shamsi, D/C Jerry na D/C Amrani ambao kwa
pamoja walikana shitaka lao katika kesi hiyo namba 35 ya mwaka 2012.
Akitoa
utetezi kabla ya hukumu hiyo wakili wa washitakiwa, Method Kabuguzi
aliiomba Mahakama kuwafutia shitaka washitakiwa hao na kuwaachia huru
kwani wote bado vijana na wameoa hivi karibuni.
Sambamba
na hilo Kabuguzi alisema kuwa askari hao walikumbwa na mkasa huo wakati
wakitekeleza jukumu lao la ulinzi wa taifa ambapo walimkamata mtuhumiwa
wa kutumia silaha na ndipo kifo kikatokea wakati wakitekeleza majukumu
yao.
Source: http://www.wavuti.com
AMANDA APIMA NGOMA, PRESHA YAPANDA YASHUKA

Stori:Gladness Mallya
MSANII
wa filamu za Kibongo, Tamrina Poshi ‘Amanda’ hivi karibuni alijikuta
akipandwa na kushukwa na presha mara baada ya kwenda hospitali kupimwa
Ugonjwa wa Ukimwi.Kikizungumza na Exclusive chanzo makini ambacho
kilishuhudia tukio zima katika Hospitali ya Dokta Mvungi, Kinondoni,
jijini Dar kilisema baada ya Amanda kupewa majibu ya vipimo na daktari,
alianza kuhaha huku na kule kama mtu aliyechanganyikiwa, kisha presha
ikampanda baadaye ikashuka.

Baada ya kuzinyaka habari hizo, paparazi wetu alimtafuta Amanda na kumuuliza juu ya tukio hilo ambapo bila hiyana alitiririka:
“Ile
ilikuwa ni mara ya tatu kupima ngoma yaani wakati nikisubiri majibu,
presha ilipanda ghafla mpaka daktari akawa na wakati mgumu wa kunipa
majibu.

“Nilienda
kuchukua majibu na sikutaka kuyaangalia, nilimpelekea daktari ambaye
aliniambia niko safi yaani sikuamini nilitoka nikiwa naongea peke yangu,
nilikuwa sijiamini si unajua tena ujana ni maji ya moto sasa presha ,”
alisema Amanda.
Saturday, June 22, 2013
HATIMAE NDUGU YETU MPENDWA CHARLES HILILA AZIKWA LEO KIJIJINI KWAO


NYUMBA YA MILELE ALIMOLALA MWANDISHI WA HABARI KITUO CHA MATANGAZO CHA CHANELL TEN
Habari Na Steven KanyephMwili wa aliyekuwa mwandishi wa habari wa chaneli ten Charles hilila umezikwa leo katika makaburi ya nyumbani kwao katika kijiji cha Dumida kata ya Tinde mkoani Shinyanga nakuhudhuriwa na mamia ya waombolezaji akiwemo mkuu wa mkoa wa shinyanga na viongozi wengine wa kiserikali , vyama vya siasa pamoja na viongozi wa kidini.
Mazishi hayo yametanguliwa na ibada ya misa takatifu iliofanyika katika kanisa la mama mwenye huruma Ngokolo mjini Shinyangsa na baade kufuatiwa na ibada ya mazishi iliyofanyika nyumbani kwao na kuongozwa na padre Emmanueli Makolo akisaidiana na padri Josephati Mahalu kabla ya maziko.
katika mahubiri padre Mahalu amewaasa wanajamii kudumisha upendo na kuwakumbusha kuwa kifo kipo mahali popote hivyo wanajamii wanapaswa kumrudia Mungu na kutenda matendo mazuri yenye kuleta amani na yanayompendeza Mungu.
Hali kadhalika mkuu wa mkoa wa Shinyanga Alli Nassoro Lufunga ametoa salamu za rambirambi kutoka katika serikali ya mkoa na kuwaomba wanahabari kudumisha upendo zaidi hasa katika umojawao kwani utawasaidia kufanya kazi kwa weledi na kuleta tija zaidi kwa wanajamii.
Marehemu Charles hilila amefariki juni 19 katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa TB ya mifupa uliokuwa unamsumbua .
