Friday, September 20, 2013

MWALIMU MKUU ANASWA NA MAGUNIA 6 YA BANGI HUKO MKOANI KAGERA.

MWALIMU Mkuu wa Shule ya Msingi Mukubu, Wilaya ya Ngara mkoani Kagera, Silidion Kaiza (43), anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kukutwa na bangi gunia sita.
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Philip Kalangi alisema kuwa tukio hilo lilitokea Septemba 17, mwaka huu, shuleni hapo katika kata na kijiji cha Muganza majira ya saa tano asubuhi.
 
Alisema kuwa raia wema walitoa taarifa kituo cha polisi Rulenge kwamba kuna mwalimu anajihusisha na biashara ya kuuza dawa za kulevya, jambo walilohofia kuwa huenda akawaathiri wanafunzi wa shule hiyo kwani anazihifadhi shuleni.

JWTZ LATOA UFAFANUZI KUHUSU AJIRA

JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA
KURUGENZI YA HABARI NA UHUSIANO
Simu ya Upepo  : “N G O M E”                Makao Makuu ya Jeshi,
Simu ya Mdomo  :                              DSM  22150463  
                                                                     Sanduku la Posta 9203,
Telex                     : 41051                            DAR ES SALAAM,19                                                                Septemba, 2013.
Tele Fax                                         : 2153426
Barua pepe          : ulinzimagazine@yahoo.co.uk
Tovuti                       : www.tpdf.mil.tz
Taarifa kwa vyombo vya Habari
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) linapenda kuwataarifu Wananchi wote kuwa taarifa zilizoenea kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno kupitia simu za mkononi (sms) na mitandao mbalimbali ya kijamii kwamba JWTZ limeanza kuajiri wataalamu Jeshini (Professionals) siyo kweli na halina utaratibu wa kutangaza ajira kupitia mitandao ya kijamii au kupitia simu za mikononi.
          Kwa kawaida, utaratibu wa kujiunga na Jeshi hutangazwa kwenye Vyombo vya Habari pale ambapo Jeshi linahitaji kuandikisha askari wapya.  JWTZ huelekeza utaratibu wa kuzingatia katika kuwasilisha maombi husika kwa taarifa hii, wananchi wote wanatahadharishwa kuhusu ujumbe huo unaoelekea kusababisha usumbufu kwa wananchi na JWTZ.  Taarifa hiyo haijatolewa na JWTZ hivyo wananchi wajihadhari na yeyote atakayejitokeza kuwarubuni na hatimaye kutapeliwa kwa namna yoyote.
                       
Imetolewa na:
Kurugenzi ya habari na Uhusiano
Makao Makuu ya Jeshi

MANGULI KATIKA WIZI WA MTANDAO WAKAMATWA KATIKA OFISI ZA TIGO BUGURUNI HAWA HAPA NA JINSI WANAVYOIBA MTANDAONI

Mrembo huyu ni mmoja wa watuhumiwa wa kesi hii ya wizi wa mtandao baada ya kutumia kitambulisho chake na  kutaka kuja kurudisha line ambayo sio yake kwa kuahidiwa kupewa pesa kidogo kama ujira wake na katika melezo yake akasema hawatambui wahusika wenzake kwani amekutana nao tu sinza na wakampa dili hilo na kuamua kuchukua bajaji ambao iliwaleta mpaka ofisi za tigo buguruni rozana 

MLOKOLE AFUMANIWA NA MKE WA MTU AKIZNI HUKO MANZESE......ADAIWA KUTUMIA KWAYA KANISANI KUMRUBUNI....!!!


MATUKIO na vitendo viovu vinaendelea kushamiri juu ya uso wa nchi! Kijana anayedaiwa kuwa muumini wa kanisa la kilokole (jina tunalo) la jijini Dar,  Faraji Oti amekutwa na mazito akidaiwa kufumaniwa na mke wa mtu aliyetajwa kwa jina moja la Jesca, Ijumaa lina kisanga kamili.
MANZESE, DAR
Tukio hilo lililoongeza furaha ya Shetani, lilichukua nafasi mwanzoni mwa wiki hii majira ya 11:00 jioni huko Manzese, jijini Dar.
Kwa mujibu wa watu wa karibu na wahusika hao, kisa kilianzia kwenye simu ambapo mwenye mke alidai kunasa mawasiliano ya jamaa huyo na mkewe.
Ilidaiwa kuwa ukaribu wa wawili hao ulianzia kwenye kwaya waliyokuwa wakiitumikia kisha kuzua mawasiliano tata.



OTI AONYWA
Habari zilidai, kuna wakati mume wa Jesca alimuonya Oti kukaa mbali na mkewe lakini jamaa alipuuza huku akidaiwa kutoa maneno makali na ya dharau kwa mwenye mali.

