Wednesday, March 11, 2015

TAZAMA PICHA ZAIDI ZA AJALI YA BASI LA MAJINJAH LILILOANGUKIWA NA KONTENA ENEO LA CHANGALAWE MAFINGA MKOANI IRINGA...!!!




 Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.


 Miongoni mwa manusura 22 wa ajali ya basi la Majinjah lenye namba za usajili T438 CED wakiwa wamelazwa katika hospitali ya Mkoa Iringa kwa matibabu. Abiria zaidi ya 40 walipoteza maisha katika ajali hiyo.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Barabarani mkoa wa Iringa, Salim Asas Abri (kulia) akiwa na viongozi wengine wakiwajulia hali manusura wa ajali hiyo.
Kontena lilokuwa limepajkiwa katika lori la mizigo Scania namba T 689 APJ, mali ya Cipex Company likiwa limelalia juu ya basi lenye namba za usajili T438 CED, mali ya kampuni ya Majinjah na kusababisha vifo vya watu 42 na wengine kadhaa kujeruhiwa jana katika eneo la Changarawe, nje kidogo ya mji wa Mafinga mkoani Iringa leo.
 Foleni ya magari katika eneo la Changarawe baada ya ajali hiyo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
 
Mkuu  wa  mkoa  wa Iringa Amina Masenza  (wa  pili kulia) akiwa na Kamanda  wa Polisi mkoa wa Iringa  Ramadhan Mungi ,Mwenyekiti wakamati ya  Usalama Barabarani mkoa wa Iringa  Salim Asas Abri (wapili kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya  Mufindi, Mboni Mhita eneo la ajali. 
 
  Hivi ndivyo Basi la Majinjah linavyo onekana mara baada ya kuondoa Lori lilikuwa limekandamiza basi hilo.

 

 Umati wa watu mbalimbali wakiwemo wasafiri wasafiri waliokuwa katika mabasi mengine wakiwa wamejaa kushuhudia Ajali hiyo.


Shughuli za uokoaji zikiwa zinaendelea





Muonekano wa basi la Abiria na Lori yaliyo athirika kwa ajali hiyo.




Mashuhuda


Basi la Abiria likiwa katika Hali mbaya baada ya ajali.


Waokoaji wakiwa wanaendelea kufanya ushirikiano namna ya kuwasaidia watu waliopata ajali hiyo.


Miongoni mwa watu wakiwa wanatazama namna Magari hayo yalivyopata ajali.







 

Askari wa usalama Barabarani wakiwa wanahakikisha watu mbalimbali waliodhurika katika ajali hiyo wanaweza  kupata msaada/huduma kwa haraka.



 Basi lililokuwa limebeba abiria waliokuwa wakitokea Mbeya kuelekea Dar es salaam  lenye namba za usajili T438 CDE likiwa katika hali mbaya.

********
 Watu zaidi ya 40 wanasadikiwa kupoteza na maisha na wengine kadhaa kujeruhiwa vibaya sana katika ajali mbaya iliyotokea mapema leo asubuhi, maeneo ya Changarawe, Mafinga Mkoani Iringa, iliyohusisha lori la mizigo na basi la abiria la kampuni ya Majinjah lililokuwa likitokea Jijini Mbeya kuelekea Jijini Dar es salaam. 

Ajali hiyo imetokea baada ya lori hilo la mizigo lililokuwa likitokea Jijini Dar kuelekea Mbeya kuligonga na kuliangukia basi hilo wakati lililokuwa likikwepa shimo kubwa lililopo katikati ya barabara wakati wakiwa kwenye mwendo walipokuwa wakipishana.

MAJINA YALIYOPATIKANA HADI SASA NI: Baraka Ndone  (dereva), Yahya  Hassan (kondakta), Ester Emanuel, Lusekelo Enock, Jeremia Watson, Digna Solomoni, Frank Chiwango, Luteni Sanga, Teresia Kamingage, Dotto Katuga, Ester Fidelis, Paulina Justine, Mbamba Ipyana, Catherine Mwate, Mwajengo, Ndulile Kasambala, Zera Kasambala, Rebeka Kasambala, Shadrack Msigwa, Mathias Justine, Juliana Bukuku, Cristina Lyimo, Martin Haule na Dominick Mashauri, Omega Mwakasege.

 Wengine ni Ester Willy, Lucy Mtenga, Erick Shitindi, Edwiga Kamiyeye, Frank Mbaula, Mustapher Ramadhani, Kelvin Odubi, Upendo William, Charles Lusenge, Neto Sanga, Pili Vicent, Daniel, Jacob Doketa Iman Mahenge, Juma Sindu, Dk A. Shitindi, Six Erick, Frank Mbaule.

Wengine waliokuwepo katika ajali hiyo wametambuliwa kwa jina moja Amadi, Musa, Elias, Raphael, Hussein na Oswald.

Basi hilo lilianza safari mjini  Mbeya likiwa na abiria 37. Mungu azipokee na kuzilaza mahala pema peponi roho za marehemu wote katika ajali hii na awajaalie kupona kwa haraka majeruhi wote. 

AMEN/ AMINA
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
 

1 comment:

Moence de dony said...

daaaaaaaaaaaaaah poleni sana

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...