Monday, March 04, 2013

WAZAZI WASHTAKIWA KWA KUMPAKA MTOTO WAO CHOCOLATE NA KUMFANANISHA NA BALOTELI

Baby 'blacked up' to look like Balotelli
HII NDIO PICHA YA MTOTO,PEMBENI NI BALOTELIWazazi wawili nchini uingereza wameshtakiwa kwa kosa la kumpaka mtoto wao Chocolate usoni na kisha kumpiga picha na kuiweka picha hiyo katika mtandao wa Twitter. Dakika chache baada ya kuiweka picha hiyo Mtandaoni watu wengi waliRT. Na haya ni baadhi ya maoni ya watu walioyatoa kuhusiana na picha hiyo



Matt Bishop, wrote: “Jesus wept, who does this to their child!?!?!?!?”
 Mwingine alisema hivi “Parents tweeted ghastly picture of baby dressed as Mario Balotelli, this must be child abuse.”  nao watetea haki za watoto hawakua nyuma, mmoja wao alitoa maoni haya “Just looking at this picture makes me very uncomfortable, especially the fact the child is blacked up. I don't like it at all.” 

MALAWI YAANZA TENA KUTISHIA NYAU WATUWAZIMA


 
Kwa ufupi
SERIKALI ya Malawi imesema ina wasiwasi kuhusu hatma ya mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa na kwamba hali hiyo inatokana na Tanzania kuvunja sehemu ya makubaliano ya usuluhishi.
SERIKALI ya Malawi imesema ina wasiwasi kuhusu hatma ya mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa na kwamba hali hiyo inatokana na Tanzania kuvunja sehemu ya makubaliano ya usuluhishi.

Kauli hiyo inakuja wakati jopo lo viongozi wastaafu kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika(Sadc), likijiandaa kuwasilisha ripoti yake baadaye mwezi huu.
Jopo hilo linaloongozwa na Rais Mstaafu wa Msumbiji, Joachim Chissano, litakabidhi ripoti hiyo kwa viongozi wakuu wa nchi zote mbili.

Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Malawi, Ephraim Chiume, ameituhumu Tanzania kwamba imeanza kuzungumzia utatuzi wa mgogoro huo wakati ikijua kuwa mzozo huo uko katika hatua ya upatanishi maalumu.

Waziri Chiume aliikosoa kauli iliyotolewa hivi karibuni na Waziri wa Mambo ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, kuwa ufumbuzi wa mgogoro wa mpaka baina ya mataifa hayo mawili, unakaribia kupatikana.
Alisema  kitendo cha  Membe kuzungumzia maendeleo ya mgogoro huo kinapingana na makubaliano ya pamoja yaliyowasilishwa kwa  Chissano na kwamba hatua hiyo inavunja moyo.

Waziri Chiume aliliambia gazeti la Nyasa Times kuwa pande zote mbili zilipokutana Nombemba 17 mwaka jana jijini Dar es Salaam, zilikubaliana kuzungumzia mgogoro huo ili kuepuka kuingilia juhudi za upatanishi. Alisema hata hivyo, hivi karibuni ya Serikali ya Tanzania imekiuka sehemu ya makubaliano hayo.
 “Tanzania wamevunja makubaliano, na sisi tunasisitiza kuwa Ziwa Nyasa ni la Malawi,” alisema waziri.

Baadhi ya wachambuzi wa mambo, wamesema kauli huyo inaashiria kuwa huenda pande hizo mbili zikashindwa kukubaliana na mapandekezo yatakayowasilishwa na mpatanishi wa mzozo huo.
Mpatanishi huyo mwezi huu anatazamiwa kukutana na Rais Jakaya Kikwete na yule wa Malawi, Joyce Banda.

