Saturday, May 04, 2013

MAGAZETI YA MAY 4 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

WABUNGE:: SERIKALI SASA IWANG'OE VIONGOZI NECTA


Baadhi ya wabunge na wadau wa elimu wametaka Serikali kutoishia kufuta matokeo ya mtihani wa kidato cha nne, bali iwajibishe Baraza la Mtihani Tanzania (Necta) kwa kufelisha wanafunzi.

 
Akizungumza kuhusu kauli ya Serikali kufuta matokeo hayo jana, Mbunge wa Bukoba Vijijini, Jason Rweikiza alisema taarifa ya tume ingekuwa tofauti na ilivyotolewa ilikuwa isababishe vurugu nchini.

“Kauli hii ya Serikali ndiyo iliyotegemewa na wadau wa elimu, tume wangefanya vinginevyo tunge-riot (fanya vurugu), kwa sababu matokeo yaliyotolewa na Necta siyohalisi. Tume imefanya kazi nzuri na kilio cha wanafunzi kimesikika,” alisema Rweikiza na kuongeza:

“Sasa na hili nalisema bila kificho, Necta lazima wawajibishwe kwa sababu wanafunzi wanne wamejiua kwa matokeo hayo yasiyo halali, kule kwangu (Bukoba Vijijini) wanafunzi wamekata tamaa na wanaolewa. Hiyo yote ni hasara ambayo haina wa kuilipa.”

Aliongeza kuwa nchi nyingi duniani ikiwamo Marekani, mtihani wa mwisho hauchukuliwi kama kigezo kwa sababu inategemea mwanafunzi jinsi alivyoamka siku ya mtihani na kwamba, wanatumia mitihani iliyopita kufanya tathmini yao.

IZZO B......... "SINA MAHUSIANO NA WEMA WEMA SEPETU"

Siku chache baada ya kukwenda Arusha kwa mapumziko mafupi kutokana na kudhalilishwa na mpenzi wake wa dhamani Diamond kupitia redio...Beutifully onyinye wa Bongo, sasa hausishwa kutoka kimapenzi na msanii wa hip hop Izzo bizness..
  izzo bizness kupitia xxl ya clous fm chini ya u-heard ya alhamisi ya wiki hii alikanusha kabisa kuwa na mahusiano ya mrembo wema na kuthibitisha kuwa wao ni washikaji na wanakutana mara mojamoja ingawa wenyewe wamezoea kuitana 'darling' kwa mazoea..
KuSikiliza  kauli ya izzo bizness bfya hapo chini !!

GADNER....... "KAMA ASINGEKUWEPO LADY JAYDEE BASI NINGEKUWA NA VANESSA MDEE"

MUME wa Legend wa Bongo Fleva, Judith Wambura ‘Lady Jadee’, Gardner G Habash ‘Kapteini’ aliwaacha watu midomo wazi baada ya kusema kama angekuwa hajaoa, basi angemuoa msanii anayekuja kwa kasi kwenye gemu, Vanessa Mdee.
Kapteini alitamka hayo juzi katika kinyang’anyiro cha kumtafuta Redds Miss Dar Indian Ocean 2013 kilichochukua nafasi katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, Posta jijini Dar ambapo mume huyo wa Lady Jaydee alikuwa MC wa shughuli hiyo hivyo kutumia kipaza sauti kumnadi Vanesa.
Gardner G Habash ‘Kapteini’.
“Kiukweli Vanesa ni msanii mzuri, ana uwezo mkubwa wa kufanya muziki wa Hip Hop na kulitawala jukwaa. Ningekuwa sijaoa kwa kweli ningemuoa Vanesa Mdee,” alisema Gardner.
Mbali na Vanesa, wasanii wengine wanaounda familia ya B Heatz walipata nafasi ya kutumbuiza katika hafla hiyo akiwemo mkongwe, Ally Baucha

Friday, May 03, 2013

AGNES MASOGANGE HAISHI KUPIGA PICHA ZA KIMITEGO

SHILOLE......... "BILA CONDOM HUWEZI KULIFAIDI PENZI LANGU HATA UKINIHONGA MABILIONI"

Mwigizaji na mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya Zena Mohamed, maarufu kwa  jina  la   shilole amedai kuwa anaweza kufanya ujinga wowote humu duniani lakini linapokuja suala la mapenzi kamwe hawezi kwenda pekupeku ( bila  condom )  ....

