Saturday, July 27, 2013

STARS WAKIWA MAZOEZI KUPAMBANA NA CRANE LEO




 Wachezaji mbalimbali wa Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Satrs' ambao wanasakata kabumbu ndani ya nchi wakijifua katika Uwanja wa Taifa wa Mandela uliopo Nambole nchini Uganda. Stars ipo nchini Uganda na leo inataraji kushuka katika dimba la uwanja huo kumenyana vikalina The Crenes ya Uganda kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa Ndani CHAN.

Moja ya mikakati ya Taifa Stars kwenye mechi ya leo (Julai 27 mwaka huu) dhidi ya Uganda kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Tatu za Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini ni kushambulia kwa muda mwingi wa mchezo.

POLISI AZUA BALAA MKUTANO WA CHADEMA NUSURA APIGWE

Na Bryceson Mathias, Kikombo
ASKARI Polisi wa Kata ya Kikombo  aliyejulikana kwa jina Moja la Sivanus (pichani), Jana alizua Tafrani kwenye Mkutano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), baada ya Kumnyanganya Kipaza Sauti (Mike) Katibu wa Wilaya wa Dodoma Mjini, Jella Mambo.
Silvanus alizua hayo Julai 26, ambapo alinusurika Kipigo cha Wananchi  waliokuwa na hasira kwa kufanya tukio hilo, ambapo walidai hata kungekuwa na makosa ya Matamko au kitu kingine chaochote, hakustahili kuingia jukwani na kumnyang’anya Kipaza sauti Katibu huyo.
Askari Silvanus aliyeonekana kulewa na kuwaacha wenzie kwenye gari, alichukuwa hatua hiyo, Mambo alipomtambulisha aliyekuwa Mgombea wa Chadema Kata hiyo, Yona Kusaja, kwamba, uchaguzi uliopita Kusaja hakushindwa ila Chama Tawala (CCM) kilichakachua kura zake na kutoa vitisho kwa wapiga kura.

Friday, July 26, 2013

HUYU NDO MSANII ALIYETANGAZA KUMPORA MUME WA AUNT EZEKIEL... !!!

KATIKA hali isiyo ya kawaida msanii anayechipukia katika filamu za Kibongo, Isabella Fransis ‘Vai wa Ukweli’ anamtafuta ubaya gwiji katika tasnia hiyo, Aunt Ezekiel kwa kusema anamtamani mumewe.

Vai wa Ukweli bila ya kupindisha maneno amedai kuwa hapati usingizi kutokana na kumzimia Sunday Demonte ambaye ni mume wa Aunt.


Akizungumza na mwandishi wetu, Vai alisema ili kuonesha kuwa anachokisema kinatoka moyoni mwake, amekata vipande vya picha za Dimonte na kuvibandika chumbani kwake.

 “Kusema ukweli nampenda sana Sunday na sijaanza kumpenda leo wala jana kwani namfahamu tangu zamani alipokuwa Kariakoo,” alisema Vai.

Msanii huyo chipukizi alisema anamuonea wivu Aunt kwa kuamini kuwa anafaidi sana kwa kuwa na mwanaume huyo.
 

Kwa upande wake Aunt alishangazwa na taarifa hizo na akaomba atafutwe baada ya kumalizika kwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ili ajue cha kufanya.

FABREGAS AFUNGUKA, ATAMANI KUJIUNGA NA MOYES, VAN PERSIE OLD TRAFFORD


Uncertain future: Cesc Fabregas could leave Barcelona for Manchester United 
Haijulikani hatima yake: Cesc Fabregas  anaweza kujiunga na Manchester United
Lakini ukweli ni kwamba  Fabregas amewaambia maswahiba wake wa England kuwa anataka kuondoka Camp Nou, na hii inawapa moyo zaidi kumnasa.

Inafahamika kuwa Fabregas amevutiwa na ahadi nzuri ya kucheza muda wote katika kikosi cha United na anapenda kujiunga na nyota mwenzake wa zamani wa Asernal, “Hakunaga” Robin Van Persie ambaye kwa sasa ndio roho ya ushambuliaji ya pale Old Trafford.

