Thursday, June 06, 2013

MTANZANIA KUONGOZA JESHI LA KULINDA AMANI DARFUR.

 
 
Kwa mara nyingine  Bendera ya  Tanzania imeendelea kupepea katika Tasnia ya Ulinzi wa Amani  ya Kimataifa.
 Mapema wiki hii,  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Bi. Nkosizana Dlamin Zuma wametangaza uteuzi wa Luteni General Paul Ignace Mella  Kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania ( JWTZ) kuwa Mkuu  Mpya wa Jeshi la   Kulinda Amani la Umoja wa Mataifa huko Darfur ( UNAMID)
 
Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa  Ban Ki Moon, na nakala yake kutumwa  katika  Uwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  imeeleza kwamba, Lt. Gen. Mella anachukua  nafasi iliyoachwa na Mkuu wa  zamani wa Jeshi hilo (UNAMID), Lt. Gen Patrick Nyamvumba kutoka Rwanda ambaye amemaliza muda wake wa  utumishi  March 31,2013.
 
Wasifu wa Luteni General Paul Ignace Mella unaelezwa  kuwa ni Mwanajeshi wa muda mrefu na  mwenye uzoefu na utumishi uliotukuka katika JWTZ akiwa amewahi kushika nyadhifa  mbali mbali  muhimu za uongozi.
Baadhi ya nyadhifa hizo ni pamoja na  Naibu Kamanda Kikosi cha Tanzania chini ya Umoja wa Mataifa huko Liberia (  1993-95), Kamanda wa Kikosi cha  JWTZ, Afisa Mnadhimu-Makao Makuu  ya Jeshi, Mwambata Jeshi-Ubalozi wa Tanzania Uganda na hadi sasa alikuwa ni  Mkuu wa Usalama na Utambuzi- JWTZ.
 Uteuzi wa Lt. Generali Mella unafuatia mchakato mrefu ulioshindanisha wateuliwa kutoka nchi mbalimbali duniani, na hatimaye  yeyé akaibuka mshindi. 
OFISI YA UBALOZI WA TZ UN

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JUNI 06, 2013



6 f55a81 37d70

Wednesday, June 05, 2013

MPYA KUHUSU BINTI WA KITANZANIA ALIYEKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA NA KUHUKUMIWA KUNYONGWA IJUMAA HII

Hii ndio picha ambayo imesambaa kwenye mitandao mingi ya msichana anesemekana ni Fatma aka Brown Berry wa Ilala Dar es Salaam ambae amehukumiwa kunyongwa huko egypt baada ya kukamatwa na unga.
Hii ni screenshot ya video hii hapa chini baada ya kukamatwa kwake na unga, Ingawa habari hizi hatuna uhakika nazo kama ni Mtanzania kama invyodaiwa na wengi au ni mswahili wa Oman kama wengine wanavyodai
Mrembo Fatma aka Brown Berry katika pose

MR NICE APIGWA CHINI NA LABEL ALIYOKUA AKIFANYA NAYO KAZI KENYA, KISA NI MVIVU.

GrandPa Records Ya Kenya Imevunja Mkataba Wake Wa kazi na Msanii Mr Nice kutoka Tanzania Baada ya miezi michache ya kufanya nae kazi. Fahamu Mr Nice alipewa mkataba na GrandPa Records huku akijua kuwa ana mkataba mwingine Tanzania na Producer Lamar. GrandPa Wamesema Mr Nice Ni Msanii Mvivu na Asiye toa ushirikiano kwenye kazi kabisa ndio maana wameamua Kuvunja mkataba wake. Hii Ni Post ya FaceBook Ya GrandPa Records. Bado Taarifa Zina Kuja Kaa Na Mimi Utaiskia Interview Yao Hapa Soon


