Tuesday, September 17, 2013

MWANAMUZIKI WA TAARAB AHMED MGENI AFARIKI DUNIA LEO ALFAJIRI

 
Mwimbaji wa kundi la Zanzibar Njema Mordern Taarab Ahmed Mgeni amefariki dunia leo alfajiri (September 17) katika Hospitali ya Mnazi mmoja, Kisiwani Zanzibar alikolazwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kifua.

Akiongea katika kipindi cha Leo Tena ya Clouds Fm mkurugenzi mwenza wa Zanzibar Njema Modern Taarab Ally Ngereja amesema msiba uko Amani Fresh, Zanzibar ambapo ni kwa baba yake na atazikwa leo (September 17) saa kumi jioni.

Marehemu aliwahi kutamba na nyimbo nyingi ikiwemo sitetereki inayofanya vizuri mpaka sasa.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...