MZEE SMALL ANAENDELEA VIZURI KIASI,LAKINI BADO ANAHITAJI MSAADA WETU WADAU


Taarifa ya Mrejesho : Hali ya Msanii nguli wa maigizo hapa nchini Tanzania, Ndg
Said Bin Wangamba almaarufu kama Mzee Small inaendelea vizuri, na
ANASHUKURU sana kwa wale wote wanaomkumbuka katika kipindi hiki kigumu
cha maradhi. Kwa sasa anaweza kujikongoja taratibu mwenyewe.,

Anaendelea na mazoezi ya kila siku, na kubwa ni dozi ya dawa kwa ajili  ya kumsaidia kuondoa uvimbe uliogundulika miezi kadhaa iliyopita,  kichwani mwake ambapo dozi moja tu inagharimu takribani 30,000TZS pamoja
na mahitaji mengine ya lazima ya kila siku,
 Kwa yeyote atakaeguswa  tafadhali unaweza kuwasiliana na Mzee wetu kupitia, M-PESA kwa kutumia  namba ya Said Ngamba (Mzee Small) 0754647265 na TIGO PESA kwa kutumia  namba ya mkewe 0658111311,

Changamoto: Ni Wakati MUAFAKA Sanaa kuwa Ajira Rasmi na yenye MAPATO STAHIKI, Alituchekesha na kutuondolea uchovu kwa kipaji chake, nasi tumkumbuke na kumuenzi,
 
Matukio-Amani OleAfrika Aranyande M Chuma

MAJANGA MADANGURO YA MAKAHABA YAZIDI KUFUMULIWA....!!!


 
 Hili ni sakata la  kikongwe mmoja anayedaiwa kumiliki idadi kubwa ya madanguro katika uwanja wake na kuwapangisha makahaba katika eneo maarufu kwa jina la Kijiji cha Makahaba.
Mwandishi wetu alipokea ujumbe mfupi ulioelezea ufuska unaofanywa na mabinti ambao hupewa eneo na kujenga vibanda kisha kujiuza kwa bei chee katika kijiji hicho maeneo ya Kigamboni jijini Dar.


Bada ya simu hiyo, uchunguzi wetu  ulibaini kwamba, eneo hilo linalofanyiwa ufuska huo linamilikiwa na kikongwe aliyejitambulisha kwa jina la mzee Matutu akidaiwa kuendesha maisha kwa biashara hiyo ya madanguro.
 
Baada ya kujiridhisha na uchunguzi kuwa ni kweli jambo hilo linafanyika eneo hilo,waandishi walivamia eneo la tukio wakiwa na mjumbe wa mtaa huo aliyefahamika kwa jina la Abbas na kujionea madanguro yaliyojengwa kwa mstari ambapo milango yake iliachwa wazi huku ndani wakionekana mabinti wakiwa wamejilaza kihasarahasara wakiwatega wateja wanaopita katika mtaa huo.

MAAJABU: BINTI ALIYEZALIWA BILA MACHO WALA PUA ATAKIWA KUTOA UBAVU WAKE ILI AFANYIWE UPASUAJI...!!!

Msichana Brave Cassidy Hooper (17) kutoka Charlotte, Kaskazini mwa Carolina Marekani aliyezaliwa bila pua wala macho anategemea kufanyiwa upasuaji mkubwa wa kurekebisha uso wake.

u-4
Brave anategemewa kufanyiwa upasuaji huo (July 31) mwaka huu ambapo inategemewa sehemu ya mfupa utaondolewa katika ubavu wake kwaajili ya kutumika kutengeneza paji la uso wake, mfupa huo utasaidia kama kiunganishi cha pua mpya atakayowekewa.

IRENE UWOYA AREJEA NCHINI KUTOKA KWA MSWATI - AMEAIDIWA MAMBO MAKUBWA

 
Mwigizaji Irene Uwoya amerejea nchini toka nchini Swaziland alipokuwa kwa takribani wiki tatu.
Irene Uwoya aliyerejea nchini leo hii amerejea na salamu toka nchini Swaziland alizoziandika kupitia ukrasa wake wa mtandao mmoja wa kijamii alisema…
 
“Mswat anawasalinmu sana! Nahiv karibun atatinga hapa nakanipa kibali chakufanyya move na ful suport...I wl prove u wrong...try me”
 
Akimaanisha, amerejea nchini na Mswati amnawasalimia sana na amesema atakuja nchini hivi karibuni na amenipa kibali cha kufanya Filamu na atanisaidia kwa kila kitu. Nijaribu nitakuthibitishia kuwa umekosea (Kwa Kiswahili fasaha).
 