TO

KESI DHIDI YA RUTO KUHAMISHIWA KENYA AU TANZANIA

 Nairobi, Kenya. Kesi inayomkabili makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) huenda ikahamishiwa nchini Tanzani au Kenya.
Hiyo inatokana na uamuzi unaotajwa kufikiwa na majaji wa ICC ambao wametoa mapendekezo wakimtaka Rais wa ICC aangalie umuhimu na kutoa ruhusa ya kesi hiyo kusikiliziwa nchini Kenya au kama ikishindikana basi isikiliziwe nchini Tanzania.
Uamuzi huo unaweza pia kusababisha athari za kuichochea mahakama hiyo kuhamisha pia kesi ya aina hiyo inayomhusu Rais Uhuru Kenyatta ambaye pia mawakili wake wameomba kesi dhidi yake ihamishiwe nchini Kenya au Tanzania.
Ruto pamoja na mtuhumiwa mwenzake, aliyekuwa mtangazaji wa Redio, Joshua Arap Sang wanakabiliwa na mashtaka kadhaa ya uhalifu dhidi ya ubinadamu wakidaiwa kuhusika kuchochea vurugu za baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007 zilizosababisha vifo vya zaidi ya watu 1,000.
Mapendekezo hayo yametokana na ombi hilo lililotumwa Januari 24 mwaka huu ambalo lilikuwa bado likiendelea kujadiliwa n amamlaka zinazohusika kwenye mahakama hiyo.
Februari mwaka huu, Mwendesha mashtaka mkuu wa ICC, Fatou Bensouda aliieleza mahakama hiyo kwamba hana pingamizi iwapo itakubalika kesi hiyo isikiliziwe Tanzania au Kenya.
Hata hivyo mahakama hiyo ilieleza kuwa mapendekezo hayo bado yanaendelea kujadiliwa kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa na mahakama hiyo.
Hata hivyo, jana ICC ilitoa taarifa ikisema kesi dhidi ya Ruto anayetuhumiwa kufanya makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu itaanza Septemba 10 mwaka huu.
Taarifa hiyo imesema majaji wameamua kupanga tarehe ya kusikilizwa kesi hiyo mapema zaidi kuliko ilivyopangwa awali.
Rais Kenyatta na naibu wake wanahitajika kupandishwa kizimbani ili kujibu mashtaka yanayowakabili ya uhalifu dhidi ya ubinadamu, makosa ambayo waliyafanya wakati wa vurugu zilizotokea baada ya uchaguzi mkuu wa Rais wa mwaka 2007/08.

"SITANYAMAZA KUSHAMBULIWA KWANGU.NI LAZIMA JAMII IJUE"...HII NI KAULI YA KIBANDA BAADA YA KURUDU TANZANIA

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda (wa tatu kulia) akiwasili jana.
 
MWENYEKITI wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda amerejea chini jana kutoka Afrika Kusini alikokuwa akitibiwa na kusisitiza kwamba hatanyamaza kuzungumzia janga la kushambuliwa kwake.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, Kibanda alisema asingependa kuona jambo hilo linamtokea mwandishi mwingine wa habari.

Kibanda, ambaye pia ni Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya New Habari (2006) Ltd, alikuwa akitibiwa huko baada ya kushambuliwa na kuumizwa vibaya na watu wasiofahamika usiku wa Machi 5, mwaka huu.

Azam yawatupia virago Babi, Uhuru



Abdi Kassim ‘Babi’

Dar es Salaam. Azam FC imetoa mkono wa kwa heri kwa kiungo wake mkongwe Abdi Kassim ‘Babi’ na Uhuru Seleiman aliyekuwa kwa mkopo. Meneja wa timu hiyo, Patrick Kahemela alisema jana kuwa sababu kubwa ya kuachana na wachezaji hao ni mikataba yao kumalizika pamoja na umri kuwatupa mikono.

