Tuesday, November 18, 2014

VIONGOZI MANYARA, KITETO WAKALIA KUTI KAVU


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akitoa kauli ya serikali bungeni jana, kuhusu mauaji ya wakulima na wafugaji wa Wilayani Kiteto, Mkoani Arusha.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amesema Serikali itafanya mabadiliko ya kiutawala katika ngazi mbalimbali Wilaya ya Kiteto na Mkoa wa Manyara wiki hii ili kuimarisha uongozi kukabiliana na mauaji ya wakulima na wafugaji yaliyosababisha vifo vya watu 17 tangu Januari 12 mwaka huu hadi sasa.

Pinda alisema hayo bungeni mjini Dodoma jana wakati akitoa taarifa kuhusu vurugu zinazoendelea Kiteto kati ya wafugaji na wakulima na kusababisha mauaji.

Alisema mabadiliko ya uongozi wa kiutawala katika eneo hilo ni moja ya hatua ambazo zinachukuliwa kitaifa nyingine zikiwa ni kuendelea kutoa elimu kwa umma juu ya kuondoa na kuepuka na kutatua migogoro inayojitokeza kwa njia ya amani. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE NOVEMBA 18, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KANALI AHUKUMIWA KUNYONGWA, CONGO

Waaandamaji wakipinga kuuawa kwa Kanal Ndala
Mahakama ya kijeshi Mashariki mwa Jamuhuri ya Demokrasi ya Congo imemhukumu kifo Kanali Birocho Nzanzu baada ya kubainika na makosa ya kutaka kumuua afisa wa jeshi la nchi hiyo aliyekuwa mstari wa mbele kutokomeza wapiganaji wa M23.
Kanal Mamadou Ndala anayedaiwa kuuawa na njama za Kanal Birocho Nzanzu
Afisa anayedaiwa kupangiwa njama za kuuawa ni Mamadou Ndala mabaye kwa kiasi kikubwa aliamini katika vita dhidi ya kundi hilo la wapiganaji na ambaye aliuawa mwezi januari mwaka huu. Hata hivyo hukumu hiyo imetolewa kwa watuhumiwa nane ambapo kati ya hao mmoja ndiye Kanali Ndala aliyehukumiwa kifo. Mahakama imebainisha kuwa Kanali Nzanzu amekuwa akitumiwa na waasi wa ADF kutoka Uganda kuandaa maujaji. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

GAVANA ATANGAZA HALI YA HATARI, MISSOURI


Machafuko Missouri

Gavana wa jimbo la Missouri nchini Marekani ametangaza hali ya hatari kabla ya kutolewa uamuzi muhimu kuhusu kumfungulia mashitaka ya jinai au la dhidi ya afisa wa polisi mzungu, ambaye alimuua kwa kumpiga risasi kijana wa Kiafrika ambaye hakuwa na silaha.
Mauaji hayo yaliyotokea katika mji wa Ferguson mwezi Agosti yalisababisha vurugu katika mitaa kwa siku kadha na kuamsha mjadala kuhusu uhusiano kati ya polisi na jamii ya watu weusi nchini Marekani.
Idara ya polisi ya Kaunti ya St. Louis ndiyo wanaosimamia maandamano yoyote. Meya wa St. Louis, Francis. Slay, amezungumzia kuhusu tahadhari wanayochukua. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Monday, November 17, 2014

MKAPA ATAKA WAZEE NCHINI WASIBEZWE


Rais Mstaafu Benjamin Mkapa  

Rais Mstaafu, Benjamini Mkapa, amewataka viongozi na Watanzania kutobeza busara na hekima za wazee kwa kuwa bado wana mchango mkubwa kwa Taifa.

Kadhalika mkuu huyo wa zamani wa nchi, alisema kuwa, mzee kuota mvi kichwani haina maana ya kupungukiwa na hekima na maarifa kama wengi wanavyofikiria

Mkapa alitoa kauli hiyo juzi jioni wakati mahafari ya kwanza ya Shule ya Sekondari ya St Peter Claver iliyoko nje kidogo ya Mji wa Dodoma.

Alisema anashangazwa kuona maeneo mengi wazee wanapuuzwa na kudharauliwa kama vile hawana mchango wowote kwa maendeleo ya jamii. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

PROF. MAGHEMBE ASEMA URAIS SIO MASHINDANO YA UREMBO

Waziri wa Maji, Prof Jumanne Maghembe akizungumza na waandishi wa habari wa gazeti hili, walipomfanyia mahojiano maalumu ofisini kwake mjini Dodoma, hivi karibuni. 

Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe ameshangazwa na utitiri wa watu wanaotaka kugombea urais kwenye Uchaguzi Mkuu 2015, akisema nafasi hiyo ya juu nchini haifanani na mashindano ya urembo ambayo mtu yeyote anaweza kujaribu.

Mbunge huyo wa Mwanga alisema watu hao wanaojitokeza kuwania urais hawaelezi wanataka kulifanyia nini Taifa na akashauri wasioweza kueleza hoja zao wasichaguliwe kushika nafasi hiyo.

“Urais unahitaji kuwa na sifa, dira na ajenda kwa Taifa,” alisema Profesa Maghembe wakati wa mahojiano maalumu na gazeti hili mjini hapa.

Kauli ya Profesa Maghembe imekuja wakati Taifa likijiandaa kwa Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba, 2015, huku chama chake, CCM kikikabiliwa na kazi ngumu ya kumpata mrithi wa Rais Jakaya Kikwete ambaye anamaliza muda wake. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SHY-ROSE, SPIKA ZZIWA KIKAANGONI TENA


Mbunge Shy-Rose Bhanji.
Bunge la Afrika Mashariki (Eala) limeitishwa tena, zamu hii jijini Nairobi, Kenya ambako litakutana kuanzia leo mchana, huku kukiwa na shinikizo kubwa kutoka kwa wabunge 32 linalotaka kung’olewa kwa Spika wa Bunge hilo, Dk Margaret Zziwa na kuwajibishwa kwa mbunge kutoka Tanzania, Shy-Rose Bhanji.
Bunge hilo linakutana baada ya kuahirishwa kwa muda usiojulikana kutokana na kukosekana kwa mwafaka baina ya wabunge kwa upande mmoja na baadhi ya wabunge na Spika Zziwa kwa upande mwingine lilipokutana Kigali, Rwanda hivi karibuni. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBA 17, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WAZIRI AJIUZULU KUPISHA UCHUNGUZI

 
Miguel Macedo waziri wa mambo ya ndani wa Ureno aliyejiuzulu 
 
Waziri wa mambo ya ndani wa Ureno amejiuzulu kupisha uchunguzi kuhusu tuhuma za rushwa inayohusishwa na utoaji vibali vya mgawo wa makazi.
Miguel Macedo amesema hahusiki na kashfa hiyo lakini anajiuzulu kulinda heshima ya taasisi za serikali.
Polisi wamewakamata watu 11, akiwemo mkuu wa idara ya uhamiaji nchini humo, siku ya Alhamisi.
Ureno inatoa visa za daraja la kwanza kwa wageni wanaotaka kuwekeza nchini humo.
Mnufaika mkuu wa uharakishaji wa vibali ni raia wa China ambao wamekuwa wakiwekeza kiasi kikubwa nchini Ureno.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAFUA YA NDEGE YATHIBITISHWA UINGEREZA

Ndege wanaofugwa wanakabiliwa na milipuko ya mafua ya ndege

Mlipuko wa mafua ya ndege umethibitishwa katika shamba moja la kuzalishia bata mashariki mwa Yorkshire, nchini Uingereza, wamesema maafisa.
Wizara ya Mazingira, Chakula na Masuala ya Vijijini (Defra) imesema hatari kwa afya ya umma ni ndogo sana. Ndege wasiohitajika wanaondolewa kutoka eneo hilo na eneo la kuwatenga limeandaliwa.
Tatizo hilo bado halijathibitishwa, lakini aina ya kirusi cha H5N1 hakijaweza kubainishwa na maafisa wa Defra.
Kirusi hicho husambaa kati ya ndege na katika matukio ya nadra, kinaweza kuwaathiri binadamu.
Picha ikimwonyesha mchuzi akiuza bata wake katika mtaa mmoja mjini Shanghai,China
Eneo la kuwatenga ndege lililopo kuzunguka shamba hilo litazuia ndege na kinyesi cha ndege ndani au nje ya eneo hilo.Ndege wote pia watatengwa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Sunday, November 16, 2014

MTOTO ANAYEDAIWA KUGEUKA NYOKA AZUA KIZAA ZAA

Mtoto mchanga mwenye umri wa miezi minne amezua kizaazaa cha aina yake, baada ya kuwapo taarifa kwamba mara kadhaa umbo lake limekuwa likigeuka na kuwa nyoka na mwili wake ukiendelea kudhoofu kutokana na kukataa kunyonya maziwa ya mama yake.
Mtoto huyo (jina lake tunalihifadhi kwa sasa), wiki iliyopita alivuta umati wa wakazi wa Kijiji cha Nkome mkoani Geita ambao walifurika ndani na nje ya Kanisa la AICT Nkome, lililopo kijiji hapo, kushuhudia maombi ambayo alikuwa akifanyiwa ili kumkomboa katika kile kilichotafsiriwa kuwa ni mateso dhidi yake.
Ilikuwa saa 4.00 asubuhi Jumamosi, Novemba 8 mwaka huu wakati mtoto huyo alipofikishwa katika kanisa hilo na kuanza kufanyiwa maombi na sababu ya hatua hiyo ikielezwa kuwa ni kutokana na kuwa na umbo la nyoka na kwamba matendo yake yanaashiria kwamba mwenye asili ya nyoka ndani ya roho yake. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MBOWE AILIPUA SERIKALI KUHUSU BANDARI BUBU NCHINI