Aidha marehemu ameacha mjane na watoto watatu ,
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema mbinguni amina
*********************************************************************************
MEYA AZIMIA BAADA YA KUPIGWA NA POLISI
Meya wa Mji Mkuu wa Kampala nchini Uganda akiwa chini ya ulinzi wa polisi baada ya kukamatwa kwa tuhumza za kusababisha vurugu.Kampala, Uganda. Watu wawili wameuawa kwa risasi nchini Uganda juzi, wakiwa katika mkusanyiko kwenye eneo la soko la Kisekka.
Meya wa mji mkuu wa Uganda, Kampala, Erias Lukwago, pia alizirai baada ya kupigwa na polisi hao waliofyatua risasi za mipira kuutawanya umati wa wafuasi wake.
Akiwa kitandani, Meya huyo amesema baada ya kupata kipigo hicho alipoteza fahamu na kukimbizwa hospitalini.
“Bomu ambalo lilinifanya nipoteze fahamu lilirushwa katika gari langu na kuingia ndani,” amesema.
Meya huyo ni mpinzani wa rais wa nchi hiyo, Yoweri Museveni, alieleza kwamba maofisa wa polisi walimpiga kifuani na kuzirarua nguo zake wakimtuhumu kwa kuchochea ghasia.
NKAMIA AZUA VURUGU TENA BUNGENI SAFARI HII ATAKA KUMPIGA MBUNGE MWENZAKE...!!!
Mbunge
wa Kondoa Kusini, Juma Nkamia (CCM), kwa mara nyingine ameingia katika
kashfa nzito akituhumiwa kutaka kumpiga Mbunge wa Viti Maalumu CUF, Moza
Abeid ndani ya Ukumbi wa Bunge.
Tukio hilo
lilitokea mwanzoni mwa wiki ambapo imeelezwa kuwa Nkamia mbali na kutaka
kumpiga mbunge huyo, pia alimtolea matusi mazito ya nguoni (gazeti hili
haliwezi kuandika).
Kwa mara ya
kwanza mbunge huyo aliingia katika kashfa baada ya kutoa kauli bungeni
kuwa hazungumzi na mbwa, bali anazungumza na mwenye mbwa kabla ya
kuingia katika mzozo na wahariri na baraza la habari aliposema kuwa
Jukwaa la Wahariri na Baraza la Habari ni NGOs za kutafuta fedha.
Uchunguzi wa
Mwananchi ambao umethibitishwa na Nkamia mwenyewe umebaini kuwa chanzo
cha tukio hilo ni kutokana na kuzomewa kwa Nkamia katika kampeni za
uchaguzi mdogo Kata ya Dalai Wilaya ya Chemba.
Kwa mujibu wa
wabunge mashuhuda ambao waliliona tukio hilo, ilielezwa kuwa Nkamia,
ambaye pia ni mwandishi wa habari, alianza kumshushia matusi Moza wakiwa
ndani ya Bunge hadi walipotoka nje alimfuata na kutaka kumpiga.
MCHUNGAJI AZAA NA HAUSIGELI WA MIAKA 17 HUKO KIMARA....AVULIWA UCHUNGAJI, MKEWE AOMBA TALAKA...!!!
HAYA
ni madai mazito! Mchungaji wa Kanisa la Kiroho la Kijito cha Utakaso
au Healing Centre International lililopo Kimara-Mwisho, Dar, Thomas
Mariki anadaiwa kuvuliwa kofia ya uchungaji baada ya kutuhumiwa kuzaa
na ‘hausigeli’ wake, Sessy Mwambashi.
Akizungumza nasi Jumamosi kwa masikitiko, mke wa ndoa wa Mariki, Joyce Thomas Mariki alidai kuwa yeye na mchungaji huyo walioana mwaka 2004 katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Lungai Mwika, Moshi.
Alisema walijaliwa kupata watoto watatu lakini mmoja hakuwa bahati.
MATESO YAANZA
Mwanamke huyo alidai amani katika ndoa yake ilipotea baada ya kujifungua mtoto wa pili (marehemu), mumewe alianza kumtuhumu kuwa alitoka nje ya ndoa na huyo mtoto hakuwa wake.

Akizungumza nasi Jumamosi kwa masikitiko, mke wa ndoa wa Mariki, Joyce Thomas Mariki alidai kuwa yeye na mchungaji huyo walioana mwaka 2004 katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Lungai Mwika, Moshi.
