Saturday, May 24, 2014

CCM: "HATUWEZI KUWAVUMILIA WATENDAJI WA SERIKALI WANAOKWAMISHA UTEKELEZWAJI WA ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI"

Katibu wa CCM wilaya ya kilolo Bw. Raphel Mahumba mwenye pama, akimuagiza Diwani wa kata ya ukumbi afuatilie nani anaye kwamisha ujenzi wa zahanati ya kitowo na hatua zichukuliwe haraka, aliye vaa skafu ni katibu mwenezi wa chama.
Wananchi waliongozana na katibu wa CCm wilaya ya Kilolo kuangalia ujenzi wa zahanati ya Kotowo ambayo imesimama bila sababu za msingi. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

ZIJUE KANUNI ZA SAYANSI ZA KUSAIDIA MTU KUISHI MAISHA MAREFU


Nyama nyekundu inaelezwa kuwa ni moja ya vyakula vinavyopunguza urefu wa maisha. 

Na Clifford Majani, Mwananchi


Kwa miaka mingi sana binadamu wa karne zote wamekuwa wakitafuta siri za maisha marefu, kuzuia uzee na hata kuzuia kifo. Lakini pamoja na jitihada nyingi mambo haya yameendelea kuwa changamoto kubwa kwenye maisha ya mwanadamu katika nchi mbalimbali duniani.  Kwa Tanzania, inakadiriwa kuwa umri wa kuishi kwa wanaume ni takriban miaka 58.2 na kwa wanawake ni miaka 60.5.
Muda huu wa kuishi ni mfupi sana ikilinganishwa na wenzetu katika nchi zilizoendelea kama vile Marekani ambako wastani wa kuishi ni unakadiriwa kuwa ni miaka 78.2. Wanasayansi wamekuwa na nadharia nyingi kuhusu sababu zinazosababisha binadamu azeeke na kufa mapema. Ila wengi hufikiri kuwa tunazeeka mapema kutokana na sababu za maumbile na vinasaba tunavyorithi kwa wazazi wetu.
Wengine husema kuwa tunazeeka haraka kutokana na kuwa na mtindo usiofaa wa maisha. Mtaalamu wa Afya, Dk Mark Stibich  anasema kwamba kuzeeka haraka na kuishi maishi mafupi ni suala mtambuka na linahusisha mambo kama vile vinasaba, kemia, fiziolojia ya mwili pamoja na tabia zetu kwa mujibu wa makala yake ya Mei 10, 2014 liyowekwa kwenye tovuti ya longevity.about.com.
Mtaalamu wa maabara nchini Ujerumani, Dk James Vaupel anadai kuwa vinasaba huchangia kasi ya kuzeeka kwa asilimia tatu pekee na sehemu kubwa ya visababishi vya kuzeeka haraka hutokana na mtindo wa maisha usiofaa pamoja na lishe duni. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI MEI 24, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

ALIYEZAA MTOTO WA AJABU HANDENI ALONGA


Mwajuma Seif (50). PICHA|MAKTABA 



Tangu mwaka 2012 zaidi ya watoto 154 wamezaliwa na wanawake walio juu ya umri wa miaka 50. Miongoni mwao, wamo waliotokana na teknolojia ya upandikizaji. Pamoja na madaktari kuonya kuwa kuzaa katika umri mkubwa kunahatarisha maisha ya mama na mtoto, wanawake hasa matajiri wamekuwa wakizaa katika umri mkubwa. Wilayani Handeni Mkoa wa Tanga, Mwajuma Seif (50) aliweka rekodi ya kujifungua watoto mapacha katika umri huo.

Lakini Mwajuma ana kingine cha ziada tofauti na wanawake wengi wanaozaa katika umri huo; alizaa kwa njia ya kawaida na si kwa teknolojia ya upandikizaji. Tofauti nyingine ya mwanamke huyo si kwamba alizaa katika umri huo kwa kuwa hakuwa na mtoto; ujauzito huo ulikuwa ni wa 13. Daktari anayemwangalia Mwajuma, Elinisa Mushi anasimulia mkasa wa mwanamke huyo akisema pamoja na umri, kingine kilichomshangaza ni mtoto wa ajabu aliyemzaa .

