Monday, January 05, 2015

VIGOGO LIGI KUU ENGLAND WATESA FA

 Heka heka katika lango la Hull wakati Arsenal ilipoibuka na ushindi wa 2-0
 
Mechi kadha zimechezwa kuwania kombe la FA kwa vilabu vya ligi kuu ya England na vile vya madaraja mengine.
Mabingwa watetezi Arsenal waliweza kuwacharaza Hull City 2-0 ambao wameshindwa kulipa kisasi baada ya kushindwa katika fainali za mwaka jana timu hizo zilipokutana. Magoli ya Arsenal yalifungwa na Per Mertesacker pamoja na Alexis Sanchez.
Wachezaji wa Chelsea wakipongezana baada ya ushindi 3-0 dhidi ya Watford
Mechi nyingine zilikuwa kati ya Chelsea na Watford, Chelsea ikiibuka na ushindi wa 3-0. Nayo Machester United ikiishindilia Yeovil 2-0. Kwa upande wake Manchester City nao waliibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Shef Wednesday.
Crystal Palace ilipata ushindi mnono dhidi ya Dover wa mabao 4-0, huku Stoke City ikiicharaza Wrexham magoli 3-1. Sunderland nayo ilivuna goli 1-0 dhidi ya Leeds.
Mechi kumi zimechezwa ambapo kwa ujumla vigogo wa soka England wameonekana kupata matokeo mazuri. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...