Alisema walijaliwa kupata watoto watatu lakini mmoja hakuwa bahati.
MATESO YAANZA
Mwanamke huyo alidai amani katika ndoa yake ilipotea baada ya kujifungua mtoto wa pili (marehemu), mumewe alianza kumtuhumu kuwa alitoka nje ya ndoa na huyo mtoto hakuwa wake.
MIMBA YA PENNY YACHOROPOKA..... PENZI LAKE NA DIAMOND LAKAA PABAYA...!!!
TAARIFA
ya ndani zinazodai kwamba, mimba ya mchumba wa Mwanamuziki wa Bongo
Fleva, Nassibu Abdul ‘Diamond’, Peniel Mgilwa ‘Penny’ imechoropoka
zimevujaKwa mujibu wa chanzo makini kilichojitambulisha kwa jina la wifi
(jina kapuni) kwa Penny, ni kwamba mtangazaji huyo wa Runinga ya
Channel 10 cha jijini Dar hivi sasa hana ujauzito tena kama wengi
wanavyodhani.
“Penny hana mimba jamani, yupo fiti kabisa na sidhani hata kama anatarajia kushika ujauzito leo wala kesho,” kilisema chanzo hicho.
“Penny hana mimba jamani, yupo fiti kabisa na sidhani hata kama anatarajia kushika ujauzito leo wala kesho,” kilisema chanzo hicho.
Hata
hivyo, wifi huyo alisema kwamba awali kulikuwa na dalili zilizoonesha
kwamba Penny alikuwa ni mjamzito kutokana na mtangazaji huyo kutumia
vitu vichachu kama vile maembe na mara kwa mara alikuwa akiumwa hadi
kufikia kulazwa hospitali.
Inadaiwa kwamba Penny alipotoka hospitali alionekana kuwa fiti zaidi na hakuwa na dalili zozote za kuwa na ujauzito kama ilivyokuwa siku za nyuma.
Baada ya gazeti hili kupata habari hizo lililimpigia simu Penny ili kuthibitisha madai hayo:
Inadaiwa kwamba Penny alipotoka hospitali alionekana kuwa fiti zaidi na hakuwa na dalili zozote za kuwa na ujauzito kama ilivyokuwa siku za nyuma.
Baada ya gazeti hili kupata habari hizo lililimpigia simu Penny ili kuthibitisha madai hayo:
Mwandishi: Mambo vipi, Penny pole sana.
Penny: Pole ya nini sasa?
Penny: Pole ya nini sasa?
Mwandishi: Si nimesikia kwamba unaumwa jamani na ukakumbwa na mkasa mwingine?
Penny: Mkasa gani huo unaousema maana mimi niko fiti tu.
Penny: Mkasa gani huo unaousema maana mimi niko fiti tu.
Mwandishi: Nilisikia kwamba baada ya kuumwa na kulazwa hopsitali mimba yako ikatoka?
Penny: (Kimya kwa dakika 3) Asante ni mipango ya Mungu.
Penny: (Kimya kwa dakika 3) Asante ni mipango ya Mungu.
Mwandishi: Sasa unatarajia lini utapata tena mimba nyingine?
Penny :(Kwachuuuuuu). Simu ilikatwa na hata ilipokuwa ikipigwa tena haikuwa ikipokelewa.
Penny :(Kwachuuuuuu). Simu ilikatwa na hata ilipokuwa ikipigwa tena haikuwa ikipokelewa.
ANGALIA PICHA ZA BOB JUNIOR AKIPEWA KICHAPO LOCATION...!!!



Bob Junior akiwa location kushoot video yake mpya, duuuuuuh...!!! kaaazi kweli kwelii
BOMU LA ARUSHA LAWATESA CCM, POLISI.
IGP SAIDI MWEMA.
KATIBU MKUU MPYA WA CCM ABDULRAHMAN KINANA.
MLIPUKO wa bomu uliotokea wiki iliyopita katika mkutano wa kufunga kampeni za udiwani kwa CHADEMA mkoani Arusha na kuua watu wanne, umeiweka kwenye wakati mgumu serikali ya CCM, Jeshi la Polisi na Bunge.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alisema juzi bomu lililolipuliwa katika mkutano wa CHADEMA ni la kijeshi na limetengenezwa China na uzoefu unaonesha hutumiwa na wanajeshi kujihami wakiwa katika makabiliano na maadui vitani.