KINANA ATAKA WALIMU WATATULIWE KERO ZAO HARAKA

2
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akifurahia waimbaji wa kwaya mara baada ya kuwasili katika kijiji cha Nyashimo Wilayani Busega katika mkoa wa Simiyu, Ndugu Abdulrahman Kinana amemaliza ziara yake kwenye mkoa huo ambapo amekagua miradi ya maendeleo na kuzungumza na wenyeviti wa mashina pamoja na wanachama wa CCM ili kuimarisha chama na kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi katika maeneo mbalimbali moani humo, Kinana anaaza Ziara ya siku sita katika mkoa wa Mara. Akihutubia katika mkutano wa hadhara leo uliofanyika mjini Lamadi Busega Kinana ametoa miezi sita kwa Waziri wa Elimu na Mfunzo ya Ufundi Dr. Shukuru Kawambwa, Waziri wa Serikali za Mitaa TAMISEMI Hawa Ghasiapamoja na watendaji wengine wa Serikali katika sekta ya Elimu kuhakikisha wanashughulikia kero za walimu hasa katika malipo yao mbalimbali ili kumaliza tatizo la malimbikizo hayo, Kinana amesema kama watendaji hao wa serikali hawatamaliza tatizo hilo atawashughulikia kwa kuwashitaki kwa wabunge wa CCM ili wawawajibishe kwa kukiuka agizo la Rais Dr.Jakaya Kikwete ambaye aliagiza watendaji hao kumaliza matatizo ya walimu, Katika picha katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Besega Ndugu Paul Mzindakaya na aliyenyanyua mkono kushoto ni Mbunge wa jimbo la Busega Dr. Titus Kamani. (PICHA NA KUKOSI KAZI CHA FULLSHANGWE-LAMADI SIMIYU) 
 1
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana na Katibu wa NEC Itikadi Siasa na Uenezi Ndugu Nape Nnauye wakifurahia ngoma za akina mama walipowasili katika wilaya ya Busega mkoani Simiyu. 9

KUDHIHIRISHA KUWA YUPO NJE KWA DHAMANA HIZI NDIZO PICHA ALIZOZISAMBAZA AGNES MASOGANGE MTANDAONI




MAGAZETI YA LEO IJUMAA SEPTEMBA 20, 2013

DSC 0032 8b966
DSC 0033 c2442

MNIGERIA ASHINDA SHINDANO LA UREMBO LA KIISILAMU

mrembo 25c93
Mwanadada wa Nigeria ndiye mshindi wa shindano la urembo kwa wasichana wa kiisilamu mjini Jakarta Indonesia.


Obabiyi Aishah Ajibola, 21, alishinda shindano la kimataifa la wasichana wa kiisilamu kwa jina Muslimah mwaka 2013 siku ya Jumatano.
Washindani 20 walishiriki mashindano hayo kuonyesha mitindo ya kiisilamu pamoja na maadili ya kiisilamu wakati wa mashindano hayo.
Mashindano yalifanyika kabla ya shindano kubwa zaidi la mwanamke mrembo zaidi duniani, ambalo limeghadhabisha makundi ya watu wenye msimamo mkali nchini Indonesaia kwa kutaka kuandaliwa huko.
Waliofuzu kwa fainali ya mashindano hayo, walichaguliwa kutoka miongoni mwa watu 500 waliochaguliwa kwa kutumia njia ya mtandao.
Moja ya vikwazo vya kuruhusiwa kushirki kwenye mashindano ilikuwa kusimulia kisa chako na ambavyo ulianza kuvalia Hijab au mtandio, ambacho kilikuwa kikwazo kwa wote waliotaka kushiriki.

JESHI LA POLISI LAPIGA MARUFUKU MAANDAMANO YA CUF, CHADEMA NA NCCR HAPO JUMAMOSI



Jeshi la Polisi Jijini Dar es Salaam limepiga marufuku maandamano ya umoja wa vyama vya CUF, NCCR na CHADEMA siku ya Jumamosi yaliyokuwa yamepangwa  kuanzia Tazara hadi Jangwani na Mwenge hadi Jangwani na sehemu mbalimbali ...

Taarifa  iliyotolewa  na kamanda Kova  kupitia  ITV   imeeleza  kuwa  Polisi wamechunguza na kugundua kwamba  maandamano  hayo  yataleta usumbufu kwa watu wengine na kwamba kwa kuwa lengo ni kufika Jangwani basi Viongozi wa vyama hivyo wawaambie wafuasi wao waende Jangwani bila Maandamano.

Source: ITV HABARI SAA 2 usiku

MILIONI 58 ZAPATIKANA mechi SIMBA SC, MGAMBO TANGA

Boniface-Wambura1 655d3
MCHEZO wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kati ya Simba SC na Mgambo Shooting Stars iliyochezwa jana (Septemba 18 mwaka huu) katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam umeingiza Sh. 58,365,000.

Watazamaji 10,241 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo namba 23 ya VPL msimu wa 2013/2014 iliyomalizika kwa wenyeji Simba kuibuka na ushindi wa mabao 6-0.

Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 13,839,327.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 8,903,135.59.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,036,946.16, tiketi sh. 2,548,890, gharama za mechi sh. 4,222,167.70, Kamati ya Ligi sh.
4,222,167.70, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,111,083.85 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,641,954.10.

Wakati huo huo; Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetoa siku 14 kwa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na za Ligi ya Daraja la Kwanza (FDL) kuwasilisha mikataba ya makocha wao.

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF iliyokutana Septemba 12 mwaka huu imebaini klabu nyingi hazijawasilisha mikataba ya mabenchi yao ya ufundi, kitu ambacho ni matakwa ya kikanuni. Siku hizo 14 zimetolewa kuanzia Septemba 17 mwaka huu.

Kwa klabu ambazo zitashindwa kuwasilisha mikataba hiyo na vielelezo vingine ndani ya mudau huo zitachukuliwa hatua kwa mujibu wa kanuni. Chanzo: TFF

HAKIMU ACHOMWA KISU MAHAKAMANI

hakimu_1e5b7.jpg
Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo iliyopo eneo la Nguzo Nane, Kata ya Kambarage Mjini Shinyanga, Satto Nyangoha amejeruhiwa kwa kuchomwa kisu katika shavu lake la kushoto baada ya kutoa hukumu ya kesi ya wizi wa baiskeli.
Kitendo hicho kinadaiwa kufanywa na mlalamikaji katika kesi hiyo, Emmanuel Izengo (28), mkazi wa Tambukareli, Shinyanga baada ya kutokuridhishwa na hukumu iliyotolewa bila ya mshtakiwa, Daniel Makelezia, mkazi wa Lubaga Shinyanga na mdhamini wake, Marko Nkelezia kuwepo mahakamani.


