Monday, December 08, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMATATU DESEMBA 08, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WAHAMIAJI 70 WAFA MAJI YEMEN

Boti iliyojaza wahamiaji haramu kuelekea Yemen 
 
Watu 70 wamekufa baada ya boti iliyokuwa imejaza wahamiaji haramu kupinduka baharini, magharibi mwa Yemen.
Maafisa nchini Yemen wamesema wengi ya watu waliokuwa katika boti hiyo ni raia wa Ethiopia.
Hali mbaya ya hewa inaelezwa kwamba ndio chanzo cha kuzama kwa boti hiyo.
Mamia kwa maelfu ya wahamiaji wamekuwa wakihatarisha maisha yao kwa safari zisizo na usalama katika nchi zilizo katika pembe ya Afrika na Yemen kila mwaka.
Umoja wa Mataifa unamini kwamba kiasi cha watu watu mia mbili wamezama maji katika kipindi cha miezi kumi na mbili iliyopita. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

EBOLA YAUA DAKTARI MWINGINE S-LEONE

Wakuu wa Sierra Leone wanasema daktari mwengine amefariki kutokana na Ebola - ni daktari wa 10 kufa na ugonjwa huo.
Aiah Solomon Konoyima alifariki Jumamosi kwenye kituo cha matibabu karibu na mji mkuu, Freetown, siku moja tu baada ya wenzake wawili kufa na ugonjwa huo huo.
Mwezi wa Julai daktari maarufu kabisa kutibu wagonjwa wa Ebola nchini Sierra Leone, Sheik Umar Khan, piya mwisho aliuliwa na virusi vya Ebola.
Vifo 1,600 vya Ebola vimesajiliwa nchini humo.
Sierra Leone imekuwa ikijaribu kukarabati huduma za afya baada ya vita vikali vya wenyewe kwa wenyewe katika miaka ya 1990s.
Na daktari kutoka Cuba ambaye alipona Ebola, ameahidi kuwa atarudi Sierra Leone kumaliza kupambana na ugonjwa huo nchini humo.
Dakta Felix Baez, ambaye alipata Ebola nchini Sierra Leone, alisema hayo aliporudi Havana baada ya kujaribiwa matibabu aina mpya nchini Uswiswi ambayo yalimponesha.
Dakta Baez alikuwa kati ya madkatari na wauguzi wa kwanza 250 walioambukizwa Ebola Afrika magharibi.
Cuba ndio nchi iliyotuma huko wafanyakazi wa utabibu wengi kabisa kwenda kupambana na Ebola.
Mchango huo wa Cuba umesifiwa kimataifa hata na Marekani, adui yake wa kisiasa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

Sunday, December 07, 2014

MUTHARIKA AJINYIMA NYONGEZA YA MSHAHARA

Rais Peter Mutharika wa Malawi na naibu wake wameakhirisha kujipa nyongeza ya mishahara baada ya kuzuka malalamiko.
Nyongeza kutoka mshahara wa dola 3,000 na kufikia dola 5,000 kila mwezi, imezusha malalamiko nchini Malawi ambako pato la nusu ya wananchi halitimii dola moja kwa siku.
Bwana Mutharika na makamo wake, Saulos Chilima wamesema hawatojipa nyongeza ya mishahara hadi uchumi wa nchi utengenee.
Kabla ya viongozi hao kushika madaraka wafadhili walisimamisha msaada wa dola 150-milioni kwa sababu ya wasiwasi kuhusu rushwa.
Mishahara ya wabunge itazidishwa asili-mia-mia-tatu (300%) Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MUGABE ATEULIWA TENA KUONGOZA ZANU-PF

Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe ameteuliwa kwa mara nyengine kuongoza chama tawala cha ZANU PF 
 
