Monday, December 08, 2014
WAHAMIAJI 70 WAFA MAJI YEMEN
Watu 70 wamekufa baada ya boti iliyokuwa imejaza wahamiaji haramu kupinduka baharini, magharibi mwa Yemen.
Maafisa nchini Yemen wamesema wengi ya watu waliokuwa katika boti hiyo ni raia wa Ethiopia.Hali mbaya ya hewa inaelezwa kwamba ndio chanzo cha kuzama kwa boti hiyo.
Mamia kwa maelfu ya wahamiaji wamekuwa wakihatarisha maisha yao kwa safari zisizo na usalama katika nchi zilizo katika pembe ya Afrika na Yemen kila mwaka.
Umoja wa Mataifa unamini kwamba kiasi cha watu watu mia mbili wamezama maji katika kipindi cha miezi kumi na mbili iliyopita. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Na BBC
EBOLA YAUA DAKTARI MWINGINE S-LEONE
Wakuu wa Sierra Leone wanasema daktari mwengine amefariki kutokana na Ebola - ni daktari wa 10 kufa na ugonjwa huo.
Aiah
Solomon Konoyima alifariki Jumamosi kwenye kituo cha matibabu karibu na
mji mkuu, Freetown, siku moja tu baada ya wenzake wawili kufa na
ugonjwa huo huo.Mwezi wa Julai daktari maarufu kabisa kutibu wagonjwa wa Ebola nchini Sierra Leone, Sheik Umar Khan, piya mwisho aliuliwa na virusi vya Ebola.
Vifo 1,600 vya Ebola vimesajiliwa nchini humo.
Sierra Leone imekuwa ikijaribu kukarabati huduma za afya baada ya vita vikali vya wenyewe kwa wenyewe katika miaka ya 1990s.
Na daktari kutoka Cuba ambaye alipona Ebola, ameahidi kuwa atarudi Sierra Leone kumaliza kupambana na ugonjwa huo nchini humo.
Dakta Felix Baez, ambaye alipata Ebola nchini Sierra Leone, alisema hayo aliporudi Havana baada ya kujaribiwa matibabu aina mpya nchini Uswiswi ambayo yalimponesha.
Dakta Baez alikuwa kati ya madkatari na wauguzi wa kwanza 250 walioambukizwa Ebola Afrika magharibi.
Cuba ndio nchi iliyotuma huko wafanyakazi wa utabibu wengi kabisa kwenda kupambana na Ebola.
Mchango huo wa Cuba umesifiwa kimataifa hata na Marekani, adui yake wa kisiasa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Na BBC
Sunday, December 07, 2014
MUTHARIKA AJINYIMA NYONGEZA YA MSHAHARA
Rais Peter Mutharika wa Malawi na naibu wake wameakhirisha kujipa nyongeza ya mishahara baada ya kuzuka malalamiko.
Nyongeza
kutoka mshahara wa dola 3,000 na kufikia dola 5,000 kila mwezi,
imezusha malalamiko nchini Malawi ambako pato la nusu ya wananchi
halitimii dola moja kwa siku.Bwana Mutharika na makamo wake, Saulos Chilima wamesema hawatojipa nyongeza ya mishahara hadi uchumi wa nchi utengenee.
Kabla ya viongozi hao kushika madaraka wafadhili walisimamisha msaada wa dola 150-milioni kwa sababu ya wasiwasi kuhusu rushwa.
Mishahara ya wabunge itazidishwa asili-mia-mia-tatu (300%) Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
MUGABE ATEULIWA TENA KUONGOZA ZANU-PF
Rais Robert Mugabe ameteuliwa tena kuongoza chama tawala nchini Zimbabwe na mke wake Grace akapewa wadhifa wa juu katika chama.
Kupandishwa
cheo kwa Grace Mugabe kuongoza tawi la wanawake la Zanu-PF kunamuweka
katika nafasi nzuri ya kumrithi mumewe katika siku zijazo,wanasema
wachambuzi.Mke huyo wa Rais amewashtumu wakinzani wake wa kisiasa akiwemo Makamo Rais Joyce Mujuru, katika miezi ya hivi karibuni.
