Monday, January 05, 2015

IPTL YASHUSHA BEI YA UMEME

Sethi Singh

KAMPUNI ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) ikiwa chini ya uongozi wa Kampuni ya Pan African Power Solutions (T) Limited (PAP), imetangaza kupunguza bei ya umeme kwa asilimia 20 baada ya kufanya marekebisho makubwa ya injini za mtambo.

IPTL pia imetangaza kuwa bei yao ya umeme inatarajiwa kushuka zaidi, kulingana na kushuka kwa bei ya mafuta mazito. Marekebisho hayo yaliyotumia zaidi ya Dola za Marekani milioni 25 ( Sh bilioni 42.5), yamewezesha mitambo ya IPTL kuwa katika nafasi nzuri ya kuzalisha umeme wa uhakika kwa kufikia megawati 100 na kuingiza katika Gridi ya Taifa mara tu baada ya marekebisho yaliyokamilika Desemba mwaka 2014.
Kwa mujibu wa taarifa ya Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni hiyo, Harbinder Singh Sethi, IPTL sasa imepunguza bei ya umeme wake inaoutoza kwa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), ambao sasa utakuwa chini ya bei ya awali iliyokokotolewa ya senti 23 ya dola ya Marekani (Sh 391) kwa kilowati; huku ikihakikisha kupatikana kwa umeme wa uhakika. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO JANUARI 05, 2015

.
.
.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MIILI 37 YA ABIRIA WA AIR ASIA IMEPATIKANA MPAKA SASA

Vikosi vya uokoaji majini wakitafuta miili ya waliokuwa kwenye ndege iliyoanguka 
 
Shirika la uokoaji nchini Indonesia limesema hivi sasa miili 37 imepatikana kutoka kwenye bahari ya Java ambapo ndege ya Air Asia iliangukia mwishoni mwa juma lililopita.
Helikopta na Meli za kijeshi zimekuwa zikifanya doria katika eneo la bahari hiyo ambapo vitu vinavyoelezwa kuwa mabaki ya ndege vimeonekana.hali ya hewa ya eneo hilo kwa sasa imetengemaa ingawa bado mikondo ya bahari ina nguvu.
Vikosi vya wapiga mbizi wa Indonesia na Urusi vina matumaini ya kupata vifaa vya kurekodia mawasiliano ndani ya ndege, ambavyo vitasaidia kujua sababu ya kuanguka kwa ndege hiyo iliyokuwa ikisafiri kutoka Surabaya kwenda Singapore.
Air Asia ilikuwa imebeba Watu 162 ilipopata ajali. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

RAIA WA SYRIA WAPEWA MASHARTI MAGUMU LEBANON

Lebanon imepokea Wakimbizi zaidi ya Wakimbizi milioni moja kutoka nchini Syria 
 
Masharti mapya yamewekwa na mamlaka ya Lebanon kwa Raia wa Syria wanaoingia nchini humo , wakati huu ambapo nchi hiyo inapokea Wakimbizi wengi.
Kwa mara ya kwanza, Raia wa Syria watalazimika kuwa na vielelezo vinavyoeleza kwa nini wanataka kuvuka mpaka na kuingia nchini Lebanon.
Masharti haya mapya yanaanza kutumika siku ya jumatatu.Awali kusafiri kati ya nchi hizo mbili kwa kiasi kikubwa hakukuwa na kikwazo lakini sasa Raia wa Syria lazima wawe na Viza.
Hatua hii inaelezwa kulenga kudhibiti idadi kubwa ya Wakimbizi wanaoingia nchini Lebanon, ambapo kwa sasa Lebanon ina wakimbizi zaidi ya milioni moja.
Hatua hii ya sasa haijulikani italeta athari gani kwa Raia wengi wa Syria walio nchini Lebanon ambao hawajajiandikisha kuwa wakimbizi.
Kabla ya sasa, Raia wa Syria waliweza kukaa nchini Lebanon mpaka miezi sita, lakini sasa raia wa nchi hiyo watalazimika kutimiza vigezo kadhaa ili kupatiwa Viza mpakani. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

