Tuesday, June 17, 2014

URENO YA RONALDO YALA KIPIGO CHA 4-0 KUTOKA KWA `WANYAMA` UJERUMANI

article-2659215-1ED2CD1400000578-919_634x442
Wachezaji wa Ujerumani wakumpongeza mwenzao Thomas Muller (kushoto) baada ya kupiga hat-trick leo
MJERUMANI Thomas Muller awa mchezaji wa kwanza  kufunga mabao matatu katika mechi moja `hat-trick`  kwenye fainali za kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil baada ya kuiongoza nchi yake kuilaza Ureno mabao 4-0 usiku huu mjini Salvador. Nyota huyo wa Bayern Munich alifunga bao la kuongoza dakika za mapema kwa mkwaju wa penati na kuwapa mwanzo mzuri katika uwanja wa Arena Fonte Nova wana nusu fainali hao wa mwaka 2010 nchini Afrika kusini. 
Mabao ya Muller usiku huu yalifungwa katika dakika za  12 (penati), 45, 78, na goli lingine lilifungwa na beki wa kati Mats Hummels katika dakika 32 Ureno walipata majanga baada ya mshambuliaji wake wa kati Hugo Almeida na Fabio Coentrao kupata majeruhi, lakini mbaya zaidi walishuhudia  beki wao wa kati Pepe  akitolewa nje kwa kadi nyekundu wakati timu yake iko nyuma kwa mabao 2-0 baada ya kumfanyiwa madhambi Muller. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Wednesday, June 11, 2014

UMRI WA KUISHI WAONGEZEKA...!!!

Wastani wa umri wa kuishi kwa Watanzania umeongezeka kutoka miaka 50 kwa sensa iliyofanywa mwaka 1988 hadi kufikia miaka 61 kwa sensa ya mwaka 2012.
Akiwasilisha taarifa za msingi za kidemografia, kijamii na kiuchumi kwenye hafla ya uzinduzi iliyofanyika jijini hapa jana, mkurugenzi mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dk Albina Chuwa alisema wanawake wanaishi umri mrefu zaidi kuliko wanaume.
“Matokeo haya yameendelea kuonyesha wastani wa umri wa kuishi kwa wanawake ni miaka 63 ambao ni mkubwa zaidi ukilinganisha na wanaume ambao ni miaka 60. Tunaamini ongezeko hilo limetokana na kukua kwa uchumi na kupungua kwa umaskini wa kipato.”
Akizungumzia kuhusu matokeo ya awali ya uzazi kwa sensa ya mwaka 2012, alisema inaashiria kupungua kwa kiwango cha uzazi kutoka wastani wa watoto 6.5 mwaka 1988 hadi kufikia watoto 5.2.
“Hii inaweza kuwa imesababishwa kuongezeka kwa umri wa kuolewa katika umri wa kuanzia miaka 22 wakati wanaume wamebainika kuwa huoa kuanzia miaka 24 na kuendelea,” alisema.
Alisisitiza kuwa inawezekana matumizi ya njia za kisasa za uzazi wa mpango na kuongezeka kwa kiwango cha elimu kwa wanawake ni sababu zinazowafanya waishi zaidi. Akizindua taarifa hiyo, Rais Jakaya Kikwete aliwapongezawalioshiriki kukusanya taarifa hizo na kuzichanganua, akieleza kwamba ni miongoni mwa shughuli ngumu kwa kuwa kuna udanganyifu unaofanywa na baadhi ya watu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
“Taarifa hizi zimechambuliwa vyema na zitasaidia kupanga masuala ya maendeleo. Idadi yetu inazidi kuongezeka pia. Mwaka 2012 tulikuwa milioni 44, pengine hadi mwaka 2016 tutakuwa milioni 48,” alisema.
Na Mwananchi

ANGALIA PICHA ZA GARI MPYA LA NAY WA MITEGO, NI BALAA...!!!

