Monday, October 05, 2015

RAIS KIKWETE ATEUA WAKUU WA WILAYA 13





Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete
Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete 

Rais Jakaya Kikwete amewateua wakuu wapya 13 wa wilaya na kuwahamisha vituo vya kazi wengine saba.
Walioteuliwa ni Shaaban Ntanambe ambaye anakwenda Chato; Thabisa Mwalapwa (Hanang), Richard Kasesera (Iringa), Ruth Msafiri (Kibondo) na Abdallah Njwayo (Kilwa).

Wengine ni Asumpta Mshama (Wanging’ombe), Mohammed Utaly (Mpwapwa), Dauda Yasin (Makete), Honorata Chitanda (Ngara), Vita Kawawa (Kahama), Christopher Ng’ubyagai (Mkalama), Hawa Ng’humbi (Kishapu) na Mrisho Gambo (Uvinza).

Wakuu wa wilaya waliohamishwa vituo vya kazi ni Fadhili Nkurlu ambaye anatoka Mkalama, kwenda Wilaya ya Arusha, Wilson Nkambaku anahamishiwa Arumeru, kutoka Kishapu, Francis Miti ambaye anahama Hanang kwenda Monduli na Jowika Kasunga ambaye anahamia Mufindi kutoka Monduli.

Wengine waliohamishwa ni Muhingo Rweyemamu kutoka Makete kwenda Morogoro; Hadija Nyembo anayehamia Kaliua kutoka Uvinza na Benson Mpesya ambaye anahamia Songea Ruvuma kutoka Kahama. Asante kwa kutembelea blog yetu, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kulike page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

DEREVA BODABODA AUAWA NA KUNYOFOLEWA KICHWA NA SEHEMU ZA SIRI



 Waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda wakiwa katika kijiwe chao. PICHA NA MAKTABA

Watu wasiofahamika wamemuua kwa kumchinja mwendesha pikipiki maarufu kama bodaboda, Hosam Abdallahaman (18) na kutoweka na kichwa chake, sehemu zake za siri na pikipiki.   

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Hamis Issa alithibitisha kutokea kwa mauaji hayo juzi usiku katika Kijiji cha Silimka, Kata ya Itilo wilayani hapa.



Kamanda Issa alisema kabla ya mauaji hayo, saa moja usiku, Hosam alikodiwa na abiria ampeleke eneo la Silimka na hakurudi kwenye kituo chake cha kazi hadi alipokutwa akiwa ameuawa majira ya saa 4 asubuhi siku iliyofuata. Asante kwa kutembelea blog yetu, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kulike page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

KIKWETE NA UHURU WAZINDUA BARABARA MUHIMU

Barabara hiyo ni ya pili kufadhiliwa na AfDB baada ya ile ya Arusha-Namanga / Namanga - Athi River
 
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na mwenzake wa Tanzania Jakaya Kikwete wamezindua mradi wa ujenzi wa barabara ya Taveta-Mwatate ambayo inatarajiwa kurahisisha uchukuzi kati ya kataifa hayo mawili.

Barabara ya Arusha-Holili upande wa Tanzania pia inakarabatiwa. Rais Kikwete yumo nchini Kenya kwa ziara rasmi ya siku tatu na Jumanne anatarajiwa kuhutubia kikao cha pamoja cha mabunge mawili ya Kenya.

Mradi wa ujenzi wa barabara hizo mbili umefadhiliwa kwa pamoja na Benki ya Maendeleo ya Afrika na serikali za Kenya na Tanzania. Asante kwa kutembelea blog yetu, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kulike page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

WENGER AFURAHIA USHINDI DHIDI YA MAN UTD

Arsene Wenger
 
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger ameeleza furaha yake baada ya klabu hiyo kupata ushindi wa 3-0 dhidi ya mahasimu wao wa jadi Manchester United katika Ligi Kuu ya Uingereza Jumapili.

Wenger amesema alifurahishwa sana na uchezaji wa timu yake na kueleza kuwa walishangaza Manchester United kuanzia mwanzo wa mechi.

“Kuanzia kwa Petr Cech hadi kwa Theo Walcott wote walicheza vyema. Nimenoa timu nyingi kali lakini hakuna hata moja iliyoweza kucheza mechi 60 katika kiwango sawa. Lazima ukubali kwamba sisi ni binadamu,” alisema.