YANGA YANG'ARA KOMBE LA MAPINDUZI

Timu ya Yanga ya Dar es Salaam 
 
Michuano ya kuwania Kombe la Mapinduzi Zanzibar, linalozishirikisha timu saba za Zanzibar, nne za Tanzania Bara na KCCA kutoka Uganda imezidi kupamba moto ikiwa katika hatua ya kukamilisha michezo ya makundi.
Timu ya Yanga ya Tanzania Bara imezidi kutoa vipigo kwa timu za kundi lake baada ya kuzicharaza timu za Taifa Jang'ombe na Polisi zote za Zanzibar magoli 4-0 kila moja na hivyo kujikusanyia mabao nane na pointi sita ikiwa haijaruhusu nyavu zake kutikiswa na timu pinzani na hivyo kuongoza kundi A lenye timu za Taifa Jang'ombe, Polisi Zanzibar na Shaba pia ya Zanzibar.
Kwa matokeo hayo imefuzu kucheza hatua ya robo fainali.
Wapinzani wao wakubwa pia kutoka Bara, Simba imekuwa na mwendo wa kusuasua ambapo katika mchezo wake wa kwanza katika kundi C ilicharazwa na Mtibwa Sugar bao 1-0 kabla ya kuzinduka na kujipatia ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mafunzo ya Zanzibar. Katika kundi hilo Simba ina timu za Mtibwa Sugar ya Tanzania Bara, Mafunzo ya Zanzibar na JKU Zanzibar.
Kundi B lina timu za KCCA ya Uganda, Azam ya Tanzania Bara, KMKM na Mtende zote za Zanzibar.
Januari saba michuano hiyo itaingia hatua ya robo fainali kwa timu sita kutoka makundi yote matatu yenye jumla ya timu 12. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

VIGOGO LIGI KUU ENGLAND WATESA FA

 Heka heka katika lango la Hull wakati Arsenal ilipoibuka na ushindi wa 2-0
 
Mechi kadha zimechezwa kuwania kombe la FA kwa vilabu vya ligi kuu ya England na vile vya madaraja mengine.
Mabingwa watetezi Arsenal waliweza kuwacharaza Hull City 2-0 ambao wameshindwa kulipa kisasi baada ya kushindwa katika fainali za mwaka jana timu hizo zilipokutana. Magoli ya Arsenal yalifungwa na Per Mertesacker pamoja na Alexis Sanchez.
Wachezaji wa Chelsea wakipongezana baada ya ushindi 3-0 dhidi ya Watford
Mechi nyingine zilikuwa kati ya Chelsea na Watford, Chelsea ikiibuka na ushindi wa 3-0. Nayo Machester United ikiishindilia Yeovil 2-0. Kwa upande wake Manchester City nao waliibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Shef Wednesday.
Crystal Palace ilipata ushindi mnono dhidi ya Dover wa mabao 4-0, huku Stoke City ikiicharaza Wrexham magoli 3-1. Sunderland nayo ilivuna goli 1-0 dhidi ya Leeds.
Mechi kumi zimechezwa ambapo kwa ujumla vigogo wa soka England wameonekana kupata matokeo mazuri. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

VINARA LA LIGA WAAMBULIA VIPIGO

  Wachezaji nyota wa ligi kuu ya Hispania, Lionel Messi na Cristiano Ronaldo wa Real Madrid
 