Bado tunamtafuta Irene amabye namba yake ya simu haipatikani kujua kama kauli hii ni ya kweli au anawatania tuu mashabiki wake.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JULAI 26, 2013


DSC 0095 1cb01
DSC 0096 51ada

Thursday, July 25, 2013

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JUALI 25, 2013

DSC 0069 7123d
DSC 0070 eba91

ALEX SONG SAYS CESC FABREGAS "WILL NOT BE LEAVING BARCELONA"

Alex Song: With Cesc Fabregas at Barcelona last season
Alex Song: With Cesc Fabregas at Barcelona last season

Alex Song is convinced Cesc Fabregas will still be a Barcelona player at the start of the new season.

Song, the former Arsenal midfielder who spent six years at the Emirates before moving to Spain in 2012, says his team-mate has no intention of quitting Camp Nou. Fabregas, also a former Gunner, has been the subject of two bids from Manchester United already this summer, and David Moyes said this week he will give the transfer "every opportunity to materialise".

But after featuring in Barca's friendly defeat at Bayern Munich Song told Sky Sports News he is "100%" sure Fabregas is going nowhere. He said: "I did not speak with him but I know Cesc is 100 per cent here. "He loves Barcelona, he loves the club. He will stay here next season and give 100 per cent because I know him very well and he'll want to fight. He's focused on the club.
"He wants just to give his best for Barcelona. He's from Barcelona, he loves Barcelona and he'll want to start the season to show what he can do.

"People are talking and talking, but we know he is focused here and ready to start the season."He's enjoying a holiday with his family and I'm sure he wants just to come back here. "It's my own opinion but I know he will stay here, 100 per cent."

MAAJABU:- MTOTO WA MWAKA MMOJA APATA UJAUZITO...!!!


Madaktari wa nchini China walishangazwa kuona mtoto wa mwaka mmoja ana ujauzito.
Mtoto Kang Mengru wa nchini China alipelekwa hospitali baada ya wazazi wake kushtushwa na hali ya tumbo lake kuzidi kuwa kubwa siku hadi siku.

Baada ya mtoto huyo kufanyiwa ultrasound, madaktari waligundua kuwa mtoto huyo wa kike alikuwa amebeba kitoto kichanga kwenye tumbo lake ambacho kilikuwa kikiendelea kukua.
Madaktari wanaamini kuwa mama wa mtoto huyo alikuwa na mimba ya watoto wawili mapacha na pacha mmoja alijitokeza ndani ya tumbo la pacha mwenzake.


Hali kama hiyo ya kichanga kuzaliwa ndani ya kichanga kingine ni nadra sana kutokea na humtokea mwanamke mmoja katika wanawake 500,000.

Mtoto Kang atafanyiwa upasuaji kukiondoa kichanga hicho tumboni mwake.

WEMA SEPETU AENDELEZA WEMA WAKE SAFARI HII AMGEUKIA RAY C



Wema Sepetu katika pozi


RIHANNA KAMA KAWAIDA, ANGALIA KIVAZI CHAKE VITU NJE NJE....!!!

 




Wednesday, July 24, 2013

HATIMAE KITUKUU CHA MALKIA ELIZABETH CHAPEWA JINA....!!!


Prince William akiwa na familia yake saa24 baada ya mtoto George Alexander Louis kuzaliwa.

Prince William akiwa na familia yake saa24 baada ya mtoto George Alexander Louis kuzaliwa.
Prince William alipokuwa amezaliwa akiwa amebebwa na baba yake Prince Charles na mama yake Princess Diana mwaka 1982.

Prince William alipokuwa amezaliwa akiwa amebebwa na baba yake Prince Charles na mama yake Princess Diana mwaka 1982.

RAIS KIKWETE AWASILI BUKOBA, AKUTANA NA TAIFA STARS MWANZA, AWATAKIA USHINDI DHIDI YA UGANDA








 Jakaya Mrisho Kikwete akifungua jengo la Kagera Coperative Union leo Julai 24, 2013
mjini Bukoba.


 Picha ya Pamoja

MBONA MAJANGAAAAA: ALIKIBA NAE ATIWA MBARONI NJE YA NCHI... KISA ........!!!


Meneja wake Guru akiongea na mama yake Ally Kiba nyumbani kwao Kariakoo amesema bwana mdogo alikuwa uwanja wa ndege wa Amsterdam akisubiri ndege za American Airlines ili aelekee jijini Oklahoma City USA akiwa na mwanamama maarufu mwenye mvuto hapa bongo ndipo alipokamatwa.

