Tuesday, August 19, 2014

UAMUZI MGUMU CCM KATIKA KAMATI KUU LEO

Kamati Kuu (CC) ya Halmashauri Kuu ya CCM inakutana leo mchana mjini Dodoma chini ya mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete huku ikitarajiwa kufanya uamuzi mgumu wa mchakato wa Katiba.

Kikao hicho kinaketi mara ya pili katika muda mfupi, baada ya hivi karibuni kukaa jijini Dar es Salaam na kueleza kuridhishwa na mchakato huo.

Hata hivyo, safari hii kikao hicho kinaketi kukiwa na maswali lukuki ambayo hayajapata majibu: Je, Bunge la Katiba liendelee au livunjwe? Je, lisitishwe kwa muda kupisha maridhiano au la? Je, kuna umuhimu wa maridhiano? Kuna ulazima wa kuwapo Ukawa bungeni?

Akizungumzia kikao hicho, mtaalamu wa sayansi ya siasa na utawala katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Alexander Makulilo alisema jambo kubwa litakalojadiliwa katika kikao hicho ni kauli tofauti zilizotolewa na wananchi kuhusu mchakato wa kupata Katiba Mpya. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

"KAULI YA WEREMA NI YA KINAFIKI" MBATIA


Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia (kulia) akizungumza na waandishi jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Mosena Nyambabe.


Siku moja baada Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema kueleza kuwa hakuna mwenye mamlaka kisheria kuvunja au kusitiza Bunge la Katiba, mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi amesema kauli hiyo imejaa unafiki na kwamba upo uwezekano wa kuahirisha vikao kwa muda mpaka mwafaka wa kitaifa utakapopatikana.

Mwenyekiti huyo, James Mbatia amesema kuahirisha Bunge kunawezekana kama ambavyo iliwezekana kusitishwa vikao vya Bunge hilo Aprili mwaka huu kupisha Bunge la Bajeti na kubadilishwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba kinyemela kwa kuongeza idadi ya siku za Bunge la Katiba kutoka 70 hadi 90 mpaka kuwa muda wowote ambao utaonekana unafaa.

Wakati Mbatia akieleza hayo, jana waliibuka wazee wa Jiji la Dar es Salaam wakiwataka Watanzania kuyaombea makundi yanayovutana na moja likisusia vikao vya Bunge hilo vinavyoendelea mjini Dodoma, ili yakutane na yakubali kufikia mwafaka kwa pamoja.

Kauli ya Mbatia

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mbatia alisema kauli iliyotolewa juzi na Jaji Frederick Werema imejaa unafiki. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE AGOSTI 19, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SOMA ALICHOANDIKA MAULID KITENGE BAADA YA KUACHA KAZI ITV/ RADIO ONE

Screen Shot 2014-08-19 at 8.22.01 AM 
Maulid Kitenge yuko kwenye orodha ya Watangazaji wa muda mrefu wa michezo nchini Tanzania ambapo ujazo wa jina lake uliongezeka baada ya kuanza kufanya kazi na ITV/RadioOne zaidi ya miaka 10 iliyopita.
August 18 2014 Maulid aliandika yafuatayo kwenye page yake ya twitter >>> ‘Namshukuru sana Mungu leo nimemaliza miaka 14 ya kutumika kuwa kama mtangazaji wa michezo Radio one stereo na hakika naondoka rasmi
Mpaka asubuhi ya August 19 2014 Maulid alikua hajaandika tweet nyingine ya anakokwenda au atakachofanya baada ya kuondoka ITV/Radio One
Screen Shot 2014-08-19 at 8.16.51 AM

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WATU WEUSI WABAGULIWA KOREA KUSINI...!!!

Watu weusi wanyanyapaliwa Korea Kusini
Tangu kuanza kwa ugonjwa wa Ebola kumekuwapo na malalamiko ya watu wanaotoka Barani Afrika kutengwa kwa kutopewa huduma za kijamii nchini Korea ya kusini ikiwamo kutoruhusiwa kuingia katika Migahawa na usafiri wa umma kwa madai ya kuwa huenda wana virusi vya Ebola.