Katika hukumu yake, Hakimu Nyangoha alisema mshtakiwa atakapopatikana atatumikia kifungo cha miaka miwili jela baada ya kupatikana na hatia ya wizi wa baiskeli hiyo aina ya Neria yenye thamani ya Sh150,000.
Awali, ilielezwa kwamba baada ya tukio hilo la wizi lililotokea Agosti Mosi, mwaka huu katika eneo la Nguzo Nane, mshtakiwa alikamatwa na kuwekwa mahabusu na kufunguliwa kesi namba 460 ya 2013 kabla ya kuachiwa kwa dhamana Agosti 23, mwaka huu huku kesi yake ikiendelea na pande zote mbili zilitoa maelezo.

Thursday, September 19, 2013

ICC YATAKA MAREKANI IMKAMATE RAIS BASHIR

al-bashir_bcdb9.jpg
Siku mbili baada ya Rais wa Sudan kuiomba Marekani kumpa Visa ya kusafiri nchini humo kuhudhuria mkutano wa baraza kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York, wito umetolewa kwa taifa hilo kumkamata Bashir na kumkamabidhi kwa mahakama ya ICC.
Mkutano huo utafanyika wiki ijayo.
Ombi hilo limetolewa na ICC kwa Marekani na kuitaka impe Visa Bashir na kisha kumkamata na kumkabidhi kwa mahakama hiyo pindi tu atakapotua nchini humo.
Bashir anatakikana na mahakama ya ICC kwa tuhuma za uhalifu dhidi ya binadamu na pia kuamuru mauaji ya halaiki katika jimbo la Darfur.
Marekani ilisema kuwa ilipokea ombi la Bashir kutaka Visa na kulitaja ombi hilo kama la kuudhi na kejeli kubwa kwa taifa hilo. Ilimtaka Bashir kwanza kujikabidhi kwa mahakamya ICC kabla ya kutaka kuingia Marekani.
Hata hivyo Marekani sio mwanachama wa mahakama ya ICC na kwa hivyo , kisheria sio lazima itimize matakwa ya mahakama hiyo juu ya Bashir.
Marekani imekuwa katika msitari wa mbele kutaka Bashir akamatwe kwa madai ya uhalifu dhidi yake ili akabiliwa na sheria za kimataifa
Shirika la habari la Reuters lilisema kua mahakama imeshauri Marekani kumkamata Bashir na kumkabidhi kwa ICC ikiwa ataingia nchini humo.
Vibali viwili vya kumkamata Bashir vilitolewa mwaka 2009 na 2010 kwa madai ya uhalifu dhidi ya binadamu.
Hata hivyo Sudan imepuuza hatua ya ICC kumtaka Bashir kwa makosa ya Darfur wakisema kuwa madai hayo yameongezwa chumvi, na nchi hiyo imekataa kuitambua mahakama hiyo ikisema kuwa ni sehemu ya njama ya nchi za magharibi dhidi ya Afrika.

TANZANIA YAMKATAA BALOZI WA UJERUMANI

Balozi Margit Hellwig-Boette 
******
Tanzania imemkataa Balozi mteule wa Ujerumani ambaye alitakiwa kuja kufanya kazi nchini.
Balozi huyo, Margit Hellwig-Boette alikuwa amemaliza muda wake nchini Kenya na alitakiwa kuja kuiwakilisha nchi yake Tanzania.
Balozi Hellwig-Boette alikaririwa na Gazeti la Standard la Kenya akieleza kuwa anajipanga kurudi kwao baada ya kukataliwa na Serikali ya Tanzania.
Alipoulizwa juu ya suala hilo, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alikataa kuzungumzia suala hilo akisema: “Watu wa Wizara ya Mambo ya Nje ndio wanaoshughulika na hayo mambo, waulizeni.”

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mkumbwa Ally alisema wizara yake haijapata taarifa za kukataliwa kwa balozi huyo.
“Suala hilo linahusu ofisi ya Rais, mambo ya uteuzi ni ya Rais. Wizara ya Mambo ya Nje haina hiyo taarifa na hata kama ingekuwapo hiyo taarifa siyo ya `public’.
“Siyo taarifa ya umma kwa maana kwamba, mchakato wake ni wa siri na hayo mambo hayana kuuliza kwa nini. Ukileta jina la mtu unayetaka aje kuwa balozi likikataliwa, hakuna kuuliza eti ni kwa nini.
“Unachofanya ni kuleta jina jingine, hata Rais hapa akipeleka jina la mtu kwenye nchi nyingine lisiporudi, hakuna kuuliza unachofanya ni kuteua tu jina jingine,” alisema Mkumbwa.
Alikariri Kifungu cha Nne cha Azimio la Vienna ambacho kinaruhusu nchi kukataa balozi wa nchi nyingine bila ya kutoa sababu.
“Nchi inayopeleka balozi katika nchi nyingine inatakiwa kutoa jina mapema kwa nchi nyingine. Hata hivyo, nchi hiyo ina uwezo wa kumkubali au kukataa uteuzi,” kinaelekeza kifungu hicho.
MWANANCHI

RAIS KIKWETE AWASHUKIA WANASIASA


 
Rais Jakaya Kikwete
 
*Asema hatawatetea wauza ‘unga’
*Ashangazwa na kiwango cha uongo

RAIS Jakaya Kikwete, amesema anashangazwa na kiwango cha uongo cha baadhi ya wanasiasa ambao hakuwataja majina, kuwa wamekuwa wakizusha madai kuwa Rais aliteua wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, bila kuongozwa na mapendekezo ya wadau mbalimbali waliopendekeza majina hayo.
Alisema bado anaendelea kuamini mchakato wa Katiba mpya utafikia mwisho wake mwaka 2014 na hivyo kuiwezesha Tanzania kufanya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, chini ya Katiba mpya.