Bwana Mugabe mwenye umri wa miaka 90,anatazamiwa kugombea tena urais mnamo mwaka 2018.
Akizungumza katika mkutano mkuu wa Zanu-PF,Bwana Mugabe aliwashukuru maelfu ya wafuasi wake kwa kumchagua kuongoza chama . "Najua nilikotoka.. mimi si bora kushinda watu walonizaa ," alisema Mugabe, ambaye ameiongoza Zimbabwe tangu mwaka 1980.
Madai ya mauaji
Kuteuliwa kwa mke wa Mugabe kuongoza tawi la wanawake kunaonekana kama ni ishara nyigine zaidi kwa Joyce Mujuru ambae wakati mmoja alionekana kama angeweza kumrithi Mugabe sasa amepigwa pande.
Bi Mujuru alipigania pamoja na Bw.Mugabe uhuru wa Zimbabwe kutoka utawala wa wazungu wachache.
Lakini alijikuta matatani wakati Bi Mugabe mwenye umri wa miaka 49, kujitumbukiza katika siasa mnamo mwaka huu na kumshutumu makamo wa rais wa kula njama dhidi ya mumewe. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Saturday, December 06, 2014
WAANDISHI WA HABARI WAZUIWA KUINGIA MAHAKAMANI KUSIKILIZA KESI YA IPTL
Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila. PICHA|MAKTABA
KATIKA hali ya kushangaza, Mahakama Kuu, Kitengo cha Biashara
imewazuia waandishi wa habari kuingia mahakamani kusikiliza maombi ya
kampuni ya Pan Africa Power Solutions (PAP) na Kampuni ya Independent
Power Tanzania (IPTL) kwa Bodi ya Rufaa ya Kodi nchini, kutaka Kamishna
Mkuu wa TRA akamatwe na kupelekwa gerezani.
Waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari nchini, waliofika
mahakamani hapo jana kusikiliza maombi hayo, walishindwa kusikiliza
kinachoendelea baada ya kuambiwa kuwa waandishi wamezuiwa kusikiliza.
Mmoja wa makarani wa mahakama hiyo, aliwaambia waandishi wa habari
kuwa hawaruhusiwi kusikiliza maombi hayo, lakini hakuwaeleza sababu. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
Friday, December 05, 2014
AJIFUNGUA MTOTO MWENYE SURA YA CHURA...!!!
MKAZI wa kijiji cha Chibwechangula –Behelo katika wilaya ya Mpwapwa
mkoani Dodoma, Ruth Matonya (26) amejifungua mtoto wa ajabu ambaye nusu
ya sura yake inafanana na binadamu na nusu ikifanana na chura.
Mtoto huyo alizaliwa Desemba 2, mwaka huu katika Kituo cha Afya cha
Mtakatifu Luka kinachomilikiwa na Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya
Mpwapwa. Alifariki dunia muda mfupi baada ya kuzaliwa.
Kwa mujibu wa Mganga Mfawidhi wa kituo hicho, Dk Edwin Kihura mara baada ya mama huyo kufika katika kituo hicho cha afya alikuwa na uchungu ambao haukuwa na kikomo, lakini alishindwa kujifungua kwa njia ya kawaida licha ya njia ya uzazi kufunguka.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Kwa mujibu wa Mganga Mfawidhi wa kituo hicho, Dk Edwin Kihura mara baada ya mama huyo kufika katika kituo hicho cha afya alikuwa na uchungu ambao haukuwa na kikomo, lakini alishindwa kujifungua kwa njia ya kawaida licha ya njia ya uzazi kufunguka.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
CAG MPYA ATAKA WANASIASA WAHESHIMU OFISI YAKE
MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa
Assad (pichani) aliyeapishwa juzi na Rais Jakaya Kikwete amekemea tabia
ya wanasiasa na wafanyabiashara kuingilia kazi za kitaaluma, akisema kwa
upande wake hatapenda kuona watu wa makundi hayo wakifanya hivyo na
kusisitiza kuwa, kufanya hivyo ni kosa.
