Saturday, February 16, 2013

urais Kenya pamoja na mashitaka yanayomkabili ICC.


Mahakama Kuu nchini Kenya imemsafishia njia mmoja kati ya wagombea urais Bw. Uhuru Kenyata kuwania kiti cha urais wa taifa hilo katika uchaguzi mkuu ujao pamoja na kukabiliwa na mashitaka ya uhalifu dhidi ya ubinadamu.
Ikiwa imebakia muda mfupi kabla ya uchaguzi mkuu wa Machi 4 mwaka, uamuzi huo umemuweka Kenyatta huru kuwania kiti hicho akionekana kama mmoja kati ya viongozi wanaongoza katika kinyang’anyiro cha urais.
Jopo la majaji watano waliokuwa wanasikiliza kesi hiyo wanasema mahakama kuu ndiyo yenye uwezo wa kuamua kesi hiyo.
Kesi hiyo ilifunguliwa kupinga ushiriki wa watu hao katika uchaguzi wa mwezi Machi, kwa kile walichokiita kukosa uadilifu kwa sababu tayari wamefunguliwa mashtaka ya kuhusika na ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka 2007 katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu ya ICC.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...