“Tuko kwenye kinyang’anyiro (cha kushindania taji), tuko alama mbili nyuma ya viongozi Manchester City na natumai matokeo ya leo yatatupa imani ya kuendelea kupigania taji.” Asante kwa kutembelea blog yetu, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kulike page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

TP MAZEMBE KUKUTANA NA ALGER FAINALI

Timu ya TP Mazembe 
 
Klabu ya TP Mazembe ya Congo DRC, Itakutana na klabu ya Algeria USM Alger katika hatua ya fainali ya klabu bingwa barani Afrika.

Mazembe ilijihakikishia nafasi yake siku ya jumapili yaani jana baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya El Merrekh ya Sudan mjini Lubumbashi.

Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania Mbwana Samatta alifunga mara mbili katika ushindi huo huku Muivarycoast Roger Assale akifunga goli la tatu. Asante kwa kutembelea blog yetu, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kulike page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMATATU OKTOBA 05, YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog yetu, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kulike page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

Sunday, October 04, 2015

LUBUVA: MABADILIKO YA WATENDAJI NEC NI YA KAWAIDA

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva.

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC),Jaji Mstaafu Damian Lubuva ametetea uteuzi wa viongozi wapya ndani ya tume huku akisema wanasiasa hawatakiwi kuingilia mambo hadi jikoni.

Jaji Lubuva alisema hayo leo wakati wa mahojiano kwenye kipindi cha Funguka kilichorushwa moja kwa moja na televisheni ya Azam.

"Kuhamishwa au kuteuliwa kwa kiongozi ni jambo la kawaida kwenye taasisi yoyote...uteuzi unaweza kutokea wakati wowote,"alisema Jaji Lubuva. Asante kwa kutembelea blog yetu, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kulike page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

MAMA NA MWANA WAUAWA KWA MAPANGA

Kaimu kamanda wa polisi wa Mkoa wa Geita, Peter Kakamba . 

Mkazi wa Kijiji cha Saragulwa, Kata ya Nyamwilolela mkoani hapa na mwanaye wameuawa kwa kukatwa mapanga na watu ambao hawajajulikana. 

Tukio hilo lilitokea juzi usiku wakati mwanamke huyo, Mageni Hongera (25) akiwa amembeba mgongoni mwanaye, Joyce Ndarusanze (1), akitokea kwenye kibanda chake cha biashara kwenda nyumbani kwake. 

Kaimu kamanda wa polisi wa Mkoa wa Geita, Peter Kakamba alisema jana kuwa askari wa jeshi hilo wanaendelea kufuatilia chanzo cha mauaji hayo. “Ni kweli tukio limetokea, bado sijakusanya vizuri taarifa zake,” alisema Kakamba.  Asante kwa kutembelea blog yetu, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kulike page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

TANESCO: UZALISHAJI WA UMEME UMESHUKA


Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) limesema kuwa mgao wa umeme unaoendelea nchini umesababishwa na kushuka kwa uzalishaji wa umeme katika mabwawa ya maji kwa asilimia 81.3. 

Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Felchesmi Mramba amesema leo jijini dar es Salaam kuwa uwezo wa juu wa mitambo yote ya kuzalisha umeme wa maji ni megawati 561, lakini kwa sasa uzalishaji wote wa umeme wa maji ni megawati 105 ambazo ni sawa na asilimia 18.7. 

Kuhusu umeme wa gesi, TANESCO walisema kuwa uwezo wa kuzalisha umeme kupitia Kampuni ya Pan Africa ulishuka kutoka megawati 340 hadi kufikia megawati 260. Asante kwa kutembelea blog yetu, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kulike page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI OKTOBA 04, YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
.
.
.

Asante kwa kutembelea blog yetu, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kulike page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

Monday, September 28, 2015

MGOMBEA UBUNGE WA CHADEMA DODOMA MJINI APATA DHAMANA

Mgombea ubunge wa jimbo la Dodoma mjini kupitia
Mgombea ubunge wa jimbo la Dodoma mjini kupitia Chadema, Benson Kigaila  

Ulinzi mkali leo umewekwa katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Dodoma ili kuzuia wafuasi wa Chadema waliokwenda kusikiliza kesi inayomkabili mgombea ubunge wa jimbo la Dodoma mjini Benson Kigaila na kusababisha lango la kuingilia lifungwe.