IMG_0514 
Wasanii mbalimbali wamekua wakionyesha magari ambayo mengi yamekua ya kifahari ambapo kwa mwaka 2014 ni mwaka unaonyesha wasanii wengi kumiliki magari ya gharama zaidi,mpaka sasa ni zaidi ya wasanii watano ambao wameonyesha magari yao ya kifahari.
Star wa single mbalimbali ikiwemo Nakula Ujana Ney wa Mitego nae yupo kwenye list ya wasanii wanaomiliki magari haya ya thamani hii ya Ney wa Mitego ni Nissan Morano ya mwaka 2007 na hii inakamilisha gari la pili kwenye kipindi kifupi baada ya ya ile Toyota Mark X.
Kwa maelezo ya Ney ingawa hakutaka kutaja bei kamili aliyonunulia lakini kasema ni zaidi ya Milioni 35,ambayo ameitoa kama zawadi kwa ajili yake siku ya kuzaliwa kwake ambayo ilikua ni 9 June 2014.
IMG_0539
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO JUNI 11, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Tuesday, June 10, 2014

SHEIKH MWINGINE AUAWA NCHINI KENYA

Marehemu Sheikh Mohammed Idris ameuawa na watu wasiojulikana
Muhubiri wa kiisilamu ameuawa mjini mombasa pwani ya Kenya , ikiwa ni mauaji ya hivi karibuni ya kiongozi mwingine wa kidini. Sheikh Mohammed Idris, ambaye ni mwenyekiti wa baraza la maimamu na wahubiri nchini Kenya, aliuawa karibu na msikiti ulio karibu na nyumba yake na watu wasiojulikana.
Duru zinasema kwa alikuwa amepokea vitisho kutoka kwa vijana wenye itikadi kali za kidini na tayari alikuwa ameelezea hofu juu ya maisha yake. Wahubiri kadhaa mashuhuri wameuawa katika hali ya kutatanisha katika miaka ya hivi karibuni.
Wengine waliuawa kwa madai ya kuwa na uhusiano wa karibu na kundi la wanamgambo la al-Shabaab huku wafuasi wao wakiilaumu serikali kwa mauaji yao, madai ambayo serikali imakenusha. 
Marahemu Idris alikuwa ameitaka serikali kukabiliana na baadhi ya watu wenye itikadi kali za kidini ndani ya msikiti hali ambayo ilisababisha baadhi ya waumini kumuita msaliti. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JUNI 10, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Monday, June 09, 2014

DALADALA ZAGOMA TENA MBEYA... WAKISHINIKIZA NAULI IONGEZWE HADI TSH 500, MALORI YATUMIKA KUSAFIRISHA ABIRIA...!!!

Moja kati ya malori yanayotumika kusafirishia abiria siku ya leo.


Askari wakifanya doria kuhakikisha usalama unakuwepo.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAALIM SEIF AZINDUA MKUTANO WA KAMATI TENDAJI PEMBA


Katibu Mkuu wa CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akizindua kamati tendaji za Wilaya za Pemba katika ofisi za CUF Wilaya ya Chake Chake
Mwenyekiti wa CUF Wilaya ya Magharibi Unguja Bi. Raisa Abdallah Mussa, akizungumza wakati wa uzinduzi wa kamati tendaji kwa Wilaya za Unguja katika ofisi za CUF Wilaya hiyo zilizoko Kilimahewa.

Hassan Hamad, OMKR.
Chama Cha Wananchi CUF kimesema hakitowavumilia watendaji watakaobainika kuendeleza fitna na majungu ndani ya chama hicho.
Katibu Mkuu wa Chama hicho Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad ameeleza hayo kwa nyakati tofauti, wakati akizindua kamati tendaji za (CUF) kwa Wilaya zote za Unguja na Pemba.

Kwa upande wa Unguja mkutano huo ulifanyika ofisi za (CUF) Wilaya ya Magharibi zilizopo Kilimahewa, ambapo mkutano kwa Wilaya nne za Pemba umefanyika ofisi za CUF Wilaya ya Chake Chake. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BAJETI YAMPELEKA JK DODOMA