Wachezaji waliotupia virago ni pamoja na Lewis Cosmas aliyejiunga na Ruvu Shooting na Abdulhalim Humoud aliyepata timu Afrika Kusini ya Jomo Cosmos. Akizungumza na gazeti hili Abdi Kassim alisema “Ni kweli mkataba wangu kuitumikia Azam umeisha ingawa walinitaka nisaini mpya, lakini tukashindwa kuafikiana. “Naamini bado nina nguvu na uwezo wa kucheza soka. Kwa hiyo niko tayari kujiunga na timu yoyote ambayo itaonyesha nia ya kunitaka.” alisema Babi aliyekipiga na klabu za Mlandege ya Zanzibar, Mtibwa Sugar, Yanga, DT Long ya Vietnam pamoja na timu ya Taifa ‘Taifa Stars’.
Anaeleza kuwa yuko tayari kujiunga na Yanga, Mtibwa Sugar ama Coastal Union iwapo zitaonyesha kutaka kumsajili kwa ajili ya msimu ujao. Klabu ya Mtibwa iliwahi kukiri kutaka kumrejesha Babi nyumbani katika dirisha dogo la usajili Januari mwaka huu.

RONALDO AGOMA KUONGOEZA MKATABA REAL MADIRD

ronaldo 7d195

MSHAMBULIAJI Cristiano Ronaldo ameziweka kiporo Manchester United na Paris Saint-Germain baada ya kusema hataongeza Mkataba Real Madrid baada ya 2015.Real imegoma kumuuza Mreno huyo msimu huu wakati United na PSG zinabakiwa mstari wa mbele atakapotiwa sokoni.Alex Ferguson alimuuza Ronaldo kwenda Madrid mwaka 2009, lakini nyota huyo mwenye umri wa miaka 28 ameeleza mara kadhaa hivi karibuni kwamba hana furaha sana katika Jiji hilo na Hispania.
Rais wa Madrid, Florentino Perez alisema anatarajia kuona Ronaldo akitungikia daluga zake katika klabu hiyo, lakini inaonekana atatafuta klabu nyingine miaka miwili ijayo.
Ikiwa Ronaldo atakuwa mkweli kwa kauli zake, ataondoka bure, kitu ambacho Madrid hawatapenda baada ya kumsajili kwa Pauni Milioni 80.

DIAMOND ANA UTAJIRI WA ZAIDI YA BILIONI 1 ZA BONGO, NA HAYA NDIO MAMBO KUMI USIYOYAJUA KUHUSU DIAMOND


1. Ana utajiri unaozidi shilingi bilioni 1.
2. Yupo kwenye mazungumzo na promoter wa Rwanda kufanya show moja ya uwanjani ambayo anaweza kulipwa dola 120,000 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 190.

3. Malipo ambayo hupokea kwa show zake nyingi za nje ya nchi hayashuki chini ya dola 25,000.
4. Tangia mwaka 2011 mwishoni akaunti yake haijawahi kushuka chini ya shilingi milioni 100.
5. Anamiliki nyumba kadhaa alizopangisha.
6. Wimbo Mawazo alimwandikia Jacqueline Wolper ambaye alikuwa mpenzi wake.
7. Kamwambie na Mbagala alimwambia mpenzi wake aitwaye Sarah aliyemkataa (Diamond) sababu hakuwa na uwezo.
8. Ukimwona alimwandikia Wema Sepetu baada ya kumsaliti.
9. Ili kuvunja mkataba na aliyekuwa meneja wake Papa Misifa, ilibidi amlipe shilingi milioni 18.
10. Ana timu (anayoilipa mshahara) ya watu zaidi ya 12 wakiwemo dancers, mtu wa mavazi, msaidizi wake, wapiga picha wawili nk.
 
d8fdca7eccf211e2a7ed22000a1f8f24_7

ANGALIA PICHA ZA HESHIMA ZA MWISHO KWA MAREHEMU ALBERT MANGWEA ZAANZA KUTOLEWA.

Dah this is it ndugu yetu mpendendwa ndo ametangulia mbele za haki na sasa ule muda wa kutoa heshima za mwisho ndo umewadia. Mungu awape nguvu wale wote waliofikwa na msiba huu.


