Wednesday, December 24, 2014

RAIS KIKWETE ATA WANAOKIUKA MAADILI KUWAJIBISHWA

Rais Jakaya Kikwete.

 RAIS Jakaya Kikwete 

RAIS Jakaya Kikwete amesema ni lazima watumishi wa umma wanaokiuka maadili ya utumishi wa umma wawajibishwe ili iwe fundisho kwao na kwa wengine.

Rais Kikwete aliyasema hayo Dar es Salaam juzi baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki kumkaribisha kuzungumza na wazee wa jiji hilo.
Awali kabla ya Rais kuzungumza, Sadiki katika hotuba yake alimwelezea Rais jinsi Uchaguzi Mkuu wa Serikali za Mitaa ulivyofanyika jijini mwake na kusema CCM imefanya vizuri kwa kuibuka na ushindi wa jumla ya asilimia 75.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

GEORGE BUSH ALAZWA BAADA YA KUPATA TATIZO LA KUPUMUA

 George H.W Bush.
 
Aliyekuwa rais wa Marekani George H.W Bush amekimbizwa katika hospitali moja ya Houston nchini Marekani baada ya kupatikana na tatizo la kupumua.
Kulingana na madaktari,Bush mwenye umri wa miaka 90 anachunguzwa katika hospitali ya Methodist.
Alipelekwa katika hospitali hiyo na ambalensi jumanne usiku.
Wawakilishi wa Bush wanasema kuwa hatua hiyo ya kupelekwa hospitali ni kama tahadhari.
Rais huyo wa 41 ndio mzee kuwahi kuiongoza Marekani akimshinda Jimmy Carter kwa miezi michache.
Alihudumu kwa muhula mmoja baada ya kushindwa na Rais Bill Clinton.
Bush ambaye hawezi kutumia miguu yake,hivi majuzi alionekana amekaa katika kiti cha magurudumo katika hafla iliofanyika mwezi November katika chuo kikuu cha Texas na mwanawe aliyekuwa rais George W Bush. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

EBOLA BADO TISHIO

 Peter Piot 
 
Shirika la Afya Duniani limesema ugonjwa wa Ebola hautaweza kudhibitiwa kikamilifu katika kipindi cha mwaka mmoja unaokuja.
Mwenyekiti kutoka kitengo maalumu kinachoshughulikia ugonjwa huo, kutoka katika Shirika la Afya Duniani Profesa Peter Piot anasema hali halisi kwa sasa ya ugonjwa huo ni kama ugonjwa utakaodumu muda mrefu.
Profesa Peter Piot ambaye amerejea kutoka nchini Sierra Leone, nchi ambayo imeathiriwa zaidi na ugonjwa huo, ameiambia BBC kwamba amehamasishwa na ahadi za kupatikana kwa kinga mpya ambayo inaaminika itakuwa tayari katika kipindi cha miezi mitatu.
Hata hivyo Profesa Piot ambaye aligundua virusi vya ugonjwa wa Ebola mwaka 1976, ameonya pia kwamba janga lililopo sasa halitakuwa la mwishon na chanjo kudhibiti kirusi hicho itachukua muda kufanya kazi. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Na BBC Swahili

VILABU VYA ULAYA NA TETESI ZA USAJILI

 Gareth Balle akiwa kazini.
 
Uongozi wa Timu ya Manchester United umesema upo tayari kutoa paundi milioni 120 kwaajili ya kumsajili winga Gareth Balle mwenye umri wa miaka 25 kwa mwezi januari kutoka klabu ya Real Madrid , winga ambaye ni miongoni mwa wachezaji ghali zaidi ulimwenguni.
Gareth Bale alijiunga na Real Madrid kwa kuweka rekodi kubwa duniani kwa usajili wa rekodi ya paundi milioni 85.3 mwaka 2013.
Wakati huo huo kocha Laurent Blanc wa Timu ya Paris St Germain anafikiria kumsajili mshambuliaji Edinson Cavani( 27), kwa gharama ya pauni milioni 50 ikiwa ndio hitaji la Timu ya Arsenal katika katika usajili wa mwezi Januari 2015.
Nayo klabu ya Manchester City inandaa pauni milioni 25 katika jitihada za kutaka kumsajili msahambuliaji wa Atletico Madrid Mario Mandzukic (28). Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

EBOSSE: ALGERIA YAPINGA RIPOTI YA MAUAJI

Marehemu Albert Ebosse aliyeaga dunia.Algeria imepinga ripoti ya mauaji yake kwamba mchezaji huyo aliuawa baada ya kuvamiwa. 
 