Wakati Pinda akitoa kauli hiyo bungeni, viongozi wa CHADEMA wamelihusisha Jeshi la Polisi na tukio hilo huku wakidai wanao ushahidi unaon
esha askari aliyevalia sare akilirusha kwenye mkutano huo.
Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kijamii, wamelidokeza Tanzania Daima kuwa kukiri kwa serikali kuwa bomu hilo limetengenezwa China, inapaswa iibane nchi hiyo ieleze iliyemuuzia na alivyoliingiza nchini.
“Kwanini isiundwe tume huru nchini ili nchi ya China iulizwe baada ya kutengeneza bomu hilo ilimuuzia nani? Na kama haikuiuzia serikali, basi ni dhahiri tuiulize China kwanini inafadhili vikundi vya kigaidi nchini kwetu ?.
NASSARI: WAZIRI MKUU MSTAFU EDWARD LOWASSA ANAHUSIKA KUNIPIGA.
Mbunge wa Arumeru Mashariki(Chadema) Joshua Nassari akiwa amelazwa katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (Moi), jana, baada ya kuhamishwa kutoka Arusha kwa ajili ya kupata matibabu zaidi baada ya kuumizwa kwenye vurugu za uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Makuyuni mkoani Arusha.Picha na Silvan Kiwale.
DAR ES SALAAM.
MBUNGE wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari amemtuhumu Mbunge wa Monduli Edward Lowassa kwamba anahusika na kipigo alichokipata kutokana na chuki aliyonayo kwake.
MBUNGE wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari amemtuhumu Mbunge wa Monduli Edward Lowassa kwamba anahusika na kipigo alichokipata kutokana na chuki aliyonayo kwake.
Aidha
amemtuhumu Spika wa Bunge, Anne Makinda kwamba naye ni miongoni mwa
watu wanaomchukia pamoja na viongozi wengine wa Bunge, kwa kuwa hakuna
kati yao aliyempigia simu au kumtumia ujumbe wa kumjulia hali kutokana
na kipigo alichopata ambacho kimemsababishia maumivu makali.
Akizungumza jana akiwa kwenye chumba alicholazwa katika Taasisi ya Tiba ya Magonjwa ya Mifupa
na Ufahamu Muhimbili (Moi), Nassari alidai Lowassa ambaye amewahi kuwa
waziri mkuu kabla ya kujiuzulu, amemchukia tangu alipomshinda mkwewe
Sioi Sumari, kwenye uchaguzi mdogo wa ubunge uliofanyika Aprili mwaka
jana.
Nassari
aliyekuwa amelazwa katika Hospitali ya Selian ya jijini Arusha kabla
ya kuhamishiwa MOI, alidai kupigwa na kuchaniwa nguo na Green Guard
wakati alipokuwa katika jitihada zake za kuhesabu kura kwenye uchaguzi
wa udiwani wa Kata ya Makuyuni-Monduli.
Friday, June 21, 2013
Mbunge wa Arumeru Mashariki-Chadema, Joshua Nassari Anendelea Vyema na Matibabu katika hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam
Mbunge
wa Arumeru Mashariki-Chadema, Joshua Nassari akionesha simu yake ya
mkononi iliyokuwa na matukio ya tukio la kufavamiwa kwake.
Mbunge
wa Arumeru Mashariki-Chadema, Joshua Nassari akiwa katika hospitali ya
Taifa muhimbili jijini Dar es Salaam jana akipata matibabu baada ya
kushambuliwa na watu wasiojulikana wakati wa mkutano wa kampeni za
udiwani jijini Arusha.
Mbunge wa Vunjo-TLP, Mh. Agustino Lyatonga Mrema akimjulia hali mbunge wa Arumeru Mashariki-Chadema, Joshua Nassari.
HII NDIO HISTORIA YA MWANDISHI WA HABARI WA CHANNEL TEN ALIYEFARIKI DUNIAI JUZI
Marehemu CHARLES HILILA
Na Mwandishi Wetu Steven Kanyeph
Mwili wa aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha matangazo cha
television cha chanel ten mkoani Shinyanga, CHARLES HILILA
unatarajiwa kuzikwa kesho katika kijiji cha tinde alikozaliwa. Mazishi hayo yatatanguliwa na ibada itayofanyika katika kanisa la mama mwenye huruma la ngokolo mjini shinyanga, ibada inayotarajiwa kufanyika saa nne kamili asubuhi ambayo itakwenda sambamba zoezi la kuaga mwili wa marehemu.