Mwili wa marhemu Albert Mangwea ukiwa kwenye jeneza tayari kwa watu kutoa heshima za mwisho

MAGAZETI YA LEO JUMATANO JUNI 5, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

1 c5c24


2 c0794

Tuesday, June 04, 2013

Jokate aongea baada ya Diamond kukiri kuwa anajuta kumkosea na kuuvunja moyo wake

Hivi karibuni Diamond aliamua kuweka ‘ego’ pembeni na kukiri kuwa Jokate Mwegelo ndiye msichana katika maisha yake aliyemkosea sana na anajuta kumuumiza
Diamond alifunguka hayo kwenye kipindi cha Take One cha Clouds TV, kilichorushwa wiki iliyopita.

Akiongelea jinsi alivyomuumiza Jokate, Diamond alisema, “Kwasababu alikuwa too innocent halafu hakuwahi kunikosea kitu chochote Jokate kabisa, halafu nikamwingiza kwenye matatizo, watu wakamchukulia tofauti kwamba ‘Jokate kamchukulia Wema boyfriend wake’ wakati nilimfuata mimi kama mimi, nilimtafuta mwenyewe halafu then nikawa niko naye halafu ghafla nikarudisha mahusiano kwa Wema. Sikujiskia vizuri halafu still haikuwa vizuri so sometimes nikikaaga hivi nasema nilimkosea.”

Akijibu swali la kwanini alimuacha Jokate, Diamond aliongeza, “Sijui nilirogwa hata sijui, I don’t know, sijui hata kwanini, hakuwahi kunikosea chochote sio, sababu nilikuwa nikikaa naye alikuwa akinishauri vitu vingi vya maendeleo, sijui ulikuwa ni utoto sielewi yaani, sijui ni kitu gani, nilijikisa vibaya sana, halafu mtoto wa watu mstaarabu sana, alijitahidi kujenga career yake sasa hivi imekaa vizuri.”

Bongo5 imewasiliana na Jokate ili kutaka kufahamu upande wake baada ya kusikia kauli ya Diamond aliyesema anafurahi kuona Diamond amefunguka ukweli.

“Watu wengi hawajui the real issue, I’m glad kama ame-acknowledge I was innocent in that whole matter,” amesema Jokate.

MAPOKEZI YA MANGWEA JIJI ZIMA LAZIZIMA

 Gari iliyobeba mwili wa Albert Mangwea ikisukumwa na washabiki,wapenzi ndugu jamaa na marafiki mara baada kuanza kuondoka eneo la Eapoti hivi punde wakielekea Muhimbili kwa taratibu nyingine,Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi--Amen

ANGALIA PICHA MWILI WA ALBERT MANGWEA ULIVYOWASILI DAR

Gari maalum la Kubeba Mwili wa Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya,Marehemu Albert Mangwea likiwa tayari  kwa kubeba mwili.
Wadau mbali mbali wakiwa wamekusanyika kwa wingi kwenye uwanja wa Ndege Julius Nyerere kwa ajili ya kuupokea Mwili wa Marehemu Albert Mangwea uliowasili mchana huu kutokea nchini Afrika ya Kusini.
Wadau kibao wapo uwanjani hapa hivi sasa tayari kwa kuupokea Mwili wa Marehemu Mangwea.
Rafiki kipenzi wa Marehemu Albert Mangwea,Jay Mo akihojiwa na vyombo vya habari uwanjani hapa.

ANGALIA PICHA ZA MWANAMKE AZAA WATOTO WATANO KWA MPIGO NCHINI CZECH.

Mmoja wa watoto wa watano akiwa amejifungua mbele ya uangalizi wa jopo la madaktari siku ya jumapili nchini Czech.
Jopo la madaktari wakimchunguza mwanamke Alexandra Kinova miaka 23.
Alexandra Kinova kipindi cha ujauzito.

