HALI TETE KWENYE SHIRIKA LA UTANGAZAJI TBC

Ndani
ya Taasisi ya Utangazaji Tanzania(TBC) kwa sasa kuna mgogoro mkubwa
sana unafukuta chini kwa chini ukihusisha pande mbili kuu, yaani
Wafanyakazi wa kawaida na Uongozi wa juu wa shirika hilo, kuhusu madai
yafuatao na huku wakitaka Mkurugenzi mkuu wa sasa wa TBC afukuzwe na
bodi ya shirika hilo ivunjwe;
1/Ubaguzi katika kupewa vyeo, Posho na marupurupu(Suala la Itikadi, Ukanda na Udini linatajwa sana)
2/Kuruhusu
wanasiasa(Viongozi wa serikali na makada wa CCM) kuingilia wanavyotaka
kazi za kitaaluma katika utoaji wa habari hususani kuhariri(Kuchuja)
habari.
3/Kutokulipwa malimbikizo ya madeni ya madai ya siku za nyuma.
4/Utendaji Duni na Mbovu wa Mkurugenzi mkuu Clement Mshana hadi kufikia kumpa jina la dhihaka la 'BOYA'
5/Vitisho vya kufukuzwa kazi kwa baadhi ya watumishi wanaohoji sana mwenendo mbovu wa shirika hilo kwa sasa.
6/Mvutano wa Chini kwa chini kati ya Wakurugenzi waliowekwa na Lowassa wakati akiwa waziri mkuu na wapya walioletwa na Pinda.
*Pia
kuna issue ya mkataba tata(White Elephant) kati ya TBC na
Startimes(Wachina!) ambao Terms, Conditions, Investment, Dividend na
Shares havijawekwa wazi na sawasawa, japokuwa Mkurugenzi mkuu na Bodi
yake ya sasa wanadai wameurithi tu lakini sio 'wapishi' kamili wa hicho
kilichopikwa!!
source: JF
No comments:
Post a Comment