Waziri wa habari nchini Algeria Mohammed Tahmi amesisiiza kwamba kifo cha mchezaji wa Cameroon Albert Ebosse kilisababishwa na mashabiki waliokuwa wakirushi vitu.
Tahmi ambaye alikuwa akizungumza na radio ya Algeria alikuwa akijibu ripoti ya wiki jana ya daktari wa kuchunguza mauaji kwamba majereha ya Ebosse yalisababishwa na mashambulizi.
Ebosse mwenye umri wa miaka 25 aliaga dunia tarehe 23 mwezi Agosti baada ya kilabu yake JS Kabylie kupoteza 2-1 nyumbani. ''Tumefanya uchunguzi wetu unaoonyesha kwamba mchezaji huyo aliuawa kutokana na kitu kilichorushwa kutoka kwa mashabiki.'',alisema
Mchezaji Ebose aliyekuwa akiichezea timu yake JC kabylie kutoka Algeria
''Mimi si mtaalamu wa sheria lakini nitasema kuwa kifo hicho ni cha bahati mbaya''.,aliongezea ''Vitu vilirushwa kutoka pande zote mbili na wachezaji wote walilengwa na kwa bahati mbaya kisa hicho kikatokea'',alisema.
Swala hilo kwa sasa liko mahakamani ambapo uamuzi utatolewa. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

IVORY COAST WAGOMEA BAJETI YA SERIKALI - AFCON

 Timu ya Ivory Coast 
 
Shirikisho la soka Ivory Coast (FIF) limegomea bajeti waliyopewa na Serikali ya nchi hiyo kwa ajili ushiriki wa timu ya taifa, The Elephants kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika kwa sababu ni ndogo.
Serikali imekubali kutoa dola za Kimarekani 575 805 kwa Tembo wa Ivory Coast kwenye Fainali za AFCON zitakazofanyika Equatorial Guinea kuanzia Januari 17 hadi Februari 8.
Pamoja na hayo, Makamu wa rais wa FIF, Sory Diabate amewaambia Waandishi wa Habari kwamba Hawawezi kwenda CAN (Mataifa ya Afrika) na faranga (za Ivory Coast, CFA Francs) Milioni 310. Kwa kuwa wamewasilisha bajeti yao kwa ufafanuzi mzuri.
Waziri wa Michezo wa nchi hiyo alikuwa tayari kutoa fungu kamili waliloombwa katika bajeti ya awali faranga bilioni 3.5, pamoja na hayo Ivory Coast ilikwenda michuano hiyo mwaka 2013 Afrika Kusini na jumla ya Faranga bilioni 3.9, huku Serikali ikichangia Bilioni 2.7 wakati Tembo walitolewa na Nigeria katika Robo Fainali.
Kikois cha Herve Renard, kitaanza maandalizi yake kwa kuweka kambi Abu Dhabi, Falme za Kiarabu Januari 5, mwakani. Ivory Coast imepangwa Kund D pamoja na Mali, Cameroon na Guinea. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Tuesday, December 23, 2014

RAIS KIKWETE ATENGUA UTEUZI WA PROFESA TIBAIJUKA

Rais Jakaya Kikwete
RAIS Jakaya Kikwete

RAIS Jakaya Kikwete, ametengua uteuzi wa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, huku pia akitengua kitendawili cha nani mmiliki wa fedha za akaunti ya Escrow na kusema sio za umma bali ni za IPTL.
Aidha, Serikali kupitia Kamati ya Maadili inaendelea kumfanyia uchunguzi kwani kuna upungufu wa kimaadili umeonekana kutendeka.
Rais Kikwete aliyasema hayo jijini Dar es Salaam jana alipokuwa anahutubia taifa kupitia wazee na wakazi wa Dar es Salaam kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, lengo likiwa kuzungumzia mambo mbalimbali ya kitaifa, yakiwemo yale yaliyokuwa yakisubiri uamuzi wake, kubwa likitajwa la sakata la Akaunti ya Escrow.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

RAIS KIKWETE: FEDHA ZA TEGETA ESCROW NI ZA EPTL

Rais Jakaya Kikwete akihutubira wazee wa mkoa wa Dar es Salaam kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini hapa.

Rais Jakaya Kikwete amesema fedha zilizochotwa katika Akaunti ya Tegeta Escrow hazikuwa zinafikia Sh306 bilioni, bali ni Sh202 bilioni na zilikuwa mali ya Kampuni ya Kufua Umeme ya IPTL.
Akijibu swali alilojiuliza mwenyewe katika hotuba yake ya zaidi ya saa mbili kuwa: “Fedha hizi mwenyewe nani, umma au IPTL?” Rais Kikwete alisema kumekuwapo na maneno mengi, kila mtu anasema yake na wenzangu Wakwere tunasema ‘tunazoza sana’ akimaanisha waongea sana.
Alisema, “Kimsingi fedha hizi ni za IPTL, katika swali pesa za nani, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) alipoulizwa na Kamati ya Bunge alisema humu yawezekana zipo za umma pia zipo za IPTL.
“Nilipomuuliza maana, akasema zamani walikuwa wanalipa moja kwa moja kwa Tanesco lakini baada ya mzozo walikubaliana kwanza waziweke Benki Kuu ya Tanzania (BoT).”
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE DESEMBA 23, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAALIM SEIF AITABIRIA CUF USHINDI MKUBWA


Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad 


Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad amesema upepo wa kisiasa unakivumia vizuri chama chake na ana matumaini Uchaguzi Mkuu ujao kitapata viti 18 vya uwakilishi katika ngome ya CCM Unguja.

