Monday, October 14, 2013

HAYA NI MAMBO 11 YALIYOPINGWA NA BABA WA TAIFA, MWALIMU NYERERE

 Ni miaka kumi na nne sasa imepita tangu mzee wetu mpendwa baba wa taifa hayati Mwl Julius Kambarage Nyerere aiage dunia.
Mwalimu Nyerere ni Rais wa kwanza na ni muasisi aliyeliletea taifa hili uhuru wa kweli toka katika makucha ya mkoloni 9 December, 1961. Mwalimu Nyerere alizaliwa April 22, 1922 katika kijiji kidogo cha mwitongo huko Butihama, kasikazini mwa Tanzania karibu kabisa na ziwa Victoria . 
Alikuwa ni mototo wa chifu Burito Nyerere wa kabila dogo la wazanaki
Nyerere alifariki dunia kwa ugonjwa wa kansa ya damu, siku ya Alhamisi Oktoba 14, 1999 saa 4:30 asubuhi [kwa saa za Afrika Mashariki], katika hospitali ya Mtakatifu Thomas London, Uingereza akiwa amezungukwa na timu ya madaktari bingwa.
Ndipo wananchi wote tulipigwa na butwaa kwa kumpoteza kiongozi mwenye msimamo thabiti na busara duniani. 
Mwalimu bado ni taa inayong’aa gizani, umuhimu wake nazidi kuonekana kadiri miaka inavyokwenda licha ya kwanza amekwisha tuacha.
Wakati wa uhai wake Mwalimu Nyerere alichukia na kukemea vikali mambo yasiyofaa kwa mustakabali wa maendeleo ya Tanzania , Afrika na Dunia kwa ujumla. Baadhi ya mambo hayo ni:

1. UJINGA 

Mwalimu Nyerere alikuwa ni miongoni mwa wasomi wachache na ni mtanzania wa kwanza kupata nafasi yamasomo ya juu katika Chuo Kikuu cha Edinburg , Uingereza na kuhitimu mwaka 1952 akiwa ni gwiji wa uchumi na historia.
Mwalimu hakupenda ujinga na hivyo alipigana vita kali dhidi ya ujinga, na alifanikiwa kwa nafasi yake kuwaondoa ujinga watanzania wengi, wakiwemo viongozi wetu wa sasa ambao walisomeshwa ‘bure’ katika mazingira mazuri yakuridhisha kwa manufaa ya nchi yetu. Ndiyo maana Rais Kikwete Februari 3, 2007 alisema “….sisi tuliwekezwa na ni lazima tuwekeze kwenu ili miaka 30 ijayo Rais atoke miongoni mwenu….”

HIVI NDIVYO MKASA WA MWANDISHI WA ITV UFOO SARO ULIVYOKUWA

Mwandishi wa habari wa ITV, aliyejeruhiwa kwa risasi jana asubuhi, alilazimika kuvumilia majeraha ili kujiokoa yeye mwenyewe na wadogo zake watatu waliokuwa wakipigwa risasi, baada ya mama yake mzazi, Anastazia Saro (58), kuuawa.



Mauaji hayo ya kusikitisha, yalifanyika katika eneo la Mbezi Kibwerere, nyumbani kwa mama yake Ufoo ambako alikuwa akiishi na wadogo zake Ufoo ambao ni Goodluck, Innocent na Jonas.

Mtuhumiwa wa unyama huo ametajwa kuwa ni Anthery Mushi, ambaye ni baba mtoto wa Ufoo, na siku ya tukio wawili hao walitokea Mbezi Magari Saba nyumbani kwa Ufoo, kwenda kuzungumza kifamilia na mama mzazi wa mwandishi huyo.
Mushi (40) ni Mhandisi wa kitengo cha Mawasiliano katika Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) nchini Sudan na aliwasili nchini juzi na kwenda moja kwa moja nyumbani kwa Ufoo Mbezi Mgari Saba.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, Ufoo amejeruhiwa katika paja na tumboni, mama yake mzazi alikufa papo hapo baada ya kupigwa risasi ya kifuani na mtuhumiwa Mushi ambaye naye alijiua baada ya kujipiga risasi kichwani katika eneo la kidevuni.

 Walivyowasili nyumbani
Akizungumza na wavuti hii jana mdogo wake Ufoo, Goodluck alisema; "Walikuja wakiwa pamoja (Ufoo na Mushi) mapema alfajiri wakiwa ndani ya gari saa 12 kabla ya kuingia ndani walitusalimia kisha wakaingia sebuleni na kuanza mazungumzo na mama."