Aliyasema hayo jana mbele ya waandishi wa habari mara baada ya
ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa kila mwaka wa Wahasibu na Wakaguzi (NBAA)
kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC), jijini hapa.
Alisema ofisi ya CAG na watendaji wengine watafanya kazi kwa kufuata
maadili ya kazi, huku akiendelea kusisitiza wanasiasa na wafanyabishara
kila mmoja aheshimu taaluma ya ukaguzi wa hesabu za serikali kwa faida
ya nchi.
Alifafanua kuwa iwapo kila mmoja atawajibika katika nafasi yake na
kuaminiana katika shughuli za kila siku, kamwe hakutakuwa na matatizo
yoyote.
‘’Matatizo ya watu binafsi yasichanganywe na shughuli za kila siku za
ofisi ya CAG na wale wenye kufanya siasa na biashara pia wawajibike
katika nafasi zao na ofisi yangu itafanya mambo kwa kufuata Katiba ya
nchi inavyoelekeza, na sio vinginevyo,” alisema Profesa Assad
aliyekabidhiwa mikoba ya Ludovick Utouh aliyestaafu kwa mujibu wa
sheria.
Alitumia fursa hiyo kuwaasa wahasibu na wakaguzi, akisema wanatakiwa
kufanya kazi kwa weledi mkubwa na kiwango cha hali ya juu ili taaluma
yao iweze kuheshimika nchini. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
IPTL YAZUA KIZAAZAA MAHAKAMANI
Kampuni za Pan Africa Power
Solution Tanzania Limited (PAP) na Independent Power Tanzania Ltd
(IPTL), zimewasilisha maombi ya kutaka Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya
Mapato (TRA) akamatwe kwa kukiuka amri ya Bodi ya Rufaa za Kodi (TRAB)
kwa kufuta Hati za Malipo ya Kodi za Mauzo ya Hisa (Capital Gain
Certificate).
Kampuni hizo mbili, ambazo ziko kwenye mgogoro wa
umiliki, ndizo zinahusika kwenye sakata la uchotwaji wa Sh306 bilioni
kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow iliyofunguliwa kuhifadhi fedha za malipo
ya tozo ya kuuza umeme unaofuliwa na IPTL, kwa Shirika la Umeme
(Tanesco), wakati wa kusubiri uamuzi wa mahakama katika kesi ya kupinga
tozo hilo.
PAP, ambayo inadai imenunua hisa zote za IPTL,
ndiyo iliyolipwa fedha zote zilizokuwa kwenye akaunti hiyo na kuamsha
mjadala mkubwa bungeni ulioisha kwa Bunge kufikia uamuzi wa
kuwawajibisha kisheria wote waliohusika, wakiwemo mawaziri. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
NAULI MPYA ZA MABASI YAENDAYO MIKOANI
Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri la Watumiaji Huduma za Usafi wa nchi kavu na Majini, Dk Oscar Kikoyo akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es salaam jana juu ya hali ya usafiri kipindi cha siku kuu za Krismas na mwaka mpya ambapo ametahadharishja abiria kuto kukubali kutozwa nauri za juu na pindi ikitokea hivyo Sumatra ipewe taarifa haraka.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
MAHAKAMA YA TANZANIA SASA KUONYESHA LIVE KESI WAKATI ZIKIENDELEA KATIKA TELEVISHENI NA REDIO.
Jaji Mkuu, Mohamed Chande Othman
MAHAKAMA
inaangalia uwezekano wa kuruhusu vyombo vya habari kurekodi picha na
sauti kuwezesha vituo vya radio na televisheni kuripoti habari za
mahakama wakati kesi zinaendelea.
Jaji
Mkuu, Mohamed Chande Othman alisema jana mahakama inajifunza kutoka kwa
nchi zinazoruhusu vituo vya redio na televisheni kurekodi na kuripoti
habari wakati kesi zinaendelea.
