Wednesday, July 24, 2013

STARS YAMALIZA KAMBI YAKE JIJINI MWANZA KUONDOKA KESHO KUELEKEA UGANDA, KASEJA BADO CHAGUO BORA.

Kocha mkuu wa Taifa Stars Kim Poulsen (kulia) akizungumza  na wandishi wa habari (hawako pichani) ikiwa ni siku moja kabla ya kuondoka jijini Mwanza mara baada ya kumaliza kambi, kushoto ni Afisa habari wa TFF Michael Wambura. 
NA ALBERT G. SENGO: MWANZA
Ni takribani majuma mawili sasa Taifa Stars imekuwa jijini Mwanza ikiweka Kambi kuelekea kipute cha marudiano na 'The Cranes', katika mchezo unaotarajiwa kuchezwa jumamosi hii ya tarehe 27 mwezi wa 7mwaka 2013 mjini Kampala.

Sasa kambi imefikia tamati, yamesalia masaa kadhaa ambapo kesho mchana majira ya saa 7 na dakika 25, wawakilishi hao wa taifa la Tanzania, Taifa Stars wataondoka kwa ndege ya Shirika la Precission Air kuelekea nchini Uganda kuisaka tiketi ya CHAN. 

Msikilize hapo chini

.

KWA UFUPI: Kocha mkuu wa Taifa Stars Kim Poulsen amezungumzia mapengo yaliyopo kwenye kikosi chake kuanzia kutokuwepo kwa Kapombe kwenye idara ya ulinzi na sasa Mwinyi Kazimoto katika idara ya kiungo, bila shaka kikosi kitakuwa na utofauti ambao anaona ni sehemu ya marekebisho na anamaboresho.

Lakini pia hakufurahishwa na namna alivyoondoka Mwinyi Kazimoto akitegemea Shirikisho la Soka nchini TFF litatumia busara zake kumwajibisha mchezaji huyo kukosa uzalendo.
Amezungumzia pia baadhi ya maoni ya wadau wa soka mfano suala la Juma Kaseja kutajwa na baadhi yao kuwa amezeeka, kiwango kimeshuka hivyo hastahili kuchezea Taifa stars. Amehoji

-Hivi factor ya msingi unayotizama kwa mchezaji ni umri wake au kiwango chake uwanjani? Kwa idara ya goalkeeping kwa uri wa Kaseja miaka 29 ni umri mzuri sana kwa golikipa, lakini pamoja na hayo yote ana kiwango kikubwa mno.

Amejaribu pia kuizungumzia idara ya difensi' kwa tathimini ya baadhi ya mechi kubwa ambazo timu ya taifa imecheza siku zilizopita akisema kuwa kwa wale wanaofikiri kuna mapungufu makubwa kwenye safu ya ulinzi, mechi ngumu dhidi ya Zambia, dhidi ya Cameroon, akiuliza magoli mangapi yalifungwa goli la Stars kwenye mechi hizo?... jibu ni goli moja huku Stars ikiibuka na ushindi.

Hivyo haoni kama kuna tatizo kubwa kama linavyozungumzwa bali kilichokosekana kwa wachezaji wake hususani kwa mechi dhidi ya Uganda ni kukosa umakini.
Afisa habari wa TFF Michael Wambura ameshukuru umma wa wapenzi wa soka wa jiji la Mwanza kwa kutimiza wajibu wao kuonyesha uzalendo siku zote za kambi akiamini kuwa kuna wadau wengi wataondoka na timu wakiungana na mashabiki wa Kagera kwenda kuipa sapoti National Teem.
Afisa habari wa TFF Michael Wambura na Kim Poulsen wakiwa mbele ya wandishi wa habari katika ukumbi wa Nyerere hotel Lakairo jijini Mwanza Tanzania

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...