Anaeleza kuwa walimpokea Mwajuma, ambaye ni mkazi wa Kata ya Sindeni zaidi ya mwezi mmoja uliopita akiwa na ujauzito, lakini walishangazwa na tumbo la mama huyo kwani lilikuwa kubwa sana kiasi cha kuhisi kulikuwa na tatizo fulani. Ndipo walipoamua kuanza kumfanyia uchunguzi. Baada ya kupima ujauzito huo kwa kutumia mashine ya ultra sound (kamera ya mionzi), waliona ni kweli tumboni kuna watoto wenye maumbo yasiyoeleweka hivyo walitaka kumsafirisha kumpeleka Hospitali ya Mkoa wa Tanga, Bombo lakini walishindwa kutokana na hali yake. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

UN: VATICAN INAPUUZA HAKI ZA WATOTO

Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis
Kamati ya Umoja wa Mataifa dhidi mateso imelaumu vikali kanisa Catholiki kwa kutoshughulikia ipasavyo suala la unyanyasaji wa ngono ndani ya kanisa hilo.
Katika ripoti iliyochapishwa hivi karibuni na Umoja huo mjini Geneva , Kamati hiyo imeushutumu utawala wa Vatican kwa kuwahamisha watawa kutoka parokia moja hadi nyingine kuwaepusha kushtakiwa, na kupuuza haki za waathiriwa za kupokea fidia .
Utawala wa Vatican uliithinisha mkataba dhidi ya unyanyasaji , ukatili na matendo yaliyo kinyume na utu.
Uchunguzi uliofanywa na kamati ya Umoja wa Mataifa dhidi ya Vatcan ni sehemu ya uchunguzi wa mara kwa mara wa kamati hiyo dhidi ya nchi wanachama ili kuhakikisha mikataba inatekelezwa. Kamati hiyo ya Umoja wa Mataifa ina hofu kuwa wakati utawala wa Vatcan umeelezea kutokubali kamwe kuwepo kwa unyanyasaji ndani ya kanisa, maneno hayaendani na vitendo.
Kamati hiyo imekasirishwa zaidi na kwamba Utawala wa Vatcan unasisitiza kuwa unahusika zaidi na wahudumu wanaofanyika kazi ndani ya Vatcan kwenyewe , kuliko makasisi wake wanaofanyika kazi kwingineko duniani.
Mwezi Januari mwaka huu utawala wa Vatican ulichunguzwa upya na kamati ya Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watoto, baada ya kupokea ukosoaji kama huo kwamba ulishindwa kuwalinda watoto waliokuwa chini ya uangalizi wake. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Chanzo: BBC

Friday, May 23, 2014

BIBI ANASWA AMEBEBA 'UNGA' UWANJA WA NDEGE DAR...!!!


“Huyu ni mzee, lakini tumeshangaa kuona bado ana nguvu za kutosha na tulishangaa baada ya kutoa kete 20 kwa mara moja katika awamu ya kwanza, jambo hili si rahisi kutokana na umri wake,” .PICHA|MAKTABA 



Dar es Salaam. Bibi mmoja raia wa Nigeria, Olabisi Ibidun Cole (65) amevunja rekodi ya umri wa watu wanaokamatwa wakiwa na dawa za kulevya katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).

Cole alikamatwa Jumatatu akiwa amemeza kete 82 aina ya heroini zilizokuwa zimefungwa kwenye karatasi zinazofanana na ganda la sigara, ambazo si rahisi kuonekana katika mitambo.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Mkuu wa Kitengo cha Kupambana na Dawa za Kulevya, Alfred Nzowa zimesema pamoja na mbinu zake na kujiamini, mwanamke huyo alikamatwa kutokana na ushirikiano wa vitengo mbalimbali vya uwanja wa ndege.

Kamanda wa Polisi wa Uwanja wa Ndege, Hamisi Selemani alisema mwanamke huyo alikamatwa Mei 19, mwaka huu saa tisa alasiri akijiandaa kwenda Paris, Ufaransa kwa ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia.

