Thursday, November 13, 2014

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS NOVEMBA 13, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MWANAMKE AFUNGWA JELA KWA KUFADHILI ISIS


Amal alimuo9mba rafiki yake kumpelekea mumewe anayepigana nchini Syria pauni 15,800

Mwanamke mmoja nchini Uingereza aliyeshitakiwa kwa kumfadhili mumewe aliyejiunga na vita nchini Syria, amefungwa jela kwa zaidi ya miaka miwili.
Amal El-Wahabi, mwenye umri wa miaka 28, alijaribu kumhadaa rafiki yake kumbebea pauni 15,800 hadi nchini Uturuki ambako mumewe angeweza kuzichukulia.
Jaji aliyetoa uamuzi katika kesi hiyo, Nicholas Hilliard, alimwambia El Wahabai kuwa alifahamu vyema kwamba mumewe Aine Davis alikuwa anapigana nchini Syria na kwa hivyo alikuwa anamsaidia katika harakati zake.
Davis, ambaye alikuwa mlanguzi wa dawa za kulevya pamoja na kushtakiwa kwa kosa la kumiliki silaha, aliondoka Uingereza mwaka 2013 kwenda Syria kupigana na kundi la Isis. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SHELL YADAIWA ILIPUUZA ONYO NIGERIA


Mafuta yaliyovuija yaliathiri mazingira na kusababisha watu kuapoteza kazi.

Mawakili wanaoiwakilisha jamii ya watu walioathiriwa na uchafuzi wa mazingira anasema wakuu wa kampuni ya mafuta ya Shell walijulishwa mapema kuhusu kuchakaa kwa mabomba yake ya mafuta.
Hii ilikuwa kabla ya kutokea kwa visa vya kumwagika mafuta mara mbili hivyo kuchafua pakubwa eneo hilo Lagoniland Kusini mwa Nigeria mwaka 2008.
Shell inakana kwamba ilikuwa na taariifa kuwa mabomba hayo yalihatarisha usalama.
Shell inadai mabomba hayo yalipasuliwa na wezi wa mafuta lakini mawakili hao wamejibu kwamba mabomba hayo yalikwa duni na yalimwaga mafuta hata kwenye ziwa la eneo hilo ambako sasa uvuvi haufanyiki tena. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Wednesday, November 12, 2014

MATUMIZI YA KONDOM YAPUNGUA NCHINI...!!!




Imeelezwa kuwa maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU), yanaweza kuongezeka nchini hasa kwa vijana kutokana na kubainika kupungua kwa kasi ya matumizi ya mipira (kondomu).

Hayo yalielezwa jana na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Dk Florens Turuka katika mkutano wa sita wa kutathmini maambukizi ya VVU nchini.

Dk Turuka alisema maambukizi mapya yameendelea kuwapo kwa sababu vijana hawatumii kondomu kujikinga.

“Matumizi ya kondomu katika jamii yamepungua na kuwafanya watu wengi hasa vijana kupata maambukizi na zaidi ni kutokana na mwamko mdogo kuhusu umuhimu wa kondomu kama kinga ya Ukimwi,” alisema. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SITTI MTEMVU KUVUA TAJI LA MISS TEMEKE NA MISS CHANG’OMBE


HAIJAKAA sawasawa! Siku chache baada ya Sitti Abbas Mtemvu (25) kujivua taji la Miss Tanzania 2014 kwa madai ya kusakamwa na vyombo vya habari kuhusu umri wake, wadau wamemwangushia uwajibikaji  mwingine wakimtaka avue mataji mengine mawili.
 
Aliyekuwa Miss Tanzania 2014 Sitti Abbas Mtemvu.
Baadhi ya wadau wa sanaa waliozungumza na Risasi Mchanganyiko Jumatatu iliyopita jijini Dar walisema kama kweli Sitti ana dhamira safi ya kukwepa kusakamwa basi ni bora kwake akavua na mataji ya Miss Chang’ombe na Miss Temeke ambayo ndiyo yaliyompa tiketi ya kwenda kambi ya Miss Tanzania na kushinda. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO NOVEMBA 12, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WAUMINI WAMZUIA ASKOFU MKUU ASIINGIE OFISINI KWAKE...!!!