kikwete_36f36.jpg
Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwasili Dodoma keshokutwa, ikiwa ni siku moja kabla ya kuwasilishwa kwa Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2014/15.
Habari zilizopatikana jana zinasema Rais ataongoza kikao cha Baraza la Mawaziri kitakachopewa muhtasari kuhusu Bajeti ya Serikali ya mwaka ujao wa fedha na baadaye atafuatilia uwasilishaji wa bajeti hiyo bungeni akiwa Dodoma.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu alisema asingeweza kuzungumzia suala hilo kwa kuwa yuko likizo lakini akaweka bayana kwamba kwa kawaida kabla ya bajeti kuwasilishwa bungeni, lazima Baraza la Mawaziri lipewe muhtasari wa bajeti husika.
"Ni kawaida kabla ya bajeti kuwasilishwa, Rais huongoza kikao cha Baraza la Mawaziri yaani pre budget cabinet meeting ambako Waziri wa Fedha hutoa briefing (muhtasari) kuhusu maeneo muhimu ya bajeti, kwa hiyo siyo jambo jipya ni suala la kawaida," alisema Rweyemamu.
Itakumbukwa kuwa mwaka jana kabla ya kusomwa kwa bajeti ya 2013/14, Rais Kikwete alikuwa Dodoma ambako pamoja na kukutana na mawaziri, pia alifanya kikao na Kamati ya Bunge ya Bajeti.
Hata hivyo, uwepo wake mjini Dodoma safari hii umekuja wakati kukiwa na dalili za mvutano mkubwa kati ya Bunge na Serikali kutokana na kutotolewa kwa fedha za kutosha za maendeleo kwa mwaka wa fedha unaoisha Juni 30 mwaka huu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ADUMAA KWA MIAKA 18, AOMBA MSAADA WA KUTIBIWA...!!!


dumaapx_72c1c.gif
Farida Abdallah (18), ambaye amedumaa kwa miaka 18.
Wazazi wa binti mwenye ulemavu wa viungo na akili, Farida Abdalah (18) mkazi wa Lukobe Juu mkoani Morogoro wameiomba Serikali, wasamaria wema na wadau mbalimbali kumsaidia binti yao huyo ambaye kwa sasa amelazwa katika hospitali ya rufaa na anaendelea kufanyiwa uchunguzi wa afya yake.
Pia wazazi hao ambao walionekana kuwa na hali ngumu ya kimaisha

waliomba msaada wa kupatiwa matibabu ya viungo na akili kwa binti yao ili aweze kutembea na kujitambua, kwani kwa sasa binti huyo amekuwa akilala tu kitandani.

Maisha ya binti huyo ambaye umri wake haulingani na umbo lake yameguswa na watu wengi, kwani amekuwa haongei, halii, hasikii na wala hajitambui hivyo amekuwa akivalishwa nepi na kubebwa kama mtoto mchanga.

Akitoa historia ya binti huyo kwa mwandishi wa habari hizi jana mama mzazi wa binti huyo Mwajuma Abdalah alisema kuwa Farida alizaliwa mwaka 1996 wilayani Muheza mkoani Tanga na alijifungulia nyumbani. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAMBO 20 MUHIMU KUHUSU KOMBE LA DUNIA



1 — Mechi zote za Kombe la Dunia 1930 nchini Uruguay  zilichezwa kwenye jiji moja: Montevideo.
2 — Beki wa Sweden, Jan Olsson, alikuwa akivaa jezi namba 2, beki huyo ndiye aliyemdhibiti vilivyo nyota wa Uholanzi, Johan Cruyff aliyekuwa akisifika kwa aina yake ya ugeukaji  na kuwatoroka mabeki “Cruyff Turn” kwenye fainali za mwaka 1974, Ujerumani Magharibi.
3 — Gwiji wa Brazil, Pele ni mchezaji pekee aliyetwaa  makombe matatu ya dunia akiwa anacheza mwaka: 1958, 1962 na 1970.
4 — Idadi ya wachezaji waliofunga mabao matatu katika mechi  mbili za Kombe la Dunia: Mhungary Sandor Kocsis (zote mwaka 1954), Mfaransa, Just Fontaine (1958), Mjerumani,  Gerd Muller (1970) na Gabriel Batistuta (moja 1994 na moja 1998).
5 — Mshambuliaji wa Russia, Oleg Salenko ndiye  anayeshikilria rekodi ya kufunga mabao matano katika mechi moja ya Kombe la Dunia, wakati Russia waliposhinda 6-1  dhidi ya Cameroon fainali za 1994 nchini Marekani. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JUNI 09, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

PAPA AWAPOKEA MARAIS WA ISRAEL NA PALESTINA VATICAN

Mahmoud Abbas, Papa na Shimon Peres Vatikani
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Papa Francis amewakaribisha Rais wa Israil, Shimon Peres, na mwenzake kutoka Palestina, Mahmoud Abbas, katika maombi ya aina ya kipekee katika makao makuu ya Kanisa Katoliki ya Vatican. Viongozi hao wawili walikutana na Papa nje ya makaazi yake kabla ya kuandamana naye, wakiandamana na kiongozi wa Kanisa la Ordhodoz, Partriarch Artholomew kwa hafula maalumu katika Medani ya Vatican. Akiongea katika hafula hiyo Papa alisema ujasiri na nguvu vinahitjika katika juhudi za kuleta amani.