Selemani alisema raia huyo aliwasili nchini Mei 15, mwaka huu na alikaa muda wote bila ya kuwa na shughuli yoyote, jambo ambalo lilitiliwa shaka na kumkamata. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

KAKA WA MTOTO ALIYEFUNGIWA KWENYE BOKSI NAYE 'APOTEA'

 Rashid Mvungi  akimuangalia mtoto wake Nasrah Rashid (4) ambaye ni mlemavu wa viungo aliyefungiwa chumbani na kufichwa kwenye boksi bila ya kufanyiwa usafi tangu akiwa na umri wa miezi tisa.  

Morogoro. Zimeibuka taarifa kwamba mtoto aliyekuwa amefungiwa kwenye boksi kwa miaka minne na mama yake mkubwa, Nasra Rashid (4) alikuwa na kaka aliyefahamika kwa jina la Nasoro ambaye hadi sasa hajulikani mahali halipo.

Wakati polisi ikisema imefurahi kupata taarifa hizo na kwamba itazifanyia kazi, habari zilizopatikana jana kuhusu hali ya Nasra zimesema atafanyiwa vipimo 18 ili kubaini hali ya afya yake. Vipimo vya awali, vimebaini kuwa amevunjika mifupa ya mikono na miguu na kwamba atapelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.

Kuhusu kaka yake, baadhi ya majirani wa nyumba aliyokuwa anaishi mama mzazi wa Nasra enzi za uhai wake walidai kuwa Mariamu alikabidhiwa watoto wawili kuwalea baada ya mama yao kufariki dunia.

Mmoja wa majirani hao, Ramadhani Mansuri alisema wakati mama mzazi wa Nasra akiishi eneo la Mjimpya alikuwa na watoto wawili akiwamo Nasoro ambaye aliachwa akiwa na umri kati ya miaka 14-15.

Vipimo

Ofisa Ustawi wa Jamii, Mkoa wa Morogoro, Oswin Ngungamtitu alisema taarifa alizopata kutoka kwa madaktari zinasema kuwa mtoto huyo atafanyiwa vipimo 18 ili kubaini hali ya afya yake.

Akizungumzia matokeo ya vipimo vya awali, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, Dk Rita Lyamuya alisema haijafahamika sababu za kuvunjika kwa mifupa hiyo. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 23, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

.

.
.
.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

DAVID MOYES AZUA BALAA, AMPIGA DOGO MMOJA BAADA YA KUMTUKANA KWA KUPOTEZA KAZI MAN UNITED

Investigation: Moyes was present at the bar in Clitheroe at the time of the assault
Incident: Joshua Gillibrand claims he was attacked at just after 10pm on Wednesday night
 Tukio: Joshua Gillibrand anadai alishambuliwa majira ya saa 10:00 usiku wa jana jumatano.
 
Inasemekana Moyes alikerwa na kijana huyo mlevi aliyemtukana kocha huyo baada ya kufukuzwa kazi hivi karibuni na kumuita ‘s*** (hatujaona haja ya kutafsiri kimaadili), akimaanisha hajawahi kushinda kombe, alisema shahidi.
Baada ya maneno hayo vurugu ziliibuka mezani ambapo glasi zote zimeanguka chini.
Mr Gillibrand, alikula vibao na alichubuka kwenye bega kutokana na ugomvi huo, lakini hakuhitaji kwenda hospitali kupata matibabu zaidi.
Leo polisi walithibitisha kufungua uchunguzi juu ya tukio hilo na wanatarajia kuongea na kocha huyo wa zamani wa Everton.
Location: The Emporium wine bar in Clitheroe, Lancashire, where the alleged assault took place

