Saturday, February 16, 2013

Mzee Mwinyi kuzindua kampeni ya uboreshaji wa wodi za kinamama jijini Dar


Rais Mstaafu wa awamu ya pili Mzee Alhaj Ali Hassan Mwinyi.
Taasisi ya Africa Youth Cross Cultural Exchange & Environment Conservation inatarajia kuzindua rasmi kampeni za uboreshaji wa wodi za kina mama wajawazito na watoto.
Mratibu wa Kampeni hiyo William Kotta amesema lengo la kampeni hiyo ni kuhakikisha wodi hizo zinakuwa na vifaa vinavyo jitosheleza kwa ajili ya kusaidia kina mama na watoto wanaoteseka na kupoteza maisha hasa wakati wa kujifungua.
Amesema taasisi hii katika kuanza kutekeleza kampeni hiyo, siku ya tarehe 22 Februari 2013 wameandaa chakula cha hisani kwa lengo la kuchangisha fedha na kusaidia upatikanaji wa vifaa hivyo.
Shughuli hiyo kwa heshima kubwa itaongozwa na Mzee Alhaj Ali Hassan Mwinyi rais mstaafu wa awamu ya pili.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...