"Kuleta amani kunahitji ujasiri mkubwa kuliko vita. Kunahitaji ujasiri wa kusema ndio kwa mkutano na La kwa vita; ndio kwa mashauriano na La kwa makabiliano; ndio kwa kuheshimu mikataba na La kwa uchokozi; Ndio kwa ukweli na La kwa Uongo; kwa haya yote tunahitaji ujasiri na nguvu moyoni," Papa alisema
Na katika hotuba yake Bwana Peres alisema alitakia vizazi vyote vijavyo amani ya kudumu:
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz


"Rafiki wapenzi, Nilikuwa mchanga, na sasa nimezeeka. Nilishuhudia vita, Nilionja amani. Sitawahi kusahau familia zilizofiwa, wazazi na watoto waliolipia gharama kubwa kwa vita hivyo. Na maisha yangu yote sitakoma kuitisha amani, kwa niaba ya vizazi vijavyo. Naomba sisi sote tuuungani mikono na kufurahi kwa sababu ni wajibu wetu kufanya hivyo kwa niaba ya watoto wetu.

UWANJA WA NDEGE WASHAMBULIWA PAKISTAN

Wanajeshi wa Pakistan wakiwa kwenye uwanja wa ndege wa Karachi kukabiliana na washambulizi.
Mapambano ya risasi yaliyodumu saa tano katika uwanja wa mji mkubwa zaidi nchini Pakistani ,Karachi yamewauwa watu 23 wakiwemo washambuliaji wote 10.
Washambuliaji hao waliokuwa na silaha nzito nzito waliingia sehemu ya majengo ya uwanja huo kupitia njia zinazotumiwa na ndege za mizigo au zile zinazotumiwa kuwapokea wageni wenye hadhi na sifa yaani V.I.Ps.
Walipenya usiku wa manane na kuanza kuwashambulia maafisa usalama kwa gruneti na kwa kuwafyatulia risasi.
Makamanda katika jeshi waliitwa kukabiliana na washambuliaji hao na milio ya risasi ilisikika hadi alfajiri wakati hali ilipodhibitiwa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Haijabainika vyema ni akina nani hasa walioshambulia lakini yamewahi kufanyika mashambulio kama hayo hasa katika maeneo ya wanajeshi wa angani na wa majini ambapo wanamgambo wa Taliban walihusika.
Na BBC

Sunday, June 08, 2014

TANZIA: MZEE SMALL AFARIKI DUNIA

1_e4ab8.jpg
Mzee Small enzi za uhai wake.
Muigizaji mkongwe nchini, Said Ngamba maarufu kwa jina la Mzee Small amefariki dunia usiku huu akiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar. Mzee Small amefariki kwa ugonjwa wa presha baada ya kuugua kwa muda mrefu kabla ya kuzidiwa jana na kupelekwa Muhimbili. Mtoto wa marehemu aitwaye, Muhidin amethibitisha kifo cha Mzee Small. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 08, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS

..
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ANGALIA PICHA ZA HARUSI YA MBUNGE JOSHUA NASSARI ILIVYOFANA



2_31d12.jpg
Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Samwel Nassari jana amefunga ndoa na Anande Nko kwenye Kanisa la Pentekoste lililopo Kilinga, Arumeru jijini Arusha ikifuatiwa na sherehe kubwa iliyofanyika katika Viwanja vya Usa-River Academy jirani na Hoteli ya Ngurdoto.
Sherehe hiyo ilianza saa 7:00 mchana  ambapo watu wote walialikwa wakiwemo ndugu, marafiki, jamaa na wananchi wote wa Arumeru Mashariki ambao wamepiga 'mpunga' wa kutosha na vinywaji hadi kila mtu akaondoka akisema 'Nassari ameacha historia'. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
CHANZO: Mitandao ya Kijamii.

