Tuesday, February 12, 2013

STEPHENI KESHI ABADILI UAMUZI - KUENDELEA KUWA KOCHA WA NIGERIA

Shirikisho la soka la Nigeria limesema leo Jumanne kwamba Kocha wa timu ya taifa Stephen Keshi amebadili uamuzi wake wa kujiuzulu na mazungumzo baina yao na kocha huyo yanaendelea baada ya kocha huyo kuiwezesha Nigeria kushinda ubingwa wa Afrika.

Keshi na Super Eagles, ambayo waliifunga Burkina Faso 1-0 Sunday  na kushinda AFCON 2013, wanatarajiwa kuwasili Nigeria leo huku wakiwa wameandalia sherehe na raisi wa nchi huko mjini Abuja.
    Kujiuzulu kwa Keshi, amabye alitangaza uamuzi wake jana kupitia radio moja huko South Africa, kumeleta aibu kwa utawala wa soka wa nchi hiyo, ambayo imekuwa kiandamwa na skendo za rushwa na utawala mbovu kwa miaka kadhaa sasa.

Shirikisho hilo lilitoa taarifa leo asubuhi kuhusu kujiuzulu kwa Keshi, na kusema kwamba kocha huyo amebadilisha uamuzi wake.

Keshi alisema jana kwamba ameamua kujiuzulu kwake kumekuja kutokana na maofisa wa NFA kumtishia kumfukuza kazi kabla ya mechi ya robo fainali dhidi ya Ivory Coast.

WAJUMBE wapya KAMATI KUU CCM

4 
6ec30
1. WASIRA
2.PINDI Chana
3.Tibaijuka
4. Jerry Slaa
5. Kimbisa
6. Nchimbi
7. Lukuvi


Zanzibar:
1. Nahodha
2. Hussein Mwinyi
3. Prof Makame Mbalawa
4. Dr Salim A.Salim
5. Maua daftari
6. lL. Abuu
7. Samia Suluhu