Rais Robert Mugabe ameteuliwa tena kuongoza chama tawala nchini Zimbabwe na mke wake Grace akapewa wadhifa wa juu katika chama.
Kupandishwa cheo kwa Grace Mugabe kuongoza tawi la wanawake la Zanu-PF kunamuweka katika nafasi nzuri ya kumrithi mumewe katika siku zijazo,wanasema wachambuzi.
Mke huyo wa Rais amewashtumu wakinzani wake wa kisiasa akiwemo Makamo Rais Joyce Mujuru, katika miezi ya hivi karibuni.
Bwana Mugabe mwenye umri wa miaka 90,anatazamiwa kugombea tena urais mnamo mwaka 2018.
Akizungumza katika mkutano mkuu wa Zanu-PF,Bwana Mugabe aliwashukuru maelfu ya wafuasi wake kwa kumchagua kuongoza chama . "Najua nilikotoka.. mimi si bora kushinda watu walonizaa ," alisema Mugabe, ambaye ameiongoza Zimbabwe tangu mwaka 1980.
Madai ya mauaji
Kuteuliwa kwa mke wa Mugabe kuongoza tawi la wanawake kunaonekana kama ni ishara nyigine zaidi kwa Joyce Mujuru ambae wakati mmoja alionekana kama angeweza kumrithi Mugabe sasa amepigwa pande.
Bi Mujuru alipigania pamoja na Bw.Mugabe uhuru wa Zimbabwe kutoka utawala wa wazungu wachache.
Lakini alijikuta matatani wakati Bi Mugabe mwenye umri wa miaka 49, kujitumbukiza katika siasa mnamo mwaka huu na kumshutumu makamo wa rais wa kula njama dhidi ya mumewe. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI DESEMBA 07, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Saturday, December 06, 2014

WAANDISHI WA HABARI WAZUIWA KUINGIA MAHAKAMANI KUSIKILIZA KESI YA IPTL

 Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila. PICHA|MAKTABA

KATIKA hali ya kushangaza, Mahakama Kuu, Kitengo cha Biashara imewazuia waandishi wa habari kuingia mahakamani kusikiliza maombi ya kampuni ya Pan Africa Power Solutions (PAP) na Kampuni ya Independent Power Tanzania (IPTL) kwa Bodi ya Rufaa ya Kodi nchini, kutaka Kamishna Mkuu wa TRA akamatwe na kupelekwa gerezani.
Waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari nchini, waliofika mahakamani hapo jana kusikiliza maombi hayo, walishindwa kusikiliza kinachoendelea baada ya kuambiwa kuwa waandishi wamezuiwa kusikiliza.
Mmoja wa makarani wa mahakama hiyo, aliwaambia waandishi wa habari kuwa hawaruhusiwi kusikiliza maombi hayo, lakini hakuwaeleza sababu. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI DESEMBA 06, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Friday, December 05, 2014

AJIFUNGUA MTOTO MWENYE SURA YA CHURA...!!!

       Kitanda cha Upasuaji.         MKAZI wa kijiji cha Chibwechangula –Behelo katika wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma, Ruth Matonya (26) amejifungua mtoto wa ajabu ambaye nusu ya sura yake inafanana na binadamu na nusu ikifanana na chura.
Mtoto huyo alizaliwa Desemba 2, mwaka huu katika Kituo cha Afya cha Mtakatifu Luka kinachomilikiwa na Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Mpwapwa. Alifariki dunia muda mfupi baada ya kuzaliwa. 

Kwa mujibu wa Mganga Mfawidhi wa kituo hicho, Dk Edwin Kihura mara baada ya mama huyo kufika katika kituo hicho cha afya alikuwa na uchungu ambao haukuwa na kikomo, lakini alishindwa kujifungua kwa njia ya kawaida licha ya njia ya uzazi kufunguka. 

Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

CAG MPYA ATAKA WANASIASA WAHESHIMU OFISI YAKE

MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad (pichani) aliyeapishwa juzi na Rais Jakaya Kikwete amekemea tabia ya wanasiasa na wafanyabiashara kuingilia kazi za kitaaluma, akisema kwa upande wake hatapenda kuona watu wa makundi hayo wakifanya hivyo na kusisitiza kuwa, kufanya hivyo ni kosa.