Haijajulikana sababu za kukamatwa kwake na mpaka leo familia wapo kimya hawajafunguka na wanailinda habari isivuje japo baadhi ya wadau washazinasa. Haijajulikana sababu za kukamatwa ila mpaka kesho media zitatuambia sababu. Sina hakika kama kisa cha kukamatwa bwana Singleboy ni kitu cha Sembe au laaaaa!!! TUSUBIRI


HII NDIO PARTY TWO YA BIFU LA IRENE UWOYA NA LUCY KOMBA...!!!


NYOTA wa filamu za Kibongo, Irene Pancras Uwoya ‘Mama Krrish’ ametoa kali ya mwaka baada ya kudai kwamba amemshika ugoni msanii mwenzake, Lucy Komba mara baada ya kuziona picha za msanii huyo akiwa na mumewe, Hamad Ndikumana ‘Kataut’ wakiigiza filamu. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu kutokea nchini Swaziland, Uwoya amepinga vikali utetezi unaosemwa kwamba Lucy na Kataut walikuwa wakishuti filamu na anaamini kuwa msanii huyo ameamua kumzunguka na kutaka kuibomoa ndoa yake. “Lazima kuna kitu kinaendelea kwani katika dunia hii sijawahi kuona filamu inayochezwa na watu wawili tu mwanzo mpaka mwisho, ninachotaka kusema ni kwamba Lucy ana mpango wa kuiharibu ndoa yangu,” alisema Uwoya kwa hasira. 

Uwoya amehoji usiri wa filamu hiyo na kila alipokuwa akimpigia simu mumewe alikuwa akimjibu kwamba yuko Rwanda kumbe alikuwa Bongo akiigiza filamu na Lucy. “Kwanza Lucy ashukuru niko mbali, laiti ningekuwa karibu angenieleza vizuri kwa sababu hata yeye angeweza kunipigia simu na kunifahamisha ushiriki wa mume wangu kwenye filamu hiyo kwa kuwa namba zangu anazo, ilikuwaje hakufanya hivyo?” alihoji.

 Kuonesha kwamba amechukizwa na kitendo hicho, Uwoya alisema kwamba akitua Bongo atamtafuta Lucy ili aweze kumshughulikia vizuri na ikiwezekana amuoneshe hiyo filamu waliyoigiza watu wawili tu. “Nitatua Bongo siku si nyingi na cha kwanza ni kumtafuta Lucy, anieleze vizuri kuhusu filamu hiyo waliyocheza na mume wangu,” alisema Uwoya. Filamu hiyo ambayo imekuwa maumivu makubwa kwa Uwoya, imechezwa na Lucy na Ndikumana tu mwanzo hadi mwisho na imepewa jina la Kwa Nini Nisikuoe

STARS YAMALIZA KAMBI YAKE JIJINI MWANZA KUONDOKA KESHO KUELEKEA UGANDA, KASEJA BADO CHAGUO BORA.

Kocha mkuu wa Taifa Stars Kim Poulsen (kulia) akizungumza  na wandishi wa habari (hawako pichani) ikiwa ni siku moja kabla ya kuondoka jijini Mwanza mara baada ya kumaliza kambi, kushoto ni Afisa habari wa TFF Michael Wambura. 
NA ALBERT G. SENGO: MWANZA
Ni takribani majuma mawili sasa Taifa Stars imekuwa jijini Mwanza ikiweka Kambi kuelekea kipute cha marudiano na 'The Cranes', katika mchezo unaotarajiwa kuchezwa jumamosi hii ya tarehe 27 mwezi wa 7mwaka 2013 mjini Kampala.

Sasa kambi imefikia tamati, yamesalia masaa kadhaa ambapo kesho mchana majira ya saa 7 na dakika 25, wawakilishi hao wa taifa la Tanzania, Taifa Stars wataondoka kwa ndege ya Shirika la Precission Air kuelekea nchini Uganda kuisaka tiketi ya CHAN. 

Msikilize hapo chini

.

KWA UFUPI: Kocha mkuu wa Taifa Stars Kim Poulsen amezungumzia mapengo yaliyopo kwenye kikosi chake kuanzia kutokuwepo kwa Kapombe kwenye idara ya ulinzi na sasa Mwinyi Kazimoto katika idara ya kiungo, bila shaka kikosi kitakuwa na utofauti ambao anaona ni sehemu ya marekebisho na anamaboresho.