Spika Anne Makinda apokea sms 600 zenye wito wa kumtaka kujiuzulu na matusi

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Anne Makinda.
Inaripotiwa kuwa Spika wa Bunge, Anne Makinda, amepokea jumbe za maneno 400 na za miito ya simu 200 zenye matusi ya nguoni kutoka kwa watu wakimtaka ajiuzulu. Mtoa habari wa HabariLeo ambaye yupo karibu na Spika Makinda amesemea jumbe hizo zimerekodiwa.Kwamba, Spika alianza kupokea jumbe hizo kuanzia juzi, baada ya viongozi wa CHADEMA kutangaza namba za simu za Spika kwenye mkutano wa hadhara na kuendelea jana ili kutumia ‘nguvu ya umma’, kumlazimisha ajiuzulu.  Sababu ya kutumwa jumbe hizo inaripotiwa kuwa ni baada ya hatua ya Spika Makinda kutangaza mabadiliko ya Kamati za Bunge, yaliyoivunja Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) na shughuli zake kuwekwa chini ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) ambapo katika mabadiliko hayo, aliyekuwa Mwenyekiti wa POAC, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe hakuridhishwa nayo na hivyo kumshitaki Spika Makinda kwa Wananchi ili wamng’oe.
Unaweza kutizama/sikiliza wito huo kupitia audio na video ya chapisho/post ya awali (bofya hapa).
Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashilillah, alipozungumza na gazeti hili juzi, alisema uamuzi huo haukufanywa na Spika Makinda peke yake, bali ni baada ya kushauriana na Kamati ya Kanuni za Bunge, ambayo iliridhika na sababu za kuchukuliwa uamuzi huo.
Wajumbe wa Kamati iliyoridhia makubaliano hayo mbali na Spika na Naibu Spika, ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA). Wengine ni Mbunge wa Mbulu, Mustapha Akunaay (CHADEMA), Mbunge wa Kibondo, Felix Mkosamali (NCCR-Mageuzi), Mbunge wa Mkanyageni, Mohamed Habib Mnyaa (CUF) na Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed (CUF). Pia Mbunge wa Viti Maalumu, Anna Abdallah (CCM), Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (CCM), Mbunge wa Tunduru Kaskazini, Ramo Makani (CCM), Mbunge wa Viti Maalumu, Pindi Chana (CCM) na Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono (CCM).
Dk Kashilillah alisema mabadiliko hayo hayakuigusa kamati ya POAC peke yake, bali kamati zingine kama ya Sheria Ndogo na ya Ulinzi, Usalama na Mambo ya Nje, ambayo imegawanywa mara mbili.
Akielezea sababu za kuvunja POAC, Dk Kashilillah alisema lengo lilikuwa ni kuunganisha wizara, taasisi zake na mashirika yaliyo chini ya wizara husika, ili yawe na msemaji mmoja. 
Alisema awali Waziri alikuwa anawajibika PAC, wakati mashirika ya umma yaliyo chini ya wizara yakiwajibika chini ya POAC.
Kwa mujibu wa Dk Kashilillah, kulikuwa na mkanganyiko mkubwa na akaeleza kuwa hatua ya kuunganisha wizara na mashirika yake ya umma, kutafanya sasa Waziri, Katibu Mkuu, Mwenyekiti wa Bodi na watendaji wakuu wa mashirika, kuwajibika kwa kamati moja ya PAC.
Dk Kashilillah alisema sababu nyingine ni kuangalia utendaji katika baadhi ya nchi, ambazo alisisitiza kuwa hazina kamati za mashirika ya umma.
Mwandishi aliwasiliana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), ambayo iliweka wazi kuwa hakuna sheria yoyote inayozuia mtu kutoa namba ya simu ya mwingine kwa mtu au watu wengine, bila ridhaa ya mwenye namba ya simu.
Ofisa wa TCRA, ambaye hakutaka jina lake litajwe kwa sababu si msemaji wa taasisi hiyo, alisema sheria ya kuzuia utoaji namba na taarifa za mtu mwingine, inakataza kampuni za simu kufanya hivyo, lakini haizungumzi kwa mtu binafsi. Ofisa huyo alinukuu sheria hiyo:
 
Taarifa ni siri ya mtu husika, isipokuwa kama mtu huyo ameitoa kwa ridhaa yake.
 
Alisema pamoja na kuwapo na kipengele hicho, mtu yeyote ambaye ana namba ya simu ya mtu mwingine, hazuiwi kutoa namba hiyo kwa watu wengine.Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya   wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, wamesema ingawa namba za simu za viongozi hao zinaweza zikapatikana kwa kila mtu, kuzigawa katika mkutano huo ambao ulikuwa na mtazamo hasi kwa Spika na Naibu wake,  kulikuwa na nia mbaya.
 
Kama ungekuwa mkutano au semina yenye nia njema na Spika, ungesema wamegawa simu kwa nia njema. Lakini mkutano huo ulivyokuwa na kauli mbovu kwa Spika na taasisi ya Bunge, kitendo cha kuwapa watu namba kinamaanisha walitaka hao watu wamtukane pia.
katika mkutano kama huo, kunakuwa na watu wa kila aina wakiwamo wasio na busara. Hivyo viongozi hao wa CHADEMA waliofanya hivyo, wameshindwa kutumia busara.
Mjumbe wa NEC, Juma Killimbah, ambaye aliwahi kuwa Mbunge na kuhadharisha wananchi wasije kujikuta katika mkono wa sheria kwa kutumia namba hizo vibaya kwa kutoa matusi, alisema simu ya kiongozi huyo kujulikana si ajabu na ni jambo la kawaida.
 
Tatizo ni maudhui. Kama kitendo hicho kina lengo zuri hakuna tatizo.
 
Sehemu ya taarifa hii imenukuliwa kutoka kwenye gazeti la HabariLeo. via Wavuti.

