Monday, February 11, 2013

Waziri Mkuu ashiriki mjadala kuhusu juhudi za Serikali ya Tanzania inavyopambana na ugonjwa wa Malaria uliofanyika Afrika Kusini


Mh. Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiwa anahojiwa na Mtangazaji wa habari za michezo wa Televisheni ya Super Sport Bi. Carol Tshabalala  katika mjadala kuhusu Tanzania inavyo jitahidi kupamabana na ugonjwa wa Malaria mjadala huo ulifanyika kwenye kituo cha mikutano cha Sandton kilichopo jijini Johannesburg Afrika Kusini.(picha na Chris Mfinanga).
Mh Waziri Mkuu Mizengo Pinda akisaini mpira ikiwa ni ishara ya kupambana na Malaria kwakupitia michezo kutoka kulia Mama Tunu Pinda, kushoto kwake Meneja wa mpango wa kudhibiti malaria nchini Dr. Ally Mohamed, Naibu waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Mh. Dr Seif Rashid  anayefuatia ni Mwana muziki marafu nnchini Afrika kusini na Balozi wa kupambana na ugonjwa wa malaria Bibi Yvonne Chakachaka, kushoto kwa waziri mkuu ni Mh Dr. Hamisi Kigwangalla (Mb) kulia. Waziri Mkuu alikuwa amehudhuria mjadala wa kupambana na Malaria uliofanyika katika kituo cha mikutano cha Sandton kilichopo Johannesburg Afrika Kusini.(Picha na Chris Mfinanga).
Mh Mama Tunu Pinda akisaini juu ya mpira ikiwa ni ishara ya kutumia michezo kupambana na Malaria. Kulia ni Mh Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiangaliatukio hilo na katikati ni Balozi wa kupamabana na Malaria na mwanamuziki marufu nchini Afrika kusini Yvonne Chakachaka. Mama Pinda aliongozana na waziri mkuu katika mjadala wa kupamabana na Malaria uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Sandton Johannesburg Afrika Kusini.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...