SERIKALI YATANGAZA AJIRA MPYA KWA WALIMU

SERIKALI imesema, mwakani inatarajia kuajiri walimu wapya 27,000 wa shule za msingi na sekondari nchi nzima. Taarifa hiyo ilitolewa jijini hapa jana na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Kassim Majaliwa (pichani) alipokuwa akifunga mkutano wa wadau wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF.
 Alisema kwamba kitendo cha kuajiriwa kwa walimu hao, kitatoa fursa ya mifuko ya hifadhi ya jamii nchini, kupata wanachama wengi na hivyo kuendelea kuboresha shughuli na maisha ya waajiriwa wao.
“Mwakani tunatarajia kuajiri walimu wapatao 27,000 nchi nzima na hii itakuwa ni fursa nzuri kwa mifuko ya jamii kwani watajiunga katika mifuko ya jamii iliyopo,” alisema Majaliwa.

ZITTO KABWE ATAJA MSHAHARA WA RAIS HADHARANI, ADAI NI ZAIDI YA MILIONI 380 KWA MWAKA


NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Kabwe, ametaja mshahara anaolipwa Rais Jakaya Kikwete. Amesema kwamba kwa wadhifa alionao, Rais Kikwete analipwa zaidi ya Sh milioni 30 kwa mwezi.
Mbali na mshahara huo, Zitto amesema kiongozi huyo wa nchi, analipwa wastani wa zaidi ya Sh milioni 380 kwa mwaka ambazo ni marupurupu pamoja na mshahara wake.

Zitto aliutaja mshahara huo mjini hapa jana, alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara.

Kwa mujibu wa Zitto, hakuna sababu kwa mshahara wa kiongozi kufanywa siri kwa kuwa kufanya hivyo ni kutowatendea haki wananchi wanaolipa kodi inayolipa mishahara ya viongozi.

Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), ametaja mshahara huo ikiwa ni wiki moja baada ya kutaja mshahara wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye alisema analipwa zaidi ya Sh milioni 20 kwa mwezi pasipo kukatwa kodi

MEMBE: HAKUNA KIONGOZI WA AFRIKA KUPELEKWA ICC

Mhe. Bernard K. Membe (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiongea na waandishi wa habari mapema leo kwenye ukumbi wa mkutano wa Wizara ya Mambo ya Nje, jijini Dar es Salaam.  Kulia ni Balozi Rajabu Gamaha, Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje. 
Waandishi wa habari waliokusanyika kumsikiliza Mhe. Waziri Membe. 
Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje ukijumuisha Balozi Irene Kasyanju (kushoto), Mkurugenzi wa Kikengo cha Sheria, Balozi Simba Yahya (wa pili kushoto), Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Balozi Mbelwa Kairuki (wa tatu kushoto), Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia na Balozi Dora Msechu (wa nne kushoto), Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika.

MWALIMU NYERERE MWENYE KADI NAMBA MOJA YANGA SC AMBAYE DAIMA ATAKUMBUKWA

nyerere_na_kikwete_na_kalikumtima_0ebe4.jpg
Katikati ni Mwalimu Nyerere akiwa na Katibu wa DABA wa enzi hizo, Jackson Kalikumtima kulia na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Jakaya Kikwete kushoto, sasa rais wa Jamhiri ya Muungano Tanzania. Hii ilikuwa Aprili mwaka 1998 Uwanja wa Ndani wa Taifa, Dar es Salaam.
Na Mahmoud Zubeiry, Bukoba
KADI namba moja ya uanachama wa klabu ya Yanga SC ya Dar es Salaam, inadaiwa alipewa hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ambaye leo anatimiza miaka 14 tangu kifo chake, Oktoba 14, mwaka 1999.
Wakati Mwalimu Nyerere anafariki dunia, mimi nilikuwa mwandishi mchanga sana- wakati huo nipo kampuni ya Habari Corporation Limited, chini ya wamiliki wake wa awali akina Jenerali Ulimwengu.
Aliyekuwa bosi wangu wakati huo, Kenny Manara, aliyekuwa Mhariri wa gazeti DIMBA alinipa kazi ya kwenda Uwanja wa Taifa, sasa Uhuru ulipowekwa mwili wa marehemu kwa ajili ya kuagwa ili kuandika habari juu ya wanamichezo waliojitokeza kuuaga mwili wa marehemu na kuchukua maoni yao.

Hakika nilijifunza mengi sana kupitia msiba huo kwa kusikia, kuambiwa na kujionea. Miongoni mwa niliyoambiwa ni kwamba, Mwalimu Nyerere ndiye alikuwa ana kadi namba moja ya Yanga SC na kadi namba mbili, alikuwa nayo hayati Abeid Amaan Karume, rais wa zamani wa Zanzibar.
Sijabahatika kuiona 'leja' ya Yanga hadi leo tangu nisikie habari hizo, kwa hivyo siwezi kusadiki, lakini kulingana na historia ya klabu ya Yanga katika harakati za ukombozi wa taifa letu, siwezi kupinga hilo.
Nashukuru Mungu nikiwa Mwandishi wa Habari, nimewahi kufanya kazi za kuandika habari katika tukio ambalo Mwalimu Nyerere alikuwepo.