Hata hivyo, alivyotafutwa ili kuzungumzia malalamiko hayo, waziri Membe  kupatikana, lakini Naibu wake Mahadhi Maalimu, alisema: “Ninachosema mimi kwanza hizo taarifa sijazipata na kama zipo basi Serikali itawasiliana kupitia mikondo sahihi. Serikali haiwezi kujibizana kupitia magazeti”

Hivi karibuni Serikali ya Tanzania na Malawi zilipeleka barua ya pamoja kwenye Jukwaa la Marais wa Wastaafu wa Nchi za Kusini mwa Afrika linaloongozwa Chissano, zikiomba zipatanishwe katika mzozo huo.

Hatua hiyo ilikuja  baada ya majadiliano ya pande zote mbili kushindwa kuzaa matunda.
Kama sehemu ya kuepusha mgongano wa kimaslahi, jopo hilo la wasuluhishi halikuwahusisha viongozi wastaafu wa Tanzania Alhaji  Ali Hassani Mwinyi na  Benjamin Mkapa.
Hali kadhalika Bakiri Muluzi wa Malawi.

Hata hivyo, duru za kidiplomasia mjini Lilongwe zinasema  Serikali ya Malawi imejiandaa kwenda katika  Mahakama ya Haki ya Kimataifa(ICJ) kama upatanishi huo utashindwa kuzaa matunda.
Gazeti la Daily Times limewanukuu maofisa wa Serikali wakisema kuwa karata ya mwisho kwa Malawi itakuwa ni kwenda katika mahakama hiyo.

Read more: http://audifacejackson.blogspot.com/#ixzz2Mc2j8Jzo

CCM YAMLAUMU MAALIM KWA KAULI YA "IKIBIDI LITOTE TUGAWANE MBAO"


Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemtupia lawama nzito Makamo wa Kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad  kwa kuanza kwenda kinyume na makubaliano yaliounda Serikali ya Umoaja  wa Kitaifa mwaka 2009.

Akihutubia mamia ya wanachama na mashabiki wa CCM waliohuidhuria mkutano wa hadhara uloiofanyika Jumba la Vigae  huko Jang’ombe mjini Ungujajana(3.3.13), Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Zanzibar, Vuai Ali Vuai amesema Maalim Seif ameanza kufanya vikao vya siri vinavyotishia kuvuruga amani na umoja wa kitaifa Visiwani humu.

Vuia ambaye ni kati ya wajumbe waasisi walioshiriki katika mchakato wa mazungumzo ya upatanishi wa kisiasa Zanazibar, amesema kama angeliijua mapema dhamira ya Maalim Seif katika mazungumzo ya kundwa kwa Serikali iliyopo, angekuwa radhi kujitoa na kutokuwa miongoni mwa wajumbe wa kamati ya muafaka.
Amesema kwamba hivi karibuni kiongozi huyo ambaye ni Katibu Mkuu wa CUF, ameitisha kikao maalum cha vijana wa chama chake na kusema, ikiwa chama chake kitawaamrisha vijana, nchi haitatawalika na ikibidi litote tugawane mbao.

MCHAKATO WA KUCHAGUA PAPA KUANZA LEO VATICAN CITY


MAKARDINALI wa Kanisa Katoliki kutoka sehemu mbalimbali duniani, leo wanaanza maandalizi ya kumchagua mrithi wa Papa Benedict XVI, aliyeachia ngazi wiki kiliyopita.

Kwa mujibu wa tovuti ya Vatican City, ilieleza kuwa mkutano mkuu wa Makardinali utaanza leo saa 3.00 asubuhi kwa saa za Vatican (Saa 6.00 mchana kwa saa za Tanzania) kwenye Ukumbi wa New Synod Hall.

Mkutano huo ndio utafungua mchakato wa uchaguzi wa Papa mpya na unatarajiwa kuandaa ratiba ya uteuzi wa papa mpya.

Makardinali hao ndio watapanga siku ya kufanyika mkusanyiko wao unaoitwa `Papal Conclave' kwa ajili kufanya uchaguzi huo.
Papa anavyochaguliwa.