RAIS MPYA WA MISRI KUAPISHWA

Raia wanaomuunga mkono Abdel Fatah al sisi
Usalama umeimarishwa katika mji mkuu wa Misri, Cairo kabla ya kufanyika kwa sherehe ya kumuapisha rasmi rais mpya wa taifa hilo Abdel Fatah el Sisi.
Rais huyo mteule atakula kiapo chake cha kuchukua mamlaka katika mahakama kuu ya kikatiba mjini Cairo.
Alishinda uchaguzi wa urais wa mwezi uliopita kwa wingi wa kura ijapokuwa idadi ya waliojitokeza kushiriki katika shughuli hiyo ilikuwa chini ya asilimia 50.
Uchaguzi huo unajiri miezi michache tu baada ya kiongozi huyo kumpindua madarakani aliyekuwa rais wa taifa hilo Mohammed Morsi.
Mkuu huyo wa jeshi wa zamani ameanzisha msako dhidi ya wanaompinga mbali na kukipiga marufuku chama cha Morsi cha Muslim Brotherhood. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC Swahili

Saturday, June 07, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JUNI 07, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAHAKAMANI KWA KOSA LA KUAGIZA MAITI IKATWE MIGUU...!!!


Mwandalizi mmoja wa mazishi nchini Afrika Kusini, anayedaiwa kuwaagiza wafanyakazi wake kuikata miguu ya maiti moja aliyodai kuwa ndefu sana alifikishwa mahakamani Ijumaa.
Ronel Mostert anayemiliki chumba cha kuhifadhi maiti ambacho pia huendesha shughuli za mazishi, alitoa amri hiyo kwa lengo la kuhakikisha kuwa maiti hiyo ingetosha katika jeneza. Anakabiliwa na kosa la kumkata miguu maiti.
Mfanyakazi mmoja aliimbia mahakama kuwa Ronel alimuagiza kuchukua kifaa kimoja cha kukata ili kuikata miguu hiyo ya marehemu na kwamba jambo hilo limekuwa likimsumbua sana kimawazo.
Mwili marehemu ulifukuliwa ili kusaidia katika uchunguzi wa polisi.Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Na BBC

MADEREVA WA UMMA WAGOMA BRAZIL

Mgomo wa wafanyakazi hao umesababisha uhaba wa magari ya usafiri
Maafisa wa polisi nchini Brazil wametumia gesi ya kutoa machozi ili kuwatawanya waandamanaji katika siku ya pili ya mgomo wa wafanyikazi wa sekta ya uchukuzi ambao umesababisha uhaba mkubwa wa usafiri wa uma katika mji wa Sao Paulo.
Takriban nusu ya vituo vya treni vilifungwa na kusababisha msongamano mkubwa wa watu katika barabara za mji huo mkubwa ambao unatarajiwa kuandaa michuano ya kombe la dunia kuanzia alhamisi ijayo.
Wafanyakazi hao wa treni wanataka mishahara yao kuongezwa kwa asilimia kumi.
Awamu nyengine ya majadiliano imefeli na wafanyikazi hao wanasema kuwa mgomo huo utaendelea kwa mda usiojulikana. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Na BBC

MWEGANE YEYA WA MBEYA CITY AAHIDI MAKUBWA TAIFA STARS, AMSHUKURU MUNGU KWA KUITWA NA MART NOOIJ


Mwagane-Yeya.pngnnnnnnnnnnnnnnNa Baraka Mpenja, Dar es salaam
MSHAMBULIAJI hatari wa Mbeya City fc, Mwegane Yeya amefurahishwa na kitendo cha kuitwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars chini ya kocha Mholanzi, Mart Nooij.
Akizungumza na mtandao huu, Mwegane amesema kuwa anamshukuru sana Mungu kwa kupata nafasi hiyo kwasababu Tanzania ina wachezaji wengi wenye viwango vya hali ya juu, lakini amechaguliwa yeye.
“Hii ni nafasi nyingine muhimu kwangu. Niliwahi kuitwa katika kikosi cha Young Future Taifa Stars na Kim Poulsen, lakini sikufanya vizuri kwasababu nilikuwa majeruhi. Naamini kwasasa nitaitumia vizuri nafasi hii”. Alisema Mwegane ambaye ni hatari kwa kufunga magoli ya kichwa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Friday, June 06, 2014

WARIOBA AZISHUKIA UKAWA NA CCM


Katika Bunge hilo, wajumbe wengi wa CCM walimshambulia Warioba na tume yake wakidai kuwa Rasimu ya Pili ya Katiba haikuzingatia maoni ya wananchi na Mabaraza ya Katiba. PICHA|MAKTABA 