Alisema hana tatizo na watu wanaopinga sera za serikali ama hata kumpinga yeye binafsi, bali tatizo lake ni wanasiasa na wanaharakati wanaochochea ghasia, fujo na uvunjifu wa amani.

Rais Kikwete, aliyasema hayo juzi, mjini San Rafael, California, nchini Marekani, wakati alipokutana na kuzungumza na jumuia ya Watanzania waishio katika Jimbo la California.

Katika hotuba yake, ambayo alizungumzia mambo mbalimbali, Rais Kikwete aligusia mjadala wa karibuni bungeni kuhusu mchakato wa Katiba mpya na kusema kuwa alishangazwa na madai kuwa yeye kama Rais, hakuongozwa na mapendekezo ya wadau wakati anateua Tume ya Katiba.

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI SEPTEMBA 19, 2013

DSC 0013 2232e
DSC 0014 fd5f3

MATOKEO KAMILI LIGI KUU TANZANIA

1111 1e313
YANGA 1 - 1 Prisons,
SIMBA 6 - 0 Mgambo
Kagera 2 - 1 JKT Oljoro (HM)
Azam 1 - 1 Ashanti
Coastal 1 - 1 Rhino
Mtibwa 0 - 0 MBEYA City
Ruvu Shooting 1 vs 0 JKT Ruvu. Chanzo: Shaffihdauda

ANGALIA VIDEO YA LINAH AKIFUNGUKA JUU YA PENZI LAKE NA AMINI




Msanii wa muziki wa bongo fleva ambaye sasa ni mjasiriamali pia Anasteria Sanga Linah au muite Ndege Mnana amefunguka kuwa producer wa studio ya Bhitz Pancho Latino ndiye mwenye siri nzito ya penzi lake na msanii mwenzake Amini ambaye kwasasa penzi lao limekuwa stori ya kale baada ya kuachana. Linah amesema tokea wanaanza mapenzi yao Pancho ndiye alikuwa mtu pekee anayejua mambo mengi kuwahusu wao na jinsi walivyotumbukia katika penzi ambalo anasema yeye binafsi ndiye hasa alikuwa akimpenda Amini kupita kiasi japo baadaye akagundua kuwa hata mwenzake naye anamzimika na hivyo penzi likawa linasonga.

"Yaani we muulize Pancho yule ndio ana siri kubwa sana ya penzi langu na Amini,yaani jamani nilimpenda sana Amini mpaka nikakubali kuingia kwenye mapenzi na nilimpenda hasa kutoka moyoni,kuna vitu vingi nyuma yake ambavyo Pancho anajua",alisema Linah.

Msanii huyo mwenye sauti tamu kiasi cha kupachikwa jina la Ndege Mnana na msanii mkongwe Patricia Hillary ameendelea kufunguka kuwa wakati ameangukia katika penzi la Amini alikuwa anawachomolea wanaume wengi waliokuwa wanamtokea tena wenye pesa zao na wengine ni watu wazito lakini aliamua kutoka moyoni kwa dhati kuwa na Amini kwahiyo akawa anamtunzia heshima yake.

RIPOTI YA GAZETI LA RAIA MWEMA KUHUSU KUACHIWA HURU KWA AGNES MASOGANGE NA MELISA HUKO AFRIKA KUSINI..!!

WATANZANIA wawili, Agnes Gerald (Masogange) na mwenzake Melissa Edward waliokamatwa nchini Afrika Kusini kwa madai ya kusafirisha kilo 150 za dawa za kulevya wanayo nafasi kubwa ya kuachiwa wakati wowote kuanzia sasa, Raia Mwema limeambiwa.
 
Ingawa ripoti za awali zilieleza kwamba Watanzania hao walikuwa wamesafirisha kilo 150 za dawa aina ya Crystal Methamphetamine zenye thamani hiyo nchini Afrika Kusini wakati zikisafirishwa kutoka Tanzania, imebainika kwamba adawa walizobeba zinafahamika kwa jina la Ephedrine ambazo hazimo katika kundi la dawa za kulevya.
 
Watanzania hao walikamatwa nchini Afrika Kusini katika Uwanja wa Ndege wa Oliver Tambo jijini Johannesburg wakiwa na dawa hizo zilizokadiriwa kuwa na thamani ya Sh bilioni 6.8.
 
Hata hivyo, Ephedrine –dawa ambayo sasa imebainika kuwa ndiyo waliyosafirisha akina dada hao inaangukia katika kundi la vibashirifu (precursors) yaani dawa ambazo malighafi yake inaweza kutumika kutengeneza dawa za kulevya.