Taarifa kutoka familia ya marehemu HILILA zinasema kuwa baada ya ibada ya mazishi msafara utaelekea katika kijiji cha tinde kwaajiri ya mazishi. Marehemu CHARLES HILILA alizaliwa tarehe 15 mwezi wa 9 mwaka 1964 katika kijiji cha tinde mkoani shinyanga na ni mtoto wa tatu kati ya watoto wanne katika familia ya bwana na bibi BARTHOROMEO HILILA wa kijiji cha mishepo-mwamtini wilaya ya shinyanga.
SERIKALI YA MKOA WA SHINYANGA YATOA TAKWIMU YA UFAULU KWA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI
Afisa elimu mkoa wa Shinyanga Bi. Eva M. Lopa
Na Steven KanyephAfisa elimu mkoa wa Shinyanga Bi. Eva M. Lopa ametoa takwimu ya ufaulu kwa elimu ya msingi na sekondari kwa muda wa miaka mitatu kwa mkoa wa shinyanga katika kikao cha taarifa ya elimu kwa mkoa wa Shinyanga kilichofanyika katika ukumbi wa Mkoa uliopo mkoani Shinyanga , siku ya jana.
Akitoa takwimu hizo kwa elimu ya msingi Bi. Lopa amesema kuwa matokeo ya elimu ya msingi yamekuwa ya yakipanda mwaka hadi mwaka , na kwa mwaka 2010 yalikuwa ni asilimia 42.5 wakati mwaka 2009 yalikuwa asilimia 31.9 mwaka 2011 matokeo yalikuwa asilimia 44.2 hivyo kuwepo na ongezeko la asilimia 1.7% kwa mwaka 2009 hadi 2011 wakati mwaka 2012 wanafunzi waliofauru ni asilimia 56.1% sawa na ong ezeko la asilimia 11.9
Afisa elimu huyo ameainisha sababu zilizopelekea ongezeko la ufaulu huo kwa mwaka 2012 kwa elimu ya msingi kwa mkoa wa Shinyanga kuwa ni pamoja na ufuatiliaji wa karibu wa viongozi wa elimu ngazi za wilaya na mkoa , ufuatiliaji wa ufundisha ji, ongezeko la walimu kutoka uwiano wa 1.74 hadi 1.54 na ongezeko la vitabu kwa wanafunzi kutoka uwiano wa f1.6 hadi 1.4
RAIS MSTAAFU WA MAREKANI GEORGE W BUSH KUTUA JIJINI DAR ES SALAAM MWEZI UJAO..!!

Rais mstaafu wa Marekani, George W. Bush na mkewe, Laura, wanatarajiwa kuwasili nchini mwezi ujao ambapo watahutubia kongamano litakalojadili wajibu wa wake za marais katika kuinua wanawake duniani.
Taasisi ya George Bush ndiyo imeandaa kongamano hilo litakalofanyika Dar es Salaam kuanzia Julai 2 hadi 3.
Taarifa iliyotolewa jana na taasisi hiyo kwa vyombo vya habari, ilisema kongamano hilo, litahudhuriwa pia na mke wa Rais Barack Obama wa Marekani, Michelle na muasisi wa Taasisi ya Wanawake ya Cherie, Cherie Blair ambaye ni mke wa Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Tony Blair.
Wake wengine wa marais wa Afrika watakaohudhuria ni Mama Salma Kikwete, Chantal Campaore wa Burkina Faso, Roman Tesfaye wa Ethiopia, Maria da Luz Dai Guebuza (Msumbiji), Penehupifo Pohamba (Namibia), Sia Nyama Koroma (Sierra Leone), Janet Museveni (Uganda) na Christine Kaseba wa Zambia.
Kongamano hilo litajikita zaidi katika kujadili masuala ya kuwekeza kwa wake, kuimarisha Afrika lakini pia wajibu wa wake za marais kuhamasisha wanawake katika maeneo ya elimu, afya na kuwakwamua kiuchumi.