Aidha, baadhi yao wamedai watu weusi wanaposimamisha TAXI hazisimami kutokana na hofu ya virusi hivyo vya Ebola. Nimezungumza na Kijana RWEHUMBIZA KALANGALI,ambaye ni mwanafunzi anayesoma huko Korea Kusini, na hapa anaeleza hali ilivyo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

OBAMA ASIFU MAJESHI YA IRAQ NA KURD

Rais wa Marekani, Barack Obama
Rais wa Marekani Barack Obama amesema majeshi ya Iraq na yale ya Kikurd yamepiga hatua kubwa kulitwaa tena bwawa muhimu la Mosul kutoka kwa wapiganaji wa kiislamu kaskazini mwa Iraq.
Amesema wamethibitisha kwamba wanauwezo wa kufanya kazi kwa pamoja na wataendelea kuungwa mkono na majeshi ya Marekani, ambayo tayari yamefanya mashambulio Zaidi ya anga katika eneo linalokaliwa na wapiganaji wa kiislamu.

Ripoti zinasema kuwa mapambano katika juhudi za kudhibiti maeneo yanayozunguka bwawa hilo yanaendelea. Katika hatua nyingine kundi la himaya ya kiislamu linalofanya mashambulizi dhidi ya Wakurd limekanusha kwamba wapiganaji wake wamepoteza udhibiti wa bwawa hilo.

Wakati huohuo kiongozi wa kanisa katoliki duniani papa Francis amesema jumuia ya kimataifa itakuwa na haki katika kuchukua hatua dhidi ya wanamgambo hao. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Papa Amesema ni halali kuzuia kile alichokiita dhuluma ya kichokozi. Lakini ametahadharisha kuwa hatua yoyote itakayochukuliwa lazima ifanyiwe tathmini. kusimamisha na kwamba hakusema. Mwandishi wa BBC MJINI Roma Italia anasema papa Fransis hajaonesha kuunga mkono mashambulio ya anga yanayofanywa hivi sasa na Marekani dhidi ya wapiganaji hao wa kiislamu.

Na BBC

Monday, August 18, 2014

MeTL GROUP YAPATA MKOPO WA BILIONI 300/- KUTOKA RMB...!!!

signing deal
Ofisa Mtendaji Mkuu wa MeTL GROUP, Mohammed Dewji (Mb) (wa pili kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Rand Merchant Bank (RMB), Bw. Bruce Macfarlane (wa pili kulia) wakitiliana saini ya mkopo huo wa bilioni 300 za kitanzania. Kushoto ni Makamu wa Rais wa MeTL GROUP, Vipul Kakad na kulia ni Gregory Havermahl wa RMB wakishuhudia tukio hilo la utiliaji saini wa mkopo baina ya RMB na MeTL Group.

 Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL) imetiliana saini mkataba na benki ya Rand Merchant (RMB) ya Afrika Kusini utakaoiwezesha kupata mkopo wa zaidi ya sh bilioni 300. Mkataba huo umetiwa saini nchini Afrika Kusini na Ofisa Mtendaji Mkuu MeTL GROUP, Mohammed Dewji.

Akizungumza kabla ya kutiwa saini kwa mkataba huo,Dewji alisema kwamba mkataba huo wa kihistoria unatokana na RMB kuiamini kampuni yake ya MeTL tangu walipoanza mahusiano ya kibiashara mwaka 2007.

“MeTL na RMB tulianza mahusiano yetu mwaka 2007, wakati RMB ilipotukopesha dola za Marekani milioni 7.5million. Wakati huo MeTLilikuwa na bidhaa mbili tu,ngano na sukari! Toka wakati huo, MeTL imekuwa ikikua na kuongeza bidhaa zaidi.” Alisema Dewji na kuongeza kuwa mwaka jana 2013, uwezo wa MeTL wa kukopa sasa umefikia dola milioni 100. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAN U TAYARI KUMTOA ‘KAFARA’ LUIS NANI ILI KUINASA SAINI YA MARCOS ROJO

1408305526734_wps_2_MANCHESTER_ENGLAND_AUGUST
United wapo tayari kumruhusu Nani (kulia) kujiunga na Sporting Lisbon kama sehemu ya kubadilishana na beki Marcos Rojo.
MANCHESTER United imefanya mazungumzo na Sporting Lisbon ili kumjumuisha Luis Nani kama sehemu ya jaribio la kutaka kumsajili beki wake, raia wa Argentina, Marcos Rojo.
Baada ya mazungumzo baina ya wakala wa Rojo na Sporting mapema wiki hii, United wanajiandaa kumjumuisha Nani kwa mkopo.
Hata hivyo winga huyo mwenye miaka 27 anaonekana kuweka ngumu kurudi katika klabu yake hiyo ya zamani ya nchini Ureno.
Sporting wao wanahitaji kumuuza Rojo kwa paundi milioni 24, lakini wiki hii Man United waliweka mezani dau la paundi milioni 16.
Rojo, 24, aliwaomba radhi mashabiki wa Sporting katika mahojiano maalumu na TV ya klabu jumapili usiku baada ya kujaribu kulazimisha kuondoka.
Apology: Rojo said sorry to the Sporting Lisbon fans on Sunday night for attempting to force through a move