Akiongea kwa  kujiamini ,Shilole  alisema kuwa hata mtu awe vipi, au awe wa dini gani au awe na pesa kiasi gani kamwe hawezi kumvulia nguo kama  hana  kondom  mkononi.....
Msanii  huyo  alienda  mbali  zaidi  na  kuzilaani   kauli   za  baadhi  ya  watu zinazosema eti ukitumia "CONDOM"  ladha ya mapenzi inapungua.Yeye  anadai  kuwa  ni  mdau  wa  "GEMU"  hilo  na  huwa  anatumia  NDOM  kama  kawa  na  hufurahia  kama  kawaida...

" Hata niwe nimelewa kiasi gani huwa nipo makini sana maana najua vijana wengi wa mjini wananimezea  mate....Waje  tu , lakini  bila  KINGA wataambulia  PATUPU!!” Alisisitiza Shilole

WOLPER "NAJUTA KUJIINGIZA KWENYE MAPENZI"...!!

DIVA wa kiwango cha juu cha filamu hapa Bongo, Jacqueline Wolper, ameonekana kujutia historia yake ya kimapenzi baada ya kufungukia kitendo cha yeye kumuanika kila aliyekuwa akimpenda kwamba kimemtibulia na sasa amejifunza kutokana na makosa.
Jacqueline Wolper.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Wolper alisema kuwa, kwenye maisha yake ya huko nyuma ameshajianika akiwa na wapenzi tofauti lakini sasa atakayempa nafasi kwenye moyo wake hatamuanika ila hilo litakuja baadaye sana kwani sasa hivi kaweka pembeni kwanza mambo ya mapenzi.
“Sitaki yajirudie yaliyotokea katika maisha yangu ya huko nyuma, hata hivyo sasa hivi niko bize sana na kazi, mambo ya wanaume nimeamua kuyaweka pembeni kwanza,” alisema Wolper na kuongeza:
“Sitaki itokee kama ilivyokuwa kwa Dallas ambapo kila mtu alijua alikuwa ni mtu wangu, kwa sasa nimeamua kutulia kwanza na hata nikimpata mwingine watu hawatamjua hadi wakati wa ndoa.”

BREAKING NEWZZZZZZZZZZZZZ!!!! : MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2012 KUSAHISHWA UPYA,

wpid-Prime-Minister-Mizengo-PindaTAARIFA  KUTOKA BUNGENI MUDA HUU AMBAPO WAZIRI LUKUVI  AMETANGAZA KURUDIWA UPYA KUSAHISHWA KWA MITIHANI YA KIDATO CHA NNE KWA MWAKA 2012,HII IMETOKANA NA MAPENDEKEZO YALIYO TOLEWA NA TUME ILIYO UNDWA KUCHUNGUZA TATIZO LA WANAFUNZI WENGI KUFELI KATIKA HUO MTIHANI,PIA AMESITISHA KUANZA KUTUMIKA KWA VIWANGO VIPYA VYA UFAULU.

MCHUMBA WA MTU ATUPWA JELA KWA KUJIUZA...........!!!


Na Richard Bukos

MREMBO Brandina Barthon (24), Jumatatu iliyopita alihukumiwa kwenda jela miezi 6 baada ya kupatikana na hatia kwenye kesi ya ukahaba iliyokuwa ikimkabili katika Mahakama ya Sokoine Drive (Jiji) jijini Dar.
Brandina alisomewa hukumu hiyo na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, William Mutaki ambaye alisema kutokana na ushahidi uliothibitika, mahakama hiyo inamhukumu kwenda jela miezi 6, ili liwe fundisho kwa wengine.
Hukumu hiyo ilimfanya mrembo huyo kuchanganyikiwa na kuangua kilio lakini mheshimiwa hakimu aliamua kukazia hukumu yake bila ya kupepesa
macho.
 
Wakati mwanamke huyo akiangua kilio, afande wa Jeshi la Magereza alimfikia na kumchukua  kwa ajili ya kumpeleka kwenye Karandinga kuelekea Gereza la Segerea kuanza maisha ya jela.
Mbali na Brandina, mwanaume aliyedaiwa kuwa ni mpenzi wa mtuhumiwa huyo aliyekuwa akifuatilia kesi hiyo naye alimwaga machozi baada ya kutolewa hukumu hiyo.

HII NDIO LIST KAMILI YA VIONGOZI WA TANZANIA NA WA KIMATAIFA WALIOJIUNGA FREEMASONS


Siri ya List za Viongozi wa Tanzania Yatajwa (Secret Society), Freemason, imedaiwa kuwa na siri nzito na viongozi wakuu wa nchi yetu, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.