Taasisi ya George Bush ndiyo imeandaa kongamano hilo litakalofanyika Dar es Salaam kuanzia Julai 2 hadi 3.
Taarifa iliyotolewa jana na taasisi hiyo kwa vyombo vya habari, ilisema kongamano hilo, litahudhuriwa pia na mke wa Rais Barack Obama wa Marekani, Michelle na muasisi wa Taasisi ya Wanawake ya Cherie, Cherie Blair ambaye ni mke wa Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Tony Blair.
Wake wengine wa marais wa Afrika watakaohudhuria ni Mama Salma Kikwete, Chantal Campaore wa Burkina Faso, Roman Tesfaye wa Ethiopia, Maria da Luz Dai Guebuza (Msumbiji), Penehupifo Pohamba (Namibia), Sia Nyama Koroma (Sierra Leone), Janet Museveni (Uganda) na Christine Kaseba wa Zambia.
Kongamano hilo litajikita zaidi katika kujadili masuala ya kuwekeza kwa wake, kuimarisha Afrika lakini pia wajibu wa wake za marais kuhamasisha wanawake katika maeneo ya elimu, afya na kuwakwamua kiuchumi.
MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU UDSM APIGWA RISASI YA TUMBO USIKU WA KUAMKIA LEO HUKO YOMBO..!!

Taarifa zilizotufikia katika chumba cha habari zinaeleza kuwa wanafunzi wanne wa chuo kikuu cha Dar es salaam maarufu kwa jina la Chuo cha Mlimani wamevamiwa na majambazi usiku wa kuamkia leo maeneo ya Yombo chuoni hapo.Wanafunzi hao wanaosemekana kuwa ni wa mwaka wa nne na wa mwisho wa masomo walikuwa wanajisomea na kuandaa “Disertation” zao na kujikuta wakivamiwa na watu wanne na kuamuriwa watoe komputa zao na pochi za fedha. Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii kutoka chuoni hapo, wanafunzi hao walikubali kuwapa komputa hizo na pochi za fedha, na majambazi kuanza safari yao.
Baadaye wanafunzi hao wakawaomba wapate hata nakala (Soft Copy) ya vitu vyao, na ndipo mmoja wao akaamua kuwafuata na kukumbana na risasi tumboni. Mwanafunzi huyo baada ya kupigwa risasi alianguka chini na kugaagaa chini huku akikosa msaada wa kupelekwa Hospitalini.
AUNTY LULU..... "MAZISHI YANGU WATAJAA MASHOGA NA WATOTO TU"
MSANII
wa filamu Bongo, Lulu Mathias ‘Aunty Lulu’ amefunguka kuwa siku akifa
anaamini mbali na watu wengine mazishi yake yatatawaliwa na mashoga
pamoja na watoto

Akizungumza na paparazi wetu hivi karibuni, Aunty Lulu alisema kutokana na ukweli kwamba wengi wanaompenda na ambao wamemzoea ni watoto waliokuwa wakimsikiliza kwenye Kipindi cha Watoto Shoo kupitia Radio One na ITV na mashoga ambao awali alikuwa kama mama yao, hao ndiyo watakaojaa kwenye mazishi yake.
Alisema sababu kubwa ya msiba wake kujaa mashoga wengi ni kwa kuwa kabla hajabadili mfumo wa maisha anayoishi sasa, alikuwa akiwalea hivyo siku ya mazishi lazima wakumbuke fadhila.
“Unajua kufa ni kama kulala, naamini siku ya mazishi yangu watakaokuwa wengi ni watoto pamoja na mashoga ambao zamani nilikuwa mama yao, wengine ni waandishi na wasanii mbalimbali wa filamu na muziki,”alisema Aunty Lulu.

Akizungumza na paparazi wetu hivi karibuni, Aunty Lulu alisema kutokana na ukweli kwamba wengi wanaompenda na ambao wamemzoea ni watoto waliokuwa wakimsikiliza kwenye Kipindi cha Watoto Shoo kupitia Radio One na ITV na mashoga ambao awali alikuwa kama mama yao, hao ndiyo watakaojaa kwenye mazishi yake.
Alisema sababu kubwa ya msiba wake kujaa mashoga wengi ni kwa kuwa kabla hajabadili mfumo wa maisha anayoishi sasa, alikuwa akiwalea hivyo siku ya mazishi lazima wakumbuke fadhila.