AU YATAKA ICC IAHIRISHE KESI YA KENYATTA


131013212235_kenyattareuters_043c3.jpg
Mkutano wa wakuu wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika uliofanyika Ehiopia umetaka mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai (ICC) huko The Hague icheleweshe kesi ya Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya, iliyopangwa kuanza kusikilizwa Novemba mwaka huu.
AU pia wamekubaliana azimio linaloeleza kuwa hakuna kiongozi mkuu wa taifa la Afrika aliyeko madarakani atakayefikishwa katika mahakama hiyo.
Wakati viongozi wa Kenya na Sudan wakikabiliwa na kesi huko ICC, viongozi wa nchi za Afrika wamekuwa wakilalamika kwa muda mrefu kuwa mahakama hiyo inafanya upendeleo na kuwaonea kwa makusudi.
AU ilijadili uwezekano wa nchi wanachama kujitoa, lakini wazo hilo halikuungwa mkono kiasi cha kutosha.
Wanasiasa na wanadiplomasia waandamizi akiwemo aliyekuwa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan wamekosoa mpango wa kujitoa kutoka ICC. Tembelea jambotz8.blogspot.com kila siku.
Kucheleweshwa
Viongozi hao wa AU, waliokutana Addis Ababa, walikubaliana kuwawekea kinga ya kutoshitakiwa kiongozi yoyote wa taifa la Afrika.
Pia wameitaka Kenya iandike barua kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataiga kuomba ucheleweshwaji wa kesi katika mahakama ya ICC dhidi ya Rais Uhuru Kenyatta, ambaye anakabiliwa na mashtaka ya jinai.

Sunday, October 13, 2013

UFO SARO BADO YUKO KATIKA CHUMBA CHA UPASUAJI MHIMBILI

IMG_0031Pichani chini baadhi ya Wafanyakazi wenzake na Ufo Saro kutoka IPP pamoja waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali wakiwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili ambako Ufo Saro ambaye mpaka sasa, yuko katika chumba cha upasuaji  baada ya kupigwa risasi na mchumba wake Anteri Mushi usiku wa kuamkia leo ambapo pia alimpiga mama mzazi wa Ufo Saro Anastazia Peter Saro miaka 59 aliyefariki hapohapo  na baadae kujipiga risasi mwenyewe na kufa hapohapo, Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo huko Mbezi Luisi 1 2Wafanyakazi hao wakibadilishana mawazo hapa na pale katika hospitali ya Muhimbili leo hii 3 4Picha Kwa Hisani ya Fullshangwe Blog

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI OKTOBA 13, 2013

DSC 0092 7ee69
DSC 0093 41bc7

SINTOFAHAMU WAIZARA YA HABARI.....!!!


makala dca7a
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla, jana alitoa taarifa kwa umma akieleza bayana kwamba yeye ndiye aliyeliruhusu gazeti hili kuendelea kutolewa kwa njia ya mtandao (online) na Gazeti la Rai kutolewa kila siku.
Makalla alitoa ufafanuzi huo muda mfupi baada ya Idara ya Habari-Maelezo kutoa taarifa kwamba Serikali imesikitishwa na Gazeti la Mwananchi na gazeti dada la Rai, Mtanzania kukiuka masharti ya adhabu walizopewa.
Septemba 27, mwaka huu Serikali iliyafungia Mwananchi kwa siku 14 na Mtanzania siku 90.
Wakati likianza kutumikia adhabu yake, Mwananchi ambalo tayari limemaliza kuitumikia, liliendelea kutoa taarifa kwenye tovuti yake wakati Kampuni ya New Habari (2006) Ltd ambayo inamiliki Mtanzania ilianza kuchapisha kila siku gazeti la Rai ambalo awali lilikuwa likichapishwa kila wiki.
Katika ufafanuzi wake alioutoa
jana Makalla alisema: "Nimelazimika kueleza haya baada ya taarifa mpya ya Idara ya Habari-Maelezo iliyohoji uhalali wa gazeti la Mwananchi kuwa online (mtandaoni) na gazeti la Rai kutoka kila siku, badala ya mara moja kwa wiki (Alhamisi)."