Bondia Japhet Kaseba alipomsambaratisha Maneno katika mpambano wa kuwania Ubingwa wa Taifa.


Bondia Maneno Osward kushoto akipambana na Japhert Kaseba wakati wa mpambano wao wa ubingwa wa taifa uliofanyika Jumamosi katika ukumbi wa DDC Magomeni Kondoa. Kaseba alishinda kwa point mpambano huo.(picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com).
Bondia Japhet Kaseba (kushoto) akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Maneno Osward wakati wa mpambano wao wa kugombea ubingwa wa taifa Kaseba alishinda kwa point.
Bondia Japhet Kaseba (kushoto) akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Maneno Osward wakati wa mpambano wao wa kugombea ubingwa wa taifa Kaseba alishinda kwa point.
Bondia Japhet Kaseba akinyooshwa mkono juu na refarii Antoni Ruta baada ya kuibuka mshindi kwa kumgalagaza Maneno Osward.
Bondia Alphonce Mchumiatumbo (kushot)o akioneshgana uwezo wa kutupiana masumbwi na Joseph Marwa mpambano wa uzito wa juu uliofanika Jumamosi. Mchumiatumbo alishinda kwa K.O raundi ya sita.
Bondia Putile Gama (kushoto) akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Tom Kato kutoka Japani anaeishi mjini Bagamoyo. Kato alishinda kwa K.O raundi ya pili.
Bondia Tom Kato (kulia) raia wa Japan anayeishi mjini Bagamoyo akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Putile Gama Kato alishinda kwa K.O raundi ya pili.(picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com)

WOMEN CELEBRATIONS 2013 YAFANA


 

Mama Tunu Pinda alikuwa mgeni wetu rasmi na hakuja peke yake aliongoza na wake wa viongozi wanaounda kundi la Millenium Women Group.
                                                     Mke wa waziri mkuu msaafu Mama Lowasa nae alikuwa mmoja wa wake wa viongozi waliokuwa nasi katika siku yetu #womencelebrations. walikuwa wengi kutoka Millenium Women Group wakiongozwa na mwenyekiti Mama Lukuvi. ntawaonesha wooote si mwajua raha ya 8020fashions blog ni picha...tufanye subrazinakujaaa  ::shukran kwenu Mama Zangu ,Great!!


 My Hawa alikuwa kwa Red opss GREEN carpet kukaribisha na kuongea na wageni akijua wameshona wapi na kupanda dondoo za siku yetu ta wanawake duniani. hapo alikuwa na Sabah Muchacho

Mkutano wa Hadhara na Kongamano la Baraza la Vijana wa Chadema (BAVICHA)


 
kamanda Jackson Makala akihutubia mkutano wa hadhara wa bavicha Mbulu
Kamanda Jackson Makala akizungumza wakati wa kuchangia hoja za Elimu,Rasilimali na Utawala Bora wakati wa kongamano la Vijana wa Chadema Mbulu

Sunday, March 03, 2013

CHADEMA WAENDELEZA WIMBI LA TIMUA TIMUA. HALI NI MBAYA SANA KUPITA MAELEZO


Chama cha Demokrasia na Maendeleo Mkoa wa Morogoro kimemfukuza uanachama ndugu Dazza na kuwarudishia uanachama wao wale wote waliokuwa wamefukuzwa uanachama na Kamati Tendaji ya wilaya. Maamuzi ya kuwarudishia uanachama wao wale waliofukuzwa na Kamati Tendaji ya Wilaya ya Morogoro Mjini ulitolewa na Baraza la Uongozi la Mkoa chini ya Mwenyekiti wake Mheshimiwa Susan Kiwanga Baada ya Baraza hilo kujiridhisha kuwa Kamati Tendaji ya Wilaya ilikiuka Katiba, Kanuni na taratibu za Chama ikiwa ni pamoja na kuwafukuza uanachama wanachama wapatao 15 pasipo kuwapa nafasi ya kusikilizwa na kujitetea.