MWINYI NA ANDY CHANDE


Madai hayo, yametokana na kile kinachoonekana kwamba Kiongozi Mkuu wa Freemason, Afrika Mashariki, Sir Andy Chande, amekuwa akijiweka karibu na viongozi wakuu wa nchi hii kila awamu, hivyo kuonesha kuwa kuna kitu anakitafuta.
Andy Chande

Andy ChandeKikubwa kinachodaiwa ni kuwa Chande anatumiwa na Freemason kuhakikisha kwamba kila kiongozi wa nchi hii anakuwa karibu na jamii hiyo ya siri.
Inazidi kudaiwa kuwa Freemason inafanya njama za hali ya juu kujiweka karibu na Ikulu, ikiwa na mpango wao wa muda mrefu wa kusimika rais ambaye ni memba wa jamii hiyo katika awamu zinazokuja.
Uchunguzi umeonesha kuwa Chande amekuwa karibu na Ikulu tangu Awamu ya Kwanza chini ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na amedumu kujiweka karibu na viongozi wa nchi mpaka awamu hii ya nne chini
ya Rais Jakaya Kikwete.

NEEMA YAWASHUKIA WALIOFELI .... MATOKEO YA KIDATO CHA NNE KUPANGWA UPYA


TUME ya kuchunguza sababu za kufeli kwa kiasi kikubwa kwa wanafunzi wa kidato cha nne waliofanya mitihani ya kuhitimu mwaka 2012 imekamilisha kazi yake na taarifa za uhakika zilizolifia gazeti hili zinasema , upangaji alama zao utafanyika upya.

Kama ambavyo gazeti hili lilivyobaini katika uchunguzi wake wa kiuandishi kwamba kulifanyika mabadiliko ya utoaji alama kwa ajili ya mitihani waliyofanya wanafunzi mwaka huo (2012) bila maandalizi kwa wadau, tume hiyo imependekeza alama zipitiwe upya (regrading).Katika alama za awali, alama D anapoyopewa mtahiniwa baada ya mtihani wake kusahihishwa ilikuwa ni kuanzia alama 21 kwenda mbele na F ilikuwa 20 kushuka chini lakini katika mabadiliko yaliyoleta ‘maafa’ ya kufeli kwa watahiniwa wa mwaka jana, alama D ilianzia 35 na kuendelea, wakati ile ya kufeli (F) ilianzia alama 34 kushuka chini.

MAGAZETI YA MAY 3, 2013

.
.

Thursday, May 02, 2013

HUSANA IDD NA NAOMI WA BONGO MOVIE WAGOMBEA PENZI LA JANUARY...!!

Msanii anayechipukia kwenye soko la filamu na muziki, Naomi Mbaga ameibuka na kumuonya Husna Idd ‘Sajent’ amuachie bwana wake, January.
 Akizungumza na mwandishi wetu, Naomi aliweka bayana kuwa January ambaye ni Mwanamuziki wa Bendi ya Victoria ni mpenzi wake wa muda mrefu hivyo alishangazwa kuona habari mitandaoni kuwa Sajent amejituliza kwa mpenzi wake huyo baada ya kumwagana na mzazi mwenzake, Charles Gabriel ‘Chaz Baba’.

“Aniachie bwana wangu, kama ameachika kwa huyo Chaz Baba atafute bwana mwingine na siyo wa kwangu. Ole wake nimkute naye siku, atanitambua,” alisema Naomi.

Sendeka, Shelukindo wamtetea Kinana

Tuhuma dhidi ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman  Kinana, (pichani) kuhusika katika usafirishaji wa pembe za ndovu, zimewalazimisha wabunge kadhaa wa  CCM kumsafisha.

Hali hiyo ilijitokeza juzi jioni wakati wakichangia hotuba hiyo ya Wizara ya Maliasili na Utalii.

Tuhuma hizo zilitolewa na Msemaji wa Kambi ya Upinzani, Mchungaji Peter Msingwa (Chadema), kuituhumu kampuni ya Sharaf Shipping Agency inayomilikiwa na Kinana kukamatwa na pembe za ndovu nchini China.

Mbunge wa Simanjaro , Christopher  Ole Sendeka (CCM), alimtetea Kinana kuwa kampuni yake haihusiki katika sakata la pembe za ndovu.