BOKO HARAM NI MAGAIDI WA KIMATAIFA - UN


Baraza la Usalama la UN
Baraza la usalama la umoja wa mataifa hatimaye limeidhinisha kuwekewa vikwazo kundi la Boko Haram baada ya utekaji nyara wa takriban wasichana 300 wa shule katika eneo la Chibok Nigeria.
Kundi hilo limeshutumiwa kuwaua maelfu ya watu nchini Nigeria katika miaka michache iliyopita.
Nigeria ni mwanachama wa baraza la usalama la Umoja wa mataifa kwa kipindi cha miaka miwili. Kwa nafasi hii imeweza kushinikiza baraza hilo kuimulikia tochi.
Hatua ya baraza hilo kuiorodhesha Boko Haram miongoni mwa magaidi wa kimataifa, wakipishana au hata kuhusishwa moja kwa moja na AL Qaeda, huenda isionekane kama hatua kubwa. Lakini hii ina maana kuwa sasa jamii ya kimataifa italichukulia kwa uzito mkubwa zaidi kundi hilo.
Baraza hilo limeidhinisha pia vikwazo kuwekewa kundi hilo, viongozi wake na yeyote anayehusishwa nalo. Hii ina maana kuwa hata mali zao zitazuiliwa na akaunti zao zote zinazojulikana kufungwa. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Thursday, May 22, 2014

UNYAMA: MTOTO AFICHWA KWENYE BOKSI NA KUFUNGIWA NDANI KWA MIAKA MINNE...!!!


Rashid Mvungi  akimuangalia mtoto wake Nasrah Rashid (4) ambaye ni mlemavu wa viungo aliyefungiwa chumbani na kufichwa kwenye boksi bila ya kufanyiwa usafi tangu akiwa na umri wa miezi tisa. Picha na Hamida Shariff 

Alikuwa akitoa maelezo hayo huku akiwa amemshikilia mtoto huyo aliyetapakaa uchafu ikiwamo haja kubwa na ndogo alizokuwa akitoa ndani ya boksi na kusema kwamba mara ya mwisho alimwogesha Julai mwaka jana.

Morogoro. Mwanamke aliyetambuliwa kuwa ni Mariamu Said mkazi wa Kiwanja cha Ndege, Morogoro juzi alishushiwa kipigo na wananchi kutokana na kumficha mtoto wa marehemu mdogo wake kwenye boksi kwa miaka minne.

Tukio hilo lilitokea juzi saa nne asubuhi baada ya majirani zake kutoa taarifa kwa Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kiwanja cha Ndege, Dia Zongo kuhusu mtoto huyo, Nasra Rashid, kufichwa ndani ya boksi tangu akiwa na umri wa miezi tisa. Zongo alisema majirani hao walimweleza pia kuwa jirani yao huyo hamfanyii usafi mtoto huyo wala kumtoa nje.

Baada ya kupata taarifa hizo, Zongo alimtafuta Mwenyekiti wa Mtaa huo, Tatu Mgagala na kuongozana naye hadi kwenye nyumba hiyo na kumhoji mwanamke huyo ambaye alikuwa akijibu kwa kubabaika. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MEI 22, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

NGASSA, SAMATTA KUGOMBEA TUZO MOJA

 Mchezaji wa Yanga, Mrisho Ngassa pamoja na Mbwana Samatta wa TP Mazembe, wanaumana katika kuwania tuzo za mwanamichezo anayependwa zaidi na watu zinazoendeshwa na Kampuni ya Bongo 5 Media Group kupitia tovuti yake ya bongo5.com.
Wengine wanaowania tuzo katika kipengele hicho ni Ramadhan Singano (Simba SC), Juma Kaseja (Yanga) na bondia Francis Cheka.
Inaonekana kuwa Ngasa na Samatta watakuwa na ushindani mkubwa zaidi hasa ikizingatiwa kuwa wachezaji wote wana mashabiki wengi na pia kila mmoja anacheza mchezo unaopendwa na wengi.
Akizungumzia tuzo hizo, mhariri mkuu wa bongo5.com, Fredrick Bundala, alisema watu wengi walijitokeza kupigia kura kuchagua watu wanawataka kushinda tuzo mbalimbali.
Bundala alivitaja vipengele vingine na majina ya waliopendekezwa kuwa ni pamoja na Nisher, Adam Juma, Nick Dizzo, Mecky Kaloka, Jerry Mushala wanaowania tuzo ya Mwongozaji Bora wa Video za wasanii.
Video Bora kwa Wanaume ni My Number ya Diamond, Jikubali ya Ben Pol, Mirror ya Baby, Love Me ya Izzo Bizness, Barnaba na Shaa, Muziki Gani ya Nay wa Mitego na Diamond.
Alisema wanaowania Tuzo ya Video ya Mwanamuziki wa Kike ni Amani ya Moyo ya Feza Kessy, Closer ya Vanessa Mdee, Sugua Gaga ya Shaa, Yahaya ya Lady Jaydee, Nakomaa na Jiji ya Shilole.
Bundala alifafanua kuwa wananchi wanatakiwa kuchagua jina moja kutoka katika majina matano ya kila kipengele kilichotajwa.
“Wiki moja baada ya majina ya washiriki watano kutangazwa, mchujo wa kwanza utafanyika katika kila kipengele,” alisema Bundala.
Aliwataka Watanzania kuwapigia kura wale wanaowapenda kwa kutuma ujumbe mfupi na baadaye kufuata maelekezo rahisi ya kupiga kura pia kupitia tovuti www.tuzozetu.com. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

