Saturday, April 13, 2013
Friday, April 12, 2013
MKE WA MTU ANASWA LIVE AKIFANYA MAPENZI NDANI YA GARI
KUFUATIA
vitendo vya usaliti wa ndoa, uasherati, ufuska na ukiukwaji wa maadili
ya Kitanzania kwa wanandoa, wiki iliyopita Ijumaa iliendelea na
Operesheni Fichua Maovu kwa kuzunguka jijini Dar usiku wa manane na
kunasa tukio la mke wa mtu akifanya uzinzi ndani ya gari.
Kabla ya kufanya operesheni hiyo, waandishi walitaarifiwa kwamba Wilaya ya Kinondoni jijini Dar ndiyo inayoongoza kwa wake na waume za watu kufanya vitendo vya ngono kwenye magari.
Maeneo
yaliyodaiwa kwamba wazinzi hao hupenda kuyatumia ni Coco Beach, Leaders
Club, Mlimani City na sehemu kubwa ya vitongoji vya Sinza na Mwenge,
Dar.
WEMA SEPETU AMFIKISHA POLISI MAMA YAKE MZAZI

NI
kivumbi! Kuna madai kwamba, staa wa Bongo asiyechuja, Wema Sepetu
amemfikisha mama yake, Miriam Sepetu kwenye Kituo cha Polisi Kijitonyama
‘Mabatini’, Dar kwa madai ya kwenda nyumbani kwake na kufanya vurugu
zilizosababisha kuharibika kwa samani mbalimbali....
Kwa mujibu wa chanzo chetu, ishu hiyo ilijiri usiku wa kuamkia Jumatano iliyopita, nyumbani kwa Wema, Kijitonyama, jijini Dar.
Mbali
na mama mtu, wengine waliofikishwa kituoni hapo ni dada mkubwa wa Wema
aitwaye Nuru na kijana aliyefahamika kwa jina moja la Bestizo ambaye
inasemekana ni mshirika mkubwa wa Diamond kwenye masuala ya mtandao wa
msanii huyo.
“Wema
alikuwa nyumbani kwake usiku huo, watuhumiwa hao wakamzukia na kuanza
kumchapa makofi ya ‘kelbu’ ambapo katika mshikemshike huo, baadhi ya
vitu vilivunjika na kumtia hasara staa huyo,” kilisema chanzo.
Haikujulikana
mara moja ni kitu gani kilisababisha mama mzazi huyo, dada mtu na
kijana asiyekuwa ndugu kwenda kwa Wema na kutenda kosa hilo.
Wema
alikwenda polisi na kuandikisha maelezo ambayo yameingizwa kwenye
jalada lenye kumbukumbu; KJN/RB/2755/2013 SHAMBULIO, KUHARIBU MALI.
JULIANA SHONZA AANIKA HADHARANI MATUKIO MAZITO YA CHADEMA YANAYOFANYWA GIZANI
WANASIASA
wawili vijana ambao wamekuwa katika vita ya maneno na Naibu Katibu Mkuu
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Kabwe, kuhusu
madai waliyoyatoa kuwa anawindwa kuuawa, mwishoni mwa wiki iliyopita,
walijitokeza katika ofisi za Mtanzania Jumatano na kufunua siri na
matukio ya utesaji raia na mauaji ya kinyama ambayo yamekuwa yakitokea
kwa nyakati tofauti kwenye shughuli za kisiasa hapa nchini.
Wanasiasa
hao, Juliana Shonza na Mtela Mwampamba, ambao wamefanya mahojiano ya
ana kwa ana na gazeti hili, walisema madai waliyoyatoa awali kuwa Katibu
Mkuu wa Chadema, Dk. Willbrod Slaa, alitajwa na kada wa chama hicho,
Ben Saanane, kuwa alimtuma amuwekee sumu Zitto kwa lengo la kumuua ni ya
kweli kwa sababu walimkamata akiwa nayo na alikiri jambo hilo na
kumuomba msamaha Zitto kwa kitendo hicho.