Ligi Kuu ya Hispania, La Liga imezidi kuleta ushindani mkubwa baada ya vinara wa ligi hiyo, Real Madrid na Barcelona kupoteza katika mechi zao za mwishoni mwa wiki.
Kikosi cha aliyekuwa kocha wa timu ya Manchester United David Moyes ambaye kwa sasa anainoa timu ya Real Sociedad ya ligi kuu ya Hispania, La Liga, imeiadhibu Barcelona kwa goli 1-0 alilojifunga mwenyewe mchezaji wa Barcelona Jordi Alba, mapema katika dakika ya pili ya mchezo.
David Moyes kocha wa Real Sociedad ya Hispania
Kipigo Real Madrid cha 2-1 kutoka kwa Valencia mapema Jumapili kingewawezesha Barcelona kuelekea mbele katika kinyang'anyiro cha ubingwa wa ligi hiyo endapo timu hiyo ingeshinda.
Lakini kocha Luis Enrique alianza mchezo huo kwa kutowaanzisha wachezaji wake mashuhuri akiwemo Lionel Messi, Neymar na Dani Alves.
Barcelona ilishindwa kusawazisha goli walilojifunga wakati Moyes akipata ushindi wa pili akiwa meneja wa timu ya Sociedad.
Messi, Neymar na Alves walirejea katika mazoezi Ijumaa wiki iliyopita baada ya mapumziko marefu ya Krismasi Amerika Kusini ambako ligi ilisitishwa ili kusherehekea siku kuu hiyo.
Enrique alifanya mchezo wa kubahatisha kwa kutowapanga wachezaji hao katika mchezo wake na Real Sociedad ambayo imekuwa kikwazo kwa Barcelona katika michezo ya nyuma.
Wachezaji wa Real Sociedad wakishangilia goli katika moja ya michezo yao ya ligi kuu ya Hispania
Na kwa hiyo imethibitika kwa mara nyingine kwamba Barcelona hawana chao katika uwanja wa Anoeta sasa ikiwa ni michezo sita, Barcelona ikipoteza kwa Real Sociedad.
Kwa upande wake Real Madrid ilijikuta ikipoteza mchezo wake dhidi ya Valencia baada ya kucharazwa mabao 2-1 licha ya Real Madrid kuongoza kipindi cha kwanza kwa bao la penalti lililofungwa na Cristian Ronaldo dakika ya 14.
Valencia ilijipatia magoli yake yote mawili kipindi cha pili yakifungwa na Barragán dakika ya 52′ na Otamendi dakika ya 65.
Real Madrid inaongoza msimamo wa ligi ya Hispania ikiwa na pointi 39 katika michezo 16 ikifuatiwa kwa karibu na Barcelona yenye pointi 38 baada ya kucheza mechi 17. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Thursday, January 01, 2015

JAMBO TZ TUNAWATAKIA KHERI YA MWAKA MPYA 2015


 Asante kwa kutembelea Blog na pia ku-like page yetu ya facebook, endelea kuwa nasi siku zote ili upate habari nzuri na za uhakika kutoka kila kona ya dunia wakati wowote kila siku.

Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

RAIS KIKWETE ATOA SALAMU ZA MWISHO ZA MWAKA AKIWA MADARAKANI

Rais Kikwete 

Mwaka wa uchaguzi umeingia. Usiku wa kuamkia leo, Watanzania wameupokea mwaka mpya 2015 huku tafakari kubwa ikiwa ni matukio makubwa yatakayotokea mwaka huu, ukiwamo Uchaguzi Mkuu na kura ya maoni ya Katiba Inayopendekezwa.
Mbali na uchaguzi wa rais wa awamu ya tano, wananchi wataamua ama kuipitisha au kuikataa Katiba Inayopendekezwa, mambo ambayo wasomi, wanasiasa na wanaharakati wameonya kuwa yanatakiwa kuendeshwa na kusimamiwa kwa weledi na umakini mkubwa.
Vilevile, kutokana na matukio hayo kugharimu fedha nyingi, wataalamu wa uchumi wanatabiri kuwa mwaka huu utakuwa mgumu na itakaowalazimu Watanzania kufunga mikanda zaidi.
Pia, macho na masikio ya wananchi yako kwa vyama vya upinzani ambavyo vimeungana na kuzaa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kuona kama vitasimamisha mgombea mmoja wa urais na katika nafasi za ubunge na udiwani kama vilivyokubaliana, ikiwa ni mara ya kwanza tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MUUMINI MBARONI KWA KUFANYA FUJO KANISANI

Leonard Paul
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonard Paulo
POLISI mkoani Morogoro linamshikilia Jackson Mnyilemi (20), ambaye ni muumini wa Kanisa la Moravian Tarafa ya Malinyi wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro kwa tuhuma za kuhusika kufanya fujo kanisani.
Fujo hizo zilisababisha kujeruhiwa kwa waumini wawili kwa kukatwa sehemu za usoni na mikononi na kitu chenye ncha kali.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonard Paulo alisema jana kuwa tukio hilo ni la Desemba 28, 2014 majira ya saa 10 : 40 asubuhi katika kijiji cha Makelele na kuwataja waumini waliojeruhiwa kuwa ni Maria Silumbwe (47) na Aron Silumbwe (20), wote wakazi wa Kijiji hicho kilichopo Tarafa ya Malinyi wilayani Ulanga. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MWAKYEMBE AFUKUZA KAZI VIGOGO 6 WA RELI