YAYA AITIA KIWEWE MANCHESTER CITY

Yaya Toure amekoleza moto kwenye sakata lake kutaka kuihama Manchester City akisema hajui hadi sasa atakapokwenda kucheza msimu ujao.
Wakala wa mchezaji huyo, Dimitri Seluk alibainisha kuwa Yaya anaweza kuondoka kwa sababu anadhani kwamba amekuwa akichukuliwa kama mtu asiyeheshimika na wamiliki wa klabu hiyo.
Hivyo kwa sasa, Toure ambaye ana miaka 31, hajaamua hatima yake kuhusu klabu atakayochezea msimu ujao.
Alipoulizwa kama anaweza kuichezea klabu nyingine msimu ujao, alijibu: “Ndio. Hatujui katika soka nini kitatokea. Kamwe hatuwezi kujua hilo.”
Katika mahojiano maalumu na mtandao wa BE IN SPORTS, nyota huyo wa timu ya taifa ya Ivory Coast alisema: “Kwa sababu ya msimu mzuri niliokuwanao klabu ya Man City, kila mtu ananizungumzia na kila kitu kiko wazi.
“Wakala wangu Dimitri, siku zote amekuwa akizungumza na watu kwa simu na anajua cha kufanya kwa sababu siku zote nimekuwa nikimuamini sana.
“Hatujui kesho itakuwaje, lakini kwa sasa akili yangu iko katika Kombe la Dunia na baada ya kumalizika kwake tutajua nini kimetokea.”
Toure alisaini mkataba mpya wa miaka minne kuichezezea City Aprili mwaka jana.
Hata hivyo, majaaliwa yake yamebaki kuwa na mashaka kutokana na wakala wake kuwalaumu wamiliki wa City kwa kutoonyesha heshima kwa kiungo huyo alipotimiza miaka 31. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

WAZIRI AJIUA BAADA YA KUSHINDWA KATIKA UCHAGUZI

Shughuli ya kuhesabu Kura Malawi
Naibu waziri wa serikali za mitaa wa Malawi amejipiga risasi na kujiua nyumbani kwake mjini Lilongwe.
Godfrey Kamanya alikuwa anayegombea kutetea kiti chake cha ubunge katika jimbo la Nzonzi Kusini amejiua alfajiri ya leo katika mojawapo ya vyumba vya nyumba yake iliyopo Area Ten mjini Lilongwe.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa kwenye hospitali kuu ya Kamuzu mjini humo, na jeshi la polisi litatoa taarifa rasmi ya kifo hicho baada kukamilisha uchunguzi.
Haijajulikana sababu za Kamanya kujiua japokuwa ameacha barua ya maelezo ambayo polisi wataitoa baadae.
Matokeo ya kura bado hayajatangazwa rasmi katika kile kinachosemekana kuwa uchaguzi wenye ushindani mkali sana.
Afisa mkuu wa uchaguzi, amesema kuwa mfumo wa elektroniki umeharibika na maafisa wanatumia matokeo kwa njia ya barua pepe. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...