Alisema
hayo alipozungumza na waandishi wa habari jana wakati wa mkutano baina
ya Baraza la Vyombo vya Habari na Mahakama uliofanyika jijini Dar es
Salaam. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
MUGABE ASEMA HANG'OKI MADARAKANI..!!!
Rais
wa Zimbabwe Robert Mugabe amelaumu baadhi ya watu ndani ya chama chake
tawala cha ZANU-PF kwamba wanapanga kumng'oa madarakani.
Akizungumza
katika kongamano la chama hicho, Mugabe amesema amebaini kuwepo
majaribio ya kuwahonga wajumbe kumpinga kama kiongozi, lakini
akasisitiza wajumbe hawawezi kupokea hongo.Mugabe ameahidi kupambana na rushwa ndani ya chama na kukabiliana na maafisa wa chama hicho ambao kazi yao ni kutoa hongo na kupokea rushwa.
Hasira ya Mugabe ilionekana kufuatia madai ya njama ya kutaka kumuua yanayodaiwa kuandaliwa na naibu wake Joyce Mujuru. Hata hivyo Mujuru alikanusha madai hayo ambayo yamekuwa yakimuandamana.Mugabe alisema kutokuwepo kwa Bi Mujuru kwenye mkutano huo wa chama kunaonyesha kuwa anaogopa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
MAREKANI: TULIPANGA KUMWOKOA SOMERS
Marekani
imeeleza kuwa ilijaribu kumwokoa raia wake mzaliwa wa Uingereza Luke
Somers, anayeshikiliwa mateka na al-Qaeda nchini Yemen.
Rais Barack Obama aliidhinisha kikosi cha kumwokoa Luke, mwezi uliopita."Kwa masikito, Luke hakuwepo, japokuwa mateka kutoka mataifa mengine walikuwepo na waliokolewa," Baraza la Usalama la Taifa, limesema.
Mtu anayejitambulisha kama Luke Somers, ambaye alitekwa mwaka 2013, ameonekana katika video, akisema maisha yake yako hatarini na anaomba msaada.
Video hiyo pia inamwonyesha mfuasi wa al-Qaeda huko Yemen akitishia kumuua Bwana Somers hadi madai yao ambayo hayajatajwa, yatakapotimizwa.
Bwana Somers, mwenye umri wa miaka 33, alifanyakazi kama mwandishi wa habari na mpiga picha wa mashirika ya huko na kazi zake zikaonekana katika vyombo vya habari vya kimataifa, ukiwemo mtandao wa BBC. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Thursday, December 04, 2014
2014 NI MWAKA WA JOTO KALI DUNIANI
Mwaka
huu unaoishia unasemekana kuwa na kiwango cha juu zaidi cha joto
duniani na kwa Uingereza tangu kumbukumbu zianze kutunzwa.
Makadirio
ya awali yanaonyesha kuwa katika miezi kumi ya kwanza ya mwaka 2014,
wastani wa kiwango cha hali ya joto duniani kilikuwa 0.57C juu ya
wastani uliokuwepo muda mrefu.Na miezi kumi na mmoja ya kwanza nchini Uingereza imezalisha wastani wa joto la 1.6C likiwa juu ya wastani uliokuwepo kwa muda mrefu.Utafiti mwingine uliofanywa na Ofisi ya Hali ya Hewa ya Uingereza umeonyesha kuwa ongezeko la viwango vya joto vilivyoshuhudiwa, visingetokea bila ya ongezeko la gesi zinazoharibu mazingira kutokana na shughuli za binadamu. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
IS WAFUNGUA KAMBI ZA MAFUNZO LIBYA
Wapiganaji wa kundi la Islamic State wafungua kambi za mafunzo Libya
Wapiganaji
wa kundi la Islamic State wameanzisha kambi za mafunzo mashariki mwa
Libya, amesema mkuu wa kamandi ya Marekani ya masuala ya Afrika.AFCON 2015 MAKUNDI YA TIMU 16 YATAJWA
Upangaji
wa makundi ya timu kumi na sita zilizofuzu kucheza fainali za
mashindano ya 30 ya kuwania Kombe la Mataifa ya Afrika kwa mwaka 2015
yamefanyika katika mji mkuu wa Equatorial Guinea, Malabo.