Kigaila na wenzake 10 wanakabiliwa na mashitaka matatu ikiwemo kumpiga na kumjeruhi polisi, kufanya maandamano bila ya kibali na pamoja na kutoa lugha za matusi katika kituo cha polisi makosa ambayo watuhumiwa hao waliyakana yote.
Mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi katika Mahakama ya Wilaya ya Dodoma, James Karayemaha, Wakili wa Serikali Beatrice Nsana amesema kuwa watuhumiwa hao walitenda makosa yote Septemba 25 mwaka huu majira ya jioni.
Nsana amesema kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na kuomba mahakama ipange tarehe ya kuanza kusikilizwa ambapo mahakama imekubali na kupanga Oktoba 12 mwaka huu huku dhamana ikiwa wazi.
Mara baada ya kutimizwa kwa masharti ya dhamana kwa washitakiwa wote, viongozi hao waliondoka chini ya ulinzi mkali wa polisi na kusindikizwa hadi katika ofisi za kanda za chama hicho ambako Kigaila alizungumza na waandishi wa habari. Asante kwa kutembelea blog yetu, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kulike page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

CELINE DION ARUDI KWENYE MUZIKI

celine dion
BAADA ya Celine Dion kukaa kwa muda mrefu bila ya kufanya muziki kutokana na kumuuguza mume wake, Rene Angelil, sasa ameanza kazi ya muziki upya.

Celine alipanda jukwaani juzi huku mume wake akiwa pembeni na kabla ya kuimba aliwaambia mashabiki: ‘Nadhani kila mmoja anajua nini ninataka kukufanyia leo siku yangu rasmi.’

Hata hivyo, msanii huyo alijikuta akidondosha chozi kutokana na mapokezi aliyoyapata kutoka kwa mashabiki wake.

Baada ya kumaliza kuimba msanii huyo aliwashukuru mashabiki hao na kuwaahidi kuwapa burudani mbalimbali siku zijazo. Asante kwa kutembelea blog yetu, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kulike page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

“Nashukuru kwa uwepo wenu hapa, lakini kikubwa kilichonifanya niwe hapa ni watoto wangu watatu na mume wangu ndio waliniambia nifanye hivi, nawapenda sana watoto wangu pamoja na mume wangu na nipo tayari afie mikononi mwangu,” alisema Celine

SIMBA WASHIKANA UCHAWI, YAMSHTAKI MWAMUZI

Simba-vs-Yanga-8

KIPIGO ilichokipata timu ya Simba kwenye mchezo dhidi ya mahasimu wao, Yanga juzi kimezua mapya kwa wekundu hao baada ya wachezaji watatu wa safu ya ulinzi kudaiwa kufanya hujuma

Yanga ilivunja uteja dhidi ya Simba kwa kuichapa mabao 2-0 yaliyofungwa na washambuliaji, Amissi Tambwe na Malimi Busungu.

Habari za kutoka ndani ya Simba zilizolifikia gazeti hili zimedai kuwa wachezaji hao wa safu ya ulinzi walishindwa kabisa kuwazuia washambuliaji wa Yanga, waliofunga mabao rahisi jioni hiyo. Asante kwa kutembelea blog yetu, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa kulike page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

Wednesday, September 23, 2015

DIEGO COSTA KUKOSA MECHI TATU


Diego Costa atakosa michezo mitatu baada ya chama cha soka cha England FA kuthibitisha kukutwa na makosa.

Costa alikana mashtaka yaliyokuwa yakimkabili kuhusiana na kumfanyia fujo mlinzi wa Arsenal Laurent Koscielny katika ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Arsenal.

Costa mwenye miaka 26 alionekana kuweka mikono yake juu ya uso wa Koscielny kabla ya kuanza kuzozana na Gabriel Paulista ambaye baadaye alitolewa nje kwa kadi nyekundu. Mlinzi huyo wa Arsenal alitolewa nje na mwamuzi Mike Dean kwa kumfanyia vurugu mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Hispania.

Costa atakosa mchezo wa kombe la ligi dhidi ya Walsall siku ya jumatano sambamba na ile ya ligi kuu kati ya Newcastle na Southampton. 

Baada ya kuthibitisha kuwa mwamuzi wa mchezo hakuona tukio la Costa na Koscielny, chama cha soka England kimesambaza kanda hizo za vidio kwa waamuzi wakongwe watatu wa zamani.