NAPE AWACHONGANISHA CHADEMA NA WAKULIMA WA PAMBA

blog_756b7.jpg
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa wilaya ya Bariadi kwenye Viwanja vya Sabasaba. Adai wamechukizwa na viwanda vya nguo,nyuzi ,nyama na ajira.
-Asema misaada ya China ni ukombozi mkubwa unaowakera Chadema.
-Awataka kanda ya ziwa kuujua unafiki huo wa Chadema.

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa CCM Nape Nnauye ameeleza kusikitishwa kwake na hatua ya Chadema kukerwa na hatua za Balozi wa China na serikali ya China kwa ujumla katika kushiriki katika hatua za kuwakwamua watanzania katika umasikini.

Nape alisema hayo jana alipokuwa akiwahutubia wananchi wa mji wa Bariadi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya CCM sabasaba Mkoani Simiyu. Alisema hoja kuwa ambayo imewakera na kuwasumbua Chadema ni hatua zinazochukuliwa hivi sasa kwa pamoja kati ya Serikali ya CCM na Serikali ya China ambayo hivi sasa inaelekea kuzaa matunda ya kutoa mwanya wa ajira zaidi ya elfu- 25 viwandani.

WABUNGE WA NIGERIA WAPIGANA BUNGENI

nigerian-parliament_bc42b.jpg
Wabunge wa bunge la waakilishi Nigeria wamerushiana ngumi wakati wa vikao vya Jumanne baada ya kuzuka bungeni suitofahamu kuhusu mrengo wa wabunge waliojitenga na chama tawala. Taarifa hizi ni kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo.
Kituo kimoja cha kibinafsi cha televisheni, pamoja na vituo vingine vilionyesha picha za mbunge mwanamke akimtosa kidole usoni kwa ghadhabu mbunge mwenzake wakati mbunge mwanamume akionekana akichukua kiti nusura kumgonga mwenzake.


Wabunge wengine walionekana wakipigana ngumi.
Mgogoro inasemekana ulianza baada ya mwenyekiti wa mrengo wa wabunge waliojiondoa kutoka kwa chama tawala, Kawu Baraje, kuingia bungeni akiandamana na magavana wanaomuunga mkono.
Inaarifiwa spika wa bunge la waakilishi ,Aminu Tambuwal, aliambia wabunge kuwa Baraje aliomba ruhusa kuwahutubia wabunge wa mrengo wake kabla ya bunge kuanza vikao vyake.
Lakini kuwepo kwa wabunge hao bungeni kuliwaghabisha mno wafuasi wa chama tawala, PDP,kiasi cha kuzuka sokomoko bungeni kati ya pande hizo mbili na kumlazimisha bwana Baraje kukatiza hotuba yake kutokana na kelele bungeni.
Chama tawala PDP kina wabunge wengi zaidi bungeni wakiwa 23 kati ya wabunge wote 36
Aidha chama hicho kimetawala Nigeria tangu kupata uhuru mwaka 1999 lakini hivi kribuni kimezongwa na migogoro ya ndani ya chama pamoja na kukabiliwa na upizani wenye ushawishi.
Wananchi wanajiandaa kwa uchaguzi mwaka 2015, lakini wadadisi wana wasiwai ikiwa chama tawala kitakuwa kimesuluhisha migogoro yake, huku kikikabiliwa na upinzani mkali.
Mgogoro huu umekuwa ukitokota kwa miezi kadhaa huku baadhi ya wabunge wakitofautiana kuhusu ikiwa Rais Goodluck Jonathanaidhinishwe na chama kugombea urais kwa mara nyingine wakati kuna wanasiasa wengine wanaotaka kugombea urais.
Hii ni mara ya kwanza kwa wabunge wa Nigeria kurushiana ngumi bungeni.

Wednesday, September 18, 2013

TANZANIA YAMEGWA EAC

*Rwanda, Kenya, Uganda na Burundi zaungana kuunda Shirikisho la Kisiasa
*Waziri Sitta asema zina ajenda ya siri, ashangaa marais kuwaburuza wananchi wao

HATIMAYE Tanzania imewekwa kando rasmi na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), katika kuunda Shirikisho la Kisiasa litakaloziongoza nchi hizo.

Tayari marais wa nchi hizo, Paul Kagame wa Rwanda, Yoweri Museveni wa Uganda, Uhuru Kenyatta wa Kenya na Pierre Nkurunzinza wa Burundi wamekwishafikia makubaliano ya kuanzisha mchakato wa kuandikwa kwa Rasimu ya Katiba ya Shirikisho la Kisiasa la nchi wanachama wa EAC, bila kuishirikisha Tanzania.

Waziri wa Serikali za Mitaa wa Rwanda, James Musoni, amekaririwa na vyombo vya habari vya nchi hiyo akieleza kuwa makubaliano ya kuanzishwa kwa mchakato wa kuandikwa kwa Rasimu ya Katiba ya Shirikisho la Afrika Mashariki, yalifikiwa Septemba 12 mwaka huu, mjini Kampala na marais wa Rwanda, Kenya na Uganda na hivi karibuni Rais wa Burundi ambaye alialikwa katika mkutano huo na kushindwa kuhudhuria, naye sasa amethibitisha ushirika wake katika shirikisho hilo jipya.

Gazeti la The Sunday Times la Rwanda, limemnukuu Waziri Musoni kuwa marais wa nchi hizo wamekubaliana kukamilisha rasimu hiyo ndani ya muda mfupi.

SERIKALI YATOA ONYO KALI KWA BALOZI WA CHINA ALIYEHUDHURIA MKUTANO NA WA CCM

Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, imehadharisha mabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini, kuepuka kujihusisha na mambo ya ndani.