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amewashauri wajumbe wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) na CCM kuacha kuzunguka mikoani kufanya mikutano inayoeleza misimamo yao kuhusu mchakato wa Katiba Mpya kwa kuwa haina tija kwa taifa.
Ameonya kuwa mikutano hiyo inajenga mwelekeo mbaya kwa taifa na kuhatarisha mchakato wa Katiba na kuzitaka pande hizo kumaliza tofauti zao.
Akizungumza katika mahojiano maalumu yaliyofanyika Dar es Salaam jana, Warioba alisema: “Kwa mustakabali mwema wa taifa, ni muhimu makundi haya ‘ya-resolve’ (yamalize), matatizo yaliyopo kabla ya Agosti, ili Bunge Maalumu la Katiba likirejea, wote washiriki na kukamilisha mchakato wa kupata Katiba Mpya. Hili ni kwa masilahi ya taifa.”
Kauli ya Waziri Mkuu huyo mstaafu ambaye pia aliwahi kuwa Mwanasheria Mkuu, imekuja huku makundi ya Ukawa linaloundwa na wabunge wengi wa upinzani na viongozi wa CCM wakiendelea kung’ang’ania misimamo yao kuhusu Rasimu ya Katiba Mpya iliyowasilishwa kwenye Bunge Maalumu la Katiba.
Wakati CCM ikipinga mapendekezo ya kuwapo kwa mfumo wa serikali tatu uliomo kwenye Rasimu, Ukawa unaunga mkono mapendekezo hayo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TIGO, AIRTEL NA ZANTEL ZAUNGANISHA HUDUMA




Meneja Mkuu wa Kampuni ya Tigo, Diego Gutierrez (Kulia) na Ofisa Mtendaji Mkuu wa DTBi, Mhandisi George Muhula wakitia saini ya makubaliano jijini Dar es Salaam jana baina ya Tigo na DTBi ya kusaidia wajasiriamali kujifunza teknolojia ya digitali na mawasiliano. Wanaoshuhudia ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof Makame Mbarawa na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dk Hassan Mshinda. Picha na Venance Nestory.


Kampuni za simu za mkononi za Tigo, Airtel na Zantel zimeunganisha huduma zao za kutoa, kutuma na kuweka fedha na sasa mteja anaweza kutuma fedha kutoka mtandao mmoja kupitia mwingine.

Taarifa ya pamoja na kampuni hizo iliyotolewa jana, ilisema kuwa wote wanaotumia huduma za kifedha za mitandao hiyo, wataweza kutumiana fedha kupitia simu zao za mikononi pasi na tatizo baada ya kampuni hizo kuunganisha huduma zao.

Huduma hiyo inayotarajiwa kuanza kutumika mwishoni mwa mwezi huu, itawafanya wateja wa mitandao hiyo kutumiana na kupokea fedha moja kwa moja kwenye akaunti zao tofauti na ilivyokuwa awali. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNI 06, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MTAWA WA KANISA KATOLIKI ASHINDA KATIKA SHINDANO LA KUIMBA...!!!

Mtawa wa Italia anyakua ushindi
Mtawa mmoja kutoka Italia ambaye alipata umaarufu katika mtandao wa kijamii ameshinda shindano la kuimba nchini humo. Mtawa huyo, Sister Christina Scuccia alitokea kwa mara ya kwanza katika televisheni kushiriki shindano la The Voice.
Scuccia aliyeonekana amevalia mavazi yake ya utawa na msalaba shingoni, alijawa na furaha na kumshukuru Mungu kwa kumfikisha katika ushindi huo. Mtindo wake wa wimbo wa Alicia Keys, kwa jina 'No One', umetizamwa zaidi ya mara milioni 50 katika mtandao wa You Tube tangu auimbe.
Mtawa huyo mwenye umri wa miaka 25 amesema kuwa aliamua kushiriki mashindano hayo kufuata ushauri wa Papa mtakatifu Francis, kuwa kanisa liwakaribie zaidi watu wa kawaida. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Na BBC Swahili

DRC YAILAUMU RWANDA KWA KUWALINDA M23




DRC yailaumu Rwanda kuwalinda M23
Serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo imeikashifu serikali ya Rwanda kwa kuwalinda wapiganaji wanaotuhumiwa kwa kusababisha mauaji ya halaiki chini ya nembo ya wapiganaji wa M23.
Afisa mmoja wa Serikali ya DRC ameiambia BBC kuwa imekuwa vigumu kwa serikali yake kuwahoji zaidi ya wapiganaji 500 ambao wamekita kambi nchini Rwanda licha yao kutuma ombi la kufanya hivyo yapata miezi saba iliyopita . Zaidi ya watu 800,000 walitoroka makwao haswa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo wakati wa mapigano hayo ya wenyewe kwa wenyewe.