ANGALIA PICHA ZA WASANII WALIOPITIA MORO KUMFARIJI AFANDE SELE KWA MSIBA WA MAMA TUNDA...!!!

Baadhi ya Wasanii waliokuwa kwenye onesho la Kilimanjaro Music Tour lililofanyika mkoani Dodoma jana, leo walipitia nyumbani kwa Mfalme wa Rhymes a.k.a Simba Mzee a.k.a Afande Sele kumpa mkono wa pole na kumfariji kufuatia kifo cha Mzazi mwenzake Mama Tunda kilichotokea mwisho mwa wiki mjini Morogoro. Pichani ni Msanii wa Muziki wa Bongofleva atambulikae kwa jina la Shilole akimfariji Afande Sele.

Malkia wa Taarab hapa nchini, Bi Khadija Kopa akimfariji Afande Sele,pichani nyuma ya Afande Sele ni guli wa muziki wa Reggae hapa nchini, Innocent Nganyagwa.
Afande Sele akifarijiwa na mkali wa Hip Hop katika anga ya muziki wa Bongofleva, Joh Makini. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

LIPUMBA: MOYO WETU UKAWA NI WAJUMBE 14

Mwenyekiti wa CUF Ibrahim Lipumba akizungumza na waandishi wa gazeti hili.

Wakati mchakato wa Katiba mpya unaendelea mjini Dodoma na suala la theluthi mbili likisumbua vichwa vya wengi, mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba ameeleza kuwa kura za wajumbe 14 kutoka Zanzibar ndizo zitauokoa au kuukwamisha mchakato huo.
Profesa Lipumba alikuwa kwenye mahojiano maalumu na Mwananchi nyumbani kwake, Mbezi Beach jijini Dar es Salaam kuhusu mustakabali wa mchakato wa Katiba baada ya kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kususia kuhudhuria vikao.
Kundi hilo lilisusia vikao Aprili 16 kwa madai kuwa Bunge lilipoteza mwelekeo kwa kuacha kujadili Rasimu ya Katiba, hasa katika suala la muundo wa serikali ya Muungano na kwamba chama tawala, CCM kiliingiza suala la serikali mbili ambalo halimo kwenye rasimu hiyo badala ya serikali tatu.
Kutokana na uamuzi wa Ukawa, ambayo inaundwa na wajumbe kutoka CUF, Chadema, NCCR Mageuzi na baadhi wa kundi la 201 kutoka taasisi mbalimbali za kijamii, kuna shaka kwamba mchakato huo huenda usifanikiwe kutokana na ukweli kuwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba inataka uamuzi upitishwe na theluthi mbili ya wajumbe kutoka Bara na idadi kama hiyo kutoka Zanzibar. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATATU AGOSTI 18, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

PHIRI AONGEZA DOZI MSIMBAZI, HANS POPPE ASAKA VIFAA KIGALI, YANGA, COASTAL WATIMKIA PEMBA

DSC_0007
WEKUNDU wa Msimbazi Simba wanaendelea vyema na maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara unaotarajia kuanza kushika kasi septemba 30 mwaka huu.
Simba wamepiga kambi visiwani Zanzibar (Unguja) chini ya kocha mkuu mpya, Mzambia, Patrick Phiri akisaidiwa na kocha msaidizi, kiungo wa zamani wa klabu hiyo na timu ya taifa ya Tanzania, ‘Taifa Stars’, Suleiman Abdallah Matola ‘Veron’ na kocha wa makipa, Idd Pazzi ‘Father’.
Simba ilianza programu ya mazoezi mara moja kwa siku hapo jana katika fukwe za bahari ya Hindi, lakini Phiri ameamua kuongeza dozi ambapo leo atafanya mazoezi mara mbili, (asubuhi na jioni).
Lengo la Phiri ni kupata muda wa kutosha wa kusuka kikosi chake akijua wazi kuwa msimu ujao atakumbana na changamoto kubwa ya kusaka ubingwa wa Tanzania bara.
Pia kocha huyo alisisitiza suala la mechi za kirafiki ili kukiona kikosi chake kwa mara ya kwanza na kujua nini cha kufanya zaidi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ROBO FAINALI KOMBE LA KAGAME: WANYARWANDA WAANZA KUTIFUANA LEO, AZAM, EL MERREIKH KESHO

