Tuesday, March 19, 2013

Mwandishi mwingine anusurika kutekwa

Andrew Chale Mwandihi wa Gazeti la Tanzania Daima anayedai kufanyiwa jaribu la kutekwa
Dar es Salaam
MWANDISHI wa Habari wa Gazeti la Tanzania Daima Andrew Chale ameanza kuishi maisha ya wasiwasi baada ya watu wasiojulikana kufanya jaribio la kumteka.
Akizungumza naHabarimpya.comChale alisema kwamba siku ya Jumamosi usiku watu wasiojulikana walikuwa wakifuatilia nyedo zake.
Alisema watu walikuwa kwenye magari mawili yenye rangi na namba za Jeshi la Polisi walikuwa wakimfuta nyuma kila alipokuwa akipita kuelekea nyumbani kwake maeneo ya Sinza jijini Dar es Salaam.
"Siku ya Jumamosi usiku nikiwa njiai kutoka Kazini, niliona magari mawili ya Polisi yakinifuata kwa karibu na baada ya kuingia uchochoro flani wakuingia nyumbani magari hayo yakapaki"alisema Chale na kuongeza"
"Watu waliokuwa eneo hilo walisema kwamba baada ya magari hayo kupaki wakakaa hapo kwa saa mbili na baadaye walishuka askari watu huku wawili wakivaa nguo za kiraia huku mmoja akiwa na Gazeti la Tanzania Daima mkononi".
Alisema kwamba baada ya watu hao kushuka na kuuliza mtu waliemwita kwa jina la ANDRESON,, ndipo wakaambiwa kwamba hakuna mtu mwenye jina hilo katika mtaa huo lakini , walipoelezea mwonekano wake, wakajibiwa kuwa kijana anayefahamika eneo hilo hupita tu lakini mahali anapoishi hapajulikani.
"Tunayemfahamu ni kijana mmoja ila huwa anapita hapa akiwa na hilo Gazeti majira ya usiku, na wakati mwingine huwa anapita hapa akiwa na mambo yake mengine, baaada ya hapo magari hayo yaliondoka"aliwanukuu mashuhuda wa tukio hilo.
"Watu hao walirudi tena hadi nyuma ya nyumba yangu na nikawasikia wakijitambulisha kuwa wao ni Polisi jamiii na kwamba walikuwa wakimtafuta kijana mmoja ambaye wamesahau anapoishi"alifafanua Chale. SOURCE JAMII FORAM

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...