Rwanda imekuwa ikipinga madai hayo na kusema kuwa imeshirikiana na serikali ya DRC. Kundi hilo la M23 lichukua silaha mashariki mwa DRC kuanzia Aprili 2012, liliaumu serikali ya Kinshasa kwa kuwabagua jamii ya watutsi na pia kupuuza makubaliano ya awali ya kusitisha mapigano. Kundi hilo hata hivyo lilishindwa katika mapigano yaliyoongozwa na jeshi la Umoja wa mataifa likisaidiwa na majeshi ya serikali ya Congo mnamo November 2013. Wapiganaji hao walitorokea Rwanda na Uganda.


DRC yailaumu Rwanda kuwalinda M23
Katika mji wa Ngoma, mashariki mwa Rwanda mwandishi wetu alikumbana na wapiganaji hao ana kwa ana katika kambi nje ya mji. Wengi wao wanasema kuwa wamechoshwa na ngoja ngoja hiyo ambayo imedumu kwa kipindi kirefu sasa na wanasema kuwa wangependa kuomba hifadhi nchini Rwanda, kwani wanahofia kurejea ndani ya Congo.
 Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Serikali ya Congo imetangaza kuwa itawapa msamaha wapiganaji hao. Tulipoingia ndani ya kambi hiyo ,hali na taswira ilikuwa tulivu na shwari. Kulikuwa na hema kubwa nyeupe, majengo kadha mbali na bustani iliyolindwa na nadhifu. Wapiganaji hao wanalala sita katika chumba kimoja .

Thursday, June 05, 2014

G7 WAKUTANA BRUSSELS BILA URUSI

mkutano wa G7
Viongozi wa mataifa tajiri ya magharibi wanaokutana mjini Brussels wamesema kuwa wako tayari kuweka vikwazo zaidi kwa Urusi iwapo itaendelea kuvuruga amani mashariki mwa Ukrain. Taarifa ya pamoja ya mataifa ya G7 imesema kuwa Mambo yanayofanywa na Urusi nchini Ukrain hayawezi kubalika kamwe na lazima yakomeshwe.
Huu ndio mkutano wa kwanza wa viongozi hao tangu waifukuze Urusi kama mwanachama.
Urusi ilibumburushwa kutoka G7 kwa kosa lake kubwa zaidi, kuinyakua Crimea kutoka Ukrain. Viongozi wa mataifa hayo ya G7 wanakutana sasa kwa mara ya kwanza tangu wakati huo.
Ukrain vita vimechacha
Lakini huku wakikutana mapigano yamechacha kati ya serikali ya Ukrain na majeshi yanayo unga mkono Urusi mashariki mwa Ukrain. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Urusi imeendelea kukana kuhusika na mapigano hayo. Miongoni mwa mikutano iliyopangwa Alhamisi hii, waziri mkuu wa Uingereza Davin Cameron atakutana na rais Obama mjini Brussels, ambapo kwa upana zaidi watazungumzia Urusi. Kisha baada ya mkutano huo, David Cameron ataelekea Paris Ufaransa kwa mkutano wa faragha na rais wa Urusi Vladmir Putin.

D-Day barani Uropa

Katika wiki hii mataifa ya Uropa yamekuwa yakiadhimisha siku ya kuikomboa bara Uropa kutoka utawala wa ki Nazzi katika vita vya pili vya dunia miaka 70 iliyopita. Huku hayo yakitokea, juhudi za kidiplomasia zimeshika kasi miongoni mwa mataifa ya magharibi kumaliza uhasama kati yao na Urusi.
G7 wamepongeza uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Ukrain na wameirai Urusi kumpokea na kushirikiana na rais mpya wa Ukrain Petro Poroshenko. Pia wameonya kuwa hawatasita kuiwekea Urusi vikwazo zaidi iwapo itakataa kusaidia kurejesha uthabiti Ukrain. Itakuwa ni mara ya kwanza kwa miaka 17 ambapo G7 inakutana bila Urusi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...