Hivi sasa CUF inashikilia majimbo manne ya Unguja kati ya 32 na kwa muda wote ngome yake imekuwa ni Pemba kinakoshikilia majimbo yote 18.

Akihutubia mkutano wa hadhara baada ya kuzindua miradi ya maendeleo katika Jimbo la Magogoni, Wilaya ya Magharibi Unguja, Maalim Seif alisema suala la Katiba Mpya na ufisadi uliokithiri vitaipa wakati mgumu CCM, hasa upande wa Zanzibar.
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

KITISHO CHA USALAMA: POLISI AUAWA NCHINI KENYA

Polisi nchini Kenya katika doria.
 
Askari mmoja ameuawa na mwingine akiwa mahututi baada ya kushambuliwa kwa kupigwa risasi kaskazini mwa Kenya.
Askari hao wa Kenya wanadaiwa kushambuliwa na watu wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa kundi la Al Shabaab.
Askari hao wa jeshi la polisi kikosi cha ziada walikutwa na kisa hicho mjini Wajir kaskazini mwa Kenya usiku wa kuamkia leo. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

RAIS WA UFARANSA AWATULIZA RAIA WAKE

Rais wa Ufaransa  

Rais wa Ufaransa amewataka raia wake wasishtushwe na visa vya kushambuliwa kwa polisi na raia katika kipindi cha siku kadhaa.
Rais Francois Hollande ameyasema hayo baada ya mtu mmoja kuendesha gari na kulivurumisha katika soko la Krismasi lililosheheni watu, magharibi mwa mji wa Nantes na kujeruhi watu kumi.
Waendesha mashtaka wamesema, shambulizi hilo linafanana na lile lililotokea katika mji wa Dijon siku ya Jumapili ambapo dereva wa gari aliyekuwa akisema kwa sauti maneno ya kiislamu mfululizo alipowagonga wapita kwa miguu katikati mwa mji.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

PLUIJM AWALILIA KASEJA NA KIIZA

Kocha wa Yanga, Hans Van Pluijm akiteta jambo na wachezaji wake, siku za hizi karibuni. Picha na maktaba 

Kocha wa Yanga, Hans Van Pluijm amesikitishwa na kitendo cha kuondoka kwa nyota wake Juma Kaseja, Hamisi Kiiza na Didier Kavumbagu, lakini akawataka wachezaji wake wasahau yaliyopita na waangalie yajayo.
Pluijm amechukua mikoba ya Marcio Maximo aliyetupiwa virago baada ya Yanga kufungwa na Simba 2-0 katika mchezo wa Nani Mtani Jembe kama ilivyokuwa mwaka jana alipoinoa timu hiyo kwa mara ya kwanza baada ya Ernie Brandts kutimuliwa kutokana na timu hiyo kunyukwa 3-1 na Simba.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Pluijm alisema Kaseja alikuwa nahodha, lakini sasa hayupo kutokana na tofauti zake na viongozi.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

PHIRI AOMBA MIAKA MIWILI


Kocha wa Simba, Mzambia Patrick Phiri amesema iwapo klabu yake itamvumilia kwa miaka miwili atatengeneza wachezaji bora kama ilivyo kwa nyota wa TP Mazembe ya DR Congo (DRC), Mbwana Samatta.

Phiri alisema: “Najivunia mafanikio ya Samatta (Mbwana). Kwanza yanatokana na uvumilivu wake na kujituma kwake pamoja na kupewa nafasi. Naamini makocha wanapopewa muda na timu wanaweza kutengeneza wachezaji wapya na hata kuinufaisha klabu kwa kuuza wachezaji hao kwa bei nzuri huku ikiendelea kutengeneza wengine.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

YANGA KWA WANAJESHI, AZAM SUDAN

Mabingwa wa Tanzania, Azam wataanza harakati zake za Ligi ya Mabingwa Afrika, kwa kuivaa El Merreikh ya Sudan, wakati Yanga wenyewe watakuwa na kibarua kwa BDF ya Botswana katika Kombe la Shirikisho.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa jana na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) inaonyesha wawakilishi wa Tanzania wataanzia nyumbani katika michezo yao itakayopigwa Februari 13, 14, 15 na mechi za marudiano zitakuwa kati ya Februari 27, 28 na Machi Mosi 2015.

Azam itawakaribisha El Merreikh na kurudiana wiki mbili baadayezijazo nchini Sudan na endapo itafanikiwa kushinda mechi hiyo katika hatua ya 16 bora itacheza na mshindi kati ya Lydia Ludic B.A (Burundi) au Kabuscord do Palanca (Angola).
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...