Aliyasema hayo jana mbele ya waandishi wa habari mara baada ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa kila mwaka wa Wahasibu na Wakaguzi (NBAA) kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC), jijini hapa.
Alisema ofisi ya CAG na watendaji wengine watafanya kazi kwa kufuata maadili ya kazi, huku akiendelea kusisitiza wanasiasa na wafanyabishara kila mmoja aheshimu taaluma ya ukaguzi wa hesabu za serikali kwa faida ya nchi.
Alifafanua kuwa iwapo kila mmoja atawajibika katika nafasi yake na kuaminiana katika shughuli za kila siku, kamwe hakutakuwa na matatizo yoyote.
‘’Matatizo ya watu binafsi yasichanganywe na shughuli za kila siku za ofisi ya CAG na wale wenye kufanya siasa na biashara pia wawajibike katika nafasi zao na ofisi yangu itafanya mambo kwa kufuata Katiba ya nchi inavyoelekeza, na sio vinginevyo,” alisema Profesa Assad aliyekabidhiwa mikoba ya Ludovick Utouh aliyestaafu kwa mujibu wa sheria.
Alitumia fursa hiyo kuwaasa wahasibu na wakaguzi, akisema wanatakiwa kufanya kazi kwa weledi mkubwa na kiwango cha hali ya juu ili taaluma yao iweze kuheshimika nchini. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

IPTL YAZUA KIZAAZAA MAHAKAMANI

Kampuni za Pan Africa Power Solution Tanzania Limited (PAP) na Independent Power Tanzania Ltd (IPTL), zimewasilisha maombi ya kutaka Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato (TRA) akamatwe kwa kukiuka amri ya Bodi ya Rufaa za Kodi (TRAB) kwa kufuta Hati za Malipo ya Kodi za Mauzo ya Hisa (Capital Gain Certificate).
Kampuni hizo mbili, ambazo ziko kwenye mgogoro wa umiliki, ndizo zinahusika kwenye sakata la uchotwaji wa Sh306 bilioni kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow iliyofunguliwa kuhifadhi fedha za malipo ya tozo ya kuuza umeme unaofuliwa na IPTL, kwa Shirika la Umeme (Tanesco), wakati wa kusubiri uamuzi wa mahakama katika kesi ya kupinga tozo hilo.
PAP, ambayo inadai imenunua hisa zote za IPTL, ndiyo iliyolipwa fedha zote zilizokuwa kwenye akaunti hiyo na kuamsha mjadala mkubwa bungeni ulioisha kwa Bunge kufikia uamuzi wa kuwawajibisha kisheria wote waliohusika, wakiwemo mawaziri. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

NAULI MPYA ZA MABASI YAENDAYO MIKOANI

Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri la Watumiaji Huduma za Usafi wa nchi kavu na Majini, Dk Oscar Kikoyo akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es salaam jana juu ya hali ya usafiri kipindi cha siku kuu za Krismas na mwaka mpya ambapo ametahadharishja abiria kuto kukubali kutozwa nauri za juu na pindi ikitokea hivyo Sumatra ipewe taarifa haraka.



 
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA DESEMBA 05, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAHAKAMA YA TANZANIA SASA KUONYESHA LIVE KESI WAKATI ZIKIENDELEA KATIKA TELEVISHENI NA REDIO.


http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/2141854/lowRes/662002/-/o2ggkjz/-/chande+clip.jpg







Jaji Mkuu, Mohamed Chande Othman 

MAHAKAMA inaangalia uwezekano wa kuruhusu vyombo vya habari kurekodi picha na sauti kuwezesha vituo vya radio na televisheni kuripoti habari za mahakama wakati kesi zinaendelea. 

Jaji Mkuu, Mohamed Chande Othman alisema jana mahakama inajifunza kutoka kwa nchi zinazoruhusu vituo vya redio na televisheni kurekodi na kuripoti habari wakati kesi zinaendelea. 

Alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari jana wakati wa mkutano baina ya Baraza la Vyombo vya Habari na Mahakama uliofanyika jijini Dar es Salaam. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MUGABE ASEMA HANG'OKI MADARAKANI..!!!

Rais Robert Mugabe awalaumu baadhi ya wapinzani wake ndani ya chama cha ZANU PF kwa kupanga kumuondoa mamlakani. 
 