  Askofu Kiongozi wa Kanisa la Moravian Tanzania, Alinikisa Cheyo


Askofu Kiongozi wa Kanisa la Moravian Tanzania, Alinikisa Cheyo amezuiwa na waumini wa kanisa hilo kuingia katika ofisi yake iliyopo Jakaranda, Mbeya kwa saa 18.
Cheyo, ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Magharibi, alifungiwa mlango na waumini wa kanisa hilo Usharika wa Jakaranda kumzuia asiingie mpaka atakapoitisha mkutano na kumrudisha Mchungaji Nosigwe Buya ambaye alimhamisha.
Akizungumzia hatua hiyo mbele ya waumini wengine, Mchungaji wa usharika huo, Jamson Mwilugumo alisema walifunga mlango huo kushinikiza Askofu Cheyo abadili msimamo wa kumwondoa Mchungaji Buya na kumrejeshea wadhifa wake wa Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya jimbo hilo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

HII NDIO SAA GHALI ZAIDI DUNIANI

Saa ghali zaidi duniani iko Uswiss
Saa ghali zaidi duniani imenunuliwa mnadani huko Geneva,Uswiss kwa gharama ya dola za kimarekani milioni 21.3.
Saa hiyo imetengenezwa kwa kutumia karati ishirini na moja za dhahabu na ina uzito wa nusu kilo,saa hiyo iliyoundwa kwa mbwembwe ilitengenezwa mahsusi kwa ajili ya mtoto wa mfanya biashara,Henry Graves mnamo mwaka 1930.
Na ilimchukua miaka nane kwa watengeneza saa maarufu wa Uswis kuikamilisha hiyo saa ghali ambaye ni Patek Philippe.
Saa hiyo ilinunuliwa siku mbili tu baada ya mmiliki wa mwisho kufariki dunia kutoka falme za kiarabu Saud Bin Mohammed Al-Thani.
Mmiliki huyo alikuwa na madeni mengi ambayo yangemgharimu nyumba yake kuuzwa na hivyo akaikabidhi saa hiyo kwenye nyumba ya mnada ya Sothebys. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WATU WATATU WACHINJWA KISA MAONI WALIYOTOA KWENYE MITANDAO

Mjini Derna, kundi la Is limeshika hatamu
Wanaharakati watatu wa kisiasa nchini Libya wamechinjwa baada ya kuandika katika mitandao ya kijamii juu ya maisha chini ya utawala wa dola ya kiislam.Miili yao ilipatikana mapema wiki hii mashariki mwa mji wa Derna karibu na Benghazi.
Tukio hilo lilianzia kwa wanaharakati hao kutekwa mapema mwezi huu.Mji huo wa Derna uko chini ya mamlaka ya kikundi cha dola ya kiislam tangu mwaka 2012 ambacho kimekiri kuwa sehemu ya kundi la is.
Mnamo mwezi August mwaka huu katika video ilooneshwa katika mitandao ya kijamii ilionesha mwanamume mmoja akipigwa risasi na kufa hadharani katika viwanja vya mpira mjini Derna.
Siku za hivi karibuni kuna picha iloachiliwa mitandaoni ikionesha kikundi cha kijamii kinachojiita mahakama ya kiislam. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC Swahili

CAF YAIENGUA MOROCCO AFCON 2015

moroc
Timu ya Taifa ya Morocco imeondolewa katika michuano ya Fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) 2015, kutokana na maamuzi ya nchi hiyo kujitoa kuwa mwenyeji wa mashindano hayo yaliyotarajiwa kuanza Januari mwakani, Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) limethibitisha leo baada ya kukutana jijini Cairo, Misri jana.


