Monday, November 10, 2014

UTATA TENA: MISS TANZANIA MPYA SI RAIA WA TANZANIA...??!

Baada ya taji la Miss Tanzania kuvishwa kwa mshindi wa pili, utata mwingine umeibuka baada ya mrithi huyo, Lilian Kamazima kudaiwa kuwa si raia.

Jana kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kulikuwa na taarifa zinazodai kuwa Lilian siyo raia wa Tanzania na kwamba anatokea Rwanda.

Akizungumzia tuhuma hizo, Mkurugenzi wa Lino International Agency ambao ndiyo waandaaji wa mashindano ya Miss Tanzania, Hashim ‘Uncle’ Lundenga alisema tuhuma hizo kuhusu Lilian siyo kweli. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MBOWE 'AMWAGA SUMU' NYUMBANI KWA SAMUEL SITTA...!!!


Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akiwasili kwenye Uwanja wa Extended mjini Urambo, Tabora alikohutubia mkutano wa hadhara juzi. 


Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amefanya mkutano mkubwa Urambo Mashariki na kumshutumu Mbunge wa jimbo hilo, Samuel Sitta kwa kuchakachua maoni ya wananchi katika mchakato wa Katiba Mpya.

Katika mkutano huo ulifanyika katika Uwanja wa Extended mjini hapa takriban mita 100 kutoka nyumbani kwa Sitta aliyeongoza Bunge la Katiba, Mbowe alisema historia ya nchi hii itamhukumu mbunge huyo kwa maovu hayo.

Alisema kutokana na uovu huo wa Sitta ambaye amekuwa akiisifia Katiba Inayopendekezwa kuwa itakuwa nzuri Afrika Mashariki na Kati, vyama vya upinzani vitaendelea kuidai katiba ya wananchi hata kwa miaka 100 ijayo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

IKULU: "TUMEFEDHEHESHWA KWA KITENDO CHA JAJI WARIOBA KUSHAMBLIWA"


Balozi Ombeni Sefue


Serikali inapitia upya ulinzi wa viongozi wastaafu ili kuepuka fedheha iliyotokana na vurugu alizofanyiwa Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba hivi karibuni.

Mpango huo umeelezwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue mwishoni mwa wiki, akisema Serikali imekerwa na kufedheheshwa kutokana na tukio hilo lililotokea wakati wa mdahalo wa Katiba Inayopendekezwa katika Hoteli ya Blue Pearl, Dar es Salaam Novemba 2, mwaka huu.

“Kimsingi tutakachokifanya ni kupitia upya mpango wa ulinzi wa viongozi wote waliostaafu, japokuwa huwa tunafanya hivyo mara kwa mara, lakini kwa hili la Mzee Warioba tunaliangalia kwa umakini wake.

“Tumekerwa sana na tukio lile, halikutufurahisha hata kidogo kama Serikali kwa kuwa limemvunjia heshima Mzee Warioba, yule ni mzee wetu, anahitaji heshima, kwanza heshima yake na ulinzi.”

Kauli hiyo ya Sefue imekuja wakati mdahalo huo uliovunjika baada ya Mzee Warioba kushambuliwa, ukiwa umetangazwa kufanyika upya Jumapili Novemba 16, mwaka huu katika hoteli hiyohiyo.

Mjumbe wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Humphrey Polepole alithibitisha jana kuandaliwa kwa mdahalo huo kuanzia saa 9.00 alasiri siku hiyo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBA 10, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

'KURA YA MAONI MWANZO WA KUDAI KATIBA MPYA'


Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo - Bisimba akizungumza na waandishi wa Gazeti la Mwananchi katika mahojiano maalumu yaliyofanyika hivi karibuni Dar es Salaam.

Wakati Serikali ikihaha kuhakikisha inaandika historia mpya kwa kupitisha Katiba Inayopendekezwa Aprili 30, mwakani, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo – Bisimba amesema siku hiyo itakuwa mwanzo wa Watanzania kudai Katiba Mpya.

Dk Kijo – Bisimba, mmoja wa wanaharakati maarufu wa haki za binadamu nchini, amesema katika mazingira ambayo mchakato wa Katiba una dosari nyingi, ilikuwa ni busara kuusimamisha kwanza ili kujitathmini kabla ya kuendelea na Kura ya Maoni.

Mhitimu huyo wa shahada ya uzamivu ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Warwick, Uingereza, alisema hayo katika mahojiano maalumu na gazeti hili yaliyofanyika wiki iliyopita.