Waziri Magufuli azindua Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Ujenzi


 Waziri wa Ujenzi, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli (katikati) akizindua kitabu cha Mwongozo wa Usanifu wa Barabara. Kulia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Saidi Amani na kushoto ni Eng. Joseph Nyamuhanga, Mkurugenzi wa Barabara katika Wizara ya Ujenzi.
Msajili wa Bodi ya Wabunifu na Wakadiriaji Majenzi, Arch. Jehad akipokea kitabu cha Mwongozo wa Usanifu wa Barabara kutoka kwa Waziri wa Ujenzi, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli (katikati) mara baada ya kuzinduliwa rasmi. Kulia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Saidi Amani.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert E. Mrango akipokea kitabu cha Mwongozo wa Usanifu wa Barabara kutoka kwa Waziri wa Ujenzi, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, mara baada ya kuzinduliwa rasmi.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro,  Eliya Ntandu akipokea kitabu cha Mwongozo wa Usanifu wa Barabara kutoka kwa Waziri wa Ujenzi, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli (katikati) mara baada ya kuzinduliwa rasmi. Kulia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Saidi Amani.
Waziri wa Ujenzi, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli (wanne kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Ujenzi na baadhi ya viongozi wa mkoa wa Morogoro.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli (Mb), leo amezindua Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Ujenzi ambalo linakutana kwa siku mbili mjini Morogoro. Wakati akiongea katika uzinduzi wa Baraza hilo linalojumuisha wajumbe kutoka katika taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi,  Mheshimiwa Magufuli amewapongeza watendaji wakuu wa wizara na taasisi zake kwa namna wanavyosimamia utekelezaji wa majukumu yao kwa ufanisi. “Mafanikio yanayoonekana kupatikana kwa upande wa wizara yetu ni matokeo ya usimamizi wenu mzuri” alielezea Waziri Magufuli na kuwataka kutorudi nyuma kwani hiyo ni dhamana waliyopewa na Taifa.
Akizungumzia changamoto zilizopo, Waziri Magufuli alisisitiza kukerwa kwa kuendelea kujitokeza vitendo vya rushwa katika vituo vya mizani na kwenye vivuko.  Mhe. Magufuli amezipongeza hatua zilizokwisha kuchukuliwa na Mtendaji Mkuu wa Tanroads kwa kutangaza ajira za wafanyakazi wa vituo vya mizani na amemtaka kukamilisha mapema ajira za Wahandisi watakaosimamia vituo hivyo. “Hatua hizi tuzimechukua baada ya kubaini kuwa karibu asilimia themanini ya watendaji waliopo katika vituo vya mizani ni wala rushwa” alibainisha Mheshimiwa Waziri Magufuli.
Kwa upande mwingine Wakala wa Ufundi na Umeme  (TEMESA) nao umepewa siku sitini ili kuanza zoezi la ukatishaji tiketi za elektoniki hasa katika kivuko cha Kuvukoni jijini Dar es Salaam. Waziri Magufuli alibainisha baadhi ya mbinu zinazotumiwa na watendaji wasio waaminifu katika vivuko hivyo, kuwa ni pamoja na kujichapishia tiketi kwa siri na wakati mwingine kutochana tiketi wanazozipokea kutoka kwa abiria kwa lengo la kuziuza tena.
Waziri Magufuli hata hivyo amepongeza zoezi la kukamata magari ya Serikali yanayotumia namba za binafsi kinyume na sheria. “Tayari hadi sasa jumla ya magari 1,830 tayari yamekamatwa na kusajiliwa kwa namba za Serikali” alifafanua Mheshimiwa Magufuli..
Wakati huo huo Waziri wa Magufuli pia amekizundua Kitabu cha Mwongozo wa Usanifu wa Barabara. Kitabu hicho kitatumiwa katika utekelezaji wa shughuli za ujenzi na matengenezo ya barabara hapa nchini.
Wakati akizindua kitabu hicho Mheshimiwa Waziri amewapongeza Mameneja wa Tanroads wa mikoa ya Dodoma na Morogoro kwa ubunifu ambao wameuonyesha kwa kutumia fedha wanazotengewa katika bajeti zao. Alielezea kufurahishwa na kazi za upanuzi wa barabara unaoendelea kuanzia eneo la Ihumwa hadi Dodoma Mjini ambao ni matokeo ya jitihada za watendaji wenyewe mkoani. Hapa Morogoro pia kazi hizi za upanizi wa barabara zimeelezwa kuanza kutekelezwa wakati ambapo mkoani Tabora tayari kuna zaidi ya kilometa sita za lami zimejengwa kwa kutumia fedha zilizotengwa katika bajeti ya mkoa. “Ninawaelekeza Mameneja wa Tanroads katika mikoa mingine nanyi muwe na ubunifu na sio kukaa bila ya kuchukua hatua zozote hata pale ambapo tayari kuna bajeti iliyopitishwa” alimalizia Mheshimiwa Magufuli.