Monday, September 14, 2015

MTUHUMIWA WA UGAIDI AJARIBU KUJIUA KWA KUJIRUSHA GHOROFANI



Kamishna wa polisi Kanda Maalum wa Dar es
Kamishna wa polisi Kanda Maalum wa Dar es Salaam, Suleiman Kova 

Mtu anayedaiwa kuwa mratibu wa matukio ya ugaidi, uporaji wa silaha na mauaji katika vituo vya polisi , Ally Ulature (60) amejeruhiwa baada ya kujirusha katika ghorofa  kwa kile kinachodhaniwa kuwa ni azimio la kujiua  au kutoroka.

Akizungumza leo, Kamishna wa polisi Kanda Maalum wa Dar es Salaam, Suleiman Kova amesema Ulature ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Mnandimkongo, wilayani Mkuranga  alikamatwa mwezi huu baada ya msako mkali wa polisi.
Kamanda Kova amesema Ulature amejirusha kutoka ghorofa ya tatu katika jengo la makao makuu ya polisi alipokuwa akihojiwa na maofisa upelelezi. Asante kwa kutembelea blog hii, endelea kuwa nasi, like page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

Sunday, September 13, 2015

MATOKEO YA MECHI ZA UFUNGUZI WA LIGI KUU TANZANIA BARA (VPL) HAYA HAPA


Pazia la ligi kuu Tanzania bara limefunguliwa rasmi jana ambapo michezo saba zimechezwa kwenye viwanja tofauti wakati jumla ya timu 14 zilikuwa viwanjani zikiwania pointi tatu muhimu, matokeo ya mechi zote zilizochezwa siku ya Jumamosi ni kama ifuatavyo; 

Azam FC 2-1 Tanzania Prisons (Azam Complex, Chamazi) 

African Sports 0-1 Simba (Mkwakwani, Tanga) 

Ndanda FC 1-1 Mgambo JKT (Nangwanda Sijaona, Mtwara)

Toto Africans 1-0 Mwadui FC (CCM Kirumba, Mwanza) 

Stand United 0-1 Mtibwa Sugar (Kambarage, Shinyanga)

Majimaji FC 1-0 JKT Ruvu (Majimaji, Songea) 

Mbeya City FC 0-1 Kagera Sugar 

Leo utachezwa mchezo mmoja wa ligi kuu Tanzania bara kwa kuzikutanisha Yanga dhidi ya Coastal Union ya Tanga mchezo utakaopigwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

MATOKEO YA MECHI ZOTE ZA EPL ZILIZOPIGWA JUMAMOSI NDIO HAYA HAPA

Jana kulipigwa michezo saba kwenye ligi kuu nchini England (VPL) ambapo mbali na mchezo wa Manchester United dhidi ya Liverpool, kulikuwa na michezo mingine ambayo huenda hukupata muda wa kuitazama yote kwa pamoja. hapa chini kuna matokeo ya mechi zote saba zilizochezwa Jumamosi.

Friday, September 11, 2015

MBUNGE WA CCM ATOA 'SALARY SLIP' KWENYE MKUTANO WA ACT


Mbunge wa Nkasi Kaskazini (CCM), aliyemaliza muda wake, Ally Keissy. PICHA|MAKTABA 

Mbunge wa Nkasi Kaskazini (CCM), aliyemaliza muda wake, Ally Keissy jana aliibuka kwenye mkutano wa kampeni wa chama cha ACT-Wazalendo na kupinga maelezo kwamba mshahara wake wa ubunge ni zaidi ya Sh10 milioni.

Keissy aliwasili kwenye mkutano huo uliokuwa wa mgombea urais wa ACT-Wazalendo, Anna Mghwira na mgombea mwenza wake, Hamad Yusuph Mussa uliofanyika Kijiji cha Namanyere, akiwa kwenye gari lake aina ya Toyota Land Cruiser. 

Mgombea mwenza, Mussa alipopanda jukwaani, alianza kuhutubia kwa kuwaeleza wananchi kwamba mbunge wao, Keissy anayemaliza muda wake ameshindwa kuwaletea maendeleo, hivyo mwaka huu wasimpe kura zao.