Walidai,
mbali na tukio hilo ambalo baada ya kuliibua limegusa hisia za wengi na
kuzua mijadala mikali, yapo matukio mengine ya mauaji na majaribio ya
kuua, ambayo yamekuwa yakiratibiwa na Chadema kwa lengo la
kuwagombanisha wananchi na Serikali.
Shonza
na Mwampamba walisema kuwa wapo tayari kutoa ushuhuda wa matukio hayo
mahali popote watakapohitajika na walipoulizwa ni kwa nini baada ya
kubaini kuwepo kwa vitendo hivyo, hawakutoa taarifa kwa vyombo vya
sheria au taasisi za ulinzi na usalama, walisema mlengwa mkuu katika
matukio hayo ambayo yalikuwa yakisababisha madhara kwa watu wengine
hakuwa tayari siri hiyo kuanikwa.
CAG abaini ubadhirifu mkubwa

Mdhibiti
na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh (katikati),
akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu ripoti ya
ukaguzi ya mwaka wa fedha ulioishia 30 Juni, 2012 zilizowasilishwa
bungeni jana mjini Dodoma. Kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya
Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe na kulia ni Mwenyekiti wa Kamati
ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa, Rajab Mbarouk Mohammed. Picha
na Edwin Mjwahuzi
Dodoma. Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ilitolewa jana ikiweka bayana madudu mbalimbali ya ubadhirifu mkubwa wa fedha za umma, udhaifu katika usimamizi wa mikataba na Serikali kushindwa kutoa fedha zilizoidhinishwa na Bunge kwa ajili ya miradi ya maendeleo.
Moja ya matatizo yaliyojitokeza ni Wizara ya Nishati na Madini kushindwa kukusanya nyongeza ya mrabaha wa madini baada ya kuongezwa kutoka asilimia tatu hadi nne.
TANZANIA YAPANDA KATIKA ORODHA YA FIFA
Na Mtandao
Kwa
mujibu wa orodha ya FIFA ya ubora wa soka duniani iliyotolewa leo
nchini Uswizi, zile timu zilizopo 3 Bora, Spain, Germnay na Argentina
bado zimeshikilia nafasi zao.
Tanzania inayoongozwa na taifa stars chini ya kocha mkuu Kim Paulsen imepanda juu nafasi tatu na kujikita Nafasi ya 116.
Katika
miezi miwili, Tanzania imepanda kwa kasi kutoka nafasi ya 127 mwezi
machi na kwenda nafasi ya 119 mwezi Aprili na sasa imekalia nafasi ya
116 baada ya kushusha kipondo kwa Simba wasiofugika kutoka pwani ya
magharibi mwa Afrika, timu ya taifa ya Cameroon bao 1-0 uwanja wa taifa,
na baadaye kuwatungua simba wa milima ya Atlas, timu ya taifa ya
Morroco mabao 3-1 katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za kombe la
dunia.
Wakati
Tanzania ikipanda nafasi tatu juu, Simba watatu yaani timu ya taifa ya
England imeporomoka nafasi 3 na sasa ipo nafasi ya 7 huku wazee wa Samba
na waandaaji wa michuano ya kombe la dunia mwakani, timu ya taifa ya
Brazil ikiporomoka nafasi 1 na sasa ipo ya 19.
Timu
toka Barani Afrika ambayo iko juu sana ni Tembo wa pwani ya magharibi
ya Afrika, timu ya taifa ya Ivory Coast iliyopanda nafasi 1 na sasa ipo
nafasi ya 12.
Orodha nyingine ya timu bora za taifa duniani itatolewa na FIFA Mei 9 mwaka huu.
JAY -Z KUNUNUA KISIWA KWA AJILI YA FAMILIA YAKE

Vyanzo vya habari vilivyopo karibu na nyota huyo vilieleza juzi kuwa ametenga pauni milioni mbili ili kununua eneo hilo lililopo kaskazini mwa wilaya ya Abaco kwa ajili ya familia yake.