WASHINDI WA TIGO ‘MILIKI BIASHARA YAKO’ WAKABIDHIWA BAJAJI ZAO


 
 Meneja Chapa wa Tigo, Bw. William Mpinga (kulia) akimkabidhi ufunguo wa Bajaji mshindi wa pili wa promosheni ya ‘Miliki Biashara Yako’, Bw. Riziki Lucas Kisemo (36) mfanyakazi wa viwandani, mkazi wa Makabe, Dar es Salaam. Tigo tayari imelipia leseni ya barabani (Road license) na bima kwa ajili ya Bajaji hizo. Anachotakiwa mteja sasa, ni kuanza biashara yake bila shida mara moja.


 
Meneja Chapa wa Tigo, Bw. William Mpinga (kulia) akimkabidhi ufunguo wa Bajaji mshindi wa kwanza wa promosheni ya ‘Miliki Biashara Yako’, Bw. Mohamed Ramadhani Mnjori (39) muuza nguo za mitumba, mkazi wa Ilala – Dar es Salaam kwenye halfla ya makabidhiano iliyofanyika eneo la Soko Kuu la Kariakoo, Dar es Salaam.

SHILOLE MATATANI WIZI SIMU ZA DIAMOND...!!!


 
Stori:Shakoor Jongo na Musa Mateja
STAA wa filamu na muziki wa Bongo Fleva, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ ..........

ameingia matatani akidaiwa kuingia mitini na simu tatu za mkononi alizoaminiwa nchini Afrika ya Kusini alikokwenda kufanya shoo.


Mfano wa aina ya simu anazo daiwa kuiba Shilole
Msanii huyo alikumbwa na kasheshe hilo Julai 19, 2013 nyumbani kwa mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Sinza Mori, Dar. Siku hiyo Diamond alikuwa akifuturisha na aliwaalika watu mbalimbali wakiwemo mastaa lakini nusura futuru iingie doa kufuatia zogo hilo.

MAGAZETI YA LEO JULAI 24, 2013

Tuesday, July 23, 2013

MASELA WAUWANA KWA MARUNGU KISA DEMU WA KISUMKUMA...!!!


Mnamo tarehe 21/07/2012 majira ya saa 23:30hrs huko kijiji cha Nkwangu wilaya ya Chunya mkoa wa Mbeya, Seni s/o Sandu, miaka 20, Msukuma, mkulima na mkazi wa Nkwangu aliuawa kwa kupigwa fimbo kichwani na Tolo s/o Seko, miaka 20, Msukuma, mkulima na mkazi wa Nkwangu.

Chanzo ni ugomvi wa kumgombania msichana aitwaye Holo d/o Kulwa, miaka 16, Msukuma mkulima na mkazi wa Nkwangu.


Mtuhumiwa amekamatwa na taratibu za kumfikisha mahakamani zinaandaliwa.


Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya kamishna msaidizi wa polisi diwani athumani anatoa wito kwa jamii kutojichukulia sheria mkononi kwani ni kinyume cha sheria na kudhibiti hasira zao kwa kuyatatua matatizo ya kimapenzi kwa njia ya mazungumzo ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza.


Signed by, [Diwani Athumani – ACP] kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya. 


Source: Watemi

MAGAZETI YA LEO JULY 23, 2013


DSC 0061 f2b62
DSC 0062 6a196

KIKWETE AWATAKA UMOJA WA MATAIFA KURUHUSU SILAA KATIKA OPERATIONI ZAO



Rais Kikwete akitoa heshima za mwisho kwa marehemu askari waliouwawa huko Darfur wakitekeleza majukumu ya umoja wa mataifa ya kulinda amani.


Dar es Salaam.
Rais Jakaya Kikwete ameutaka Umoja wa Mataifa (UN), kuruhusu kutumika kwa mtutu katika operesheni za kulinda amani zinazoendelea.
Alitoa kauli hiyo jana baada ya kutoa heshima zake kwa wapiganaji saba wa Tanzania waliokuwa Darfur, Sudan katika operesheni ya kulinda amani ya UN na Afrika (Unamid) ambao waliuawa na kundi linalodaiwa la wanamgambo wa Janjaweed wanaoungwa mkono na Serikali ya Sudan inayoongozwa na Rais Omar al-Bashir.
Wapiganaji waliouawa ni Oswald Chaula kutoka 42KJ Chabruma, Songea, Peter Werema (44KJ Mbeya), Fortunatus Msofe (36KJ Msangani, Pwani), Rodney Ndunguru (92KJ Ngerengere), Mohamed Juma (94KJ Mwenge), Mohamed Chukilizo (41KJ Nachingwea) na Shaibu Othman (MMJ- Upanga).
“Lazima nikiri kuwa taarifa hiyo ya vifo vya vijana wetu ilinihuzunisha, kunisikitisha na kunikasirisha. Kwa nini watu wa Darfur wawaue wanajeshi wetu ambao wamekwenda kule kuwasaidia wapate utulivu ili kunusuru maisha yao, kuwaondolea wasiwasi na kuwawezesha wafanye shughuli zenye tija kuendesha maisha yao?
“Moja kwa moja sikusita kuamini kuwa waliofanya hivyo ni watu wahalifu. Tangu uhuru ni sera ya nchi yetu kutetea wanyonge dhidi ya ukoloni, ubaguzi, uonevu, dhuluma na watu wote walioko katika mazingira hatarishi Afrika na duniani. UN ifanyie marekebisho sheria ili majeshi yanayolinda amani yawe na nguvu za kujihami ili kuzuia maafa yanayoweza kujitokeza.”