ABUBAKAR ZUBERI ACHAGULIWA KUWA MUFTI MPYA WA TANZANIA


Mufti mpya, Sheikh Abubakari Zuberi (aliyeketi katikati) ambaye amechaguliwa leo na wajumbe wa BAKWATA mkoani Dodoma kuwa Mufti wa Tanzania akichukua nafasi ya hayati Sheikh Issa Bin Simba 

ALIYEKUWA Kaimu Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zuberi amechaguliwa kuwa Mufti Mkuu wa Tanzania.

Sheik Zuberi amewashinda wagombea wengine watatu waliokuwa wakiwania nafasi hiyo ya juu ya kuwaongoza waislamu katika Mkutano mkuu wa Bakwata ulioshirikisha wajumbe zaidi ya 550 ambapowajumbe 310 wa Baraza Kuu la Waislamu nchini (Bakwata) walipiga kura na kumchagua.

Mashehe wengine waliokuwa wakiwania nafasi hiyo ni pamoja na Ally Muhidin Mkoyogole, Khamis Abbas Mtupa na Hassan Ibrahim Kiburwa. 

Mufti Zuberi anakuwa ni Mufti wa tatu kuchaguliwa kushika wadhifa huo akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Marehemu Muftu Issa Shaaban Bin Simba aliyefariki Juni 22 mwaka huu jijini Dar es Salaam. Mufti wa kwanza alikuwa Mufti Hemed Bin Jumaa bin Hemed. 

Kabla ya kuchaguliwa , Sheikh Abubakar Zuberi alikuwa Naibu Mufiti wa Sheikh Mkuu wa Tanzania na pia Mjumbe wa Baraza Kuu la Ulamaa nchini.

MAN U YAMRUDIA TENA DE GEA

David De Gea

Manchester United imeanza mazungumzo ya mkataba mpya na mlinda mlango wake David De Gea. 

Mkataba wa sasa na Muhispaniola huyo unafikia ukingoni mwaka 2016 na United wameonyesha matumani ya kurefusha muda wa De Gea kutumika ndani ya klabu hiyo kwa muda mrefu zaidi hii ikitokana na mipango ya De Gea kutimkia kunako klabu ya Real Madrid kukwama.

Manager Louis van Gaal hakumtumia mchezaji huyo wa zamani wa Atletico Madrid mpaka dirisha la usajili lilipofungwa kwa vile hakukuwa na uhakika juu ya mustakabali wake.

Bado haijajulikana kama De Gea ataanza katika mchezo wa jumamosi wa Ligi ligi dhidi ya Liverpool.

Thursday, September 10, 2015

ZIJUE REKODI ZA RONALDO NA MESSI KWENYE MICHUANO YA ULAYA

Messi vs Ronaldo
Lionel Messi na Cristiano Ronaldo wote kwa pamoja wana magoli 80 katika michuano ya Ulaya–lakini je, kila mmoja amefunga kuoka eneo gani? je, kwa mguu gani (kushoto ama kulia)? ndani ya boksi au nje ya boksi? dhidi ya nani (timu gani)? Takwimu zote zipo hapa

Asante kwa kutembelea blog hii, endelea kuwa nasi, like page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

KUMBE ARSENE WENGER ALIKUA ANAKARIBIA KUJIUGA NA REAL MADRID

dadff

Kocha wa club ya Arsenal alikaribia sana kujiunga na club ya Real Madrid, rais wa zamani wa Real Madrid Ramon Calderon ametoa hiyo siri kwamba walijaribu kumpata kocha mara kadhaa lakini Arsene Wenger alisisitiza kubaki na club yake ya Arsenal.

Ramon Calderon alisema,“Nafikiria kila mtu akiwa kama kocha au mchezaji katika wakati wake kucheza soka lazima atakua na hamu ya kujiunga na club ya Real Madrid, hasa ukiwa kwenye club moja kwa miaka 15. 

Kwa kipindi kile Arsene Wenger alikua anapenda kilichokua kinaendelea kwenye club yetu. Nakumbuka aliniuliza unapanga kutengeneza Hollywood au unataka kutengeneza club ya soka. Alikua anazungumzia sera yetu ya kusajili nyota.”

“Mambo hayakwenda kama tulivyotegemea kwasababu alikua anaipenda sana Arsenal, Wenger ni mtu mwenye heshima sana. Hauwezi kumuona yupo kwenye mzozo, anaweza kuwa kwenye mzozo na marefa lakini haiwezi kuwa kama anavyofanya Mourinho.”