Monday, February 11, 2013

Papa Benedict kujiuzulu

Huko Ujerumani, msemaji wa serikali amesema kuwa anaheshimu kazi kubwa iliyofanywa na Papa huyu aliyezaliwa katika Jimbo la Bavaria la nchini humo.
Papa Benedict
Baba Mtakatifu ameelezea kwamba matatizo ya kiafya yamemfanya kutangaza kujiuzulu
Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron, amemsifu Papa kwa jitihada zake za kuimarisha mahusiano baina ya Vatican na Uingereza.

Askofu mkuu wa Canterbury amesema amazipokea taarifa za kujiuzulu kwa Papa kwa huzuni mkubwa ingawa anaelewa undani wa hatua yake.
Kiongozi wa Ujeremani, Bi. Angela Merkel amesifu mchango wa Papa wa kupendekeza mjadala baina ya makanisa, waislamu na wayahudi.

Alikumbusha hotuba ya Papa alipozuru bunge la Ujerumani mnamo mwaka 2011.
Uwamuzi na hatua ya Papa Benedict XVI wa kujiuzulu mwishoni mwa mwezi huu baada ya takriban miaka minane akiongoza Kanisa Katoliki kwa hoja kuwa umri wake wa miaka 85 ni mkubwa kiasi kwamba hawezi kuendelea kuhudumu zaidi ya umri huo.

Makao makuu ya Kanisa Katoliki huko Vatican yanasema yanatarajia Papa mpya atachaguliwa kabla ya mwisho wa mwezi wa tatu, na sherehe za Pasaka.

Tabia ya kujiuzulu kwa Papa si ngeni, ingawa ni tukio jipya katika karne za hivi karibuni.
Mwandishi wa BBC mjini Roma Alan Johnston anasema habari hizi zimetokea kama radi, na kwamba hakukua natetesi yoyote juu ya uwezekano kama huu.

Msemaji wa Vatikani Father Federico Lombardi, amesema kuwa hata wasaidizi wa Papa wa karibu mno hawakuwa na fununu juu ya tukio hili.

Kakake Papa huyu mzaliwa wa Ujerumani alipewa ushauri na Daktari wake asifanye ziara nyingine yoyote ya Marekani na kwamba kwa miezi kadhaa Mtakatifu Papa amekuwa akitafakari kujiuzulu.
Akizungumza kutoka nyumbani kwake huko Regensburg, Ujerumani, Georg Ratzinger amesema kuwa Kaka yake alikuwa ameanza kupata shida ya kutembea na kwamba kujiuzulu kwake ni hatua ya kimaumbile.
Wakati wa kutawazwa kama Papa, Kadinali Joseph Ratzinger alikuwa mmojawapo wa mapapa wapya kuchaliwa akiwa mwenye umri mkubwa wa miaka 78.

Alitangazwa Papa mnamo mwezi Aprili 2005 kufuatia kifo cha marehemu John Paul wa pili.
Uongozi wake ulitokea wakati wa wimbi kali la ubakaji kulikumba kanisa katoliki katika kipindi cha miongo mingi, ubakaji uliofanywa na watawa dhidi ya watoto wavulana.