Chadema yachelea kujitoa mchakato wa Katiba

Sina mpango wa kujitoa kwenye Tume kwa kuwa nimekula kiapo kwa ajili ya Watanzania, hadi sasa sijaona sababu ya kutaka kujitoa, alisema Profesa Baregu.
Dar es Salaam. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeshindwa kutoa kauli kuhusu kujitoa kwake kwenye mchakato wa Katiba Mpya baada ya muda kilioutoa kwa Serikali kutaka kurekebishwa kwa baadhi ya mambo katika mchakato huo kumalizika juzi.
Mwenyekiti wa Chadema na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alisema bungeni Aprili 11, mwaka huu kuwa chama chake kitajitoa katika mchakato huo endapo mambo muhimu mawili hayatapatiwa ufumbuzi hadi kufikia Aprili 30, mwaka huu.
Mambo hayo ni kufutwa kwa uchaguzi wa wajumbe wa mabaraza ya wilaya ya katiba uliofanywa na Kamati za Maendeleo za Kata (WDC), badala yake wachaguliwe moja kwa moja na wananchi wa kata husika bila kuchujwa na kamati hizo.

YULE MHINDI ALIYEDAIWA KUMUUA MWALIMU WA SHULE YA MSINGI NAYE AJIUA.......!!!

MHINDI mwenye uraia wa India, Srinivasa Rao Talluri, 36 anayedaiwa kumuua Mwalimu Elizabeth Mmbaga wa Shule ya Msingi Atlas, jijini Dar es Salaam amejiua Aprili 17 mwaka huu katika Hoteli ya Transit iliyopo Karakata.

Talluri ambaye alikuwa akifanya kazi katika kampuni ya vinywaji vikali ijulikanayo kwa jina la Moan’s Drinks Ltd iliyopo Oysterbay, Dar maiti yake ilikutwa chumbani saa mbili asubuhi na inadaiwa alijiua kwa kunywa sumu ambayo mabaki yake yamepelekwa Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwa uchunguzi.
Habari za kipolisi zimesema kuwa baada ya wafanyakazi wa Hoteli ya Transit jijini Dar kugundua kuwa Mhindi huyo amekufa, walitoa taarifa polisi ambao walifika na walipochunguza chumbani, walikuta kuna pombe aina ya Pushkin chupa tatu, chupa yenye sumu ya kuulia wadudu, chips na maziwa glasi moja.
Marehemu Elizabeth Mmbaga enzi za uhai wake.
Inadaiwa kwamba Mhindi huyo aliachishwa kazi katika kampuni hiyo Aprili 2, mwaka huu baada ya kugundulika kuwa alitumia vibaya zaidi ya shilingi 400,000 ambapo Aprili 3, mwaka huu alifikishwa polisi Kituo cha Oysterbay, jijini Dar.
Mwandishi wetu alifika katika ofisi za Moan’s Drinks Ltd alikokuwa akifanyia kazi Mhindi huyo na kuonana na mmoja wa viongozi wa kampuni hiyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Raju na akakiri kutokea kwa kifo cha Talluri.
Habari zinasema mwili wake ulifanyiwa uchunguzi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Jumatatu iliyopita na ukasafirishwa kupelekwa India Jumatano ya wiki iliyopita  kwa ajili ya mazishi.
Kitanda walichokuwa wakilala wapenzi hao.
Mhindi huyo anadaiwa kuwa alikuwa mpenzi wa Mwalimu Elizabeth ambaye siku moja kabla ya kifo chake imeelezwa kuwa alikuwa naye kwenye baa moja karibu na nyumba ya Eliza, hata hivyo, alikutwa amekufa katika chumba chake Kimara Baruti, Dar Aprili 15 mwaka huu huku shingoni kukiwa na michubuko iliyoashiria kuwa alinyongwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, ACP Marietha Minangi amethibitisha kutokea kwa kifo hicho katika hoteli hiyo.
“Ni kweli alikutwa amekufa katika Hoteli ya Transit na chumbani tulikuta sumu ambayo tumepeleka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwa uchunguzi,” alisema.

CCM WAMVAA MKUU WA MKOA WA ARUSHA.....WANADAI AMEMUONGEZEA UMAARUFU GODBLESS LEMA...!!

VIGOGO wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakiwemo wabunge, wamemjia juu Mkuu wa Mkoa (RC) wa Arusha, Magessa Mulongo kwa jinsi alivyoshughulikia kesi ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA).

Wabunge hao waliliambia gazeti hili mjini Dodoma kuwa kesi ya uchochezi iliyofunguliwa na serikali dhidi ya Lema kwa shinikizo la mkuu huyo, itaiathiri kwa kiasi kikubwa CCM.

Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola alisema kuwa amefuatilia kwa makini chanzo cha kesi ya Lema na hatimaye kukamatwa na polisi mithili ya gaidi, na kubaini kuwa hulka 

za utendaji kazi wa baadhi ya viongozi wa serikali zinawapa sifa na umaarufu zaidi CHADEMA.
“Mimi sitaki kuingilia kesi, lakini ukiangalia kuanzia ile inayoitwa video ya vurugu za Chuo cha Uhasibu Arusha na jinsi Mkuu wa Mkoa alivyofika eneo la tukio na kuondoka, utabaini udhaifu mkubwa wa kiongozi huyo ambao leo unamfanya Lema aonekane shujaa.
“Leo tunaingia kwenye uchaguzi mdogo wa madiwani pale Arusha, tunaweza tukashinda, lakini tutafanya kazi ya ziada kwa sababu tu ya udhaifu wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha,” alisema Lugola.

LIL WAYNE AZIDIWA TENA, AKIMBIZWA HOSPITALI.


According to TMZ, rapper Lil Wayne was rushed to Cedars-Sinai Hospital in L.A on Tuesday night after suffering another seizure. He was treated and released yesterday morning.
Wayne then did a radio interview yesterday afternoon and explained he's an epileptic, and has been suffering from seizures since he was a kid.

MWAKA MMOJA KABURINI... KANUMBA THE GREAT FILM INAPUMULIA MASHINE

Mojawapo ya ofisi za Kampuni ya Kanumba The Great Films illiyopo Sinza Mori.
MIPANGO endelevu inapaswa kufuatwa na kila mwanadamu, katika familia zetu za Kiafrika mara nyingi tunaanguka katika suala la mipango mikakati ya muda mrefu. Mwanadamu akifariki, mara nyingi wanaoachwa kuendeleza kazi za marehemu wanaishia kusuasua na kutofikia malengo.

Yapata mwaka mmoja tangu, aliyekuwa legend wa simema za Kibongo, Steven Kanumba ‘The Great’ afariki dunia na kuiacha Kampuni yake ya Kanumba The Great Film ikiendeleza shughuli zake za kuzalisha filamu kama kawaida.
Kampuni aliyoiacha pale Sinza-Mori, jijini Dar ilibaki chini ya mikono ya wafanyakazi wake  wakiongozwa na mdogo wa marehemu, Seth Bosco, mpiga picha za video, Zakayo Magulu pamoja na Mayasa Mrisho ‘Maya’ ambaye alikuwa akifanya kazi kama msimamizi wa ‘location’ (location manager) na masuala ya makeup.
Kadiri siku zilivyozidi kusonga, umoja kati yao ulianza kupungua. Kila mmoja anaonekana kuhangaika kivyake licha ya kwamba kampuni bado ipo. Mikakati ya jumla ikawa haijadiliwi, kila mmoja akawa anaangalia namna ya kujikwamua kivyake.
Mara kadhaa nimekuwa nikizungumza na baadhi ya wasanii waliokuwa tegemezi katika kampuni hiyo, wamekuwa wakiniambia wapo bize kufanya kazi zao binafsi nje ya Kanumba The Great Film. Hiyo inaonesha dalili kwamba kazi za umoja zimeanza kulegalega.

Marehemu Steven Kanumba akiwa na tuzo za filamu enzi za uhai wake.

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MEI 2, 2013

DSC 0001 bc82f


DSC 0003 2124b


DSC 0005 0924a

Mh. Rais Ang'atwa na Chui............!!!

 
Rais wa Botswana, Ian Khama ameshonwa baada ya kung'atwa na Duma, kwa mujibu wa maafisa wakuu nchini humo.

Mnyama huyo alikuwa analishwa alikokuwa anahifadhiwa katika kambi ya kijeshi wakati alipomrukia rais Khama na kumgwara

Tukio hilo ilikuwa ajali tu wala sio shambulio kali, kwa mujibu wa msemaji wa serikali Jeff Ramsay aliyezungumza na waandishi wa habari.

Majeraha ya Bwana Khama, yalikuwa madogo wala haikujitokeza kama ajali kubwa.
Inaarifiwa ajali ilitokea ghafla na kumgutukia Rais Khama na walinzi wake.

"Duma alimgwara tu lakini sio kumshambulia, kama wanavyodahani watu wengi,'' alisema bwana Ramsay.

Bwana Khama alionekana akiwa amevalia plaster kwenye mkutano ulioandaliwa baada ya tukio hilo.

Duma, ambao ndio wanyama wenye kasi kubwa zaidi ardhini, ni moja ya wanyama wanaokabiliwa na tisho kubwa la kuangamia.

Ni wanyama 12,400 pekee wanaosemekana kusalia mbugani katika baadhi ya nchi za Afrika ikiwemo Botswana.

