Monday, August 18, 2014

MAN U TAYARI KUMTOA ‘KAFARA’ LUIS NANI ILI KUINASA SAINI YA MARCOS ROJO

1408305526734_wps_2_MANCHESTER_ENGLAND_AUGUST
United wapo tayari kumruhusu Nani (kulia) kujiunga na Sporting Lisbon kama sehemu ya kubadilishana na beki Marcos Rojo.
MANCHESTER United imefanya mazungumzo na Sporting Lisbon ili kumjumuisha Luis Nani kama sehemu ya jaribio la kutaka kumsajili beki wake, raia wa Argentina, Marcos Rojo.
Baada ya mazungumzo baina ya wakala wa Rojo na Sporting mapema wiki hii, United wanajiandaa kumjumuisha Nani kwa mkopo.
Hata hivyo winga huyo mwenye miaka 27 anaonekana kuweka ngumu kurudi katika klabu yake hiyo ya zamani ya nchini Ureno.
Sporting wao wanahitaji kumuuza Rojo kwa paundi milioni 24, lakini wiki hii Man United waliweka mezani dau la paundi milioni 16.
Rojo, 24, aliwaomba radhi mashabiki wa Sporting katika mahojiano maalumu na TV ya klabu jumapili usiku baada ya kujaribu kulazimisha kuondoka.
Apology: Rojo said sorry to the Sporting Lisbon fans on Sunday night for attempting to force through a move

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...