“Wenger ni manager mzuri na mtu safi na nina imani hiyo ndiyo sababu ya mafanikio yake.” Asante kwa kutembelea blog hii, endelea kuwa nasi, like page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

Wednesday, September 09, 2015

WANNE WAJITOSA KUWANIA UMUFTI WA TANZANIA


KAIMU Mufti wa Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata), Shekhe Abubakar Zuberi Ally ni miongoni wa mashehe wanne waliojitokeza kuwania kuchaguliwa kwenye nafasi ya Mufti kwenye uchaguzi utakaofanyika kesho jijini hapa. 

Akizungumza jana, Shehe wa Mkoa wa Dodoma, Mustafa Rajab aliwataja mashekhe wengine waliochukua fomu kwa ajili ya kuwania nafasi hiyo kuwa ni Ally Muhidin Mkoyogole, Khamis Abbas Mtupa na Hassan Ibrahim Kiburwa. 

Alisema maandalizi ya mkutano mkuu kwa ajili ya uchaguzi huo, yamekamilika na kwamba wajumbe zaidi ya 550 kutoka mikoa mbalimbali, wameanza kuingia. Katika mkutano huo wa uchaguzi, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Chiku Gallawa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi. 

Alisema wajumbe wa mkutano huo wa kumchagua Mufti wa kuiongoza Bakwata ni wengi, ambapo utawashirikisha mashekhe wote wa mkoa, wilaya, mwenyeviti na makatibu wa mkoa na wilaya na Baraza la Maulamaa, pia viongozi wa serikali wataalikwa.

Alisema Mufti atakayechaguliwa atakuwa wa awamu ya tatu, ambapo walitanguliwa na Mufti Hemed Bin Jumaa bin Hemed na Mufti Issa Bin Simba aliyefariki dunia Juni 22, mwaka huu katika Hospitali ya TMJ, Dar es Salaam.

WANAFUNZI 775,729 KUFANYA MTIHANI WA DARASA LA SABA


JUMLA ya watahiniwa 775,729 wanatarajiwa kuanza mtihani wa kumaliza elimu ya msingi utakaofanyika leo na kesho nchi mzima.

Aidha, serikali imesema hakuna mtu yeyote atakayeruhusiwa kumzuia mtahiniwa yeyote kufanya mtihani kwa sababu yoyote ile, hata ikiwa ni kutolipa ada.

Akizungumza jana, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania, Dk Charles Msonde alisema kati ya hao, watahiniwa wavulana ni 361,502 ambao ni sawa na asilimia 46.6 na wasichana ni 414,227 sawa na asilimia 53.4.

Watahiniwa wasioona walioandikishwa kufanya mtihani ni 76, wakiwemo wavulana 49 na wasichana 27 wakati wale wenye uoni hafifu wanaohitaji maandishi makubwa ni 698, wavulana wakiwa ni 330 na wasichana 368.

Monday, August 31, 2015

MAMBO 10 YA KUZINGATIA ILI SHERIA YA MTANDAO ISIKUPITIE

1. Epuka Kusambaza ujumbe wa uchochezi ama ushawishi wa kisiasa unaoweza kuleta athari kwa jamii yetu kupitia mitandao

2. Epuka Kusambaza au kutunga ujumbe unaoleta uchochezi wa kidini unaoweza kupelekea kuvuruga amani na maelewano kwa jamii kupitia mitandao

3. Epuka Kusambaza picha ama video za utupu ama zilizokosa maadili kwa jamii kupitia mitandao mbalimbali ( Whatsapp, Facebook, YouTube, Instagram n.k)

4. Epuka Kusambaza picha ama video za uchochezi wa kidini ama kisiasa kupitia makundi mbalimbali ama mitandao ya kijamii

Friday, August 28, 2015

ANGALIA MAJINA YA WALIOKOSEA KUJAZA FOMU ZA MIKOPO KWENDA CHUO KIKUU 2015/2016

https://www.facebook.com/jambotz
Kuangalia majina ya waliokosea bofya hapa. Asante kwa kutembelea blog hii, endelea kuwa nasi, like page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz upate habari zetu haraka zaidi.
http://jambotz8.blogspot.com/
Bofya Hapa au picha yeyote hapo juu.

BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU (HESLB) YAWATAKA WAOMBAJI WAREKEBISHE TAARIFA ZAO

 
Mkurugenzi Mtendaji HESLB Bw. George Nyatega

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza orodha ya waombaji wa mikopo kwa mwaka wa masomo 2015/2016 ambao fomu za maombi zimegundulika kuwa na upungufu na kuwataka kufanya marekebisho kabla au ifikapo tarehe 11 Septemba mwaka huu (2015).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Bodi hiyo leo (Ijumaa, Agosti 28, 2015), jumla ya fomu za waombaji wa mikopo 7,788 kati ya 68,445 zilizopokelewa na kuhakikiwa zimegundulika kuwa fomu zina upungufu na kuwataka waombaji kusoma majina yao katika tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz).

Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. George Nyatega, waombaji ambao fomu zao zimegundulika kuwa na upungufu wanatakiwa kurekebisha kabla au ifikapo tarehe 11 Septemba mwaka huu (2015). Asante kwa kutembelea blog hii, endelea kuwa nasi, like page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

JOKATE MSEMAJI KAMATI MPYA YA MISS TANZANIA

MSIMAMIZI wa mashindano ya Urembo Tanzania, ‘Miss Tanzania’, Hashimu Lundenga, ametambulisha kamati mpya ya muda inayoundwa na wajumbe 12 akiwemo Jokate Mwegelo aliyekuwa Miss Tanzania namba mbili mwaka 2006.

Mwenyekiti wa kamati hiyo ni Juma Pinto, makamu mwenyekiti, Lucas Ritta, katibu mkuu ni Doris Mollel na Joketi Mwegelo ambaye ndiye anakuwa msemaji wa kamati hiyo. 

Wajumbe wengine ni Hoyce Temu, Mohamed Bawazir, Gladyz Shao, Magdalena Munisi, Shah Ramadhani, Hamm Hashim, Khalfan Saleh na Ojambi Masaburi.

Lundega alidai ameunda kamati hiyo ili kubadilisha mwonekano mpya wa wajumbe katika shindano hilo kwa mwaka huu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page yetu ya facebook bofya Jambo Tz sasa

WATU 9 WA FAMILIA MOJA WATEKETEA KWA MOTO, ANGALIA PICHA ZAIDI


Askari na wakazi wa Buguruni Malapa, Dar es Salaam wakitazama nyumba iliyoteketea kwa moto na kuua watu tisa wa familia moja usiku wa kuamkia jana.

Watu tisa wa familia moja wameteketea kwa moto baada ya nyumba yao kuungua usiku wa kuamkia jana jijini Dar es Salaam, huku mashuhuda wakisema walikuta miili yao ikiwa imeshikana.

Juhudi za kuwaokoa watu hao waliofariki dunia wakiwa kwenye moja ya vyumba vya nyumba hiyo namba 40 iliyoko katika Mtaa wa Ulam, Buguruni Malapa wilayani Ilala, zilishindikana na chanzo cha moto huo hakijajulikana ingawa mashuhuda wanasema mtungi wa gesi ulilipuka baada ya moto kuwaka kwa muda mrefu.

Walioteketea katika tukio hilo ni mama wa familia hiyo, Samira Juma Ibrahim (42), maarufu kwa jina la Mama Aisha na watoto wake wanne, Ahmed Masoud (15) aliyekuwa mwanafunzi wa kidato cha kwanza, Aisha Masoud (17), aliyekuwa mwanafunzi wa darasa la sita, Abdillah Masoud (10) na Ashraf Masoud (5).

Wengine ni Bimdogo Masoud (72), ambaye alikuwa mgonjwa na mama wa Samira, pamoja na wadogo zake wawili wa kike, Samira Harood (17) na Wahat Saleh (27), ambaye alitokea Unguja, pamoja na Fahir Fesal mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page yetu ya facebook bofya Jambo Tz sasa.

Tuesday, August 25, 2015

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMANNE AGOSTI 25, YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.

.
Asante kwa kutembelea blog hii, endelea kuwa nasi, like page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

MASHA AFIKISHWA MAHAKAMANI LEO

Aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrence Masha 

Waziri wa zamani wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha leo amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu jijini Dar es Salaam baada ya kukamatwa jana jioni. 

Bado waziri huyo wa zamani ambaye sasa amehamia chama cha upinzani cha Chadema hajasomewa mashitaka yake lakini kwa mujibu wa vyanzo vya polisi, Masha anakabiliwa na kosa la kutumia lugha ya matusi kituo cha polisi. 