MAMA NA MPENZI WAKE WAMUUA MTOTO WA MIAKA 4 ILI WAFAIDI PENZI LAO

Wakati mwingine unaweza kudhani binadamu tunageuka kuwa wanyama, lakini huu sio mfano tosha kwani hata wanyama wakali kama simba huwa na huruma na huwalinda watoto wao hadi kufa, baadhi ya binadamu wamekuwa na roho ya ukatili isiyo ya kawaida hata kwa mtoto waliyemzaa wenyewe.
Huko Uingereza mama mmoja aliyejulikana kwa jina la Magdelena Luczack na mpenzi wake Mariusz Krezolek ambao walihamia uingereza wakitokea Poland, wamefikishwa katika mahakama kuu mjini Birmingham wakikabiliwa na mashtaka ya mauaji. 
Watu hao wanashtakiwa kwa kushirikiana kumuua kwa kumtesa wka vipigo na  kumyima chakula  kwa makusudi mtoto Daniel aliyekuwa na umri wa miaka minne tu,aliyefariki mwezi march mwaka jana akiwa na jeraha kichwani.
Magdalena ambae ni mama mzazi wa mtoto huyo anatuhumiwa kushirikiana kwa karibu na baba wa kambo wa mtoto huyo kusababisha kifo chake wakiwa na nia ya kutafuta amani na utulivu katika nyumba yao.

M2 THE P ANA USHAHIDI WOTE KATIKA KIFO CHA ALBERT MANGWAIR.

 
Na Mwandishi Wetu
MBIVU na mbichi sasa zinaweza kujulikana, kinachoombwa ni muda tu, kwani mng’amuzi halisi kuhusu kifo tata cha mwanamuziki mwenye kipaji kikubwa Bongo, Albert Mangwea ‘Ngwea’, yupo kwenye mazingira mazuri kueleza kilichotokea.

KWA NINI ANA USHAHIDI WOTE?
Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Mgaza Pembe ‘M2 The P’, ndiye mwenye ushahidi wote kwani aliambatana na Ngwea kila sehemu waliyotembelea mpaka nukta ya mwisho nchini Afrika Kusini.
M2 The P, alipatwa na matatizo sawa na marehemu Ngwea, isipokuwa mwenzake ilifikia hatua mbaya na kupoteza maisha huku yeye akibaki mahututi kwenye chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum (ICU) katika Hospitali ya St. Helen Joseph, jijini Johannesburg nchini humo.
Jambo la faraja ni kwamba, M2 The P yupo vizuri kwa sasa, atakaporuhusiwa kutoka, atajibu maswali mengi tata ambayo yamejitokeza tangu Ngwea alipofariki dunia Juni 28, mwaka huu, nchini humo  alipokwenda kwenye shughuli zake.

JAWABU LA SUMU 
Moja ya mambo yanayozungumzwa pembeni ni kwamba kuna uwezekano mkubwa marehemu Ngwea na M2 The P  waliwekewa sumu kwenye chakula au kupuliziwa ‘laivu’ kisha kutokea yaliyotokea, lengo likiwa kuwadhulumu mzigo wa fedha nyingi waliokuwa nao, hivyo kupona kwa mmoja huyo ni matakwa ya Mungu ili awe shahidi namba moja wa kifo cha Ngwea.

H0TUBA YA MAPENDEKEZO YA RASIMU YA KATIBA NA YALIYOMO KWENYE RASIMU HIYO NI HAYA HAPA .....



warioba 89a51
1.0. UTANGULIZI
Awali ya yote namshukuru mwenyezi mungu kwa kutuwezesha kufikia hatua hii ya leo ya kuzindua Rasimu ya Katiba. pia, niwashukuru ninyi nyote mliohudhuria halfa hii ikiwa ni mwendelezo wa mchakato muhimu wa Mabadiliko ya Katiba ya nchi yetu.
Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ilipitishwa Bungeni Novemba, 2011 na kufanyiwa mabadiliko Februari, 2012. Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliundwa kwa mujibu wa Kifungu 6(1) cha sheria hiyo (Cap.83). Wajumbe 34 wa Tume waliteuliwa na kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, mwezi Aprili, 2012. Kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Tume imepewa miezi kumi na minane kukamilisha kazi yake kuanzia siku ilipoanza kazi rasmi ambayo ilikuwa Mei 2, 2012.
Tume iliandaa ratiba ya utekelezaji wa majukumu yake. Kufuatana na ratiba hiyo Tume ilijipanga kukusanya maoni ya wananchi katika kipindi cha miezi mitano kuanzia Mwezi Julai hadi Disemba, 2012. Kazi hiyo ilifanywa kama tulivyopanga. Tume ilijigawa katika makundi na ilitembelea mkoa yote thelathini.