Katika taarifa yake, Mtakatifu Papa amesema: "baada ya kujichunguza binafsi na nafsi yangu mbele ya Mola wangu, nimefikia uwamuzi kua uwezo wangu na afya, ukiambatana na umri mkubwa, ni mambo yatakayokwaza jitihada zangu za kuendelea kuliongoza Kanisa Katoliki.

Kuna kipengele katika sheria ya Kanisa kinachosema kuwa kujiuzulu kwa Papa kunakubalika iwapo kitendo hicho kimefanywa kwa hiari na kwa utaratibu unaostahiki

Sokoni kwetu hapaaaa!!!

   
Hili ni soko la lililopo eneo la Ilomba jijini Mbeya, na izo ndizo ofisi za soko hilo ambapo camera yetu ilikuta mbwa zikiwa nje ya ofisi hiyo na haijulikani zipo hapo kwa lengo gani. ( Picha na Keny Pino)

Ubunifu

Maisha ni magumu kweli hadi tunalazimika kuwa wabunifu, huyu ni mbunifu wa hereni, katumia makopo ya maji

Picha na Keny Pino

Profesa Jay awavulia Kofia wakali wa MIC walipozichana kwa ufasaha nyimbo zake

Mshiriki wa kinyang’anyiro hicho, Bahati Charles Kuyela, kutoka Kigamboni akionesha ‘maukali’ yake.
Profesa Jay (kulia) na Nick Mbishi wakifurahia baada ya kunogeshwa na wakali hao.
…Wakali hao wakionesha jinsi ya kuchana mistari jukwaani baada ya washiriki hao kumaliza mpambano.
DJ Juice akipangilia ‘beat’ katika kipute hicho.
Majaji wa kipute hicho kutoka kushoto ni Abdallah Mrisho ‘Abby Cool’, John Dilinga ‘DJ JD’ na Ally Mohammed ‘Baucha’ wakifuatilia kwa makini mpambano huo.
Kundi la TOT Taarab likifanya mambo baada ya kinyang’anyiro hicho.
Malkia wa mipasho, Khadija Kopa (kulia) akiserebuka na mashabiki wake ukumbini hapo.
WASHIRIKI wa kinyang’anyiro cha kumsaka ‘The Mic King’ kinachotimua vumbi kila Jumapili ndani ya Ukumbi wa Dar Live ambacho mshindi anatarajiwa kujinyakulia gari jipya la kisasa, jana usiku walimtoa jasho mkali wa rap hapa nchini, Joseph Haule ‘Profesa Jay’ kwa kuchana mistari ya nyimbo zake kiufasaha.
(PICHA: RICHARD BUKOS NA ISSA MNALLY/GPL)

WASANII WENGI WA KIBONGO WANATEGEMEA UCHAWI"...T.I.D



Mnyama TID amefunguka kuizungumzia ‘indirectly’ scandal inayomzunguka hitmaker wa Kesho, Diamond ya kupata mafanikio kwa kutumimia waganga wa kienyeji.



Kupitia Twitter Top in Dar ambaye jina lake halisi ni Khalid Mohamed alitweet kwa utani akisema, “ I really want to meet a witch doctor who can make me win big brother money ntatoa percentage we go thru a contract,Yupo?!

Tuliamua kumuuliza kama anamaanisha alichokiandika ambapo alijibu, “ am kidin mate I just heard some of them were making foolish artist look big ndo maana I make fool out it.”

Akijibu swali kama anaamini katika uchawi ama kama unaweza kumsaidia msanii asiye na kipaji afanikiwe, TID alisema, “I don’t mean nobody all I know is all this mathaf**z they don’t have talent all they have is witchcravity, huh.