Mmoja kati ya wahanga wa maamuzi hayo ya Kamati Tendaji ya wilaya ni Mbunge Kivuri wa CHADEMA jimbo la Morogoro mjini mheshimiwa Amani Mwaipaja ambaye pia ni mwanasheria na mmiliki wa Blog ya MWAIPAJA BLOG. wito wangu kwa CHADEMA Morogoro ni kwamba wakati wa kuendekeza siasa za chuki na majungu umepitwa na wakati. Watanxzania wa leo ni waelewa kuliko wanavyofikiri CCM. Fanyeni kazi.

KENYA WAENDELEZA UBABE WAO KILIMANJARO MARATHON 2013


Na Mroki Mroki-Father Kidevu Blog-Moshi
 
Wanariadha kutoka Nchini Kenya wameendeleza Umwambawao katika mbio za Nyika za Kilimanjaro ‘Kilimanjaro Marathon 2013’ zilizofanyika leo mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

Wakenya walidhihirisha umwamba katika Mbio za Kilometa 42 baada ya Mkimbiaji wao Kipsang Kipkemoi kunyakua nafasi ya kwanza katika mbio hizo za mwaka huu upande wa wanaume na Wanawake ilinyakuliwa na Mwana dada Edna Joseph alebeba Medali ya Dhahabu.

Nafasi ya pili hadi ya tano kwa wanaume ni Julius Kilimo, Dominick Kiagor, Onesmo Maithiya Loshile Moikari ambapo upande wa wanawake ni Eunice Muchiri, Frida Too, Rosaline David na Jane Kenyara.
 
Jumla ya wakimbiaji 65000 walishiriki mbio za Kilimanjaro Marathon 2013.

TBL YATOA MSAADA WA MAGODORO 210, VYANDARUA 200 HOSPITALI MKOANI KILIMANJARO


Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), SteveKilindo (katikati), akimkabidhi Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dk. Ibrahim Msengi msaada wa magodoro kwa ajili ya Hosptali ya Huruma ya wilayani Rombo pamoja na Kituo cha Afya cha Uru Kiaseni katika hafla iliyofanyika Mjini Moshi. Kulia kwake ni Mganga Mkuu wa mkoa huo, Dk. Mtumwa Mwako. Jumla ya magodoro 210 na vyandarua 200 vimetolewa na TBL kwa ajili ya kituo hicho na hospitali hiyo.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dk. Ibrahim Msengi akikabidhi msaada wa magodoro kwa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dk. Mtumwa Mwako baada ya kukabidhiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), mjini Moshi . Katikati ni Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa TBL, Steve Kilindo. Jumla ya magodoro 210 na vyandarua 200 vimlitolewa na TBL kwa ajili ya kituo Afya cha Uru Kiaseni na Hosptali ya Uhuruma .
Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL, Steve Kilindo,(katikati)wakifurahia jambo na kaimu mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Dk Ibrahm Msengi (Kulia )pamoja na mganga mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Dk Mtumwa Mwako mara baada yaTBL kukabidhi msaada wa magodoro 210 na vyandarua 200 kwa kituo cha Afya cha Uru Kiaseni na hosptali ya Uhuruma .
Magodoro yaliyokabidhiwa na TBL kwa Hospitali mkoani Kilimanjaro