Hadhari hiyo imetolewa jana katika taarifa ya wizara hiyo kwa vyombo vya habari, baada ya Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China, Lu Younqing, kuonekana katika mkutano wa hadhara wa CCM, akiwa amevalia kofia yenye nembo ya chama hicho.

“Wizara inaelekeza kwamba kitendo cha Balozi yeyote kuhudhuria mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa, na kuvaa sare zenye nembo ya vyama vya siasa, sio sahihi na kinakiuka Mkataba wa Vienna wa mwaka 1961, unaoongoza uhusiano wa 
kidiplomasia.

“Mkataba huo wa Vienna unazuia wawakilishi wa nchi za nje kujihusisha na masuala ya ndani ya nchi, ikiwemo siasa wanapofanya kazi zao katika nchi za uwakilishi,” ilieleza taarifa hiyo iliyotumwa na msemaji wa wizara hiyo, Mkubwa Ally.

Taarifa hiyo pia ilieleza kuwa hata Sheria ya Diplomasia ya Tanzania ya Mwaka 1986, ambayo ni zao la Mkataba wa Vienna, pia hairuhusu Balozi au mfanyakazi wa Ubalozi, kujihusisha na masuala ya ndani ya nchi.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO SEPTEMBA 18, 2013

DSC 0013 c0ea2
DSC 0014 12cc6

MSEMAJI WA BROTHERHOOD AKAMATWA MISRI

misri b89cf
Msemaji rasmi wa vuguvugu la Muslim Brotherhood amekamatwa nchini Misri. Hii ni kwa mujibu wa vyombo vya habari vya serikali
Gehad al-Haddad alikamatwa akiwa na mwanachama mwingine mmoja wa vuguvugu hilo katika nyumba moja mjini Cairo.
Taarifa zinazohusianaMisri
Bwana Haddad aliwahi kuhudumu kama afisa wa ngazi ya juu wa naibu mkuu wa majeshi, Khairat al-Shater, wa vuguvugu hilo na kawaida alizungumza na vyombo vya habari vya kigeni.
Serikali ya Misri imekuwa ikifanya msako dhidi ya makundi ya kiisilamu tangu jeshi kumwondoa mamlakani aliyekuwa rais Mohammed Morsi mwezi Julai.
Awali, mahakama ya uhalifu mjini Cairo, iliamua kuwa mali zote za viongozi wa vuguguvu hilo pamoja na lile la Gamaa Islamiya kupigwa tanji.
Viongozi wa mashtaka waliwaekea vikwazo maafisa wa ngazi ya juu wa Brotherhood akiwemo, Mohammed Badie, Shater na wengine wengi mnamo mwezi Julai.
Wengi wao wamezuiliwa kuhusiana na madai ya kuchochea ghasia na mauaji.
Mamia ya watu wanataka Bwana Morsi kurejeshwa mamlakani , wengi wakiwa wanachama wa Brotherhood .
Aidha makabiliano yaliyotokea mwezi jana kati na polisi na wafuasi wa Morsi yalisababisha vifo vya wanachama wengi pale polisi walipovamia kambi zao mbili walipokuwa wanataka Morsi kurejehswa mamlakani. Chanzo: bbcswahili

BABU WA MIAKA 95 AMUOA BABU MWENZIE WA MIAKA 65



Wanaume wawili wazee ambao ni maaskari wakongwe walioshiriki vita ya pili ya dunia, ijumaa iliyopita (September 13) walifunga ndoa ya jinsia moja (mashoga) baada ya kuwa katika uhusiano kwa miaka 20 kabla ya kufikia uamuzi wa kuoana.
gays-1

John Banvard mwenye miaka 95 alimuoa Gerald Nadeau mwenye miaka 67 huko Diego, California Marekani.

RPF CHAIBUKA NA USHINDI NCHINI RWANDA

zkagame_32c2c.jpg
Chama tawala nchini Rwanda, RPF kimeibuka mshindi katika uchaguzi wa wabunge uliofanyika Jumatatu.
Chama hicho chake Rais Paul Kagame kimeshinda uchaguzi huo kwa asilimia 76 ya kura zote zilizopigwa .
Aidha chama hicho kiliingia mamlakani baada ya mauaji ya kimbari yaliyofanyika mwaka 1994 na kimepata viti 40 kati ya 53 vilivyokuwa vinawaniwa.


Chama cha upinzani, FDU-Inkingi, ambacho kiongozi wakeVictoire Ingabire yuko jela, hakikushiriki uchaguzi huo kwani hakijasajiliwa rasmi.
Vyama vingine viwili vya kisiasa vinavyosemekana kuwa washirika wa RPF, vilipata asilimia 13 na asilimia tisa ya kura.
Shughuli ya kupiga kura ilifanyika siku mbili baada ya vifo vya watu wawili kutokana na shambulio la maguruneti mjini Kigali.

MAGUFULI AAGIZA VITUO VYA MIZANI YA BARABARANI MKOANI IRINGA VICHUNGUZWE


Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli (pichani) ambaye yuko katika ziara ya kikazi mkoani Iringa ameagiza kufanyika kwa uchunguzi kuhusu utendaji wa vituo vya mizani mkoani Iringa. Agizo hilo lilitolewa katika mkutano ambao Waziri huyo wa Ujenzi alikutana na wafanyakazi wa taasisi zinazosimamiwa na Wizara ya Ujenzi mkoani humo.