Tume ilifanya mikutano 1,942 ambayo ilihudhuriwa na wananchi wapatao 1,365,337 ambao kati ya hao wananchi 333,537 walitoa maoni ama kwa mazungumzo ya ana kwa ana au kwa maandishi. Tume pia ilipata maoni ya wananchi wengi, wa ndani na nje ya nchi kwa njia mbali mbali kama vile; Mikutano ya hadhara, Fomu maalum za Tume, barua kupitia Masanduku ya Barua ya Tume, Mitandao ya Kijamii ya barua pepe; facebook ya Tume, Tovuti ya Tume; Makala mbalimbali kutoka kwenye magazeti na ujumbe mfupi wa simu.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JUNI 04, 2013

1 c2a93
17 cdc7f

VITI MAALUMU VYAFUTWA, UBUNGE KUWA NA UKOMO


Tume ya Mabadiliko ya Katiba imependekeza katika rasimu ya Katiba Mpya ukomo wa wabunge na kufutwa kwa nafasi za Viti Maalumu bungeni.
Mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji Mstaafu Joseph Warioba alisema jana, wanapendekeza kwamba ubunge uwe na ukomo wa vipindi vitatu vya miaka mitano, mitano akimaanisha kwamba kipindi cha mtu kuwa mbunge hakiwezi kuvuka miaka 15.

Rasimu hiyo ya Katiba imependekeza kutokuwapo tena kwa Viti Maalumu na badala yake, imetaka kuwapo kwa nafasi tano za uteuzi zibaki kwa Rais ambazo zitahusisha makundi maalumu ya watu wenye ulemavu pekee.

Jaji Warioba alisema Tume imependekeza kuwapo kwa
majimbo 25 ya uchaguzi kwa Tanzania Bara na 20 kwa Zanzibar ambayo kila moja litakuwa na wabunge wawili, mwanamke na mwanamume. Kwa mujibu wa rasimu hiyo, majimbo hayo ni mikoa 25 ya Tanzania Bara na wilaya 10 za Zanzibar. Kwa maana hiyo, Bunge la Muungano litakuwa dogo lenye wabunge 75.

Monday, June 03, 2013

MAPYA YAIBUKA KUHUSU KIFO CHA MANGWEA....ALIYELALA NAE ASIMULIA ALIYOYAONA WAKATI NGWEA AKIKATA ROHO..!!

HUKU mwili wake ukitarajiwa kuwasili Bongo kesho, kifo chake Albert Mangweha ‘Ngwea’ kilichotokea katika hali ya utata Mei 28, 2013 nchini Afrika Kusini, kimeibua mambo mapya, Ijumaa Wikienda lina mzigo wote.

MAMA MANGWEA NAYE AZIDIWA, AKIMBIZWA HOSPITALI YA MKOA
Habari kutoka msibani Moro jana zilisema mama mzazi wa marehemu Mangwea, Denisia Mangwea naye alizidiwa na kukimbizwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa matibabu zaidi.
Kwa mujibu wa baadhi ya waombolezaji msibani hapo, mama huyo alipata mshtuko wa moyo kufuatia kifo cha mwanaye ambapo taarifa za kifo hicho zilimshtua tangu Jumanne mpaka alipozidiwa jana. 

HABARI KUTOKA SAUZI SASA
Habari kutoka kwenye Jiji la Johannesburg ambako Ngwea alifia, mtiririko wa maelezo ya wenyeji wa Mangwea na Mgaza Pembe ‘M 2 The P’ nayo yanaibua mapya ambayo awali yalikuwa hayajulikani.
MAELEZO YA SAUTI ZA WENYEJI
Wakizungumza hewani kupitia redio moja ya jijini Dar, wenyeji wao wawili waliojitambulisha kwa jina moja moja la Godfrey na Godluck ambao walikuwa na Mangwea na M 2 The P, kila mmoja alisema lake huku maelezo yao yakionesha dalili ya kutofautiana au kuzua maswali masikioni mwa watu.