 
Mwenyekiti wa Chacha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe. PICHA|MAKATBA  

Mwenyekiti wa Chacha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amesema kuwa uwepo wa bandari bubu zinazopitisha bidhaa kwa magendo kutoka nje ni miongoni mwa sababu zinazoua viwanda vya sukari hapa nchini.
Amesema kuwa viwanda vya miwa vinapokufa, wanaoumia siyo wenye viwanda bali wakulima wa miwa. Mbowe alisema hayo juzi alipohutubia mamia ya wafuasi wa chama hicho mjini Turiani , Mkoa wa Morogoro katika siku ya kwanza ya ziara yake mkoani humo.

Ziara hiyo ni ya Operesheni Delete CCM (ODC) yenye lengo la kuvihamasisha vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kuiondoa CCM madarakani kuanzia katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

PINDA AHIMIZA KUCHANGIA ELIMU

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. PICHA|MAKTABA 

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ametoa rai kwa Watanzania kujenga utamaduni wa kuchangia maendeleo ya sekta ya elimu, badala ya kujikita kuchangia sherehe za harusi.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Stephen Kwebwe aliyezungumza kwa niaba ya Pinda katika sherehe ya kuchangia ujenzi wa mabweni ya Shule ya Sekondari Mwenyeheri Anuarite iliyopo Makoka, jijini Dar es Salaam.
“Urithi pekee kwa watoto wetu ni elimu, unaweza kumwachia mali, lakini itakwisha, ukimwachia elimu hakika huu ndiyo urithi pekee…: Watanzania wenzangu, tujitoe kuchangia sekta ya elimu kama ambavyo tunafanya katika sherehe,” alisema Kebwe akiongeza:
“Utamkuta mtu anachangia fedha nyingi katika harusi na kama tunavyojua harusi moja, ukianza na ‘send off’, ‘kitchen part’ na harusi yenyewe ni fedha nyingi, lakini mtu huyo huyo ukimwambia achangie masuala ya elimu, hutamwona.”
Naye Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Gaudence-Makoka wamiliki wa shule hiyo, Padre Evarist Tarimo, alisema kuwa malengo ya sherehe hiyo ni kuchangisha Sh250 milioni kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa bweni la wavulana ili kuondoa adha wanayoipata kwa sasa.
“Hivi sasa vyumba vya madarasa tunavitumia kama mabweni, hivyo wanasomea humo na kulala humo humo, jambo ambalo kitaaluma si zuri. Tunatarajia tutakapomaliza ujenzi huo tutawawezesha wanafunzi wetu kusoma na kulala katika mazingira mazuri na nina hakika juhudi za wadau zitaweza kukamilisha ujenzi huu,” alisema. Habari tulizozipata baadaye zilisema jumla ya Sh41.2 milioni zilikusanywa. Fedha taslimu ni Sh13.3 milioni. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOVEMBA 16, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
. 
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Saturday, November 15, 2014

BUTIKU AMKINGIA KIFUA WARIOBA

Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya Mwalimu Nyerere , Joseph Butiku 

Taasisi ya Mwalimu Nyerere imesema kuwa wanaotaka aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba akae kimya kuhusu Katiba Inayopendekezwa hawana hoja.
Imesema kuwa wanaosema hivyo hasa wale wa chama tawala (CCM) wanatakiwa kujiuliza kwa kipindi cha miaka 50 iliyopita wamefanya nini kuhusu Katiba, ikisisitiza kuwa itaendelea kufanya midahalo ya kuwaelimisha Watanzania kuhusu mchakato wa Katiba ili utakapofika wakati wa kura ya maoni waelewe kipi wanatakiwa kukifanya kwa mustakabali wa taifa.
Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Joseph Butiku alisema hayo jana ofisini kwake jijini Dar es Salaam katika mahojiano maalumu na gazeti hili kuhusu kazi na majukumu ya Taasisi ya Mwalimu Nyerere tangu ilipoanzishwa hadi sasa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...