WASTARA AKATAA KUWA MKE WA PILI

http://api.ning.com/files/rCNzRKkcZYaRl8rT2Ghdp11G9XsjfHgOhCzL8GUhxCcWXmVRrcxNgzbihjqVgYMmwttiYFQiMBFUCChccEmDHRHxexbh7OqI/Wastara.jpg 
                                                          Wastara Juma.
MSANII wa filamu za Kibongo, Wastara Juma hivi karibuni alikataa kuolewa na kuwa mke wa pili baada ya kupigiwa simu na mwanamke mmoja jijini Dar akimtaka awe mke mwenzake.
Wastara ambaye hivi sasa yuko Uarabuni kwa ajili ya mapumziko baada ya kufiwa na mumewe, Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’, Januari mwaka huu, alikataa ofa hiyo na kusema kwamba kwa sasa hafikirii kabisa kuolewa.
Kwa mujibu wa chanzo chetu makini, mwanamke huyo aliamua kufanya hivyo baada ya kushauriana na mumewe kuhusu Wastara kuingia katika familia yao.
“Mwenyewe alisema alishauriana na mumewe na haoni tatizo Wastara kuwa mke mwenzake kwa sababu imani ya dini yao inaruhusu,” kilieleza chanzo hicho.

MHASHAMU TITUS ASIMIKWA KUWA ASKOFU MSAIDIZI DAR

IMG_0286  
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na MwadahamaPolycarp Kaldianali Pengo (kushoto) wakishuhudia wakati Mhashamu Titus Mdoe, Askofu Msaidi wa Jimbo Kuu la Dar es salaam katika Misa ya kumsimika Askofu huyo zilizofanyika kwenye viwanja vya Msimbazi Centre jijini Dar es salaam Me 1, 2013. (Picha na  Ofisi ya Waziri Mkuu)
IMG_0326 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimkabidhi zawadi ya picha Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es slaam, Mhashamu Titus Mdoe katika ibada ya kumsimika askofu huyo iliyofanyika kwenye viwanja vya Msimabazi Centre jijini Dar es salaam, Mei 1, 2013 . kulia ni Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda. (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)IMG_0330 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na  Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es slaam, Mhashamu Titus Mdoe katika ibada ya kumsimika askofu huyo iliyofanyika kwenye viwanja vya Msimabazi Centre jijini Dar es salaam, Mei 1, 2013 . kulia ni Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda. (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Wednesday, May 01, 2013

Kimenuka! Sasa hivi vimini ‘No’ kwenye filamu, bodi ya filamu imeona ilivalie njuga suala hili.

TAARIFA iliyotua kwenye dawati la gazeti hili hivi karibuni inaeleza kuwa, mavazi yasiyo ya heshima vikiwemo vimini yamepigwa marufuku...
kuvaliwa na wasanii kwenye filamu wanazorekodi na yoyote atayekiuka atakiona cha mtemakuni.Chanzo chetu makini kilichoomba hifadhi ya jina lake, kimeeleza kuwa waliotoa agizo hilo ni Serikali ya Tanzania kupitia Bodi ya Filamu lengo likiwa ni kuhakikisha maadili ya taifa yanazingatiwa.
Ikaelezwa kuwa hatua hiyo imekuja kufuatia uwepo wa filamu nyingi mtaani ambazo wasanii wanaoshiriki huvaa mavazi yasiyo ya heshima, mazingira yanayoiharibu jamii. 

“Kama wanavyosema vijana huko mtaani kwamba kimenuka na kweli kimenuka! Sasa hivi vimini ‘no’ kwenye filamu, bodi ya filamu imeona ilivalie njuga suala hili ili kulinda maadili ya taifa,” kilieleza chanzo hicho.


Katika kujua ukweli wa jambo hili, mwandishi wetu alimtafuta Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Simon Mwakifwamba ambaye alikiri kuwepo kwa utaratibu mpya wa Bodi ya Filamu wa kuzipitia filamu zinazoingia mtaani na kwamba zinazokiuka maadili zinafungiwa. 
Mwakifwamba alisema ni kweli mavazi ya nusu utupu hayataruhusiwa tena kuonekana kwenye filamu kama ilivyokuwa huko nyuma na wale watakaojifanya vichwa ngumu watashughulikiwa.
“Sasa hivi kuna sheria mpya kabisa, hakuna kuvaa nguo zisizo za maadili na ukikiuka basi filamu yako haioneshwi au kama unaweza urudie na kuondoa vipande vilivyoharibu filamu hiyo,” alisema Mwakifwamba huku kukiwa na maelezo kuwa, hilo pia litasimamiwa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo chini ya Waziri Fenella Mukangara.