BINTI AANIKA MAKALIO MBELE YA WABUNGE KATIKA SHINDALO LA MISS TABORA


Mmoja wa washabiki wa muziki wa kizazi kipya ambaye alivaa vazi lililoacha  matako  nje....

Shabiki huyo  alipanda jukwaani kumkumbatia  msanii  maarufu nchini , Ommy Dimpoz  wakati alipokuwa akitoa burudani katika mashindano ya Redds Miss Tabora.

Tukio hilo la aibu lilitokea  mbele ya  wabunge....
Mbunge wa Jimbo la Sengerema  Bw.William Ngereja akiwa na Diwani wa kata ya Kitete manispaa ya Tabora Bw.Daniel Mhina ambaye alikuwa MC katika onesho hilo lililofanyika katika ukumbi wa Frankman Hotel mjini Tabora.

Sophia Simba, Anne Kilango nusura wazichape walipokutana gafla benki

Kushoto Mh. Sophia Simba na kulia ni Mh. Anna Kilango
UHASAMA wa kisiasa kati ya Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na watoto, Sophia Simba na Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango, umevuka mipaka na sasa ni uadui wa wazi wazi. Hali hiyo ilidhihirika wiki iliyopita mjini Dodoma, wakati wawili hao walipokutana katika Benki ya CRDB iliyopo bungeni na badala ya kusalimiana, waliishia kutofautiana.
Shuhuda wa tukio hilo, aliiambia MTANZANIA, kuwa tukio hilo lilitokea saa 6 mchana, baada ya Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, kuahirisha Bunge kutokana na vurugu zilizosababishwa na wabunge wa upinzani, wakati wa mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.


Shuhuda huyo alisema kuwa, kabla ya tukio hilo, Anne Kilango pamoja na wabunge wengine wa CCM, walikuwa ndani ya benki hiyo wakibadilishana mawazo.

Wakati wakiendelea kuzungumza, Sophia Simba aliingia ndani na kuanza kuwasalimia kila mmoja kama ilivyo kawaida.
 

MWANA FA NA JIDE KWA MARA NYINGINE WATAFANYA SHOW ZAO SIKU MOJA

Ikiwa ni siku chache baada ya wasanii kuahirisha show zao kufuatia kuondokewa mpendwa wetu Albert Mangwea, miongoni mwa show kubwa zilizoahirishwa ni ya Lady Jay Dee (Miaka 13 ya Lady JayDee) na ya Mwana FA (The Finest) zilizokuwa zifanyike siku moja (May 31),show hizi zinaweza kufanyika tena siku moja kwa kuwa wasanii hao wametaja tarehe inayofanana.

May 28 ambayo ndiyo siku aliyofariki Mangwea mwana FA alithibitisha kuahirisha show yake, lakini alipoulizwa siku ambayo anadhani atairudia show hiyo, yeye alifunguka kupitia akaunti yake ya twitter na kuitaja June 14.

 “Sina uhakika,but I'll pick June 14th kama brother tutakuwa tushampumzisha"@umykitwana”, alitweet Mwana FA a.k.a Binamu.
 
 
Kwa upande wake Lady Jay Dee ambae kwa sasa a.k.a yake mpya ‘Anaconda’ inaonekana ku-take over ametumia akaunti yake ya twitter kuiweka wazi tarehe ya show yake alipokua akijibu swali la fan wake ambae atasherehekea siku moja ya kuzaliwa na msanii huyo (June 15).

“@MteiHaikaJ Gud. Chukua hii tar 13 June Mahakamani, tar 14 June miaka 13 ya Jide na tar 15 June Bday ya Jide. Let's celebrate long week end.”Alitweet Lady Jay Dee June 2.

