Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohammed Shein
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohammed
Shein, amepata mpinzani iwapo ataamua tena kugombea nafasi hiyo katika
uchaguzi mkuu ujao mwakani, baada ya Katibu Mkuu wa Chama cha Tadea,
Juma Ali Khatib (50), kutangaza nia ya kuwania nafasi hiyo visiwani
humu.
Mgombea huyo ni watatu kujitokeza hadharani na
kutangaza nia ya kuwania nafasi hiyo, baada ya katibu mkuu wa CUF,
ambaye ni Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad,
kutangaza nia hiyo akifuatiwa na Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed
aliyetangaza pia nia hiyo.
Hamad Rashid alitangaza nia na kusema kuwa
atawania nafasi hiyo kupitia CUF, mgombea binafsi au kwa tiketi Chama
cha Alliance for Democratic Change (ADC).
Ikiwa Maalim Seif atawania tena nafasi hiyo,
itakuwa ni mara ya tano tangu mwaka 1995, ulipoanza mfumo wa vyama vingi
mwaka 1992. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz


