WOSIA WANGU KAMA IKITOKEA NIMETANGULIA KUFA KABLA YA RUGE AU JOE KUSAGA:..........JIDE

Watu wanashtuka mtu akiongelea kifo, Utafikiri hawafahamu fika kuwa kila nafsi itakionja, Kwenye maisha yangu nimepitia mambo mengi, magumu na mepesi
Na bado naendelea ku experience mambo magumu zaidi kadri ninavyozidi kuwa mkubwa.

Siku za karibuni nimekuwa nikipigwa vita sana na watu wenye uwezo mkubwa kifedha , ki umri na hata wenye ukubwa wa connection katika hii industry ya muziki. Wanaomiliki chombo cha habari.

Nasimama na kusema kuwa sitokata tamaa, kwani lengo lao kubwa ni kuona na kuhakikisha nimeanguka kabisa na sipo katika ramani ya muziki.

Watu hao ambao vita yao ilikuwa baridi miaka kumi iliopita, sasa inazidi kuwa moto baada ya kutambua kuwa mimi ni mtu mwenye maamuzi yangu na misimamo yangu bila kuburuzwa.
Wanapita kila mahali kuhakikisha kila mrija unaoniingizia chochote unakatika, na hiyo ni kutaka kuuthibitishia umma wa Tanzania kuwa hakuna msanii anaeweza ku survive bila wao.

HUYU NDO MODAL KUTOKA GERMANY, ALIYEAMUA KWENDA KAZINI AKIWA UCHI WA MNYAMA

 
A STUNNING model gives fellow commuters a wake-up call to remember by riding the train completely starkers. The brunette wore only glasses and shoes for her nude ride to work. And in place of clothes, she daubed herself with words describing what they might have expected her to have been wearing. Model rides without clothes Skin full view ... model rides without clothes TNI Press
The woman carried out the stunt in Dusseldorf, Germany. After boarding a train without blushing, the lady ensured she purchased a ticket before taking her seat as normal. THE model showed her flawless figure to fellow commuters on the train in Germany as part of an art project Stunned passengers gawked open-mouthed as the woman showed off her flawless figure.
Naked model on a train in Germany Wake-up call ... but some passengers on the train still managed to stay asleep TNI Press But remarkably, some of them gave barely a sideways glance as she walked through the carriage in the buff. The model’s naked journey was part of a project put together by Swiss artist Milo Moire. Entitled The Script System, the stunt was intended as a way of "shaking up the ordinary". Swiss artist dreamed up scheme to have naked model take a train ride in Germany Stunt ...

 Swiss artist dreamed up scheme TNI Press Milo Moire said the model walking around the train without clothes was meant to make people think outside the box on their commute. He wrote on his website: “Radical nudity becomes the defence shield against the stereotypes and makes the artist invisble.” And he went on to say that the timing of the early morning stunt meant ordinary performance art was out of the question.TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

ANGALIA PICHA ZA DIAMOND PLATNUMZ AKIWA NYUMBANI KWA MTOTO WA KAMANDA KOVA UINGEREZA


Taarifa mbalimbali za michezo kutoka TFF ikiwemo ligi kuu ya Vodacom kuingia raundi ya 25 hapo kesho.

Afisa Habari wa TFF Boniface Wambura.
LIGI KUU YAINGIA RAUNDI YA 25
Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inaendelea katika raundi yake ya 25 kesho (Mei Mosi) kwa mechi tano zitakazochezwa katika miji ya Dar es Salaam, Turiani, Morogoro na Mlandizi.
Licha ya kuwa tayari Yanga imetawazwa kuwa mabingwa wa VPL msimu huu (2012/2013), mechi dhidi ya Coastal Union itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni moja kati ya zitakazovuta macho na masikio ya washabiki wa mpira wa miguu nchini.
Mechi hiyo namba 172 itachezeshwa na mwamuzi Simon Mberwa kutoka Pwani akisaidiwa na Said Mnonga na Charles Chambea wote wa Mtwara wakati mwamuzi wa mezani atakiwa Hashim Abdallah wa Dar es Salaam. Kamishna wa mechi hiyo ni David Lugenge kutoka Iringa.
Viingilio katik mechi hiyo itakayoanza saa 10.15 jioni ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya bluu na kijani, sh. 8,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 kwa VIP C na B wakati VIP A itakuwa sh. 20,000. Tiketi zitauzwa uwanjani siku ya mchezo.
Mtibwa Sugar itakuwa mwenyeji wa African Lyon katika mechi namba 170 itakayochezeshwa na mwamuzi Dominic Nyamisana wa Dodoma kwenye Uwanja wa Manungu ulioko Turiani mkoani Morogoro. Nayo Kagera Sugar iliyo katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi hiyo itakuwa mgeni wa Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Kambi ya Upinzani Bungeni imetoa tuhuma nzito kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.

