Polisi Zanzibar wameanza
uchunguzi kubaini mazingira ya safari tata ya mtoto Karine Godfrey
aliyesafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar kwa ndege bila tiketi
wala kugundulika.
Mtoto huyo, Karine au Jenipher Godfrey anayesoma
darasa la tatu katika Shule ya Msingi Jitihada, Dar es Salaam alionekana
kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Septemba
Mosi saa 11.30 jioni, akieleza kuwa aliingia Zanzibar kwa ndege ambayo
hata hivyo, haikufahamika mara moja ni ya shirika gani.
Alikutwa uwanjani hapo akijiandaa kuondoka kwenda mahali asipopajua.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Mkadam
Khamis alisema mbali ya kushangazwa na mazingira ya safari ya mtoto
huyo, polisi kwa kushirikiana na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar
wanalifanyia kazi suala hilo.
“Ni
jambo la kushangaza. Tunajiuliza, huyu mtoto
alifikaje katika ndege bila ya kuwa na tiketi wala taarifa zozote
kuelezea safari yake na je, huko Dar es Salaam aliondokaje hadi kuingia
katika ndege bila ya hivyo vitu, sielewi ilikuwaje. Kuwa wa kwanza
kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz