Monday, November 17, 2014

MKAPA ATAKA WAZEE NCHINI WASIBEZWE


Rais Mstaafu Benjamin Mkapa  

Rais Mstaafu, Benjamini Mkapa, amewataka viongozi na Watanzania kutobeza busara na hekima za wazee kwa kuwa bado wana mchango mkubwa kwa Taifa.

Kadhalika mkuu huyo wa zamani wa nchi, alisema kuwa, mzee kuota mvi kichwani haina maana ya kupungukiwa na hekima na maarifa kama wengi wanavyofikiria

Mkapa alitoa kauli hiyo juzi jioni wakati mahafari ya kwanza ya Shule ya Sekondari ya St Peter Claver iliyoko nje kidogo ya Mji wa Dodoma.

Alisema anashangazwa kuona maeneo mengi wazee wanapuuzwa na kudharauliwa kama vile hawana mchango wowote kwa maendeleo ya jamii. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz


“Wazee wasibezwe wala kupuuzwa, kwani mvi zao kichwani siyo ishara ya kuishiwa busara na hekima,” alisema Mkapa.

Aliwataka wanafunzi na watu wengine kujenga tabia ya kusoma zaidi na kudadisi mambo ili wawe na uelewa mpana wa kuisaidia nchi yao katika mambo mbalimbali ya maendeleo.

“Tumekosa utamaduni wa kupenda kujisomea, watu ni wavivu, hawataka kusoma. Naomba tupende kusoma kwa faida yetu binafsi na hata Taifa,” alisema.

Alisema kuwa elimu ya kidato cha nne siyo mwisho wa kupata mafanikio, bali ni mwanzo wa kufikiria na kuona mbali zaidi ili kufikia malengo ya kuelemika.

Hata hivyo, kiongozi huyo alisisitiza zaidi vijana kupenda kusoma masomo ya sayansi.

“Kuna shida ya wanafunzi wa masomo ya sayansi, hii inakwanza maendeleo ya Taifa. Jitokezeni msome masomo haya ili muikomboe Tanzania,” alisema.

Katika mahafali hayo, Mkapa alichanga Sh5 milioni kwa ajili ya kuimaisha maabara ya shule hiyo.

Kwa upande wake, Mkuu wa shule hiyo Padre James Ayaga, alitaja moja ya changamoto wanazokabiliana Aliwaomba wazazi kuendelea kuchangia na kuisaidia shule hiyo ili iweze kufikia ndoto zake kwa kutoa wanafunzi wengi wa masomo ya sayansi.nazo kuwa ni pamoja na ukosefu wa vifaa vya kutosha vya maabara. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...