Tuesday, March 19, 2013

MUGABE ATINGA VATICAN KUHUDHURIA KUTAWAZWA KWA PAPA FRANSIS I

Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe amewasili nchini Italia jana kwa ajili ya kuhudhuria kutawazwa  kwa Papa Francis na maafisa wamejaribu kupuuzia ukiukaji wa kiutaalamu wa marufuku ya kusafiri  katika mataifa ya Umoja wa Ulaya dhidi ya kiongozi huyo wa siku nyingi barani Afrika.

Mugabe, ambaye amepigwa marufuku kuingia katika mataifa ya Ulaya tangu mwaka 2002 kwa sababu ya  madai ya udanganyifu katika kura na ukiukaji wa haki za binadamu nchini Zimbabwe, alichukuliwa  moja kwa moja kutoka katika ndege iliyomleta mjini Rome kwa gari, pamoja na mkewe, Grace na  walinzi wake. 

Licha ya kuwa uwanja huo wa ndege uko katika ardhi ya Italia, kiongozi huyo mwenye  umri wa miaka 89 alilakiwa na padri, ambaye alimwambia: "Kwa niaba ya Papa Francis, karibu  Vatican, karibu mahali patakatifu". Baadaye alipelekwa katika hoteli katika eneo maarufu la Via Veneto. Kiongozi wa Kanisa Katoliki, Papa Francis, anatawazwa rasmi leo Jumanne.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...