Mashindano hayo yataanza Januari 17, 2015.
Upangaji
wa makundi ulirudishwa wiki moja nyuma ili kuiwezesha Equatorial
Guinea, kujiandaa baada ya kuchukua nafasi ya Morocco, iliyokuwa iandae
mashindano hayo, lakini ilishindwa kufanya hivyo baada ya kutaka
mashindano hayo yasogezwe mbele kuhofia ugonjwa wa Ebola ambao
umeyakumba baadhi ya mataifa ya Afrika Magharibi, ambako zinatoka timu
nyingi zinazoshiriki michuano hiyo.
Mabingwa watetezi Nigeria ni
moja ya timu kubwa zilizoshindwa kufuzu kucheza fainali za mwakani,
pamoja na Misri na Angola ambazo zote kwa mshangao hazitaweza kushiriki.
Haya hapa makundi manne ya AFCON 2015:
Kundi B Zambia, Tunisia, Cape Verde, DR Congo
Kundi C Ghana, Algeria, South Africa, Senegal
Kundi D Ivory Coast, Mali, Cameroon, Guinea
Wenyeji
Equatorial Guinea na Congo zitacheza mechi ya ufunguzi wa michuano
hiyo. Kundi D ndilo linaloonekana kuwa gumu zaidi kutokana na timu
zilizopangwa kundi hilo. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
CHELSEA HAISHIKIKI LIGI KUU ENGLAND
Mzunguko wa 14 umekamilika kwa timu zote 20 za ligi kuu ya England kushuka viwanjani.
Chelsea,
wameendeleza wimbi la ushindi na kukataa katakata kuzipa nafasi timu
nyingine 19 kupunguza pengo la pointi lililopo kati yake na timu hizo.Chelsea imeendelea kuwa na tofauti ya pointi sita na Man City inayoifuatia baada ya kuirarua Tottenham mabao 3-0, huku Manchester City yenye pointi 30 ikiisasambua Sunderland magoli 4-1. Sergio Aguero ameifungia timu yake ya Manchester City magoli mawili katika mchezo huo, huku Jovetic na Zabaleta kila mmoja akifunga bao moja. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Wednesday, December 03, 2014
KAFULILA ALIVYOIBUA UFISADI WA AKAUNTI YA ESROW
Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila. PICHA|MAKTABA
Mbunge wa Kigoma Kusini
(NCCR-Mageuzi), David Kafulila ameeleza namna alivyoibua sakata la
uchotwaji wa Sh306 bilioni kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow na kudokeza
kuwa kitendo cha baadhi ya watuhumiwa kugoma kujiuzulu, kinaonyesha kuna
watu zaidi wanahusika.
Kafulila (32), ambaye alikuwa akiulizia suala hilo
kila mara bungeni hadi uamuzi wa kulijadili ulipofikiwa, amesema
ataendelea kulifuatilia hadi aone mwisho wake.
Akaunti hiyo ilifunguliwa Benki Kuu ya Tanzania
(BoT) kuhifadhi fedha za malipo ya tozo ya ufuaji umeme baada ya Tanesco
kuingia kwenye mgogoro na Kampuni ya IPTL na suala hilo kupelekwa
mahakamani.
Kwa mujibu wa masharti ya uendeshaji wa akaunti za
escrow, fedha hizo zilitakiwa zitolewe baada ya Mahakama kutoa uamuzi
wa mgogoro huo, lakini wakati ilitaka pande hizo mbili zikutane na
kukokotoa viwango vya tozo hizo, fedha hizo zilitolewa na kulipwa kwa
mmiliki mpya wa Kampuni ya Pan African Power Solutions (PAP), jambo
lililosababisha kuibuka kwa kashfa hiyo. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza
kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
MAGAZETI YA LEO JUMATANO DESEMBA 03, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
WARIOBA: ESCROW NI MATOKEO YA KATIBA ISIYO NA MAJIBU
Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba. PICHA|MAKTABA
Mwenyekiti wa
iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amesema wizi
wa Sh306 bilioni katika Akaunti ya Tegeta Escrow, mvutano kati ya
mihimili ya dola na viongozi kukosa maadili ni matokeo ya nchi kuwa na
Katiba isiyo na majibu ya masuala hayo.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na gazeti hili, Jaji Warioba alisema Bunge la Katiba lilifanya makosa kutoviweka vifungu vinavyozungumzia mambo hayo katika Katiba Inayopendekezwa ambavyo awali vilipendekezwa na Tume yake katika rasimu ya pili.