Thursday, April 11, 2013
JOHARI AGOMA KUTINGISHA MAUNO YAKE MBELE YA RAY

MKONGWE
kwenye ‘Industry’ ya Filamu Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’ alitoa
kali ya aina yake baada ya kukataa kuzungusha nyonga mbele ya mwigizaji
mwenzake, Vincent Kigos ‘Ray’ anayedaiwa ni mpenzi wake
Tukio
hilo lililonaswa na mwandishi wetu juzikati, lilitokea katika Viwanja
vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar wakati wasanii hao walipojumuika
pamoja kwa ajili ya kumbukumbu ya mwaka mmoja tangu kitokee kifo cha
msanii mwenzao, Steven Kanumba.
Akiwa
viwanjani hapo, Johari aliitwa kupanda jukwaani na wasanii wenzake kwa
ajili ya kucheza sebene kidogo lakini yeye alikataa na mwandishi wetu
alimsikia akijitetea kuwa hawezi kukata nyonga mbele ya wasanii wenzake
hususan Ray ambaye ni bosi mwenzake kwenye kampuni yao ya RJ Company.
“Siwezi
kujidhalilisha mbele ya umati huo kwa kukata kiuno tena na bosi
mwenzangu yupo pale, labda ningekuwa nimelewa kiasi cha kutojitambua
hapo ningefanya madudu kama hayo,” alisema Johari.
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, MULUGO ATANGAZA VITA NA WAZUSHI WAKE
NAIBU
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo amesema
atawafikisha mahakamani watu wanaodai kuwa ameghushi vyeti vya elimu ya
sekondari. Mulugo alisema amechoshwa na kashfa hizo zinazosambazwa na
baadhi ya watu atawafikisha mahakamani endapo wataendelea
kumdhalilisha.
Mulugo
alitoa kauli hiyo alipofungua mkutano wa mwaka wa Umoja wa Wamiliki wa
Shule za Sekondari na Vyuo Binafsi Tanzania (TAMONGSCO0) jijini Mbeya.
“Wanasema
eti nimeghushi vyeti, mara ooh sijui natumia jina la mtu. Nimechoshwa
na maneno haya… ni kweli nimerudia darasa kama walivyorudia watu
wengine, kwa nini iwe tatizo kwangu. Hata hapa tulipo wapo wengi tu
waliorudia darasa.
“Kama
kweli ningekuwa nimeghushi vyeti hivi leo ningekuwa naibu waziri wa
elimu? Sasa nimechoshwa, nitawachukulia hatua watu hawa, siwezi kusema
ni lini nitafanya hivyo ila nitakapoamua nitaanza,”alisema.
Kwa
miezi kadhaa sasa Mulugo amekuwa akidaiwa kughushi vyeti na kutumia
jina la mtu ili kufikia kiwango cha elimu alichonacho madai ambayo
alisema yanamchafulia jina katika jamii.
Kuhusu
suala la matokeo mabaya ya kidato cha nne mwaka jana, Mulugo alisema
matokeo hayo mabaya yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na mmomonyoko wa
maadili miongoni mwa wanafunzi.
Naye
Ruth Mnkeni kutoka Dar es Salaam anaripoti kuwa Mlugo amezindua tovuti
ya elimu kwa wanafunzi wa shule ya sekondari ijulikanayo kama Shule
Direct.
Muluigo
alisema kuzinduliwa kwa tovuti hiyo kutawafanya wanafunzi kupata
maarifa mengi ya vitabu mbalimbali na kuinua kiwango cha elimu nchini
HALI TETE KWENYE SHIRIKA LA UTANGAZAJI TBC

Ndani ya Taasisi ya Utangazaji Tanzania(TBC) kwa sasa kuna mgogoro mkubwa sana unafukuta chini kwa chini ukihusisha pande mbili kuu, yaani Wafanyakazi wa kawaida na Uongozi wa juu wa shirika hilo, kuhusu madai yafuatao na huku wakitaka Mkurugenzi mkuu wa sasa wa TBC afukuzwe na bodi ya shirika hilo ivunjwe;source: JF
1/Ubaguzi katika kupewa vyeo, Posho na marupurupu(Suala la Itikadi, Ukanda na Udini linatajwa sana)
2/Kuruhusu wanasiasa(Viongozi wa serikali na makada wa CCM) kuingilia wanavyotaka kazi za kitaaluma katika utoaji wa habari hususani kuhariri(Kuchuja) habari.