Kenya yatakiwa uchaguzi wa amani kudhidirisha ukomavu wa demokrasia

Wagombea wa uraisi nchini Kenya
Wakati harakati za kampeni za uchaguzi wa uraisi zinafikia ukingoni nchini Kenya, Marekani imewataka raia wa Kenya kufanya uchaguzi wa amani ili kumpata kiongozi mpya kwa amani.
Akizungumza kwa niaba ya serikali naibu msemaji wa serikali ya Marekani Patrick Ventrell ameongeza kuwa Kenya inapita katika kipindi cha muhimu na kihistoria na hivyo kuwasihi wagombea kuhakikisha wanaepuka kuwa sababisho la umwagaji damu kama uliowahi kutokea katika uchaguzi wa mwaka 2007.
Hata hivyo hali ya mvutano imeongezeka ambapo serikali ya Marekani imewataka wakenya kutumia fursa hiyo kudumisha ukomavu wa demokrasia na kutekeleza matakwa ya katiba mpya.
Msemaji huyo amesema kuwa ni matarajio ya wengi kuwa wakenya hawatajali jinsi,kabila,dini,eneo analotoka mgombea ili kuchagua bali bali watamchagua kiongozi bora kulingana na sifa stahiki.
Takribani raia elfu moja walipoteza maisha huku laki sita wakiyakimbia makazi yao katika machafuko yaliyotokea katika kipindi cha uchaguzi wa mwaka 2007.

DHARURA ZA KUOKOA ELIMU YA TANZANIA

images
MHESHIMIWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,
DK. JAKAYA MRISHO KIKWETE,
Kwa heshima kubwa, Chama cha NCCR-Mageuzi kinapenda kuwasilisha rasmi mapendekezo yake kwako yenye lengo la kuinusuru elimu ya Watanzania, kama ifuatavyo:
Utangulizi
Mheshimiwa Rais,
Sisi Chama cha NCCR-Mageuzi tumeguswa sana na hali isiyoridhisha ya ubora wa elimu katika Taifa letu la Tanzania. Hivyo tunaona ipo haja ya kuchukuliwa kwa hatua za dharura kuinusuru elimu, ili taifa lisiharibikiwe zaidi, badala yake kuwe na elimu yenye ubora wa hali ya juu na utimilifu wa malengo tuliyonayo kama taifa.
Mheshimiwa Rais,
Katika muktadha wa mapendekezo tunayoyaleta kwako, tunazingatia masuala ya kitaifa yafuatayo:-
(i) Tangu Taifa letu lipate uhuru wake mwaka 1961 (kwa Tanganyika) na mwaka 1964 (Mapinduzi ya Zanzibar) tulitambua umuhimu wa kufuta ujinga, kwa kuelimisha wananchi ili tujiletee maendeleo. Ingawa hadi sasa kazi kubwa imefanyika katika kukuza elimu hapa nchini, bado hatujafika katika hali ya kuwa na taifa ambalo karibu kila raia mwenye umri stahiki anajua kusoma na kuandika.
(ii) Katika Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2025, tunataja pamoja na mambo mengine kwamba, ifikapo mwaka 2025 tuwe tumejenga taifa la watu walioelimika kwa upeo wa juu katika nyanja mbalimbali.
(iii) Tanzania ni miongoni mwa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, ambao una malengo nane ya milenia; lengo la pili likiwa ni upatikanaji wa elimu bora kwa wote (achieving universal primary education)); na
(iv) Ifikapo mwaka 2015 (takribani miaka miwili toka sasa) tutalazimika kama taifa kupima utekelezaji wa malengo hayo ya milenia ili kuendana na viwango vya kimataifa.
Mheshimiwa Rais,
Wakati tukikabiliwa na malengo hayo ya Kitaifa, kwa muda mrefu kumekuwepo na viashiria vingi vinavyoonesha kwamba ubora wa elimu itolewayo hapa nchini katika ngazi zote hauridhishi. Viashiria hivyo ni pamoja na:-

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI TAREHE 03.03.2013 HAYA HAPA

l 001 c4e42

VAZI LA NUSU UCHI LAMTIA AIBU AUNT LULU

MSANII wa filamu asiyekaukiwa na skendo, Lulu Semagongo 'Anti Lulu' hivi karibuni alijikuta akiaibika kwenye onyesho la Bendi ya Extra Bongo baada ya kuvamia jukwaa na kuanza kucheza huku akizianika sehemu zake nyeti. 

