Wednesday, March 20, 2013

Kwa mujibu wa matokea ya kura nchini Zimbabwe Wananchi waunga mkono Katiba mpya.

Wapiga kura nchini Zimbabwe wameunga mkono mabadiliko ya katiba.
Katika kura ya maoni iliyopigwa mwishoni mwa wiki ililopita, asilimia 95 ya wapiga kura hao wamepiga kura ya ndio.
Kura hiyo imetayarisha mchakato wa uchaguzi mwishoni mwa mwaka huu, ambao utamaliza kipindi cha utawala wa mpito wenye mivutano, unaoshirikisha rais Robert Mugabe na mpinzani wake Waziri Mkuu Morgan Tsvangirai.
Mabadiliko hayo ya katiba yanaweka kikomo cha mihula miwili ya miaka mitano kwa rais, na yanalipa bunge madaraka makubwa.
Mabadiliko hayo hali kadhalika yanaondoa wadhifa wa Waziri Mkuu.-DW.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...