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe amelaumu baadhi ya watu ndani ya chama chake tawala cha ZANU-PF kwamba wanapanga kumng'oa madarakani.
Akizungumza katika kongamano la chama hicho, Mugabe amesema amebaini kuwepo majaribio ya kuwahonga wajumbe kumpinga kama kiongozi, lakini akasisitiza wajumbe hawawezi kupokea hongo.
Mugabe ameahidi kupambana na rushwa ndani ya chama na kukabiliana na maafisa wa chama hicho ambao kazi yao ni kutoa hongo na kupokea rushwa.
Wanachama wengi wa chama hicho wangali ni wafuasi sugu wa Rais Mugabe
Hasira ya Mugabe ilionekana kufuatia madai ya njama ya kutaka kumuua yanayodaiwa kuandaliwa na naibu wake Joyce Mujuru. Hata hivyo Mujuru alikanusha madai hayo ambayo yamekuwa yakimuandamana.Mugabe alisema kutokuwepo kwa Bi Mujuru kwenye mkutano huo wa chama kunaonyesha kuwa anaogopa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAREKANI: TULIPANGA KUMWOKOA SOMERS

Luke Somers raia wa Marekani mwandishi wa habari anayeshikiliwa mateka na al-Qaeda huko Yemen
Marekani imeeleza kuwa ilijaribu kumwokoa raia wake mzaliwa wa Uingereza Luke Somers, anayeshikiliwa mateka na al-Qaeda nchini Yemen.
Rais Barack Obama aliidhinisha kikosi cha kumwokoa Luke, mwezi uliopita.
"Kwa masikito, Luke hakuwepo, japokuwa mateka kutoka mataifa mengine walikuwepo na waliokolewa," Baraza la Usalama la Taifa, limesema.
Mtu anayejitambulisha kama Luke Somers, ambaye alitekwa mwaka 2013, ameonekana katika video, akisema maisha yake yako hatarini na anaomba msaada.
Video hiyo pia inamwonyesha mfuasi wa al-Qaeda huko Yemen akitishia kumuua Bwana Somers hadi madai yao ambayo hayajatajwa, yatakapotimizwa.
Bwana Somers, mwenye umri wa miaka 33, alifanyakazi kama mwandishi wa habari na mpiga picha wa mashirika ya huko na kazi zake zikaonekana katika vyombo vya habari vya kimataifa, ukiwemo mtandao wa BBC. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Thursday, December 04, 2014

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS DESEMBA 04, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

2014 NI MWAKA WA JOTO KALI DUNIANI

Viwanda vikitoa moshi angani na kuchafua mazingira
Mwaka huu unaoishia unasemekana kuwa na kiwango cha juu zaidi cha joto duniani na kwa Uingereza tangu kumbukumbu zianze kutunzwa.
Makadirio ya awali yanaonyesha kuwa katika miezi kumi ya kwanza ya mwaka 2014, wastani wa kiwango cha hali ya joto duniani kilikuwa 0.57C juu ya wastani uliokuwepo muda mrefu.
Dhoruba nchini Uingereza iliyosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi
Na miezi kumi na mmoja ya kwanza nchini Uingereza imezalisha wastani wa joto la 1.6C likiwa juu ya wastani uliokuwepo kwa muda mrefu.Utafiti mwingine uliofanywa na Ofisi ya Hali ya Hewa ya Uingereza umeonyesha kuwa ongezeko la viwango vya joto vilivyoshuhudiwa, visingetokea bila ya ongezeko la gesi zinazoharibu mazingira kutokana na shughuli za binadamu. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

IS WAFUNGUA KAMBI ZA MAFUNZO LIBYA

 Wapiganaji wa Islamic State katika jimbo la Anbar,Syria Marchi 2014 
Wapiganaji wa kundi la Islamic State wafungua kambi za mafunzo Libya
Wapiganaji wa kundi la Islamic State wameanzisha kambi za mafunzo mashariki mwa Libya, amesema mkuu wa kamandi ya Marekani ya masuala ya Afrika.
Wapiganaji wa Kikurd wakiwa katika mafunzo ya kijeshi kukabiliana na wapiganaji wa Islamic State Septemba 2014 nchini Iraq.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