Anti Lulu alikuwa ameongozana na mtangazaji Maimartha Jesse kwenye shoo hiyo iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Meeda, Sinza jijini Dar ambapo kila alipokuwa akicheza alikuwa akimwaga lazi kufuatia kigauni chake kifupi alichokuwa amevaa hivyo kuwafanya wanaume wakware wamkosekose kumfanyia kitu mbaya.
Katika tukio lingine, Maimartha naye alijikuta akipata aibu baada ya kunusurika kung’oa meno kufuatia viatu virefu alivyokuwa amevaa kumpiga mwereka ambapo kama siyo Lulu kumshika, tungekuwa tunazungumzia mambo mengine.
Licha kunusurika huko, Mai alionekana kutembea kwa shida sana kana kwamba alilazimishwa kuvaa viatu hivyo ambapo kuna wakati wanaume walimzomea hali iliyomfanya akose amani.

TFF YAIKOMALIA SERIKALI

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesema ipo haja kwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara kufikiria upya uamuzi wake wa kutengua usajili wa Katiba ya TFF ya mwaka 2012 na kutaka itumike ya mwaka 2006, kwani hautekelezeki.

Akizungumza na waandishi wa habari leo mchana, mara baada ya kikao cha Kamati ya Utendaji, Rais wa TFF, Leodegar Tenga amesema ni muhimu jambo hilo likaangaliwa upya kwa sababu athari zake ni mbaya, na pengine Dk. Mukangara hakushauriwa vizuri kabla ya kufanya uamuzi huo.

“Kamati ya Utendaji ya TFF haitaki kubishana na Mheshimiwa Waziri hata kidogo, ila tunaamini wakati anatamka haya hakufahamu madhara yake, athari zake na ugumu wa utekelezaji wake. Kwa waliomshauri hili, wamemshauri vibaya,” amesema Rais Tenga.

Amesema rai ya TFF kwa Waziri ni kuwaita ili wamweleze ni kitu gani wafanye kunusuru mpira wa miguu wa Tanzania, kwani wanaamini jambo hili litakwisha baada ya kumwelimisha hasa kutokana na ukweli kuwa kabla ya kufanya uamuzi huo hakuwasikiliza.

Katika mkutano huo, Rais Tenga alianza kwa kusema kuwa TFF inaiheshimu sana Serikali, hivyo inaheshimu maagizo yaliyotolewa na Waziri, lakini akaongeza kuwa TFF ina wajibu wa kutoa ufafanuzi juu ya maagizo hayo.

Amesema lengo la kuelezea historia ya TFF ilikotoka ni kubaini migongano ya maagizo hayo na taratibu za TFF ambazo kwa bahati mbaya zinasigana na maagizo hayo.

Rais Tenga amesema TFF ni chombo cha wanachama, ambapo wanachama wake ni vyama vya mikoa, vyama shiriki na klabu za Ligi Kuu, na ina taratibu za kufanya uamuzi kwa mujibu wa Katiba yake na za wanachama wake ambazo zimeidhinishwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Amesema si TFF pekee, bali vyama vya nchi zote ambavyo vimeunganishwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), zinaheshimu na kufuata maagizo na miongozi ya shirikisho hilo la kimataifa la mpira wa miguu.

Rais Tenga amesema TFF haitakiwi kuingiliwa katika uongozi na uendeshaji wake, kwani jambo hilo likitokea rungu la FIFA litaiangukia TFF, na madhara yake ni makubwa. Miongozo ya FIFA inasisitiza uhuru wa wanachama wake katika uendeshaji shughuli za mpira wa miguu, na iko kwenye Katiba ya TFF.

“Sheria za nchi ndizo zilizozaa Katiba ya TFF. TFF ni chama kamili kinatakiwa kufanya uamuzi wake ili mradi uzingatie madhumuni ya kuanzishwa kwake. Leo TFF ikiacha mpira wa miguu na kuanza kujishughulisha na gofu, hapo Msajili ana haki ya kuingilia,” amesema Rais Tenga.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...