Wakati akisomewa taarifa za utekelezaji wa majukumu ya kila taasisi mkoani humo ndipo lilipojitokeza suala la tozo iliyokusanywa kwa magari yaliyokamatwa yakiwa yamezidisha uzito kwa kipindi cha mwezi mmoja wa Julai mwaka huu wa 2013 katika kituo cha mizani cha Wenda kilichopo kati ya Iringa na Ifunda katika barabara kuu ya TANZAM.


Meneja wa Tanroads wa mkoa wa Iringa Injinia Poul Lyakurwa alimtaarifu Waziri Magufuli kuwa kiasi cha Shilingi milioni 31.9 kilikusanywa katika kipindi hicho cha mwezi mmoja.
 
Akishitushwa na kiwango hicho Waziri Magufuli  alibainisha kuwa, kiasi hicho kilichosomwa katika taarifa kimetokana na magari 735 yaliyokamatwa kati ya magari 20,700 yaliyopimwa sawa na asiliamia 3.5. “Takwimu hizi sizikubali kwani wastani wa magari yanayokamatwa katika nchi nzima unakaribia asiliamia 40 iweje barabara kuu kama hii iwe na kiwango kidogo kiasi hicho cha magari yaliyokutwa na makosa” hapa ni lazima pafanyike uchunguzi” alisisitiza Mheshimiwa Magufuli na kueleza kuwa hali hiyo hawezi kuiruhusu hata kidogo kuendelea.

KIGOGO WA MAGARI YA WIZI TZ ANASWA....!!!


Jengo ambalo linadaiwa ndiyo kiwanda hatari cha kubadilisha magari ya wizi, kimefumuliwa na mmiliki wake sasa hivi yupo nyuma ya nondo akingoja kufikishwa mahakamani.
 
Kigogo wa magari ya wizi, Benovilla Luhanga baada ya kunaswa.
Benovilla Luhanga, 43, ametajwa kuwa ndiye mmiliki wa kiwanda hicho na siku ananaswa, alikutwa na magari ya kihafari matano ambayo yote inadaiwa ni ya wizi.
Vilevile, Luhanga alikutwa na Bajaj moja ambayo imedaiwa nayo ni ya wizi na kwamba alikuwa tayari ameshaibadili rangi.
Luhanga alikamatwa akiwa na mkewe ambaye jina lake halikupatikana mara moja.
 
Moja ya gari alilokutwa nalo mtuhumiwa.

KESI YA MAKAMU WA RAIS KENYA, SHAHIDI WA KWANZA ATOA USHAHIDI ICC

zruto_fecef.png
Shahidi wa kwanza kutoka upande wa mashtaka, amefika mbele ya mahakama ya kimataifa ICC kutoa ushahidi dhidi ya naibu Rais wa Kenya William Ruto.
Mahakama inamlinda shahidi huyo kwa kutoonyosha sura yake.
Ruto anakabiliwa na tuhuma za ukiukwaji wa haki za binadamu wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi nchini Kenya mwaka 2007-2008
Kesi dhidi ya Ruto na mshtakiwa mwenzakeJoshua Arap Sang, ilianza tarehe 10 mwezi Septemba, baada ya wawili hao kutuhumiwa katika kuhusika na ghasia hizo za mwaka 2007.
Kumekuwa na wasiwasi kuhusu mashahidi kujiondoa kwenye kesi hiyo wakihofia usalama wao. Mwishoni mwa wiki, mashahidi wanne walijiondoa katika kesi hiyo baada ya kuelezea wasiwasi kuhusu usalama wao ikiwa watatoa ushahidi mbele ya mahakama hiyo.
Wiki jana mkuu kwenye kesi hiyo, aliakhirisha kesi hiyo kwa sababu mashahidi hawakuwa wamefika kwenye mahakama hiyo kutoa ushahidi wao.
Rais Uhuru Kenyatta, anatarajiwa kufika mbele ya mahakama hiyo mwezi Novemba kwa mashtaka sawa na hayo.

MADEREVA WA BODABODA DAR WAUA JAMBAZI

MAJAMBAZI wawili wameuawa katika matukio mawili tofauti Dar es Salaam akiwamo mmoja aliyeuawa na madereva wa pikipiki katika eneo la Vingunguti karibu na kituo cha mafuta. Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema jana kuwa majambazi wapatao wanne walimvamia mfanyabiashara Abas Mussa (47) wa Vingunguti wakiwa na bunduki na mapanga.

Alisema mfanyabiashara huyo akiwa dukani kwake, ghafla walifika vijana wawili, mmoja akiwa na bunduki fupi na mwingine akiwa na panga na kumpora mwenye duka Sh 1,400,000.

Pia walimpora simu moja ya Nokia na ufunguo wa gari na alipotoka nje ya duka alisikia mlio wa bunduki na kumuona mfanyakazi wake Ally akiwa chini na watu wengi wakiwa wamejikusanya.

Alisema baada ya tukio hilo kutokea madereva wa pikipiki waliwaona majambazi hao na kuwafukuza na walipofika njia panda ya Tabata Relini walimkamata jambazi mmoja na kuwashambulia hadi kumjeruhi.

Kamanda alisema polisi walipata taarifa na walipofika eneo la tukio walimkuta jambazi huyo akiwa na hali mbaya. Walimchukua na kumpeleka hospitali lakini alifariki dunia akiwa njiani.

Alisema jambazi mmoja alikimbia baada ya kuacha pikipiki ya Sunlag na polisi waliweza kuwakamata waliokimbia baada ya tukio hilo.

Katika tukio jingine, jambazi mmoja aliuawa na polisi wakati majambazi sita walipojaribu kupora mamilioni ya fedha katika mtaa wa Jamhuri Kitumbini.