“Unajua kufa ni kama kulala, naamini siku ya mazishi yangu watakaokuwa wengi ni watoto pamoja na mashoga ambao zamani nilikuwa mama yao, wengine ni waandishi na wasanii mbalimbali wa filamu na muziki,”alisema Aunty Lulu.
WEMA SEPETU NA KAJALA MASANJA WAGEUKA "PAKA NA CHUI "....ZILE MILIONI 13 ZALETA BALAA ZITO
Utabiri wa wengi kuwa ushosti wa waigizaji masistaduu wa Bongo Movies, Wema Isaac Sepetu na Kajala Masanja kutumbukia nyongo unadaiwa kutimia na sasa wametibuana,
Habari za ndani kutoka kwa mtu wa karibu (jina linahifadhiwa), mwanzoni baada ya Wema kumlipia Kajala faini ya Sh. milioni 13 na kumnusuru kutokwenda Segerea a.k.a Segedansi, wawili hao walikuwa marafiki kama pete na kidole.
“Walishinda wote, walilala wote, walikwenda klabu wote yaani Kajala alikuwa anamnyenyekea ‘madam’ Wema kwa kumuepusha na kifungo cha miaka 7 jela,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:

“Kabla hajaenda Mwanza kwa ajili ya mapumziko kwa bibi zake, nilimsikia Kajala akilalama kuwa madam aliamka siku moja akawa amemchunia, unaambiwa hata salamu ikawa hakuna. “Hapo ndipo maneno ya pembeni yakaanza kwa sababu mbali na Kajala, Wema pia ana wapambe wengine na mbali na Wema, Kajala naye ana kampani. Kwa hiyo sosi ya manenomaneno ni hizo kampani zao.
“Ipo siku kabisa Wema alimlalamikia Kajala hadharani kuwa amekuwa akimsema vibaya kwa watu.
“Yale maneno yalimuuma sana Kajala, ikabidi arudi nyumbani kwao lakini akawa anaogopa kumwambia mama yake kuwa ametibuana na Wema hadi alipotimkia Mwanza.
“Lakini kabla ya hii ishu ya kulaumiana, kipindi cha nyuma kidogo Kajala alipata dili la kwenda kurekodi filamu nchini China na mastaa wengine lakini ikadaiwa kuwa Wema alichomoa hivyo mwigizaji huyo hakwenda pamoja na kwamba alishapewa baraka zote na baba yake.
MABONDIA WANNE WA TANZANIA WAFUNGWA JELA MIAKA 15 BAADA YA KUNASWA NA MADAWA YA KULEVYA NCHINI MAURITIUS

Mabondia wanne wa Tanzania wafungwa miaka 15 jela nchini Mauritius kwa makosa ya kuingiza dawa za kulevya aina ya heroin.
Mabondia hao ni Case Ramadhani Fills, Nathanael Elia Charles, Ally Rajabu Msengwa na Petro Charles Mtagwa.
Wakati kesi hiyo ilipoanza kusikilizwa, wote walikiri makosa ya kuingiza mihadarati hiyo nchini Mauritius wakati walipokwenda kushiriki mashindano ya ndondi barani Afrika mwaka 2008.
Wakiwa mbele ya Jaji, waliiambia mahakama kuwa walilazimika kuingia katika biashara hiyo haramu kutokana na hali zao za maisha kuwa maskini.
"Tunaomba radhi kwa taifa la Mauritius", waliiambia mahakama.
"Tu watu maskini na tunategemewa na familia, watoto na wazee wetu wanaotugemea. "Kwa dawa hizi tungepata kiasi cha Pauni £4,000". walisema
Jaji Benjamin Marie Joseph alisema katika kutoa adhabu hiyo yote hayo ameyafikiria, kwani walitoa ushirikiano mzuri wakati wote wa uchunguzi wa kesi hiyo, kulikowezesha hata wafanyabiashara hiyo, raia wa Mauritius kukamatwa.
Wamekuwa mahabusu kwa siku 1,722, sawa na miaka miatano, hivyo watatumikia miaka kumi iliyobakia jela. Pia watatakiwa kulipa faini ya pauni £1,600 na gharama nyingine za uendeshaji wa kesi hiyo.
