Thursday, April 11, 2013

HATARI : WALA MAHINDI HATARINI KUDUMAA AKILI

WATAALAMU wa masuala ya afya na kilimo kutoka mataifa mbalimbali duniani, wamebaini mahindi, karanga na mihogo yenye sumukuvu ni moja ya vitu vinavyochangia saratani ya ini, udumavu wa mwili na akili kwa watoto.
Ingawa takwimu sahihi hazijapatikana kuonesha madhara ya kila 
nchi kutokana na utafiti hizo kuendelea, tatizo limeelezwa kuwa ni kubwa hasa katika nchi za Afrika kutokana na mfumo mzima wa uzalishaji katika sekta ya kilimo na ukuzaji wa mazao usiozingatia utaalamu.

Kutokana na ukubwa wa tatizo, wataalamu hao kutoka nchi 20, wanakutana jijini Dar es Salaam kwa siku tatu, kuanzia jana, kutafuta njia madhubuti za kukabiliana na sumukuvu. Tanzania inatajwa kuwa miongoni mwa nchi zilizochukua hatua za awali dhidi ya tatizo hilo.
Akizungumza jana katika ufunguzi wa mkutano huo, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi alisema,
“Lengo la mkutano huu ni kuwapa fursa wataalamu kuja na mikakati itakayoisaidia serikali na sekta binafsi kupambana na sumu ya aflatoxin kwa kuwa hata hapa Tanzania ni tatizo kubwa.”
Dk Mwinyi alifafanua kuwa, tatizo kubwa linaonekana kwenye mazao yanayoathiriwa zaidi na sumukuvu ambayo ni mahindi, mihogo na karanga na husababisha watumiaji kupata saratani ya ini na watoto hudumaa akili na mwili.
Alisema pamoja na serikali kupitia Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kuwa na sheria ya kudhibiti vyakula vinavyoingia nchini, lakini sheria pekee haziwezi kumaliza tatizo hasa ikizingatiwa kuwa Watanzania wengi wanatumia nafaka hizo wakati zikiendelea kukua shambani bila kuzipima kiwango cha sumukuvu kinachotakiwa.
Sumukuvu ni aina ya sumu inayosababishwa na kuvu katika mazao na ingawa haiepukiki katika nafaka, kuna kiwango kinachopaswa kuwepo na kinapozidi, huleta madhara hayo.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...