Thursday, April 05, 2018

ALIEKUWA RAIS KUFUNGWA MIAKA 12 JELA

Mahakama ya rufaa nchini Brazil leo imeagiza aliekuwa rais wa nchi hiyo, Luiz Inacio Lula da Silva kuwa ni sharti aanze kutumikia kifungo chake cha miaka kumi na mbili gerezani, baada ya kupatikana na hatia ya kuhusika katika ufisadi.
Majaji sita kati ya kumi na mmoja wa mahakama ya rufaa walipinga rufaa hiyo huku watano kati yao wakimuunga mkono. Kesi hiyo imezua hali ya wasi wasi wa kisiasa nchini humo.

Lula amekutwa na hatia kutokana na uchunguzi wa muda mrefu wa sakata la rushwa linalojulikana kama ”Operation Car Wash" Lula aligundulika kukubali rushwa yenye thamani Euro laki 7.

WAZIRI ATAJA HATUA ZINAZOCHUKULIWA NA SERIKALI KUFIKIA UCHUMI WA VIWANDA

 Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Paramagamba Kabudi akizungumza na wadau wa utafiti wakati akifungua Warsha ya siku mbili kwa watafiti wa Tanzania na kutoka nje iliyoandaliwa na Tasisi ya Utafiti ya REPOA jana jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi  Amina Salim Alli akizungumza wakati anaongoza mjadala juu ya Uchumi wa Viwanda kufikia 2025
 
Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi amesisitiza  Serikali ya Awamu ya Tano inaendelea na hatua  za kuhakikisha kunakuwepo mazingira wezeshaji yatayofanikisha ujenzi wa viwanda nchini. 

Prof.Kabudi amesema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akifungua warsha ya utafiti iliyoandaliwa na Taasisi ya Utafiti ya REPOA ambapo mada kuu ilikuwa kujadili kuelekea jamii inayoendeleza viwanda 2025 kwanini ushindani ni muhimu.

Pia kwenye warsha hiyo wadau wamejadili masuala ya kisera katika safari ya Tanzania kuelekea kwenye uchumi mseto na shindani, ukiongozwa na viwanda, pamoja na kufikia nchi yenye kipato cha kati ifikapo mwaka 2025 kama inavyotarajiwa kwenye dira ya Taifa ya Maendeleo 2025.

ZITTO KUMPELEKA NONDO UHAMIAJI KUHOJIWA

Mbunge wa Kigoma mjini Zitto Kabwe amesema atamsindikiza kiongozi wa mtandao wa wanafunzi Abdul Nondo katika makao makuu ya uhamiaji Tanzania.
Hii ni baada ya taarifa iliotoka mtandao huo ambayo ilieleza kuwa Nondo alipata barua ya kuitwa na uhamiaji ili 'akahojiwe kuhusu taarifa za uraia wake pamoja na za ndugu zake'.

Taarifa hizo zilisema 'afisa uhamiaji mkoa alitamka kuwa sheria inawaruhusu kumuhoji mtu yeyote wanaotilia mashaka uraia wake. Na kuwa wanamashaka na uraia wa Abdul Nondo,hivyo awathibitishie kuwa yeye ni Raia wa Tanzania'.

SOMA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS APRIL 05, 2018 YA UDAKU, MICHEZO NA HARDNEWS




Wednesday, April 04, 2018

TAZAMA MUONEKANO MPYA WA MBOWE BAADA YA KUKAA MAHABUSU KWA SIKU SABA



Baada ya kukaa mahabusu kwa siku saba na kusherehekea sikuu ya Pasaka wakiwa gerezani, Mwenyekiti wa Chadema Taifa  Mhe. Freeman Mbowe pamoja na vigogo wengine sita wa chama hicho leo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia kwa dhamana, baada ya kukamilisha masharti.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRIL 04, 2018 YA UDAKU, MICHEZO NA HARDNEWS





KIKWETE AINGILIA KATI AFYA YA MZEE MAJUTO, HII HAPA AHADI YAKE

LICHA ya kufanyiwa upasuaji wa tezi dume bado hali ya staa wa filamu za Kibongo, Amri Athuman ‘Mzee Majuto’ ni tete ambapo Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dk Jakaya Mrisho Kikwete ‘JK’, amejitosa baada ya kumuona alivyodhoofu kwa sasa.

JK na Mzee Majuto walikutana uso kwa uso wikiendi iliyopita katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar ambako kulikuwa na shughuli ya utoaji tuzo za filamu zilizojulikana kwa jina la Tuzo za Kimataifa za Sinema Zetu ambapo walionekana wakiteta kwa dakika kadhaa kabla ya kila mmoja akaenda kukaa kwenye siti yake.

