Monday, August 18, 2014

PHIRI AONGEZA DOZI MSIMBAZI, HANS POPPE ASAKA VIFAA KIGALI, YANGA, COASTAL WATIMKIA PEMBA

DSC_0007
WEKUNDU wa Msimbazi Simba wanaendelea vyema na maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara unaotarajia kuanza kushika kasi septemba 30 mwaka huu.
Simba wamepiga kambi visiwani Zanzibar (Unguja) chini ya kocha mkuu mpya, Mzambia, Patrick Phiri akisaidiwa na kocha msaidizi, kiungo wa zamani wa klabu hiyo na timu ya taifa ya Tanzania, ‘Taifa Stars’, Suleiman Abdallah Matola ‘Veron’ na kocha wa makipa, Idd Pazzi ‘Father’.
Simba ilianza programu ya mazoezi mara moja kwa siku hapo jana katika fukwe za bahari ya Hindi, lakini Phiri ameamua kuongeza dozi ambapo leo atafanya mazoezi mara mbili, (asubuhi na jioni).
Lengo la Phiri ni kupata muda wa kutosha wa kusuka kikosi chake akijua wazi kuwa msimu ujao atakumbana na changamoto kubwa ya kusaka ubingwa wa Tanzania bara.
Pia kocha huyo alisisitiza suala la mechi za kirafiki ili kukiona kikosi chake kwa mara ya kwanza na kujua nini cha kufanya zaidi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Kocha huyo aliyerejea nchini kwa mara ya tatu kuifundisha Simba baada ya kutimuliwa kwa Mcroatia, Zdravko Logarusic ‘Loga’ aliahidi mambo mazuri kwa Simba iliyoshinda kuwika kwa miaka mitatu mfululizo.
Wakati huo huo, mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba, Keptein wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Zacharia Hans Poppe yuko mjini Kigali, nchini Rwanda kufuatilia michuano ya kombe la Kagame inayoendelea nchini humo.
Uwepo wa Poppe huko Kigali unatafsiriwa kuwa ni kujaribu kuona vifaa vipya vya kuongeza Msimbazi ikizingatiwa Shirikisho la soka Tanzania jana limetangaza kuongeza siku 10 zaidi za usajili mpaka Agosti 27 mwaka huu badala ya siku ya mwisho iliyokuwa jana Agosti 17.
Katika siku hizo zilizoongezwa mtu makini na mwenye mapenzi makubwa na Simba sc, Hans Poppe anaweza kuibuka na vifaa vipya hususani wakati huu Kombe la Kagame likifikia hatua ya robo fainali itakayoanza kutimua vumbi leo hii.
Wakati hayo yakijiri Msimbazi, nao mahasimu wao, Dar Young Africans wanatarajia kuondoka wiki hii jijini Dar es salaam kuelekea kisiwani Pemba, Zanzibar ambapo wataweka kambi ya kujiandaa na ligi kuu Bara.
Yanga sc watakuwa huko chini ya kocha anayesemekana kurudisha morali ya kila mchezaji kwasasa, Mbrazil, Marcio Maximo.
Nao wagosi wa Kaya, Coastal Union wanatarajia kutua Pemba kesho jumanne,.
Kwa maana hiyo, mashabiki wa Zanzibar watashuhudia timu tatu za ligi kuu soka Tanzania bara zikijivua katika ardhi yao inayosifika kwa uzalishaji wa zao la Karafuu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Na Baraka Mpenja

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...