AFCON 2015 MAKUNDI YA TIMU 16 YATAJWA

Kombe la Shirikisho la Soka Afrika, AFCON 
 
Upangaji wa makundi ya timu kumi na sita zilizofuzu kucheza fainali za mashindano ya 30 ya kuwania Kombe la Mataifa ya Afrika kwa mwaka 2015 yamefanyika katika mji mkuu wa Equatorial Guinea, Malabo.
Mashindano hayo yataanza Januari 17, 2015.
Upangaji wa makundi ulirudishwa wiki moja nyuma ili kuiwezesha Equatorial Guinea, kujiandaa baada ya kuchukua nafasi ya Morocco, iliyokuwa iandae mashindano hayo, lakini ilishindwa kufanya hivyo baada ya kutaka mashindano hayo yasogezwe mbele kuhofia ugonjwa wa Ebola ambao umeyakumba baadhi ya mataifa ya Afrika Magharibi, ambako zinatoka timu nyingi zinazoshiriki michuano hiyo.
Mabingwa watetezi Nigeria ni moja ya timu kubwa zilizoshindwa kufuzu kucheza fainali za mwakani, pamoja na Misri na Angola ambazo zote kwa mshangao hazitaweza kushiriki.
Haya hapa makundi manne ya AFCON 2015:

Kundi A Equatorial Guinea, Burkina Faso, Gabon, Congo
Kundi B Zambia, Tunisia, Cape Verde, DR Congo
Kundi C Ghana, Algeria, South Africa, Senegal
Kundi D Ivory Coast, Mali, Cameroon, Guinea

Wenyeji Equatorial Guinea na Congo zitacheza mechi ya ufunguzi wa michuano hiyo. Kundi D ndilo linaloonekana kuwa gumu zaidi kutokana na timu zilizopangwa kundi hilo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

CHELSEA HAISHIKIKI LIGI KUU ENGLAND

Ivanovic akishangilia na Drogba baada ya Drogba kuifungia timu yake ya Chelsea bao la pili katika mechi hiyo 

Mzunguko wa 14 umekamilika kwa timu zote 20 za ligi kuu ya England kushuka viwanjani.
Chelsea, wameendeleza wimbi la ushindi na kukataa katakata kuzipa nafasi timu nyingine 19 kupunguza pengo la pointi lililopo kati yake na timu hizo.

Sergio Aguero, mchezaji wa Manchester City akishangilia moja ya magoli yake katika ligi kuu ya England
Chelsea imeendelea kuwa na tofauti ya pointi sita na Man City inayoifuatia baada ya kuirarua Tottenham mabao 3-0, huku Manchester City yenye pointi 30 ikiisasambua Sunderland magoli 4-1. Sergio Aguero ameifungia timu yake ya Manchester City magoli mawili katika mchezo huo, huku Jovetic na Zabaleta kila mmoja akifunga bao moja. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Wednesday, December 03, 2014

KAFULILA ALIVYOIBUA UFISADI WA AKAUNTI YA ESROW


Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila. PICHA|MAKTABA 

Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila ameeleza namna alivyoibua sakata la uchotwaji wa Sh306 bilioni kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow na kudokeza kuwa kitendo cha baadhi ya watuhumiwa kugoma kujiuzulu, kinaonyesha kuna watu zaidi wanahusika.
Kafulila (32), ambaye alikuwa akiulizia suala hilo kila mara bungeni hadi uamuzi wa kulijadili ulipofikiwa, amesema ataendelea kulifuatilia hadi aone mwisho wake.

Akaunti hiyo ilifunguliwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kuhifadhi fedha za malipo ya tozo ya ufuaji umeme baada ya Tanesco kuingia kwenye mgogoro na Kampuni ya IPTL na suala hilo kupelekwa mahakamani.