Nchi hiyo ya Kaskazini mwa Afrika ilifikia maamuzi ya kujitoa kuwa mwenyeji wa mashindano hayo ya Bara la Afrika kwa kuonesha hofu ya kuenea kwa Ebola, ugonjwa ambao umelipuka Magharibi mwa Afrika. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Tuesday, November 11, 2014

POLISI YAWATAWANYA WAFUASI WA MBOWE KWA MABOMU


Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (chadema), Freeman Mbowe 

Wafuasi wa (Chadema) wilayani Mpanda jana jioni walilazimika kutafuta vichochoro vya kukimbilia baada ya polisi kusambaratisha kwa mabomu ya machozi, maandamano ya kumsindikiza Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe baada ya mkutano.

Patashika hiyo ilitokea baada ya mkutano wa Mbowe kumalizika na wafuasi wake kutaka kumsindikiza hotelini, jambo ambalo polisi hawakulikubali.

Baada ya wananchi hao kuanza maandamano hayo, polisi walifyatua mabomu takriban 15 yaliyowafanya wafuasi wote kutawanyika na kusababisha taharuki miongoni mwa wakazi wa mji huo. Dakika chache baada ya tukio hilo, umeme ulikatika mji mzima.

Tofauti na maeneo mengine aliyofanya ziara zake kama Tabora, Sikonge na Igunga ambayo wafuasi walikuwa wakimsindikiza, polisi wa Mpanda walijipanga ipasavyo tangu mapema kuhakikisha hali hiyo haitokei. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

INTERPOL YAWASAKA WACHINA 30 KWA UJANGILI WA TEMBO

Kamishna wa Interpol Tawi la Tanzania, Gustav Babile 

Siku tano baada ya Serikali kukanusha vikali ripoti ya Shirika la Kimataifa la Mazingira (EIA) iliyoihusisha China na utoroshaji wa meno ya tembo nchini wakati wa ziara ya Rais wa nchi hiyo, Xi Jinping mwaka jana, Shirika la Polisi la Kimataifa (Intepol), Tawi la Tanzania limesema linawatafuta raia zaidi ya 30 wa China ambao wanatuhumiwa kusafirisha meno ya tembo na kufanya uharamia wa kimazingira katika hifadhi za Taifa nchini.
Kauli ya Interpol inakuja huku kukiwa na mkanganyiko kuhusu kashfa hiyo iliyosambaa wiki iliyopita kupitia vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa ambayo hata hivyo, Serikali imekanusha kupitia Ikulu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Wizara ya Maliasili na Utalii huku ubalozi wa China nchini nao ukitoa tamko la kukanusha taarifa hizo.
Kamishna wa Interpol Tawi la Tanzania, Gustav Babile alisema jana kuwa raia hao wa China wanatafutwa popote walipo duniani na hivyo watakapopatikana watakamatwa.
“Tunawatafuta popote duniani kwa usafirishaji wa meno ya tembo na uharamia wa mazingira, wakipatikana watachukuliwa hatua,” alisema Kamishna Babile. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ASKOFU ANASWA NA UNGA!