3/Kutokulipwa malimbikizo ya madeni ya madai ya siku za nyuma.
4/Utendaji Duni na Mbovu wa Mkurugenzi mkuu Clement Mshana hadi kufikia kumpa jina la dhihaka la 'BOYA'
5/Vitisho vya kufukuzwa kazi kwa baadhi ya watumishi wanaohoji sana mwenendo mbovu wa shirika hilo kwa sasa.
6/Mvutano wa Chini kwa chini kati ya Wakurugenzi waliowekwa na Lowassa wakati akiwa waziri mkuu na wapya walioletwa na Pinda.
*Pia kuna issue ya mkataba tata(White Elephant) kati ya TBC na Startimes(Wachina!) ambao Terms, Conditions, Investment, Dividend na Shares havijawekwa wazi na sawasawa, japokuwa Mkurugenzi mkuu na Bodi yake ya sasa wanadai wameurithi tu lakini sio 'wapishi' kamili wa hicho kilichopikwa!!
KAULI YA ZITTO KUTOKA BUNGENI ASUBUHI HII
CAG
ameweka mezani taarifa yake asubuhi hii. Katika mkutano wa Kumi wa
Bunge, Serikali ilifanya mabadiliko ya Sheria ya Ukaguzi ya mwaka 2008
Kwa kubadilisha vifungu 38, 39 na 40 ambapo Serikali ingeleta majibu
yake sambamba na Taarifa ya CAG. Serikali haikuleta majibu hayo.
Wamevunja Sheria wakiisha nikiwa siku ya kwanza ya kuanza kutekelezwa
kwake. Spika alipowataka Serikali kutoa majibu, Mawaziri walibaki
kutazamana tu
HATARI : WALA MAHINDI HATARINI KUDUMAA AKILI

WATAALAMU
wa masuala ya afya na kilimo kutoka mataifa mbalimbali duniani,
wamebaini mahindi, karanga na mihogo yenye sumukuvu ni moja ya vitu
vinavyochangia saratani ya ini, udumavu wa mwili na akili kwa watoto.
Ingawa takwimu sahihi hazijapatikana kuonesha madhara ya kila
Kutokana
na ukubwa wa tatizo, wataalamu hao kutoka nchi 20, wanakutana jijini
Dar es Salaam kwa siku tatu, kuanzia jana, kutafuta njia madhubuti za
kukabiliana na sumukuvu. Tanzania inatajwa kuwa miongoni mwa nchi
zilizochukua hatua za awali dhidi ya tatizo hilo.
Akizungumza jana katika ufunguzi wa mkutano huo, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi alisema,
“Lengo
la mkutano huu ni kuwapa fursa wataalamu kuja na mikakati
itakayoisaidia serikali na sekta binafsi kupambana na sumu ya aflatoxin
kwa kuwa hata hapa Tanzania ni tatizo kubwa.”
Dk
Mwinyi alifafanua kuwa, tatizo kubwa linaonekana kwenye mazao
yanayoathiriwa zaidi na sumukuvu ambayo ni mahindi, mihogo na karanga na
husababisha watumiaji kupata saratani ya ini na watoto hudumaa akili na
mwili.
Alisema
pamoja na serikali kupitia Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kuwa na
sheria ya kudhibiti vyakula vinavyoingia nchini, lakini sheria pekee
haziwezi kumaliza tatizo hasa ikizingatiwa kuwa Watanzania wengi
wanatumia nafaka hizo wakati zikiendelea kukua shambani bila kuzipima
kiwango cha sumukuvu kinachotakiwa.
Sumukuvu
ni aina ya sumu inayosababishwa na kuvu katika mazao na ingawa
haiepukiki katika nafaka, kuna kiwango kinachopaswa kuwepo na
kinapozidi, huleta madhara hayo.
Subscribe to:
Comments (Atom)













