
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe
Siku moja baada ya Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutangaza kumvua uanachama, Mbunge wa
Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe kesho atatua jimboni kwake kuzungumza na
wananchi kupitia mikutano ya hadhara.
Uamuzi wa kumfukuza Zitto (pichani) ulifikiwa juzi
ikiwa ni muda mfupi baada ya Mahakama Kuu kutupilia mbali kesi
aliyofungua Januari 2, 2014, dhidi ya Bodi ya Wadhamini na katibu mkuu
wa Chadema, iliyokuwa imeshikilia uanachama wake.
Mwanasheria mkuu wa Chadema, Tundu Lissu ndiye
alitangaza kutimuliwa kwa Zitto akisema ni kutokana na kufungua kesi
mahakamani, kinyume na Katiba ya Chadema kipengele cha 8 (a) (x). Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.




















.jpg)








