Monday, October 14, 2013

SERIKALI YATANGAZA AJIRA MPYA KWA WALIMU

SERIKALI imesema, mwakani inatarajia kuajiri walimu wapya 27,000 wa shule za msingi na sekondari nchi nzima. Taarifa hiyo ilitolewa jijini hapa jana na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Kassim Majaliwa (pichani) alipokuwa akifunga mkutano wa wadau wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF.
 Alisema kwamba kitendo cha kuajiriwa kwa walimu hao, kitatoa fursa ya mifuko ya hifadhi ya jamii nchini, kupata wanachama wengi na hivyo kuendelea kuboresha shughuli na maisha ya waajiriwa wao.
“Mwakani tunatarajia kuajiri walimu wapatao 27,000 nchi nzima na hii itakuwa ni fursa nzuri kwa mifuko ya jamii kwani watajiunga katika mifuko ya jamii iliyopo,” alisema Majaliwa.


Awali, Mkurugenzi Mkuu wa LAPF, Eliud Sanga alisema, kwa miaka minne mfululizo, mfuko huo umeongoza kwa utunzaji wa hesabu kwa viwango vya NBAA.

Kwa mujibu wa Sanga, mwaka jana mfuko huo uliandikisha wanachama 17,840 na kukusanya michango ya Sh bilioni 119.7 wakati mwaka huu, mfuko unatarajia kukusanya Sh bilioni 163.

Alisema, LAPF inaendelea kuongeza uwekezaji katika vitega uchumi kwa kuwekeza Sh bilioni 570, ambapo imefanikiwa kupata faida ya Sh bilioni 48.7.

Naye Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka, akichangia katika mkutano huo, aliitaka mifuko ya pensheni nchini kushindana katika utoaji wa mafao bora ili wanachama wa mifuko wafaidike na mafao bora.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi za Jamii, Irene Isaka, aliwataka wananchi kujiunga na uchangiaji wa hiari katika mifuko mingi kadiri wawezavyo, ili utakapofika umri wa kustaafu wapate mafao bora kuliko mishahara waliyokuwa wakilipwa.


MTANZANIA
SERIKALI imesema, mwakani inatarajia kuajiri walimu wapya 27,000 wa shule za msingi na sekondari nchi nzima. Taarifa hiyo ilitolewa jijini hapa jana na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Kassim Majaliwa (pichani) alipokuwa akifunga mkutano wa wadau wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF.
 Alisema kwamba kitendo cha kuajiriwa kwa walimu hao, kitatoa fursa ya mifuko ya hifadhi ya jamii nchini, kupata wanachama wengi na hivyo kuendelea kuboresha shughuli na maisha ya waajiriwa wao.
“Mwakani tunatarajia kuajiri walimu wapatao 27,000 nchi nzima na hii itakuwa ni fursa nzuri kwa mifuko ya jamii kwani watajiunga katika mifuko ya jamii iliyopo,” alisema Majaliwa.


Awali, Mkurugenzi Mkuu wa LAPF, Eliud Sanga alisema, kwa miaka minne mfululizo, mfuko huo umeongoza kwa utunzaji wa hesabu kwa viwango vya NBAA.

Kwa mujibu wa Sanga, mwaka jana mfuko huo uliandikisha wanachama 17,840 na kukusanya michango ya Sh bilioni 119.7 wakati mwaka huu, mfuko unatarajia kukusanya Sh bilioni 163.

Alisema, LAPF inaendelea kuongeza uwekezaji katika vitega uchumi kwa kuwekeza Sh bilioni 570, ambapo imefanikiwa kupata faida ya Sh bilioni 48.7.

Naye Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka, akichangia katika mkutano huo, aliitaka mifuko ya pensheni nchini kushindana katika utoaji wa mafao bora ili wanachama wa mifuko wafaidike na mafao bora.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi za Jamii, Irene Isaka, aliwataka wananchi kujiunga na uchangiaji wa hiari katika mifuko mingi kadiri wawezavyo, ili utakapofika umri wa kustaafu wapate mafao bora kuliko mishahara waliyokuwa wakilipwa.


MTANZANIA

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...