AIRTEL YATOA SARE NA VIATU VYA SHULE KWA WANAFUNZI WOTE WA SHULE YA KIROMO


 Afisa uhusiano na matukio wa Airtel Tanzania Dangio Kaniki akimvalisha sare za shule na viatu mwananfunzi wa shule ya msingi Kiromo zilizotolewa na Kampuni ya simu ya Airtel mwishoni mwa wiki hii.Airtel metoa msaada wa sare za shule zikiwemo Kaptura 600 , skirt 600 , mashati 1193 na viatu 728 vyote vyenye dhamani ya shilingi milioni 50 kwa shule ya msingi Kiromo.
Meneja wa uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando (kushoto) akimkabidhi sare za shule Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kiromo Nasib Pangahela  mwishoni mwa wiki hii, akishuhudiwa na meneja wa huduma kwa jamii (katikati) bi Hawa Bayumi.
Meneja wa uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando (kushoto) akimkabidhi  mmoja wa wanafunzi wa shule ya msingi Kiromo sare za shule zilizotolewa na Kampuni ya simu ya Airtel mwishoni mwa wiki hii, akishuhudia makabidhiano hayo (wa pili kushoto) meneja wa huduma kwa jamii bi Hawa Bayumi akifuatiwa na Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kiromo Nasib Pangahela,  Airtel metoa msaada wa sare za shule zikiwemo Kaptura 600 , skirt 600 , mashati 1193 na viatu 728 vyote vyenye dhamani ya shilingi milioni 50 kwa shule ya msingi Kiromo.
 Afisa uhusiano na matukio wa Airtel Tanzania Dangio Kaniki  (Kulia) akimpongeza Mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Kiromo (kulia) baada ya makabidhiano yaliyofanyika mwishoni mwa wiki hii wakishuhudiwa na meneja wa huduma kwa jamii wa Airtel Hawa Bayumi (wa pili kulia) akifuatiwa na mmoja wa wazazi wa wanafunzi wa shule hiyo bi Zuwena Salumu, Airtel metoa msaada wa sare za shule zikiwemo Kaptura 600 , skirt 600 , mashati 1193 na viatu 728 vyote vyenye dhamani ya shilingi milioni 50 kwa shule ya msingi Kiromo.
 
Airtel Tanzania yatembelea shule ya Kiromo mwishoni mwa wiki hii na kukabidhi sare za shule pamoja na viatu vyenye dhamani ya shilling milioni 50. Katika msaada huo Airtel imetoa sare za shule zikiwemo Kaptura 600 , skirt 600 , mashati 1193 na viatu 728, hafla ya makabidhiano ilifanyika katika shule hiyo iliyopo Kiromo -Bagamoyo.
***  ***
 Alhamisi 10 February 2013,  Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel inayotoa gharama nafuu zaidi Tanzania, leo imegawa sare za shule pamoja viatu katika shule ya msingi Kiromo iliyopo Bagamoyo ikiwa ni sehumu ya shughuli zao za kusaidia jamii.

Shule ya kiromo ni moja kati ya shule zilizofaidika na mpango wa shule yetu na kuingia kwenye ukarabati wa majengo na madarasa na kubadili mazingira ya shule na kutoa vifaa vya kufundishia pamoja na computer. sasa Airtel imetoa Sare na viatu vya shule kwa wanafunzi wote shuleni hapo.

Katika kauli iliyotoleawa na kampuni ya Airtel Tanzania kupitia Meneja shughuli za kijamii bi. Hawa Bayumi alisema” Airtel imedhamiria kuendelea kuisadia shule mbalimbali kwa kutoa vifaa mbalimbali ikiwepo vya kufundishia ili kuhakikisha elimu bora inatolewa kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla. Na leo tunaendelea kuboresha shule yetu ya Kiromo kwa kutoa msaada wa uniform na viatu kwa wanafunzi.

M msaada wa sare zashule tunazoto ni pamoja na Kaptura 600 , skirt 600 , mashati 1193 na viatu 728 vyenye dhamani ya shilingi milioni 50 kwa shule ya msingi Kiromo.

