Monday, January 05, 2015

RAIA WA SYRIA WAPEWA MASHARTI MAGUMU LEBANON

Lebanon imepokea Wakimbizi zaidi ya Wakimbizi milioni moja kutoka nchini Syria 
 
Masharti mapya yamewekwa na mamlaka ya Lebanon kwa Raia wa Syria wanaoingia nchini humo , wakati huu ambapo nchi hiyo inapokea Wakimbizi wengi.
Kwa mara ya kwanza, Raia wa Syria watalazimika kuwa na vielelezo vinavyoeleza kwa nini wanataka kuvuka mpaka na kuingia nchini Lebanon.
Masharti haya mapya yanaanza kutumika siku ya jumatatu.Awali kusafiri kati ya nchi hizo mbili kwa kiasi kikubwa hakukuwa na kikwazo lakini sasa Raia wa Syria lazima wawe na Viza.
Hatua hii inaelezwa kulenga kudhibiti idadi kubwa ya Wakimbizi wanaoingia nchini Lebanon, ambapo kwa sasa Lebanon ina wakimbizi zaidi ya milioni moja.
Hatua hii ya sasa haijulikani italeta athari gani kwa Raia wengi wa Syria walio nchini Lebanon ambao hawajajiandikisha kuwa wakimbizi.
Kabla ya sasa, Raia wa Syria waliweza kukaa nchini Lebanon mpaka miezi sita, lakini sasa raia wa nchi hiyo watalazimika kutimiza vigezo kadhaa ili kupatiwa Viza mpakani. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...