Saturday, February 16, 2013

Rais Deby wa Chad awafukuza kazi mawaziri wawili, ikiwa ni muda mfupi tu baada ya kuwasimamisha kazi askari wa jeshi la polisi nchini humo.


Rais Idriss Deby wa Chad amewafukuza kazi mawaziri wawili wanaohusika na masuala ya ulinzi ikiwa ni baada ya wiki iliyopita kuwasimamisha kazi takriban polisi zaidi ya 6,000 kwa tuhuma za rushwa, upendeleo na udhalilishaji.
Katika tangazo lililotolewa katika radio ya taifa, rais Deby amemfukuza Waziri wa Usalama wa Umma Ahmat Mahamat Bachir na Waziri wa Usimamizi dhidi ya Ugaidi Bachar Ali Souleymane.
Kufukuzwa kwa mawaziri hao kunafuatia pia kufukuzwa kazi kwa Mkuu wa Polisi nchini humo, ikiwa ni siku mbili baada ya kulisimamisha kazi jeshi hilo.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...