Mzee Majuto alionekana akiwa amedhoofu kwani aliingia ukumbini akitembea kwa msaada wa fimbo huku akionekana kutokuwa mchangamfu kama ilivyo kawaida yake, hali iliyowahuzunisha mashabiki wake waliokuwa ukumbini hapo.

AGNES MASOGANGE AKWEPA KWENDA JELA BAADA YA KULIPA FAINI

Msanii wa kupamba video za muziki (Video Queen), Agnes Gerald ‘Masogange’ amekwepa kifungo cha miaka mitatu jela baada ya kulipa faini ya Sh. milioni 1.5.

Msanii maarufu nchini, Agnes Gerald maarufu Masogange alikutwa na hatia ya kutumia dawa za kulevya na kuhukumiwa kwenda jela au kulipa faini.

 Hakimu wa Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu, Wilbard Mashauri, ametoa hukumu hiyo leo Aprili 3 na kuieleza mahakama kuwa Masogange katika kosa la kwanza amekutwa na hatia ya kutumia dawa za kulevya aina ya heroin na kosa la pili kutumia dawa za kulevya aina ya Oxazepam.

“Hivyo katika kosa la kwanza, mahakama inamhukumu kwenda jela miaka miwili au kulipa faini ya Sh1 milioni na kwa kosa la pili, amehukumiwa kwenda jela miezi 12 au kulipa faini ya Sh 500, 000,” amesema Hakimu Mashauri.

Februari 17 mwaka jana, aliyekuwa Kamanda wa polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro aliwaeleza wanahabari kuwa Masogange amepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kupimwa iwapo anatumia dawa hizo za kulevya.

NUKUU SITA (6) MAARUFU ZA WINNIE MANDELA ENZI ZA UHAI WAKE

Winnie Madikizela-Mandela, ex-wife of former South African President Nelson Mandela, arrives at the Union Buildings in Pretoria 27 April 2004 for the inauguration of President Tahbo Mbeki second and final term as the country celebrated the 10th anniversary of the end of apartheid. 
Winnie Madikizela-Mandela enzi za uhai wake.
 
Mwanasiasa na mwanaharakati aliyepigana dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi Afrika Kusini Winnie Madikizela-Mandela alifariki dunia Jumatatu akiwa na miaka 81.

Alikuwa mke wa zamani wa rais wa kwanza mweusi Afrika Kusini Nelson Mandela lakini alikuwa na msimamo mkali zaidi kumshinda hata Bw Mandela mwenyewe. Winnie alifahamika sana na wengi kama Mama wa Taifa.
Winnie Mandela, former wife of former South African President Nelson Mandela attends the opening of the 53rd National Conference of the African National Congress (ANC) on December 16, 2012 in Bloemfontein.
Winnie alikuwa nembo kuu ya vita dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi, na ingawa sifa zake ziliingia doa miaka ya baadaye, lakini bado alitambuliwa kama mtetezi wa wanyonge.

Tuesday, April 03, 2018

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMANNE APRIL 03, 2018 YA UDAKU, MICHEZO NA HARDNEWS

Tunapenda kuwataarifu wadau wetu kuwa hivi karibuni tutapatikana kwa website ya jambotz.co.tz

MBOWE NA WENZIE KUACHIWA LEO...??!

Viongozi sita wa Upinzani nchini (CHADEMA) wanatarajiwa kuachiliwa kutoka kizimbani baada ya kulipa dhamana, siku ya Alhamisi.

Viongozi hao akiwemo mwenyekiti Freeman Mbowe, walishtakiwa kwa uchochezi, kuleta vurugu na kuandamana mwezi wa Februari mwaka huu.

Alhamisi iliopita, mahakama ya hakimu mkazi Kisutu iliwapatia dhamana viongozi hao sita lakini kusema kuwa watasalia rumande hadi kesi leo tarehe 3 Aprili ambapo wataletwa mahakamani kukamilisha masharti ya dhamana.

Wanasiasa hao hawakuletwa mahakamani katika uamuzi wa dhamana yao huku afisa wa magereza akiiambia mahakama ni kutokana na gari lililotakiwa kuwasafirisha kuja mahakamani hapo kuwa bovu.

Miongoni mwa mashtaka waliyosomewa ni pamoja na maandamano yaliyosababisha kifo cha mwanafunzi wa chuo cha NIT Akwilina Akwiline. Wanashtakiwa pia kuendelea kufanya mkusanyiko usio halali wilayani Kinondoni shtaka linalowakabili washtakiwa wote.