          
KIMENUKA! Vigogo wa madawa ya kulevya wakiwemo viongozi wa dini sasa wanaanza kupukutika kutoka kwenye mstari wa siri huku baadhi yao wakikimbilia nje ya nchi kufuatia oparesheni kali inayofanywa na Kikosi cha Kupambana na Kudhibiti Madawa ya Kulenya Tanzania kuwanasa kila kukicha, Uwazi  lina mchoro kamili.Askofu Emeka Nwachukwu Mert raia wa Nigeria anayehusishwa na biashara ya madawa ya kulevya.
Hivi karibuni kikosi hicho kimemkamata askofu (mwangalizi mkuu wa kanisa) aliyetambulika kwa jina la Emeka Nwachukwu Mert raia wa Nigeria ambaye ana kanisa la kiroho maeneo ya Sinza jijini Dar.
Jina la kanisa hilo limedhibitiwa na vyombo husika kwa sababu ya uchunguzi zaidi na uhalali wake wa kuwepo nchini.
SIKU YA TUKIO
Vyanzo vyetu makini ndani ya kikosi kazi vinaeleza kwamba, mchungaji huyo alikamatwa Oktoba 31, mwaka huu saa kumi usiku Tegeta wilayani Kinondoni, Dar es Salaam akiwa na madawa ya kulevya ‘unga’ aina ya heroine kilo 35.
KAMA UNGEINGIA SOKONI
 Habari za ndani kutoka kwenye oparesheni hiyo zinasema kuwa, endapo unga huo ungeingia sokoni na kununuliwa, basi mtumishi huyo wa Mungu angevuna kitita cha zaidi ya shilingi bilioni mbili.
NYUMBA ALIYONASIWA YA PROFESA
Mchungaji huyo ambaye serikali imeanza kazi ya kulichunguza kanisa lake, alidakwa na mzigo huo haramu kwenye makazi aliyopanga ambayo ni nyumba ya profesa mmoja wa chuo kikuu, Mbezi jijini Dar es Salaam.
Askofu akiwa chini ya ulinzi.
WASHIRIKA NAO WADAKWA
Kwa mujibu wa chanzo, kamatakamata ya mchungaji huyo pia iliwakumba watuhumiwa wengine ambao ni Walyat Khan raia wa Pakistani, Chuksi Sylvester Agbazuo na Tony Olafor wote raia wa Nigeria na inadaiwa kwamba walikuwa wakikamatwa maeneo mbalimbali na kutoroka.
HABARI NYETI
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MKE ANAYEISHI NA WAUME WAWILI MAPYA YAIBUKA


Sakata la mke kuishi na waume wawili  limechukua sura mpya baada ya kikao cha ndugu wa mume halali, Rogers Halinga kuketi kikao katika Kijiji cha Ishungu, Kata ya Ruiwa Mbarali, mkoani Mbeya na kumtaka Biton Mwashilindi kufanya mazungumzo nao kabla hawajafungua madai ya ugoni mahakamani na kudai fidia.
Rogers Halinga akiwa na baba yake mzee Jason Halinga na mtoto anayedaiwa kugombaniwa.
Kikao hicho kizito kilichofanyika nyumbani kwa baba mzazi wa Rogers, mzee Jason Halinga (95), Novemba mosi mwaka huu na kuhudhuriwa na ndugu lukuki nia ilikuwa kumsikiza mke wa Rogers, Juliana (22)  ili abainishe ukweli juu ya mtoto aliyezua utata kuwa ni wa nani baina ya mumewe (Rogers) na Biton Mwashilindi. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ROONEY AKIJIANDAA KUICHEZEA ENGLAND MCHEZO WA 100,ATEMBELEA SHULE YAKE YA MSINGI

7
Mshambuliaji wa England Wayne Rooney akijiandaa kuandika historia ya kuwa miongoni mwa wachezaji walioichezea timu yao ya Taifa michezo 100 na zaidi.
Mara nyingi wachezaji wa England wanapokuwa wamecheza michezo 99 huwa na utamaduni wa kwenda kwenye shule zao na kupigia picha na jumla ya wanafunzi 99
England inajiandaa kucheza mchezo wa kufuzu fainali za Euro 2016 dhidi ya Slovenia mwishoni mwa juma hili kwenye dimba la Wembley,huenda Rooney ambaye pia ni nahodha wa kikosi hicho akatimiza mchezo wa 100 siku iyo na kuwa mchezaji wa 9 kuichezea England michezo 100.
6 Baadhi ya wachezaji wengine waliofanikiwa kuvaa jezi ya England mara 100 na zaidi katika kipindi cha miaka 142 tangu timu hiyo ianzishwe ni: 5 Peter Shilton, David Beckham, Steven Gerrard, Bobby Moore, Ashley Cole, Frank Lampard, Bobby Charlton na Billy Wright – Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...