Airtel Tunayo malengo ya dhati kabisa katika kusaidia kuinua kiwango cha elimu hapa nchini na kuhakikisha kiwango cha ufaulu kinaongezeka na upatikanaji wa vitabu kwa wanafunzi wa shule za sekondari. 

Leo tunathibitisha dhamira yetu ya kusaidia mashule kwa kutoa sare za shule na viatu Kiromo shule ya msingi”, alisema Bayumi Airtel itaendelea kusaidia mashule kwa kutoa vitabu na vifaa mbali mbali vya kufundishia ikiwa ni sehemu ya shughuli zetu za kusaidia jamii, nia yetu ni kuwafikia shule nyingi zaidi katika mikoa yote ya Tanzania aliongeza.

Kampuni ya simu ya Airtel imekuwa mstari wa mbele katika kuchangia sekta ya elimu hapa nchini. Tangu tulipoanza mradi wa “ shule yetu” mpango wa  kusaidia vitabu na vifaa vya shule , shule mbalimbali nchini zimeshafaidika na mradi huu mpaka sasa.

Kutoweka kwa mashahidi wa mashitaka kesi inayowakabili vigogo wa CHADEMA Singida kwasababisha kesi kuahirishwa


Mshitakiwa wa kwanza katika kesi ya kumtolea lugha ya matusi mbunge wa jimbo la Iramba Magharibi Mwita Waitara Mwakibe akitoka nje ya mahakama ya hakimu mkazi mjini Singida baada ya kesi yao kuahirishwa leo, Kesi hiyo imeahirishwa hadi Machi 11 mwaka huu,baada ya mashahidi wa upande wa mashitaka kuingia mitini.
Wakili wa washitakiwa vigogo wa CHADEMA Onesmo Kyauke (katikati) akiwaeleza jambo wateja wake muda mfupi baada kesi ya wateja wake kuahirishwa hadi Machi 11 mwaka huu.Vigogo hao wanaoshitakiwa kwa kumtolea lugha ya matusi mbunge wa jimbo la Iramba magharibi, Mwigullu Lameck Nchemba.  Dk.Kitila Mkumbo (kushoto) na afisa sera na utafiti, Mwita Waitara Mwakibe (kulia).(Picha na Nathaniel Limu).

Mashahidi watano wa upande wa mashitaka yanayowakabili vigogo wawili wa CHADEMA taifa, wameingia mitini na kusababisha kesi kuahirishwa kusikilizwa hadi Machi 11 mwaka huu.
Mashahidi hao walikuwa watoe ushahidi dhidi ya washitakiwa Afisa Sera na Utafiti wa CHEDEMA Makao Makuu Mwita Waitara Mwikwabe (37) na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam na Mshauri wa CHADEMA Dk.Kitila Mkumbo.
Vigogo hao wanatuhumiwa kutoa lugha ya matusi kwa mbunge wa jimbo la Iramba magharibi Mwigullu Lameck Nchemba.
Mwendesha mashitaka mwanasheria wa serikali Mary Mudulugu amedai mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya hakimu mkazi mjini Singida Rusth Massam, kuwa askari polisi ambaye ni mpelelezi wa kesi hiyo yupo Dar-es-salaam kitendo kilichopelekea mawasiliano baina yao,yakatike.
Amesema kutokana na mpelelezi huyo kuwa jijini Dar-es-salaam, mawasiliano na mashahidi hao watano ambao ni wa mwisho katika kesi hiyo,yamekuwa magumu na yamesababisha washindwe kufika mahakamani.
Kabla ya kuahirishwa kwa kesi hiyo,wakili wa washitakiwa Onesmo Kyauke, aliiomba mahakama hiyo kutaja tarehe ya mwisho kwa upande wa mashitaka kuleta mashahidi wao na endapo watashindwa kuwaleta, mahakama ifunge ushahidi kwa upande wa mashitaka.