IVORY COAST WAIFUMUA SENEGAL 3-1 NA KUBISHA HODI KOMBE LA DUNIA

WASHAMBULIAJI Didier Drogba, Salomon Kalou na Gervinho wote wamefunga jana Ivory Coast ikiifumua 3-1 Senegal na kuongeza matumaini ya kufuzu Fainali za Kombe la Dunia mwakani.Drogba alifunga kwa penalti dakika ya tano, kabla ya winga wa zamani wa Arsenal, Gervinho kufunga la pili dakika tisa na baadaye kipindi cha pili Salomon Kalou akafunga la tatu mjini Abidjan.
article-2456451-18B3202400000578-136_634x423_49689.jpg
Tembo wauwaji: Wachezaji wa Ivory Coast wakishangilia ushindi wao leo
Sasa Ivory Coast watahitaji sare au kufungwa si zaidi ya wastani wa bao moja katika mchezo wa marudiano moja ili kujikatia tiketi ya Brazil mwakani. Seneal yenyewe itahitaji kushinda 2-0 tu nyumbani, ili kujihakikishia kurejea Fainali za Kombe la Dunia.
article-0-18B2FA6200000578-877_634x446_38bb0.jpg
Didier Drogba ameifungia Ivory Coast leo
article-2456451-18B3209700000578-178_634x453_e3f22.jpg
Salomon Kalou na Drogba walicheza pamoja Chelsea miaka kadhaa
article-2456451-18B3D49200000578-154_634x416_2ec82.jpg
Umefanya vizuri: Gervinho akizungumza na kocha Sabri Lamouchi baada ya mechi
Bao pekee la Senegal lilifungwa na Papiss Cisse dakika tano kabla ya filimbi ya mwisho.

Saturday, October 12, 2013

HUU NDIO UTARATIBU MPYA WA KUINGIA MLIMANI CITY BAADA YA KUTOKEA UVAMIZI WESTGATE

 
 Kijana akikaguliwa kwa umakini baada ya kutiliwa mashaka na walinzi wa Mlimani City leo mchana
 
 Mlinzi wa kike akiwasubilia wananwake watakaotaka kuingia kwenye jengo la mlimani city ili hawakague
Ukaguzi ukiendela
PICHA NA PAMOJAPURE/PAMOJA BLOG

STEWART ADAI SIMBA NA YANGA ZINABEBWA NA TFF


Hall1 1eb67
KOCHA Mkuu wa Azam FC, Muingereza Stewart Hall amesema kwamba ni kazi ngumu Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kupata bingwa nje ya Simba na Yanga kwa sababu timu hizo zinapendelewa mno na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).



Akizungumza Hall amesema kwamba timu nyingine nje ya Simba na Yanga SC ili kuwa bingwa inabidi ifanye kazi ngumu sana ambayo kwa sasa yeye na timu yake, Azam FC wanajaribu.
Kwanza amesema ratiba ya Ligi Kuu inapopangwa inakuwa katika mazingira mazuri kwa timu hizo na mazingira magumu kwa timu nyingine ambazo zinaonekana zikitendewa haki zinaweza kuzima ubabe wa timu hizo katika soka ya Tanzania.
Stewart alitoa mfano hadi sasa katika mechi za Ligi Kuu ambazo tayari zimechezwa, Simba na Yanga kila moja imecheza mechi mbili tu ugenini, wakati Azam FC imecheza mechi sita ugenini, jambo ambalo amesema huwezi kulikuta katika ligi nyingine yoyote duniani.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI, OKTOBA 12, 2013

DSC 0092 59997
DSC 0093 e41e4

RIPOTI YA UN: YAIANIKA SERIKALI, YADAI WATANZANIA NI WATU WASIO NA FURAHA


saada_35554.jpg
Naibu waziri wa fedha, Saada Salum
Wakati Tanzania ikitajwa kuwa ni miongoni mwa nchi zenye amani na utulivu, imebainika kuwa Watanzania ni miongoni mwa watu wasio na furaha na waliokata tamaa hapa duniani.
Ripoti inayoonyesha orodha ya nchi zenye furaha duniani ya mwaka 2013 (World Happiness Report 2013), imeitaja Tanzania kuwa ni miongoni mwa nchi 10 za mwisho duniani kati ya nchi 156 zilizofanyiwa utafiti huo.
Ripoti hiyo iliyoandaliwa na kundi la wataalamu kutoka Umoja wa Mataifa (UN), kati ya mwaka 2010 na 2012, inaonyesha kuwa Tanzania imeshika nafasi ya 151 ikiburuta mkia pamoja na nchi za Rwanda, Burundi, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Benin na Togo.
Upatikanaji wa huduma za jamii, mtazamo wa watu kuhusu rushwa, umri wa kuishi, ukosefu wa kazi, pato la taifa na ukarimu wa watu katika nchi husika, ni baadhi ya vigezo vilivyoangaliwa wakati wa kuandaa taarifa hiyo.
Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka alieleza kushtushwa na ripoti hiyo kwa maelezo kwamba ni asilimia 11.7 tu ya Watanzania wasio na ajira na kwamba wale wanaofanya kazi, wanapata huduma zote za msingi, ikiwa ni pamoja na kwenda likizo na mishahara inayolingana na taaluma zao.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...