Dk Harison Mwakyembe.
 Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe

Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe ameagiza wafanyakazi sita wa Shirika la Reli Tanzania (TRL), wafukuzwe kazi na polisi wawakamate na kuwalaza rumande kuanzia jana kutokana na tuhuma za wizi.
Pia, ameagiza mali za watuhumiwa hao, zichunguzwe na ikibainika ni zaidi ya kipato chao cha kawaida, zipigwe mnada na Bodi ya Wakurugenzi ikae na kuangalia hatua zaidi za kuchukua.
Dk Mwakyembe alitoa maamuzi hayo jana baada ya kuzungumza na wafanyakazi wa TRL na kuonekana kutoridhishwa na vitendo vya wizi, vinavyoendelea katika shirika hilo.
Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Stanley Makunja, Stanley Andrew, Edward Benedicto, Lucy Mtinya, B. Ruoga na Jackson Moses.
Hata hivyo, Mwakyembe alipoombwa na waandishi wa habari, kufafanua vituo vya kazi vya watuhumiwa hao, alidai kwamba wote ni wa TRL na wamewajibishwa kama wafanyakazi wa TRL. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO SIKU YA KWANZA YA MWAKA 2015

.
.
.

Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ZITTO: NITAMUUNGA MKONO MBOWE


HAKI SAWA: Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba (kulia) na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali, Zitto Kabwe wakiwasili kwenye Uwanja wa Mashujaa mjini Mtwara jana, ambako walihutubia mkutano wa hadhara.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe amesema atamuunga mkono Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani, Freeman Mbowe pale atakapowasilisha hoja yake bungeni kuhusu ufisadi wa zaidi ya Sh1 trilioni katika mradi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam.
Zitto aliyasema hayo jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Mashujaa mkoani hapa uliandaliwa na Chama cha Wananchi (CUF) kuwashukuru wakazi wa mkoa huo kwa kuwachagua viongozi wa chama hicho katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
“Najua bado mnalia kuhusu bomba la kupeleka gesi Dar es Salaam, machozi yenu yatafutika kwani tayari habari za ufisadi mkubwa katika ujenzi wa bomba hili zimeanza kuchomoza. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

WATU 20 WAFARIKI HARUSINI

Mmoja ya watoto waliojeruhiwa wakati bomu liliporushwa katika nyumba moja iliokuwa ikifanya sherehe ya harusi mkoani Helmand nchini Afghanistan.Takriban watu 20 waliaga dunia 
 
Sherehe moja ya harusi nchini Afghanistan, imeshambuliwa kwa mzinga uliorushwa na roketi na kusababisha mauaji ya watu 20 na kuwajeruhi wengine zaidi ya kumi na mbili.
Kisa hicho kilitokea wakati wa makabiliano makali kati ya walinda usalama wa Afghanistan na wapiganaji wa Taliban katika jimbo la Helmand.
Mmiliki wa jumba lilofanyiwa harusi hiyo amesema kuwa wageni walikuwa wanajikusanya nje kumkaribisha bi harusi,na kuongezea kuwa watoto wake tisa wametoweka.
Waliojeruhiwa walipelekwa katika hospitali ya Lashkar Gah,mji mkuu wa mkoa huo.
Shambulio hilo limetokea wakati wa siku ya mwisho kwa ujumbe wa wanajeshi wa Marekani na wale wa shirika la kujihami la NATO wanaoondoka nchini Afghanistan. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

PAPA AKEMEA UFISADI MWAKA MPYA

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis 
 
Papa Francis ametumia sherehe za kuupokea mwaka wa 2015 kuzungumzia tatizo la rushwa katika mji wa nyumbani wa Rome nchini Italia.
Akizungumza katika Kanisa kuu la St. Peter Basilica, papa amesema rushwa ni shumbulizi dhidi ya maskini na wasiokuwa na uwezo ambapo ametaka mabadiliko ya kiroho na kimaadili katika mji huo.
Papa ambaye ndiye Askofu wa Rome amefanya utetezi dhidi ya maskini kama nguzo muhimu katika uongozi wake wa upapa.
Maafisa wa polisi kwa sasa wanawachunguza maafisa wa Roma wanaotuhumiwa kujihusisha na kundi la Mafia na ufisadi dhidi ya fedha za umma zikiwemo zilizotengwa kwa ajili ya kituo wahamiaji. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...