“Katika mchakato wa Katiba Mpya tulisema kuwe na mgawanyo wa madaraka na kila mtu ajue madaraka yake ni nini na kutenganisha Serikali na Bunge. Kama Serikali na Bunge vingetenganishwa bungeni usingeibuka mvutano kuhusu waliochota fedha za escrow. Bunge lingekuwa huru katika utendaji wake wa kazi,” alisema. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Akizungumza katika mahojiano maalumu na gazeti hili, Jaji Warioba alisema Bunge la Katiba lilifanya makosa kutoviweka vifungu vinavyozungumzia mambo hayo katika Katiba Inayopendekezwa ambavyo awali vilipendekezwa na Tume yake katika rasimu ya pili.
“Katika mchakato wa Katiba Mpya tulisema kuwe na mgawanyo wa madaraka na kila mtu ajue madaraka yake ni nini na kutenganisha Serikali na Bunge. Kama Serikali na Bunge vingetenganishwa bungeni usingeibuka mvutano kuhusu waliochota fedha za escrow. Bunge lingekuwa huru katika utendaji wake wa kazi,” alisema. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
SPIKA ASEMA WALIOKEKETWA HAWAFAI
Spika
wa Bunge la Uganda Bi Rebecca Kadaga amewashauri wanaume kutowaoa
wanawake waliokeketwa akiwataja kuwa mzigo ambao hauwezi kuijenga jamii.
Kulingana
na gazeti la daily Monitor,Spika Kadaga alitoa wito huo wakati wa
sherehe ya kitamaduni ambayo inapinga ukeketaji ilioandaliwa na mfuko wa
umoja wa mataifa unaosimamia idadi ya watu na wahisani wengine. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza
kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo TzMLIPUKO MKUBWA MOGADISHU
Mlipuko mkubwa umetokea katika mji wa Mogadishu nchini Somalia karibu na uwanja wa ndege.
Duru zimearifu kuwa mlipuko huo huenda umesababishwa na mtu aliyejitolea muhanga aliyejilipua ndani ya gari.Kundi la wapiganaji wa kiislamu la Al- Shaabab mara kwa mara hutumia milipuko ya magari, lakini kufikia sasa halijakiri kuhusika na mlipuko huo.
Haijajulikana ni watu wangapi wameuwawa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
DROO YA KOMBE LA AFRIKA KUFANYIKA LEO
Mabingwa
wa zamani Zambia na waandalizi wa kombe la bara Afrika Equitorial
Guinea ni miongoni mwa timu zitakazoorodheshwa katika droo ya kombe hilo
la mwaka 2015 Jumatano usiku.
Shirikisho la soka barani Afrika
CAF tayari limezigawanya timu hizo 16 katika makundi vyungu vinne vya
kinyang'anyiro hicho cha january 17 hadi februari 8.Hatua hio ilifanyika kulingana na utendaji wa timu hizo katika awamu tatu ya michuano hiyo na mechi za kufuzu katika kipindi hicho hicho.
Miongoni mwa vitu ambavyo vilitiliwa mkazo ni matokeo ya mechi za kufuzu kwa kombe la dunia mwaka 2014.
Droo hiyo ambayo itabuni makundi manne yanayoshirikisha timu moja moja kutoka kila chungu itafanyika mjini malabo jumatano usiku. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Ghana na Ivory Coast ni timu nyengine kubwa huku washindi wa pili wa mwaka 3013 Burkina Faso wameorodheshwa katika kundi la Pili.