Masha amefikishwa mahakamani hapo akiwa na vijana wengine 19 ambao wamesomewa shitaka la kutaka kukusanyika bila kibali. Awali taarifa zinasema Masha alifika katika Kituo cha Polisi cha Osterbay jijini Dar es Salaam jana jioni kwa lengo la kutaka kuwadhamini vijana hao na baadaye alishikiliwa na polisi kituoni hapo. 

Masha alikihama Chama cha Mapinduzi hivi karibuni na kujiunga na Chadema na kuteuliwa kugombea Ubunge katika Jimbo la Sengerema katika Uchaguzi Mkuu wa mwezi Oktoba. Mashitaka yanayomkabili waziri huyo wa zamani yanatarajiwa kusomwa baadaye leo mchana. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page yetu ya facebook bofya Jambo Tz sasa.

"SI KAZI NGUMU MWANAMKE KUWA RUBANI" ANNE-MARIE LEWIS

LICHA ya kwamba uwepo wa wanawake katika sekta ya usafiri wa anga kuwa mdogo, uwezo wa kuwa viongozi katika usafiri wa anga hauna mwiko.

Akizungumza na gazeti hili, rubani mwanamke wa kwanza kuongoza ndege aina ya Airbus A380 inayomilikiwa na kampuni ya Fastjet Tanzania, rubani Anne-Marie Lewis anasema wanawake barani Afrika hawapaswi kuogopa kuwa sehemu ya sekta hii inayokua barani kote. 

Anasema si kazi ngumu mwanamke kuwa rubani na kwamba yeye anajiamini na hana woga katika jambo lolote lile ndio maana akaaminiwa na kupata fursa ya kungoza ndege hiyo katika mikoa ya Tanzania na nchi nyingine za jirani.

“Wanawake wanapaswa kuelewa kwamba hakuna aina ya kazi ambayo ipo kwa ajili ya wanaume peke yao, bali wanawake wataleta katika sekta ya usafiri wa anga uwezo wao wa kufanya kazi kwa bidii, kulea na ujuzi wao wa usimamizi bora,” anasema. Kwa mujibu wa Lewis, wanawake wa Afrika wanahitaji kuelewa kwamba nia na uamuzi wao utaondoa hofu au hasara ya kiuchumi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page yetu ya facebook bofya Jambo Tz sasa.

Tuesday, August 18, 2015

KIPINDU PINDU CHAZUKA DAR CHAUA WATU WAWILI


UGONJWA wa kipindupindu umeripotiwa katika Jiji la Dar es Salaam na watu wawili wamethibitika kufa.

Wengine zaidi ya 30 wamelazwa katika hospitali za Mwananyamala na Sinza zilizopo Manispaa ya Kinondoni. Kutokana na tishio la ugonjwa huo, shughuli za kampeni za kisiasa za uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu wa Rais, wabunge na madiwani, zilizo kuwa zianze mwishoni mwa wiki hii, zimesogezwa mbele.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki alithibitisha hayo jana alipokuwa akitoa taarifa ya ugonjwa huo kupitia Kituo cha Televisheni ya Taifa (TBC 1). Alisema watu hao wawili waliofariki, mmoja ni mwanamume na mwingine ni mwanamke na wanatoka Manispaa ya Kinondoni.

MENINAH AOLEWA NA MTOTO WA PROF. MUHONGO


MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Meninah Atick ‘Mennahladiva’ mwishoni mwa wiki aliuaga ukapera kwa kufunga ndoa na mtoto wa aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, Abdukarim Haule.

Meninah, ambaye kipaji chake cha muziki kilianza kuonekana kupitia shindano la Bongo Star Search, ametamba na nyimbo za ‘Dream Tonight’, ‘Ka-Copy Ka-Paste’. Mtoto huyo wa Waziri Muhongo, Peter Haule, amebadili dini na kuitwa Abdukarim Haule na harusi yao ilifanyika Kigamboni, Wilaya ya Temeke, jijini Dar es Salaam.

Licha ya wengi kumpongeza msanii huyo, ameandika katika ukurasa wake wa Instagram kwamba: “Usichague msichana ambaye ni mzuri duniani, chagua anayekupa furaha duniani, maisha ni mafupi na huwezi jua kesho kuna nini, fanya mazuri, asante Mungu kwa kila njia ninayopitia, nazidi kukumbuka kwa kubadilisha maisha yangu na kutumaini milele”.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...