GODBLESS LEMA AFYATUA KOMBORA LINGINE....!!!




CHAMA cha demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetangaza kuanza kutoa mafunzo ya kujihami kwa vijana wao maarufu kama Red brigedi kuanzia Agosti mosi, mwaka huu.

Akitangaza tarehe hiyo jana wakati wa mkutano wa chama hicho uliofanyika Mbalizi wilaya ya Mbeya Vijijini, kiongozi wa ulinzi wa chama hicho kanda ya Nyanda za juu kusini Lucas Mwampiki, alisema kuwa ameamua kuweka wazi adhima hiyo ili serikali isiendelee kusumbuka kuwa inao uwezo wa kuwazuia.

‘’Polisi msisumbuke kutafuta kuwa tutaanza lini, ni hivi, tutaanza tarehe 1, mwezi wa nane mwaka huu’’ alisema Mwampiki ambaye pia ni diwani wa kata ya Mwakibete Jijini Mbeya.

TAIFA STARS KUIFUATA UGANDA 'THE CRANES' JUMATANO, KUKIPIGA JUMAMOSI

 
 
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inaondoka Mwanza keshokutwa (Julai 24 mwaka huu) kwenda Kampala, Uganda kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la CHAN itakayochezwa Jumamosi (Julai 27 mwaka huu) Uwanja wa Mandela kuanzia saa 10 kamili jioni.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iko kambini jijini Mwanza chini ya Kocha Kim Poulsen tangu Julai 14 mwaka huu kujiandaa kwa mechi hiyo itakayoamua ni timu ipi kati ya hizo mbili itacheza Fainali za CHAN zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.
Timu hiyo itaondoka Uwanja wa Ndege wa Mwanza saa 7.25 mchana kwa ndege ya PrecisionAir, na inatarajiwa kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe saa 10.15 jioni.
Wakati huo huo, Kocha Kim Poulsen kesho (Julai 23 mwaka huu) atakuwa na mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia maandalizi ya kikosi chake. Mkutano huo utafanyika saa 5 kamili asubuhi kwenye hoteli ya La Kairo jijini Mwanza.

HAWA NDIO ASKARI WALIOKUFA DARFUR WAKILINDA AMANI - MUNGU ZILAZE ROHO ZAO PEMA PEPONI AMINA


 MT 97024 PTE Fortunatus Wilbard Msofe- 36 KJ

Monday, July 22, 2013

RATIBA YA LIGI KUU MSIMU UJAO MZUNGUKO WA KWANZA

clip_image001clip_image001[8]

HIZI NDIZO NYUMBA ZITAKAZOSHINDANIWA KATIKA PROMOTION YA AIRTEL YATOSHA

Meneja Mawasiliano wa shirika la nyumba la Taifa Bw, Yahaya Charahani
akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati ambapo waandishi hao walitembelea eneo la kibada wilaya ya Temeke kujionea Nyumba 3 zinazoshindaniwa katika promosheni ya Airtel Yatosha. Nyumba
hizi zimenunuliwa na Airtel toka shirika la nyumba la taifa kwaajili
ya promosheni ya AIRTEL shinda Nyumba.kulia ni Meneja Uhusiano wa
Airtel Bw, Jackson Mmbando
Meneja Uhusiano wa Airtel Bw Jackson Mmbando akiongea na waandishi wa
habari (hawapo pichani) wakati ambapo waandishi hao walitembelea eneo
la kibada wilaya ya Temeke kujionea Nyumba 3 zinazoshindaniwa katika
promosheni ya Airtel Yatosha.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JULAI 22, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC 0047 97a9a

DSC 0048 4d765

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...