Monday, February 11, 2013

Kutoweka kwa mashahidi wa mashitaka kesi inayowakabili vigogo wa CHADEMA Singida kwasababisha kesi kuahirishwa


Mshitakiwa wa kwanza katika kesi ya kumtolea lugha ya matusi mbunge wa jimbo la Iramba Magharibi Mwita Waitara Mwakibe akitoka nje ya mahakama ya hakimu mkazi mjini Singida baada ya kesi yao kuahirishwa leo, Kesi hiyo imeahirishwa hadi Machi 11 mwaka huu,baada ya mashahidi wa upande wa mashitaka kuingia mitini.
Wakili wa washitakiwa vigogo wa CHADEMA Onesmo Kyauke (katikati) akiwaeleza jambo wateja wake muda mfupi baada kesi ya wateja wake kuahirishwa hadi Machi 11 mwaka huu.Vigogo hao wanaoshitakiwa kwa kumtolea lugha ya matusi mbunge wa jimbo la Iramba magharibi, Mwigullu Lameck Nchemba.  Dk.Kitila Mkumbo (kushoto) na afisa sera na utafiti, Mwita Waitara Mwakibe (kulia).(Picha na Nathaniel Limu).

Mashahidi watano wa upande wa mashitaka yanayowakabili vigogo wawili wa CHADEMA taifa, wameingia mitini na kusababisha kesi kuahirishwa kusikilizwa hadi Machi 11 mwaka huu.
Mashahidi hao walikuwa watoe ushahidi dhidi ya washitakiwa Afisa Sera na Utafiti wa CHEDEMA Makao Makuu Mwita Waitara Mwikwabe (37) na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam na Mshauri wa CHADEMA Dk.Kitila Mkumbo.
Vigogo hao wanatuhumiwa kutoa lugha ya matusi kwa mbunge wa jimbo la Iramba magharibi Mwigullu Lameck Nchemba.
Mwendesha mashitaka mwanasheria wa serikali Mary Mudulugu amedai mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya hakimu mkazi mjini Singida Rusth Massam, kuwa askari polisi ambaye ni mpelelezi wa kesi hiyo yupo Dar-es-salaam kitendo kilichopelekea mawasiliano baina yao,yakatike.
Amesema kutokana na mpelelezi huyo kuwa jijini Dar-es-salaam, mawasiliano na mashahidi hao watano ambao ni wa mwisho katika kesi hiyo,yamekuwa magumu na yamesababisha washindwe kufika mahakamani.
Kabla ya kuahirishwa kwa kesi hiyo,wakili wa washitakiwa Onesmo Kyauke, aliiomba mahakama hiyo kutaja tarehe ya mwisho kwa upande wa mashitaka kuleta mashahidi wao na endapo watashindwa kuwaleta, mahakama ifunge ushahidi kwa upande wa mashitaka.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...