“Katiba hata ikiwa nzuri kiasi gani, kama haitokani na wananchi, haiwezi kukubalika,” alisema Dk Kijo – Bisimba akisisitiza hoja yake. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MLIPUKO WATIKISA SHULE NIGERIA

Kumetokea shambulizi katika shule moja ya upili wakati watoto wakiwa wamekusanyika shuleni humo mjini Potiskum Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
Hata hivyo hakuna taarifa kamili kuhusu idadi ya majeruhi kufikia sasa.
Mlipuko huo ulitokea katika shule ya mafunzo ya sayansi ya vijana mjini humo.
Kundi la wapiganaji wa kiisilamu Boko Haram huenda ndilo limefanya shambulizi hilo, ila taarifa bado hazijathibitisha hilo.
Kundi hiulo limekuwa likishambulia shule katika harakati zake za miaka 5 likitaka kuunda dola ya kiisilamu. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC Swahili

RAIS OBAMA AIZUNGUMZIA IRAQ

Rais wa Marekani Barack Obama
Rais Obama amesema awamu ya kwanza ilikuwa ni kwa ajili ya kuandaa serikali ya pamoja na yenye kuaminika nchini Iraq. Kitu ambacho amesema kimefanyika, na kuongeza kwamba muungano huo wa kijeshi unaopambana dhidi ya kundi hilo la wapiganaji unajiandaa kwa mashambulizi.
Tulichojua ni kwamba awamu ya kwanza iulikuwa ni kupata serikali ya umoja wa Kitaifa na ya uhakika Iraq. Na tumefanya hicho. ''..Na sasa tulichofanya ni zaidi ya kulimaliza nguvu kundi hilo la ISIL.
Kwa sasa tupo katika nafasi ya kuanza tena mashambulio kama ya awali. Mashambulizi ya anga yaliyofanywa yalifanikiwa katika kushusha uwezo wa kundi hilo la ISIL na kupunguza nguvu hatua waliyopiga.
Sasa tunachohitaji ni jeshi la ardhini, Jeshi la ardhini la Iraq, litakaloweza kuwarudisha nyuma..'' Nchini Iraq kwenyewe maafisa wanasema jeshi limekuwa likipiga hatua katika jihada za kuwaondoa wapiganaji hao wa kiislamu katika mji wa Baiji. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Saturday, November 08, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI NOVEMBA 08, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TAZAMA PICHA ZA BILIONEA ALHAJ ALIKO DANGOTE ALIPOTEMBELEA KIWANDA CHAKE MTWARA, NI KILE CHA KUZALISHA SARUJI

Gari iliyombeba mfanyabiashara maarufu barani Afrika, Mwenyekiti wa kundi la makampuni ya Dangote, Alhaj Aliko Dangote, likipita mbele ya majengo yatakayokuwea kiwanda cha kuzalisha sarujit nje kidogo ya mji wa Mtwara, Nov 6, 2014. Ujenzi wa kiwanda hicho unatarajiwa kukamilika Juni 2015

mfuko wa kwanza wa sementi utaanza kufyatuliwa Juni 8, 2015.
Alhaj Dangote akiteta jambo na kaimu mkuu wa mkoa wa Mtwara, Ponsiano Nyami, baada ya kumaliza ziara yake ya kutembelea kiwanda hicho
Alhaj Dangote, (Kulia), akipokelewa na mwakilishi mkazi wa kampuni ya Dangote hapa nchini, Esther Baruti kwenye uwanja wa ndege wa Mtwara
Mainjinia wakimpatia maelezo ya maendeleoya ujenzi wa kiwanda hicho, mmiliki wake, Alhaj Aliko Dangote, (akiwa ndani ya gari) Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WATU 10 WAUAWA KATIKA MLIPUKO NIGERIA

Mlipuko katika eneo la bauchi nchini Nigeria
Ripoti kutoka kaskazini mwa Nigeria zinasema kuwa watu kadhaa wameuawa na mlipuko wa bomu karibu na mashine ya kutoa pesa ya ATM.
Walioshuhdia walisema kuwa ,mwanamume mmoja alikaribia watu waliokuwa wamepanga foleni kwenye mashine hiyo kwenye mji wa Azare ulio katika jimbo la Bauchi .
Walisema kuwa mwanamme huyo alikuwa amebeba bahasha ambayo baadaye ililipuka.
Siku ya Jumatano watu wanaoshukiwa kuwa wanachama wa kundi la Boko Haram walivamia kiwanda kimoja cha saruji ambapo walichukua baruti wanayotumia kwenye milipuko. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Thursday, November 06, 2014

NUSU YA WANAFUNZI WAFAULU DARASA LA SABA


Wanafunzi wa Shule ya Msingi Peaceland ya mkoani Mwanza wakishangilia baada ya kupata taarifa ya shule yao  kushika nafasi ya tatu kitaifa katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba wa mwaka 2014 yaliyotangazwa jana. 

Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), limetangaza matokeo ya mtihani wa darasa la saba mwaka 2014 yakionyesha kuwa zaidi ya nusu ya wanafunzi waliofanya mtihani huo Septemba mwaka huu, wamefaulu.
Matokeo hayo yaliyotangazwa jana na Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde yanaonyesha kuwa wasichana wamefanya vizuri zaidi ya wavulana, huku ufaulu kwa jumla ukiwa umeongezeka kwa asilimia 6.38 ikilinganishwa na mwaka 2013.
Katika matokeo hayo Shule ya Twibhoki iliyopo mkoani Mara iliibuka ya kwanza kitaifa kati ya shule 15,867 zilizofanya mtihani huo ikifuatiwa na Mugini, Peacland na Alliance zote za mkoani Mwanza.
Shule ya tano ni Kwema ya Shinyanga ikifuatiwa na St Severine ya Kagera, Rocken Hill ya Shinyanga, Tusiime ya Dar es Salaam, Imani ya Kilimanjaro na iliyoshika nafasi ya 10 ni Palikas ya Shinyanga.
Wakuu wa shule vinara wazungumza
Mkuu wa Shule Twibhoki iliyopo Mugumu - Serengeti, Alphonce Magori alisema siri ya mafanikio hayo ni kila mwalimu kutambua nafasi yake. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WASOMI, WANASIASA WAPINGA KAULI YA KIKWETE




Rais Jakaya Kikwete. PICHA|MAKTABA 
Makundi mbalimbali ya wasomi, wanaharakati na wanasiasa nchini wamepinga kauli ya Rais Jakaya Kikwete ya kuzuia kampeni za utoaji wa elimu juu ya Katiba Inayopendekezwa wakisema yeye mwenyewe na chama chake ndiyo waliohusika kuanza kampeni mapema hivyo hana haki ya kuzuia makundi mengine.

Juzi, Rais Kikwete alisema muda wa kampeni za ama kuiunga mkono au kuipinga Katiba Inayopendekezwa bado na hakukuwa na sababu ya wanasiasa na taasisi za kiraia kuanza kampeni mapema, lakini wakati huo huo yeye na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein wamenukuliwa wakiipigia debe.

Wakati Mwenyekiti wa Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Nyerere, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Penina Mlama akisema si sahihi kuzuia makundi fulani kutoa elimu hiyo wakati wengine wakiendelea na kampeni za kuipigia debe, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa alisema Kikwete ameshindwa kuficha hisia zake kama mwenyekiti wa CCM. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAKONDA: "VURUGU ZILIZIMA NDOTO ZANGU"



Katibu wa Uhamasishaji Umoja wa Vijana wa CCM, Paul Makonda akizungumza na waandishi wa gazeti la Mwananchi alipotembelea makao makuu ya Mwananchi Communications Limited, Tabata jijini Dar es Salaam jana. 

Katibu wa Hamasa wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Paul Makonda amesema alitamani kuzungumza siku ya mdahalo ulioandaliwa na Kigoda cha Mwalimu Nyerere Foundation lakini vurugu zikazima ndoto yake.

Makonda ambaye anatuhumiwa kuwa ndiye aliyepanga vurugu hizo zilizosababisha aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji mstaafu Joseph Warioba kushambuliwa, alikana na kudai kuwa hata yeye alitamani kukisikia kile kilichopangwa kuzungumzwa na wasemaji wakuu wa mdahalo huo ili ajibu hoja zao katika mkutano huo.

Akizungumza jana katika ofisi za gazeti hili, Makonda alisema aliingia ukumbini akiwa na nakala ya Katiba Inayopendekezwa kwa madai kuwa ingeweza kumsaidia kuainisha yale ambayo yangejadiliwa na ikibidi achangie hoja kwa kutetea au kutoa ufafanuzi wa kile kilichoandikwa ndani ya Katiba hiyo.

“Nasikitika kwa sababu malengo yangu hayakutimia kutokana na vurugu zile. Lengo langu lilikuwa; nipate nafasi ya kuzungumza ili nitoe hoja zangu na kufafanua uzuri wa Katiba Inayopendekezwa,” alisema.

Hata hivyo, alisema yaliyosemwa na Jaji Warioba kabla ya mdahalo kuvunjika, yalimpa fursa ya kujua ni vifungu vipi vina kasoro na vipi viko sahihi. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI NOVEMBA 06, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

OBAMA AAHIDI KUSHIRIKIANA NA REPUBLICAN


Rais Barack Obama

Kiongozi mpya wa Baraza la Senate la Marekani kutoka chama cha Republican na Rais Barack Obama wote wameahidi kumaliza mvutano wa kisiasa ambao umewavunja moyo wapiga kura wa Marekani.
Wanachama wa Republican wamepata ushindi wa kihistoria katika uchaguzi wa nusu muhula na kwa sasa wanadhibiti mabunge yote mawili nchini Marekani. Kiongozi wa baraza la Senate anayeingia madarakani Mitch McConnell amesema ataliwezesha baraza hilo kufanya kazi na kupitisha miswada ya sheria.
Bwana Obama amesema alikuwa na "hamu ya kufanyakazi na baraza jipya la Congress na kufanya miaka miwili yake aliyobaki kukaa madarakani kuwa na tija kadiri iwezekanavyo".

Senata Mitch McConnell kiongozi wa Republican katika Baraza la Senate, akipunga mkono na mke wake.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...