Tuesday, September 17, 2013

MWANAMUZIKI WA TAARAB AHMED MGENI AFARIKI DUNIA LEO ALFAJIRI

 
Mwimbaji wa kundi la Zanzibar Njema Mordern Taarab Ahmed Mgeni amefariki dunia leo alfajiri (September 17) katika Hospitali ya Mnazi mmoja, Kisiwani Zanzibar alikolazwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kifua.

Akiongea katika kipindi cha Leo Tena ya Clouds Fm mkurugenzi mwenza wa Zanzibar Njema Modern Taarab Ally Ngereja amesema msiba uko Amani Fresh, Zanzibar ambapo ni kwa baba yake na atazikwa leo (September 17) saa kumi jioni.

Marehemu aliwahi kutamba na nyimbo nyingi ikiwemo sitetereki inayofanya vizuri mpaka sasa.

KESI YA SHEIKH PONDA, AKOSA DHAMANA, KESI YAHAIRISHWA HADI OKTOBA 1

ponda_26617.jpg
Sheikh Ponda Akishuka kwenye basi la Magereza tayari kuingia Mahakamani Kusikiliza kesi yake inayomkabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoani Morogoro. Sheikh Ponda alishatikiwa katika Mahakama Hiyo akikabiliwa na Mashtaka Matatu Ambayo inadaiwa aliyatenda Mkoani Morogoro katika Mkutano Hadhara mwezi uliopita. Kesi hiyo imearishwa tena Mpaka Tarehe 01.10.2013. Sheikh Ponda amenyimwa Dhamana na amerudishwa Rumande.

WATUHUMIWA WA MAUAJI YA BILIONEA ERASTO MSUYA WAKUTWA KWA SANGOMA

Jeshi la polisi mkoa wa kilimanjaro linawashikilia watu wanne zaidi wakidaiwa kuhusika na mauaji ya mfanyabiashara bilionea wa madini ya tanzanite Arusha Erasto Msuya 43 wawili kati yao walikutwa kwa mganga wa kienyeji (sangoma) wakifanyiwa zindiko ili wasikamatwe na vyombo vya dola.

Pia jeshi limenikiwa kunasa bunduki aina ya SMG yenye namba za usajili KJ10520,inayoaminika kutumika katika mauaji hayo.Msuya aliuawa kwa kupingwa risasi zaidi ya 10 kifuani Augost 7mwaka huu,katika eneo la mijohoroni wilayani Hai.

Akizungumza na waandishi wa habari jana,kamanda wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Robert Boaz aliwataja watuhumiwa kuwa ni Sadiki Jabiri 32 mkazi wa Dar es Salaam na Lang'angata wilayani Hai .

KINANA AMPONZA BALOZI WA CHINA... CHADEMA KUMSHITAKI KWENYE MAHAKAMA YA KIMATAIFA

http://3.bp.blogspot.com/-tB-YS2RGEHk/UjfrTKmUq2I/AAAAAAAAl3k/wO2eYdRF-0M/s1600/1.png
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema kitamshitaki Balozi wa China nchini, Lu Younqing Umoja wa Mataifa (UN) kwa kukiuka Mkataba wa Vienna (Vienna Convention) wa mwaka 1964 ambao unaeleza uhusiano wa kibalozi kati ya nchi na nchi.

Aidha, kimesema kitaiandikia barua Serikali ya China ili kutaka ufafanuzi kama imemtuma Balozi wake kufanya kazi ya uenezi siasa kwenye vyama.


Tukio la Balozi huyo kuhudhuria mkutano wa hadhara wa CCM lilitokea Septemba tisa mwaka huu kwenye mkutano wa chama hicho uliofanyika Wilaya ya Kishapu Shinyanga, ambapo Katibu Mkuu wake, Abdulrahman Kinana alimtambushisha balozi huyo huku akiwa amevaa sare za chama hicho.


Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Waziri kivuli wa mambo ya nje ambaye pia ni Mbunge wa Nyamagana Jijini Mwanza, Ezekiel Wenje alisema Chadema wameamua kuchukua hatua hizo ili kukomesha vyama vya siasa kutumia mabalozi kama wawakilishi wa vyama vyao kwa kufanya uenezi kwenye mikutano ya siasa.

HATMA YA DHAMANA YA PONDA LEO...!!!

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Morogoro, leo inatarajiwa kuamua iwapo Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Shekhe Ponda Issa Ponda, anastahili dhamana au la, kutokana na kesi inayomkabili.  
Shekhe Ponda alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Agosti 19 na kusomewa mashitaka matatu ya uchochezi yanayomkabili. Upande wa mashitaka ulidai mahakamani hapo kuwa utaleta mashahidi 15 na vielelezo vitatu, ili kuthibitisha mashitaka hayo. 
Baadhi ya vielelezo vitakavyotolewa mahakamani hapo ni pamoja na DVD mbili, kibali kilichotolewa Agosti mosi cha kongamano la Kiislamu, kutoka kwa Mkuu wa Polisi Wilaya ya Morogoro (OCD) na Hati ya Hukumu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. 
Kesi hiyo ya jinai namba 128 ya mwaka 2013, iko mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa Morogoro, Richard Kabate. Shekhe Ponda katika kesi hiyo, anatetewa na mawakili watatu wakiongozwa na Wakili Juma Nasoro, wakati upande wa mashitaka, ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Benard Kongola.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE SEPTEMBA 17, 2013

DSC 0094 87348
DSC 0095 5e40c
DSC 0096 f0fee

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...