AZAM FC
MICHUANO ya klabu bingwa Afrika Mashariki na kati, Kombe la Kagame, imefikia patamu mjini Kigali, Rwanda ambapo hatua ya robo fainali inaanza kutimua vumbi leo hii.
Mechi ya kwanza itaanza majira ya 9:00 alasiri kwa kuwakutanisha Polisi dhidi ya Atletico, zote za Rwanda.
Robo fainali ya pili itaanza majira ya saa 11:00 jioni ambapo timu mbili pinzani nchini Rwanda, Rayon Sport na wanajeshi wa APR wataoneshana kazi.
Kibarua kingine kitaendelea kesho ambapo mechi iliyotabiriwa kuwa ngumu zaidi katika hatua hii ya kombe la Kagame itawakutanisha mabingwa wa Tanzania, Azam fc dhidi ya El Merreikh ya Sudan.
Kutokana na historia nzuri ya El Merreikh katika soka la Afrika mashariki na kati, hakika Azam wametumbukia katika daraja zito, lakini kama watajipanga vizuri wanaweza kuibuka na ushindi.
Meneja wa Azam fc, Jemedari Said alisema wamejiandaa vizuri na wanafurahia kuchuana na timu ngumu ambayo itawapa kipimo kizuri  cha kujua maendeleo ya kikosi chao.
“Sio pambano jepesi, El Merreik ni timu yenye historia kubwa. Sisi kama Azam hatuwaogopi, tunawaheshimu, tutapambana kupata ushindi ili kutinga nusu fainali na hatimaye fainali na kutwaa ubingwa”. Alisema Jemedari.
Jemedari alisema katika mazoezi ya jana jioni, wachezaji wote waliokuwa majeruhi, Waziri Salum ambaye hajacheza mechi yoyote, Saint Prex Lionel, Shomari Salum  Kapombe wote walifanya mazoezi, na kwa mara ya kwanza kikosi kizima kilikuwa uwanjani kujiandaa na mchezo huo.
Mechi nyingine ya kesho jumatano itawakutanisha KCC ya Uganda dhidi ya Altabara ya Sudan Kusini. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na Baraka Mpenja

'MCHAWI' AKATALIWA KUINGIA DUBAI

Rolf Bushholz
Mwanamume wa Ujerumani ambaye anaongoza rikodi ya dunia kuwa na mwili uliotogwa mara nyingi kabisa ameketaliwa ruhusa ya kuingia Dubai, baada ya kwenda huko kutokeza katika klabu ya starehe.
Rolf Buchholz, ametogwa mwahala 453 kwenye mwili na uso wake na ana pembe mbili kwenye kipaji.
Ameeleza kwenye mitandao ya kijamii kuwa alikataliwa na maafisa wa uwanja wa ndege kuingia nchini kwa sababu, kama alivosema, alikuwa "mchawi".
Bwana Buchholz ameapa kuwa hatarudi tena Falme za Kiarabu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

WALIOTOROKA ZAHANATI YA EBOLA WATAFUTWA

Ebola  Liberia
Kituo kilichotengwa na kuwekewa karantini kwa sababu ya ebola, kimeshambuliwa na zana kuporwa katika mji mkuu wa Liberia, Monrovia. Watu kama 20 hadi 30 waliowekwa hapo kuangaliwa kama wana dalili za ebola walitoroka baada ya kituo hicho kuporwa Jumamosi usiku..
Kituo kiko kwenye mtaa wa West Point, wenye wakaazi wengi. Washambuliaji walipora magodoro na vitu vyengine. Mwandishi wa BBC katika kanda hiyo anasema pengine washambuliaji walikerwa kuwa kituo hicho kimewekwa katika mtaa wao.

Wakuu wa Liberia wanajaribu kuwatafuta wagonjwa waliotoroka ili kuwarejesha tena kwenye kituo hicho.
Watu zaidi ya 400 wamekufa kwa sababu ya ebola nchini Liberia kati ya zaidi ya 1,000 katika kanda ya Afrika Magharibi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...