Chris Brown anusurika kifo baada ya kupata ajali ya gari akiwakimbia Paparazzi

Muimbaji machachari wa Marekani Chris Brown amenusurika baada ya kugonga gari yake katika ukuta akidai alikuwa akifuatwa na mapaparazzi .
Polisi mjini Beverly Hills wamesema mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 23 ambaye katika ajali hiyo hakujeruhiwa, alishindwa kulimudu gari lake aina ya Porsche Turbo Nyeusi  alipokuwa ajaribu kuwatoroka.
Taarifa zinasema Brown alikuwa akiendesha gari hilo mwenyewe na aligonga ukuta.
Ajali hiyo imetokea siku moja kabla ya kutolewa kwa tuzo za Grammy huko LA’s Staples Center ambapo alikuwa mmoja wa wagombea.
Mapema wiki iliyopita rekodi za kimahakama zilidai kuwa  mwezi uliopita Chris Brown alimtishia kumpiga risasi muimbaji Frank Ocean  wakati wa mapambano ya kugombea sehemu ya kuegesha gari.

Taswira za maandamano ya Chadema jana




 Picha Juu Mamia ya wakazi wa Dar es salaam walijitokeza kuunga mkono maandamano yaliyoandaliwa na chadema kupinga Uonevu wanaofanyiwa wabunge wa Upinzani Bungeni.
 Viongozi wa chadema wakiwa katika mshikamano mkubwa, wakiandamana kupinga vitendo vya uonevu vinavyofanywa na Spika na Naibu wake dhidi ya wabunge wa Upinzani.
 Katibu mkuu wa Chadema Dr Wilbroad Slaa akiwa jukwaani katika mkutano wa kulaani vitendo vya uonevu kwa wapinzani. Mkutano uliofanyika katika kiwanja cha mwembeyanga Temeke leo.
 Mbunge wa singida Magharibi-Chadema na Mnadhimu mkuu wa kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu akiongea kwenye mkutano uliofanyika Viwanja vya Mwembeyanga
 Mbunge wa Jimbo la Ubungo-Chadema,John Mnyika akiongea katika mkutano.
 Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema,Godbless Lema naye akimwaga cheche jukwaani.
 Mbunge wa iringa Mjini-Chadema, Pter Msigwa akiunguruma
 
 Mbunge wa Kawe-Chadema,Halima  Mdee amesema tukianza 2014 itakula kwetu, tuanze sasa.
 Katibu mkuu wa AFP amesema chama chao kinaunga mkono chama makini kama Chadema
 Viongozi wa Chadema wakiwa Meza kuu kutoka kushoto katibu mkuu Dr Wilbroad Slaa, Mwenyekiti Mh Freeman Mbowe na naibu katibu mkuu Mh Zitto Kabwe.Picha Zote na CHADEMA

VODACOM WAENDELEA NA PROMOSHENI YA KUBORESHA MTANDAO WAO

1 
dc8de
Mtoa huduma wa kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Najma Rashid akiwahudumia wateja eneo la Buguruni Sokoni jijini Dar es Salaam jana wakati Vodacom Tanzania walipokuwa wakifanya promosheni ya kuwajuza wananchi pamoja na wateja wake kuwa imeboresha mtandao kwa ajili ya kuwafikia wananchi mahali popote Tanzania.

Mh.Lowassa ahudhuria mazishi ya mama yake Dr Kimei

msiba1 a23b2
Mawaziri wakuu wastaafu Mh Edward Lowassa na Mh Fredrick Sumaye wakijumuka na viongozi wengine katika msiba wa mama yake mkurugenzi mtendaji mkuu wa CRDB, Dr Kimei mwishoni mwa wiki huko Komakundi Marangu Mkoani Kilimanjaro.
msiba2 b42ff
Mh Lowassa akitia saini kitabu cha maomolezi ya kifo cha bibi Eliangichopasia, ambaye ni mama yake mkurugenzi mtendaji wa CRDB Dr Kimei.bibi huyo alifariki wakiwa na umri wa miaka 97.

msiba3 7034b
Mh Lowassa akiwapa pole Dr Kimei(katikati) na dada yake
msiba 
6634d

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...