Wednesday, November 19, 2014

WAPINZANI WAMSULUBU MWAKYEMBE BUNGENI


Dk Harrison Mwakyembe

Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, jana ilimsulubu Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe ikieleza kuwa wizara yake iliingia mkataba wa mradi wa treni za kisasa kutoka Stesheni ya Dar es Salaam hadi Pugu kupitia Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA) bila kufuata taratibu.
Kambi hiyo ililieleza Bunge kuwa mkataba huo ulisainiwa baina ya mmiliki wa Kampuni ya M/s Shumoja, Robert Shumake na Shirika la Reli Tanzania huku Waziri Mwakyembe akishuhudia.
Msemaji Mkuu wa kambi hiyo, Ofisi ya Waziri Mkuu,  Uwekezaji na Uwezeshaji, Pauline Gekul alitoa madai hayo wakati akiwasilisha maoni ya kambi hiyo kuhusu muswada wa marekebisho ya Sheria ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPP). Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

NABII: "URAIS 2015 BALAA!... JK ASINGEWAHI KUPASULIWA, NCHI INGECHAFUKA"

NABII wa Kanisa la The Revelation lililopo Buza Kipera jijini Dar, Yaspi Bendera amesema uchaguzi mkuu ujao utakuwa balaa kubwa kufuatia maono anayoyaona wakati akishiriki ibada katika nyakati mbalimbali, Risasi Jumatano linakupa mkanda kamili.

Nbii wa Kanisa la The Revelation lililopo Buza Kipera jijini Dar, Yaspi Bendera.
Akizungumza wakati wa ibada kanisani kwake na baadaye na waandishi wetu Novemba 16 mwaka huu, Nabii Yaspi alisema kuna mgongano mkubwa miongoni mwa watu wanaotajwa kugombea urais, ili kumrithi rais Jakaya Kikwete ambaye alimwelezea kama kiongozi anayemuona kiroho kila mara.


“Nilimuona katika maono yangu kama mtu aliye kwenye majaribu makubwa kiroho, nikaandaa maombi hapa kanisani na tukamuombea kwa muda wa nusu saa na tunashukuru Mungu hali yake inaendelea vizuri baada ya kufanyiwa upasuaji wa tezi dume nchini Marekani. Bado namuona akiwa na maumivu kuanzia sehemu za kiuno, uti wa mgongo na shingoni mwake.

Mhe. Edward Lowasa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO NOVEMBA 19, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MOTO WATEKETEZA SOKO LA BIDHAA ZA UTAMADUNI JIJINI ARUSHA


Baadhi ya Mabaki ya bidhaa zilizoteketea kwa moto katika SOKO la bidhaa za utamaduni lijulikanalo kwa jina la MT.MERU CURIOS& CRAFTS MARKET usiku wa kuamkia leo. 

Bango la Soko hilo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

UJERUMANI YAIUA HISPANIA 1-0

Mario Gotze, who scored Germany's winning goal at the World Cup final, is put under pressure by Cesar Azpiliciueta and Sergio Busquets 
Mario Gotze akiwapita Cesar Azpiliciueta wa Sergio Busquets wa Hispania katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa mjini Vigo. Ujerumani ilishinda 1-0, bao pekee la Toni Kroos dakika ya mwisho.
Gotze is grounded under the challenge of Spain defender Sergio Ramos as the rain beings to fall in Vigo on Tuesday evening
Gotze akienda chini baada ya kukwatuliwa na beki wa Hispania, Sergio Ramos. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Tuesday, November 18, 2014

VIONGOZI MANYARA, KITETO WAKALIA KUTI KAVU


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akitoa kauli ya serikali bungeni jana, kuhusu mauaji ya wakulima na wafugaji wa Wilayani Kiteto, Mkoani Arusha.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amesema Serikali itafanya mabadiliko ya kiutawala katika ngazi mbalimbali Wilaya ya Kiteto na Mkoa wa Manyara wiki hii ili kuimarisha uongozi kukabiliana na mauaji ya wakulima na wafugaji yaliyosababisha vifo vya watu 17 tangu Januari 12 mwaka huu hadi sasa.