2015 Nations Cup :Timu zilivyowekwa.
Pot 1: Equatorial Guinea, Ghana, Ivory Coast, Zambia
Pot 2: Burkina Faso, Mali, Tunisia, Algeria
Pot 3: Cape Verde, South Africa, Cameroon, Gabon
Pot 4: Guinea, Senegal, DR Congo, Congo
Monday, December 01, 2014
RAIS KIKWETE AMTEUA PROFESA ASSAD KUWA CAG MPYA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Profesa Mussa Juma Assad kuwa
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Taarifa iliyotolewa leo, Jumatatu, Desemba Mosi,
2014 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, inasema kuwa uteuzi
wa Bwana Assad ulianza Novemba 5, mwaka huu, 2014.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa Bwana Assad ataapishwa kesho, Jumanne, Desemba 2, saa nne asubuhi, Ikulu, Dar es Salaam. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza
kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
BOKO HARAM WAVAMIA MIJI MIWILI NIGERIA
Watu
wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa Boko Haram wamefanya mashambulizi
katika miji miwili eneo la Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
La kwanza lilikuwa la kujitoa mhanga pamoja na shambulizi lengine katika kituo cha polisi cha Damaturu.Wenyeji wa mji wa Maiduguri walielezea kusikia milipuko miwili kwenye soko moja.
Mashambulizi mengine ya kujitoa mhanga eneo hilo wiki iliyopita yaliwaua zaidi ya watu 70.
Mapema leo Jumatatu watu wanaokisiwa kuwa wanamgambo wa Boko Haram waliteketeza kituo cha polisi katika mji wa Damataru kilicho umbali wa kilomita 100 Magharibi mwa mji wa Maiduguri.
Inaarifiwa watu 5 wameuawa katika mashambulizi hayo ya mabomu yaliyotokea katika soko lililokuwa na watu wengi.
Mjini Damaturu , milipuko na milio ya risasi ilisikika huku wanamgambo hao walipokuwa wanashambulia mjini huo.
Boko Haram imeahidi kubuni dola ya kiisilamu katika maeneo ambayo kundi hilo linadhibiti.
Milipuko hio ilitokea Jumatatu katika soko la Maiduguri , mji mkuu wa jimbo la Borno ambayo ilisababishwa na wasichana wawili waliojilipua.
Takriban watu 32 walijeruhiwa katika milipuko hio. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
ICC YAKATAA OMBI LA MUASI LUBANGA
Mahakama
ya kimataifa ya ICC mjini Hague, imetupilia mbali ombi la rufaa
lililowasilishwa na muasi wa zamani nchini DRC Thomas Lubanga dhidi ya
hukumu aliyopewa kwa makosa ya kuwatumia watoto kama wanajeshi.
Viongozi
wa mashtaka walisema wavulana wadogo wenye umri wa miaka 10 walitekwa
nyara na kusajiliwa kama wanajeshi DRC katika vita hivyo vilivyoanza
mwaka 1999.Wasichana nao walitumiwa kama watumwa wa ngono.
Mnamo mwaka 2012, Lubanga alikuwa mtu wa kwanza kuhukumiwa na mahakama hio.
Aliwahi kuwa kiongozi wa kundi la wapiganaji la (UPC), ambalo lilikuwa la kabila la Hema ambalo lilihusika katika vita eneo la Ituri Mashariki mwa DRC.
Mahakama ilimpata na hatia kwa kuwatumia watoto kama wanajeshi na kuwatuma kwenda kumpigania. Alihukumiwa kifungo cha miaka 14.
Kundi la UPC, lilikuwa moja ya makundi sita ya wapiganaji waliopigana kudhibiti eneo lenye utajiri wa madini la Ituri hadi mwaka 2003.
Mgogoro ulianza kama mvutano wa kupigania mali asili, ingawa baadaye ilipanda daraja na kuwa vita vilivyohusisha jeshi la Uganda.
Kadhalika mgogoro huo uligeuka na kuwa vita kati ya jamii za Hema na Lendu ambapo takriban watu 50,000 waliachwa bila makao. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Subscribe to:
Posts (Atom)