Kwa mujibu wa masharti ya uendeshaji wa akaunti za escrow, fedha hizo zilitakiwa zitolewe baada ya Mahakama kutoa uamuzi wa mgogoro huo, lakini wakati ilitaka pande hizo mbili zikutane na kukokotoa viwango vya tozo hizo, fedha hizo zilitolewa na kulipwa kwa mmiliki mpya wa Kampuni ya Pan African Power Solutions (PAP), jambo lililosababisha kuibuka kwa kashfa hiyo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO DESEMBA 03, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


DSC06413
DSC06413
DSC06414
DSC06415
DSC06416 
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WARIOBA: ESCROW NI MATOKEO YA KATIBA ISIYO NA MAJIBU

Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba. PICHA|MAKTABA 

Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amesema wizi wa Sh306 bilioni katika Akaunti ya Tegeta Escrow, mvutano kati ya mihimili ya dola na viongozi kukosa maadili ni matokeo ya nchi kuwa na Katiba isiyo na majibu ya masuala hayo.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na gazeti hili, Jaji Warioba alisema Bunge la Katiba lilifanya makosa kutoviweka vifungu vinavyozungumzia mambo hayo katika Katiba Inayopendekezwa ambavyo awali vilipendekezwa na Tume yake katika rasimu ya pili.

“Katika mchakato wa Katiba Mpya tulisema kuwe na mgawanyo wa madaraka na kila mtu ajue madaraka yake ni nini na kutenganisha Serikali na Bunge. Kama Serikali na Bunge vingetenganishwa bungeni usingeibuka mvutano kuhusu waliochota fedha za escrow. Bunge lingekuwa huru katika utendaji wake wa kazi,” alisema. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SPIKA ASEMA WALIOKEKETWA HAWAFAI

Spika wa Bunge la Uganda Bi Rebecca Kadaga awashauri wanaume kutowaoa wanawake waliokeketwa.

Spika wa Bunge la Uganda Bi Rebecca Kadaga amewashauri wanaume kutowaoa wanawake waliokeketwa akiwataja kuwa mzigo ambao hauwezi kuijenga jamii.
Kulingana na gazeti la daily Monitor,Spika Kadaga alitoa wito huo wakati wa sherehe ya kitamaduni ambayo inapinga ukeketaji ilioandaliwa na mfuko wa umoja wa mataifa unaosimamia idadi ya watu na wahisani wengine. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MLIPUKO MKUBWA MOGADISHU

Mlipuko wakumba mji wa Mogadishu nchini Somali.
 
Mlipuko mkubwa umetokea katika mji wa Mogadishu nchini Somalia karibu na uwanja wa ndege.
Duru zimearifu kuwa mlipuko huo huenda umesababishwa na mtu aliyejitolea muhanga aliyejilipua ndani ya gari.
Kundi la wapiganaji wa kiislamu la Al- Shaabab mara kwa mara hutumia milipuko ya magari, lakini kufikia sasa halijakiri kuhusika na mlipuko huo.
Haijajulikana ni watu wangapi wameuwawa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

DROO YA KOMBE LA AFRIKA KUFANYIKA LEO

Droo ya kombe la mataifa ya Afrika mwaka 2015 kufanyika leo usiku mjini Malabo nchini Equitorial Guinea.
 
Mabingwa wa zamani Zambia na waandalizi wa kombe la bara Afrika Equitorial Guinea ni miongoni mwa timu zitakazoorodheshwa katika droo ya kombe hilo la mwaka 2015 Jumatano usiku.
Shirikisho la soka barani Afrika CAF tayari limezigawanya timu hizo 16 katika makundi vyungu vinne vya kinyang'anyiro hicho cha january 17 hadi februari 8.
Hatua hio ilifanyika kulingana na utendaji wa timu hizo katika awamu tatu ya michuano hiyo na mechi za kufuzu katika kipindi hicho hicho.
Miongoni mwa vitu ambavyo vilitiliwa mkazo ni matokeo ya mechi za kufuzu kwa kombe la dunia mwaka 2014.
Droo hiyo ambayo itabuni makundi manne yanayoshirikisha timu moja moja kutoka kila chungu itafanyika mjini malabo jumatano usiku. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Ghana na Ivory Coast ni timu nyengine kubwa huku washindi wa pili wa mwaka 3013 Burkina Faso wameorodheshwa katika kundi la Pili.
2015 Nations Cup :Timu zilivyowekwa.
Pot 1: Equatorial Guinea, Ghana, Ivory Coast, Zambia
Pot 2: Burkina Faso, Mali, Tunisia, Algeria
Pot 3: Cape Verde, South Africa, Cameroon, Gabon
Pot 4: Guinea, Senegal, DR Congo, Congo

Monday, December 01, 2014

RAIS KIKWETE AMTEUA PROFESA ASSAD KUWA CAG MPYA


Profesa Mussa Juma Assad 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Profesa Mussa Juma Assad kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Taarifa iliyotolewa leo, Jumatatu, Desemba Mosi, 2014 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, inasema kuwa uteuzi wa Bwana Assad ulianza Novemba 5, mwaka huu, 2014.