Monday, April 02, 2018

TAZAMA PICHA ZA NDEGE MPYA YA TATU AINA YA BOMBARDIER Q400 IKIWASILI NCHINI TOKA CANADA



Ndege ya 3 aina ya Bombardier Q400 imewasili leo nchini toka Canada na kupokelewa na kuzinduliwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli. Tunapenda kuwataarifu wadau wetu kuwa hivi karibuni tutapatikana kwa website ya jambotz.co.tz

MKE WA MANDELA AFARIKI DUNIA AKIWA NA MIAKA 81

Winnie Mandela, mke wa zamani wa Nelson Mandela, ambaye pia alipigana dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi Afrika Kusini amefariki dunia akiwa na miaka 81. Habari za kifo chake zimethibitishwa na msaidizi wake.

Winnie alizaliwa Oktoba 26, 1936 ingawa yeye na mumewe  Nelson Mandela walitalikiana mapema miaka ya 1990, Winnie Madikizela Mandela kama alivyofahamika rasmi alisalia kutoa mchango katika maisha ya Mandela.

Alikuwepo na walishikana mikono alipokuwa akiondoka gerezani baada ya kufungwa kwa miaka 27. Lakini maisha yake pia yalikumbwa na utata. Winnie alikuwa na miaka 20 hivi pale alipojipata katika siasa.

MWIGULU AWAASA MAASKOFU KUHUBIRI INJILI ILI WANANCHI WAWE NA HOFU YA MUNGU KUEPUSHA MATUKIO YA KIKATILI

 Waziri wa Mambo ya Ndani Dk. Mwigulu Nchemba akionesha albam ya "Usife Moyo" ya Rose Muhando, kulia ni Mkurugenzi wa Msama Promotion Alex Msama na Kushoto ni Rose Muhando wakishiriki tukio hilo katika Tamasha la Pasaka lililofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza jana jioni
 Waziri wa Mambo ya Ndani,Dkt Mwigulu Nchemba akipokelewa na Mkuu wa Mkoa Mwanza Mh. John Mongela mara baada ya kuwasili uwanja wa CCM Kirumba,tayari kwa kuzindua tamasha la pasaka kwa mara ya kwanza chini ya Kampuni ya Msama Promotions Ltd sambamba na uzinduzi wa albamu ya Muimbaji nyota wa muziki wa Injili Rose Muhanda iitwaya 'Usife Moyo' yenye jumla ya nyimbo saba. 
 Baadhi ya Wakazi wa jiji la Mwanza wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri katika tamasha la pasaka mapema jana jioni ndani ya uwanja wa CCM 
Mbunge wa Jimbo la Ilemela mkoani Mwanza ambae pia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mh. Angelina Mabula akimtunza muimbaji wa nyimbo za injili Christopher Mwahangila mapema jana jioni ndani ya tamasha la pasaka.

Waziri Wa mambo ya ndani Mhe. Dkt Mwigulu Lameck Nchemba amewasihi viongozi mbalimbali wa dini nchini wakiwemo Maaskofu na Mashekh kutumia muda wao mwingi kwa kutembelea mikoa mbalimbali nchini kunapotokea zaidi matukio ya kikatili ikiwemo mauaji ili kuhubiri injili wananchi wawe na hofu na Mungu jambo litakalopelekea kupunguza ukatili na watu kumjua Mungu.

TANZANIA YASHIKA NAFASI YA 13 KWA NCHI ZINAZOVUTIA UWEKEZAJI


Shirika la Utafiti la Quantum Global limetoa ripoti ya nchi ambazo zinaongoza kwa kuvutia uwekezaji barani Afrika ambapo nchi ya Morocco imeshika nafasi ya kwanza ikifuatiwa na Misri na Algeria.

Nafasi ya nne imeshikwa na Botswana, Ivory Coast nafasi ya tano, Afrika Kusini nafasi ya sita, Ethiopia nafasi ya saba, Zambia nafasi ya nane, Kenya nafasi ya tisa na Senegal ikishika nafasi ya 10.

Ripoti hiyo imeitaja Tanzania kuwa nchi ya 13 kwa kuwa na kuvutia uwekezaji. Nchi 10 ambazo zimetajwa kuwa hazivutii uwekezaji ni;
1. Afrika ya Kati
2. Liberia  
3. Somalia  
4. Eritrea
5. Equatorial Guinea
6. Gambia
7. Sierra Leone
8. Guinea  
9. São Tomé and Príncipe
10. Zimbabwe

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...