Pinda alisema hayo bungeni mjini Dodoma jana wakati akitoa taarifa kuhusu vurugu zinazoendelea Kiteto kati ya wafugaji na wakulima na kusababisha mauaji.

Alisema mabadiliko ya uongozi wa kiutawala katika eneo hilo ni moja ya hatua ambazo zinachukuliwa kitaifa nyingine zikiwa ni kuendelea kutoa elimu kwa umma juu ya kuondoa na kuepuka na kutatua migogoro inayojitokeza kwa njia ya amani. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE NOVEMBA 18, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KANALI AHUKUMIWA KUNYONGWA, CONGO

Waaandamaji wakipinga kuuawa kwa Kanal Ndala
Mahakama ya kijeshi Mashariki mwa Jamuhuri ya Demokrasi ya Congo imemhukumu kifo Kanali Birocho Nzanzu baada ya kubainika na makosa ya kutaka kumuua afisa wa jeshi la nchi hiyo aliyekuwa mstari wa mbele kutokomeza wapiganaji wa M23.
Kanal Mamadou Ndala anayedaiwa kuuawa na njama za Kanal Birocho Nzanzu
Afisa anayedaiwa kupangiwa njama za kuuawa ni Mamadou Ndala mabaye kwa kiasi kikubwa aliamini katika vita dhidi ya kundi hilo la wapiganaji na ambaye aliuawa mwezi januari mwaka huu. Hata hivyo hukumu hiyo imetolewa kwa watuhumiwa nane ambapo kati ya hao mmoja ndiye Kanali Ndala aliyehukumiwa kifo. Mahakama imebainisha kuwa Kanali Nzanzu amekuwa akitumiwa na waasi wa ADF kutoka Uganda kuandaa maujaji. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

GAVANA ATANGAZA HALI YA HATARI, MISSOURI


Machafuko Missouri

Gavana wa jimbo la Missouri nchini Marekani ametangaza hali ya hatari kabla ya kutolewa uamuzi muhimu kuhusu kumfungulia mashitaka ya jinai au la dhidi ya afisa wa polisi mzungu, ambaye alimuua kwa kumpiga risasi kijana wa Kiafrika ambaye hakuwa na silaha.
Mauaji hayo yaliyotokea katika mji wa Ferguson mwezi Agosti yalisababisha vurugu katika mitaa kwa siku kadha na kuamsha mjadala kuhusu uhusiano kati ya polisi na jamii ya watu weusi nchini Marekani.
Idara ya polisi ya Kaunti ya St. Louis ndiyo wanaosimamia maandamano yoyote. Meya wa St. Louis, Francis. Slay, amezungumzia kuhusu tahadhari wanayochukua. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Monday, November 17, 2014

MKAPA ATAKA WAZEE NCHINI WASIBEZWE


Rais Mstaafu Benjamin Mkapa  

Rais Mstaafu, Benjamini Mkapa, amewataka viongozi na Watanzania kutobeza busara na hekima za wazee kwa kuwa bado wana mchango mkubwa kwa Taifa.

Kadhalika mkuu huyo wa zamani wa nchi, alisema kuwa, mzee kuota mvi kichwani haina maana ya kupungukiwa na hekima na maarifa kama wengi wanavyofikiria

Mkapa alitoa kauli hiyo juzi jioni wakati mahafari ya kwanza ya Shule ya Sekondari ya St Peter Claver iliyoko nje kidogo ya Mji wa Dodoma.

Alisema anashangazwa kuona maeneo mengi wazee wanapuuzwa na kudharauliwa kama vile hawana mchango wowote kwa maendeleo ya jamii. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

PROF. MAGHEMBE ASEMA URAIS SIO MASHINDANO YA UREMBO

Waziri wa Maji, Prof Jumanne Maghembe akizungumza na waandishi wa habari wa gazeti hili, walipomfanyia mahojiano maalumu ofisini kwake mjini Dodoma, hivi karibuni. 

Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe ameshangazwa na utitiri wa watu wanaotaka kugombea urais kwenye Uchaguzi Mkuu 2015, akisema nafasi hiyo ya juu nchini haifanani na mashindano ya urembo ambayo mtu yeyote anaweza kujaribu.

Mbunge huyo wa Mwanga alisema watu hao wanaojitokeza kuwania urais hawaelezi wanataka kulifanyia nini Taifa na akashauri wasioweza kueleza hoja zao wasichaguliwe kushika nafasi hiyo.

“Urais unahitaji kuwa na sifa, dira na ajenda kwa Taifa,” alisema Profesa Maghembe wakati wa mahojiano maalumu na gazeti hili mjini hapa.

Kauli ya Profesa Maghembe imekuja wakati Taifa likijiandaa kwa Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba, 2015, huku chama chake, CCM kikikabiliwa na kazi ngumu ya kumpata mrithi wa Rais Jakaya Kikwete ambaye anamaliza muda wake. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SHY-ROSE, SPIKA ZZIWA KIKAANGONI TENA


Mbunge Shy-Rose Bhanji.
Bunge la Afrika Mashariki (Eala) limeitishwa tena, zamu hii jijini Nairobi, Kenya ambako litakutana kuanzia leo mchana, huku kukiwa na shinikizo kubwa kutoka kwa wabunge 32 linalotaka kung’olewa kwa Spika wa Bunge hilo, Dk Margaret Zziwa na kuwajibishwa kwa mbunge kutoka Tanzania, Shy-Rose Bhanji.
Bunge hilo linakutana baada ya kuahirishwa kwa muda usiojulikana kutokana na kukosekana kwa mwafaka baina ya wabunge kwa upande mmoja na baadhi ya wabunge na Spika Zziwa kwa upande mwingine lilipokutana Kigali, Rwanda hivi karibuni. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBA 17, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WAZIRI AJIUZULU KUPISHA UCHUNGUZI

 
Miguel Macedo waziri wa mambo ya ndani wa Ureno aliyejiuzulu 
 
Waziri wa mambo ya ndani wa Ureno amejiuzulu kupisha uchunguzi kuhusu tuhuma za rushwa inayohusishwa na utoaji vibali vya mgawo wa makazi.
Miguel Macedo amesema hahusiki na kashfa hiyo lakini anajiuzulu kulinda heshima ya taasisi za serikali.
Polisi wamewakamata watu 11, akiwemo mkuu wa idara ya uhamiaji nchini humo, siku ya Alhamisi.
Ureno inatoa visa za daraja la kwanza kwa wageni wanaotaka kuwekeza nchini humo.
Mnufaika mkuu wa uharakishaji wa vibali ni raia wa China ambao wamekuwa wakiwekeza kiasi kikubwa nchini Ureno.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAFUA YA NDEGE YATHIBITISHWA UINGEREZA

Ndege wanaofugwa wanakabiliwa na milipuko ya mafua ya ndege

Mlipuko wa mafua ya ndege umethibitishwa katika shamba moja la kuzalishia bata mashariki mwa Yorkshire, nchini Uingereza, wamesema maafisa.
Wizara ya Mazingira, Chakula na Masuala ya Vijijini (Defra) imesema hatari kwa afya ya umma ni ndogo sana. Ndege wasiohitajika wanaondolewa kutoka eneo hilo na eneo la kuwatenga limeandaliwa.
Tatizo hilo bado halijathibitishwa, lakini aina ya kirusi cha H5N1 hakijaweza kubainishwa na maafisa wa Defra.
Kirusi hicho husambaa kati ya ndege na katika matukio ya nadra, kinaweza kuwaathiri binadamu.
Picha ikimwonyesha mchuzi akiuza bata wake katika mtaa mmoja mjini Shanghai,China
Eneo la kuwatenga ndege lililopo kuzunguka shamba hilo litazuia ndege na kinyesi cha ndege ndani au nje ya eneo hilo.Ndege wote pia watatengwa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...