Taarifa hiyo imeongeza kuwa Bwana Assad ataapishwa kesho, Jumanne, Desemba 2, saa nne asubuhi, Ikulu, Dar es Salaam. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz 

BOKO HARAM WAVAMIA MIJI MIWILI NIGERIA

Nia kuu ya Boko Haram ni kuwa na dola ya kiisilamu inayofuata sheria za kiisilamu.
 
Watu wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa Boko Haram wamefanya mashambulizi katika miji miwili eneo la Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
La kwanza lilikuwa la kujitoa mhanga pamoja na shambulizi lengine katika kituo cha polisi cha Damaturu.
Wenyeji wa mji wa Maiduguri walielezea kusikia milipuko miwili kwenye soko moja.
Mashambulizi mengine ya kujitoa mhanga eneo hilo wiki iliyopita yaliwaua zaidi ya watu 70.
Mapema leo Jumatatu watu wanaokisiwa kuwa wanamgambo wa Boko Haram waliteketeza kituo cha polisi katika mji wa Damataru kilicho umbali wa kilomita 100 Magharibi mwa mji wa Maiduguri.
Inaarifiwa watu 5 wameuawa katika mashambulizi hayo ya mabomu yaliyotokea katika soko lililokuwa na watu wengi.
Mjini Damaturu , milipuko na milio ya risasi ilisikika huku wanamgambo hao walipokuwa wanashambulia mjini huo.
Boko Haram imeahidi kubuni dola ya kiisilamu katika maeneo ambayo kundi hilo linadhibiti.
Milipuko hio ilitokea Jumatatu katika soko la Maiduguri , mji mkuu wa jimbo la Borno ambayo ilisababishwa na wasichana wawili waliojilipua.
Takriban watu 32 walijeruhiwa katika milipuko hio. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ICC YAKATAA OMBI LA MUASI LUBANGA

Mahakama ya ICC imetupilia mbali ombi la Lubanga kupunguziwa kifungo jela.
 
Mahakama ya kimataifa ya ICC mjini Hague, imetupilia mbali ombi la rufaa lililowasilishwa na muasi wa zamani nchini DRC Thomas Lubanga dhidi ya hukumu aliyopewa kwa makosa ya kuwatumia watoto kama wanajeshi.
Viongozi wa mashtaka walisema wavulana wadogo wenye umri wa miaka 10 walitekwa nyara na kusajiliwa kama wanajeshi DRC katika vita hivyo vilivyoanza mwaka 1999.
Wasichana nao walitumiwa kama watumwa wa ngono.
Mnamo mwaka 2012, Lubanga alikuwa mtu wa kwanza kuhukumiwa na mahakama hio.
Aliwahi kuwa kiongozi wa kundi la wapiganaji la (UPC), ambalo lilikuwa la kabila la Hema ambalo lilihusika katika vita eneo la Ituri Mashariki mwa DRC.
Mahakama ilimpata na hatia kwa kuwatumia watoto kama wanajeshi na kuwatuma kwenda kumpigania. Alihukumiwa kifungo cha miaka 14.
Kundi la UPC, lilikuwa moja ya makundi sita ya wapiganaji waliopigana kudhibiti eneo lenye utajiri wa madini la Ituri hadi mwaka 2003.
Mgogoro ulianza kama mvutano wa kupigania mali asili, ingawa baadaye ilipanda daraja na kuwa vita vilivyohusisha jeshi la Uganda.
Kadhalika mgogoro huo uligeuka na kuwa vita kati ya jamii za Hema na Lendu ambapo takriban watu 50,000 waliachwa bila makao. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...