Thursday, March 12, 2015

UMOJA WA MATAIFA WALAUMIWA KUHUSU SYRIA

Hali ya uharibifu nchini Syria
Ripoti ya mashirika zaidi ya ishirini ya misaada ya kibinadamu na yale ya kutetea haki za binaadamu yamelishutumu Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kushindwa kutetea raia walio katikati ya vita nchini Syria.
Ripoti hiyo imezishutumu nchi zenye nguvu kubwa ya ushawishi duniani kwa kushindwa kutumia nguvu zao kuandaa maazimio ya kusaidia uhuru wa huduma za misaada ya kibinadamu kwa waathirika.
Ripoti ya masharika hayo ni ya kuadhimisha miaka minne ya vita nchini Syria ambavyo vinaendelea hadi hivi sasa.
David Milband ambaye ni Rais wa Shirika la kimataifa la Uokoaji International Rescue Committee amesema kuna ongezeko dogo la misaada inayotolewa kuwasaidia raia wa Syria. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...