Kwa tweets za wakali hawa wa bongo fleva inaonesha kabisa kuwa show zao zinaweza kufanyika june 14 japo Mwana FA alisema hana uhakika, labda kama atatangaza siku nyingine tena. June 14,tunatarajia kuwa marehemu Ngwair atakuwa amekwisha pumzishwa kwenye nyumba yake ya milele huko Morogoro.
CHANZO : LEOTAINMENT

WABUNGE WAKUTWA KWENYE DANGURO LA UCHI DODOMA

 Watu wanaingia mmoja mmoja, wengine kwa makundi na baadhi wapo nje wakipunga kwanza upepo kabla ya kuingia.

Siku hizi wanawake wanaingia bure au kwa jina jingine ‘ladies free’ jambo linalosababisha ukumbi huu ufurike watu.

Katika ukumbi huu, yapo maeneo mawili. Kuna sehemu ya kawaida ambayo kiingilio chake ni kuanzia Sh5,000 hadi Sh10,000 kutegemeana na matukio au burudani ya siku hiyo.

Pia kuna eneo jingine ambalo ni kwa watu maalumu ama waweza kusema ni ‘VIP’ ambapo wateja wake hutakiwa kulipa Sh20,000.

Ukumbi wa VIP upo juu na ule wa kawaida upo chini. Hata hivyo maeneo yote haya hujaza watu kwa kiasi kikubwa.

Mwandishi wetu alifika katika ukumbi wa VIP saa tano usiku, hata hivyo bado watu ni wachache katika eneo hili ukilinganisha na kule kwa watu wa kawaida.

Ukumbi wa VIP si mkubwa kieneo . Kuna kaunta ya vinywaji, makochi madogo madogo aina ya sofa yenye meza mbele yake, viti vilivyoizunguka kaunta na katikati ya ukumbi huu kuna meza mbili za duara zenye mti wa chuma katikati.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JUNE 03, 2013

1 a9412
17 20f78
5 173d6

Sunday, June 02, 2013

DIAMOND ATOA SIRI YAKE NA MANGWAIR.

 
DIAMOND.

 https://encrypted-tbn1.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcTcbPsmB8oL0NdNY9ZTMuOtFcF-881836OfLxvYzL9xEVxaoG1Z5Q


WAKATI watu mbalimbali maarufu nchini, hususan wasanii wa muziki wa kizazi kipya (Bongo Fleva), wakiendelea kutoa historia ya mahusiano yao na aliyekuwa msanii wa Hip Hop nchini Tanzania Albert Mangweair.

wea, msanii maarufu wa muziki nchini Nassib Abdul (Diamond Platnumz) amevunja ukimya na kutoa siri yake na marehemu Mangwea.

Akielezea hisia zake pamoja na mipango mingi aliyokuwa nayo kuhusu kufanya kazi ya muziki na marehemu katika ukurasa wake wa mtandao wa Instagram, Diamond alisema kwamba alijaribu kufanya kazi ya pamoja na msanii huyo lakini kwa bahati mbaya kazi zote zikaharibika.


"Kinacho niumiza ni jinsi tulivyo jaribu kutengeneza HIT bila mafanikio yaani siyo nilizo mshirikisha hata zile alizo nishirikisha na tuka amua kuplan kutengeneza nyingine akirudi kutoka Afrika Kusini, lakini haikuwezekana yani mungu alimpenda zaidi":alisema Platnumz.


Kila binadamu huwa na jambo lake muhimu ama siri ya mafanikio baina yake na mtu mwingine ambayo pengine si rahisi kuizungumzia hadharani ama wakati wowote, lakini inapotokea mmoja kati yao akifariki dunia anayebaki duniani hujikuta akitoa siri hiyo.


Hatua ya Binadamu kuamua kutoa siri yake na mwenzake wakati wa msiba wa mmoja wao inaweza ikawa na tafsiri nyingi lakini ukweli nikwamba huzuni na machungu ya kuondokewa na mtu muhimu kwake aliyekuwa akitarajia kufanya naye jambo flani muhimu ndiyo husababisha mtu huyo kutoa siri.R.I.P Mgwea.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...