Kambi ya Upinzani Bungeni imetoa tuhuma nzito kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana ikidai kuwa anajihusisha na mtandao wa ujangili nchini.
                                        Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana. 
Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi amejibu tuhuma hiyo akisema ni za uongo huku akiituhumu kambi hiyo kuwa imedanganya wakati inajua ukweli kuhusu tuhuma dhidi ya Kinana.
Akiwasilisha maoni ya upinzani kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii mwaka 2013/14, Msemaji wa Kambi ya Upinzani kuhusu Maliasili, Mchungaji Peter Msigwa alisema vitendo vya ujangili vimekuwa vikilitia doa taifa kwenye jumuiya za kimataifa.
“Kwa bahati mbaya ni kwamba wahusika wengi ambao wanatajwa kwa ushahidi ni makada maarufu na wengine ni viongozi waandamizi wa CCM,” alisema Mchungaji Msigwa.
“Tumeshuhudia watuhumiwa wengine wa ujangili ambao Ikulu imediriki kuwapatia nafasi kubwa za uongozi wa taifa hili, licha ya kutajwa kwenye ripoti ya uchunguzi kuhusiana na ujangili.”
Alisema mwaka 2009, meli ya Kampuni ya Wakala wa Meli ya Sharaf Shipping inayomilikiwa na Kinana ilikamatwa China ikiwa na makontena yenye nyara za Serikali ikiyasafirisha kwenda Hong Kong.

RAIS KIKWETE AUNGA MKONO HOJA YA MBATIA KUHUSU MITAA YA ELIMU.

Rais Kikwete. Mbunge wa kuteuliwa, James Mbatia. 
RAIS Jakaya Kikwete amekubaliana na hoja ya Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia kuhusu kufanyiwa marekebisho kwa mitalaa ya elimu nchini ili iendane na viwango vya elimu inayohitajika.

Rais Kikwete alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na wenyeviti na wamiliki wa shule na vyuo vya binafsi kwenye Ukumbi wa Benjamin Mkapa, Mbeya.

Katika kikao cha Tano cha Bunge, Januari mwaka huu, Mbatia aliwasilisha hoja binafsi kuhusu ubovu wa elimu na mitalaa, hoja aliyodai kufinyangwa na Bunge kabla ya kupatiwa majibu stahiki na hata kuzua mjadala mkali miongoni mwa wadau wa sekta hiyo.

Akizungumza jana, Rais Kikwete alisema: “Mitalaa na mihutasari ya elimu itarekebishwa ili kuzingat
ia mazingira ya sasa ya dunia na ni lazima tuwe na viwango vya elimu vya kimataifa.”

RAIS OBAMA AMPONGEZA MWANAUME SHOGA ALIYEJITANGAZA HADHARANI


Mchezaji wa mpira wa kikapu nchini Marekani mwenye asili ya Afrika Jason Collins amejitangaza kuwa yeye ni shoga hatua ambayo imewashitua watu wengi hususani wapenzi wa mchezo huo.

Jason Collins anakua mchezaji wa kwanza wa kimataifa mwanaume ambaye bado anacheza mpira wa kikapu kutangaza kuwa ni shoga huku akisema kuwa yeye ni mwanamme mweusi na ni shoga.

Rais wa Marekani Barack Obama amempongeza mwanababa huyo shoga mwenye umri wa miaka 34 anayecheza katika ligi ya NBA kwa kujitangaza hadharani.

Rais Obama ambaye mwaka jana alitangaza kuunga mkono ndoa za mashoga alimpigia simu Collins na kumpongeza kwa ujasiri alioonyesha na amesema atamuunga mkono.

Mchezaji wa zamani wa NBA John Amaechi mwaka 2007 alijitokeza hadharani na kutangaza kuwa ni shoga lakini yeye alifanya hivyo akiwa tayari amestaafu kucheza kikapu.

Naye Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton alimpigia simu Collins na kusema kuwa hatua hiyo ni muhimu kwa wanamichezo wa kimataifa na ni historia kwa jumuiya ya mashoga na wasagaji.

Binti wa Bill Clinton, Chelseea ambaye amesema kuwa alimfahamu Collins wakati wakiwa wanachuo katika chu kikuu cha Stanford na meandika katika ukurasa wake wa tweeter kwamba anaona fahari kubwa kwa rafiki yake Collins kwa kuwa na ujasiri wa kuwa mchezaji pekee wa NBA shoga na kuweka hadharani hali yake.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 01.05.2013

.
.
.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...