Kwa mujibu wa mwandishi wa habari wa BBC nchini Mauritius Yasine Mohabuth in Mauritius, Jaji aliwashutumu kwa kuukosea umma wa Mauritius kwa kuingiza dawa hizo za kulevya aina ya heroin.
Mabondia hao waliwasili Mauritius tarehe 10 Juni 2008 na kuweza kupita uwanja wa ndege bila kunaswa hadi walipokamatwa katika hoteli waliyofikia ya Quatre Bornes.
Kwa pamoja walimeza gram 4639.04 za heroin zikiwa katika vifuko 358 vijulikavyo kama pipi.
Thursday, June 20, 2013
MAMA LANGA.... "NINGEKUWEPO TANZANIA MWANANGU ASINGEKUFA HARAKA"

MAMA wa marehemu Langa Kileo, Vanessa Kimei amefungua kinywa chake na kusema kifo ni mipango ya Mungu lakini kama angekuwepo nyumbani kwake Mikocheni, Dar, mwanaye asingekufa haraka kiasi hicho.Akizungumza na Amani hivi karibuni, Mama Langa alisema wakati mwanaye alipoanza kuugua hadi kupatwa na umauti Juni 13, mwaka huu, yeye alikuwa safarini nchini Marekani kumuona mwanaye mwingine aliyekuwa amejifungua.
“Wakati mwanangu ameanza kuumwa sikuwepo, nilikuwa safarini Marekani nilikoenda kumuona mwanangu wa kike aliyekuwa amejifungua, kwa mila za kwetu ni lazima mama kwenda kumuogesha mtoto lakini ningekuwepo mwanangu asingeondoka jamani,’’ alisema mama Langa.
Akifafanua kauli yake, mama huyo alibainisha kuwa kipindi alipokuwa akiishi na mwanaye kabla hajasafiri, mara nyingi alikuwa akimhudumia alipokuwa akiumwa hivyo hata katika ugonjwa uliosababisha mauti yake basi angeweza kumtibu yeye mwenyewe.
Alisema kuwa wakati mwingine alikuwa akimuwekea hadi dripu za dawa akiwa pale nyumbani na kunusuru maisha ya mwanaye lakini ghafla kifo kimetokea wakati yeye hayupo.
“Nilikuwa namuwekea dripu za dawa mwanangu hapahapa nyumbani, alikuwa anaugua kwa muda na kisha anarudi katika hali ya kawaida,” alisema kwa uchungu mama Langa.
Hata hivyo baadhi ya waombolezaji waliokuwepo msibani walimsihi mama huyo kukubaliana na mipango ya Mungu kwamba kila mwanadamu lazima atakufa, hali iliyompa faraja na kumfanya anyamaze.
Marehemu Langa aliyefariki baada ya kusumbuliwa na kile kilichoelezwa kuwa ni ugonjwa wa malaria kali na homa ya uti wa mgongo, alizikwa Jumatatu iliyopita katika Makaburi ya Kinondoni, Dar.
MWANDISHI WA HABARI WA CHANNEL TEN AFARIKI DUNIA
Na Steven Kanyeph.
Mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha chanel Ten CHARLES HILILA amefariki dunia usiku wa kuamkia jana katika hospital ya Mkoa wa Shinyanga.
Marehemu Charles Hilila alilazwa katika hospital ya mkoa tarehe kumi mwezi june mwaka huu akisumbuliwa na maradhi ya TB ya mifupa ambapo tarehe kumi na sita mwezi huu alihamishiwa chumba cha wagonjwa mahututi mpaka mauti yalipomchukua .
Kwa mujibu wa mke wa marehemu amesema kuwa mazishi yatafanyika katika kijiji cha Jomu Tinde mahali alipozaliwa marehemu yakitanguliwa na misa takatifu ya mazishi itakayofanyika katika kanisa kuu la mama mwenye huruma la Ngokolo mjini Shinyanga.
Marehemu Hilila ameacha mjane mmoja na watoto watatu, wakike mmoja na wakiume wawili.
Marehemu Hilila enzi za uhai wake alifanya kazi katika kituo cha televisheni cha chanel Ten lakini aliwahi kufanya kazi katika kituo cha matangazo cha radio Faraja. Mungu alaze roho ya marehemu mahala pema peponi. Amina.
Subscribe to:
Comments (Atom)














