Friday, December 13, 2013

AZIMIO LA KUWANG'OA MAWAZIRI LAPITISHWA RASMI NA BUNGE...!!!


Waziri wa Tamisemi, Hawa Ghasia.
********
Bunge limepitisha azimio la kuwataka mawaziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), kujipima iwapo wanatosha kuendelea kuongoza wizara hiyo nyeti.
Azimio hilo lilipitishwa jana na wabunge kwa kura ya ndiyo bila kupingwa, baada ya kuhojiwa na Spika wa Bunge Anne Makinda iwapo wanaipokea taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (Laac) iliyowasilishwa na Mwenyekiti wake Rajabu Mbaruku.
Moja ya mapendekezo yake ni Waziri wa Tamisemi, Hawa Ghasia na manaibu wake, Aggrey Mwanri na Kassim Majaliwa kujipima kama wanatosha kuendelea kuongoza wizara hiyo kutokana na kugubikwa na vitendo vya ufisadi.
Kwa mujibu wa taratibu za Bunge, taarifa ya kamati inapowasilishwa na kupitishwa pamoja na mapendekezo yake, huwa ni azimio kamili ambapo Serikali hutakiwa kutoa maelezo ya utekelezaji wake.
Kabla ya azimio hilo kupitishwa, Mwenyekiti wa Laac, Rajabu Mbaruku alijibu michango ya wabunge waliochangia katika taarifa ya kamati yake iliyowasilishwa Ijumaa iliyopita, akiwemo Waziri Ghasia.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA DESEMBA 13, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.

KUMBE GRACA MACHEL NA WINNIE MANDELA NI MTU NA 'DADA YAKE'

https://www.facebook.com/jambotz

Winnie Madikizela-Mandela, (77) aliinama kumbusu Graca Machel (68), kabla ya kukaa katika kiti cha tatu kutoka kile alichokalia mwanamke huyo. Graca Machel alimwambia maneno machache ‘dada yake’ Winnie wakati akimbusu.
Wanawake hao wote wakiwa wamevalia majaketi meusi na vilemba, walikumbatiana kwa sekunde kadhaa huku Winnie akitabasamu na Graca akitazama mbele.
Wote wawili wanaheshimika nchini Afrika Kusini kutokana na sababu mbalimbali. Winnie anaheshimika kwa mchango wake mkubwa wa kupigania ubaguzi wa rangi; Graca kwa moyo wake wa kujitolea kumtunza kiongozi wao mpaka anafariki dunia.

Hata hivyo Winnie amekuwa akikosolewa kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo ile ya kuruhusu wapinzani wake wauawe kwa kuchomwa moto wakitumia mafuta ya petroli na matairi ya magari.

ZITTO AWASHA MOTO MPYA CHADEMA...!!!



Siku moja baada ya kuwasilisha maelezo yake ya utetezi baada ya kuvuliwa nyadhifa zake ndani ya Chadema, aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe amekata rufaa Baraza Kuu kupinga hatua hiyo.


Zitto pamoja na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba na Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk Kitila Mkumbo walivuliwa nyadhifa zao na Kikao cha Kamati Kuu kilichofanyika Novemba 20 na 21 jijini Dar es Salaam.


Akizungumza jana, Mwanasheria wa Zitto, Albert Msando alitaja sababu mbili za kukata rufaa kuwa ni kukiukwa kwa taratibu za kuchukua hatua za nidhamu na sababu zilizotolewa kutokuwa sahihi.


Hata hivyo, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika alisema mambo hayo yalishatolewa ufafanuzi na chama na kwamba kukata rufaa ni haki ya kikatiba kwa mwanachama yeyote.


“Kukata rufaa ni haki ya kikatiba ya wanachama yeyote. Rufaa ikatwe tu, itashughulikiwa kwa mujibu wa katiba, kanuni, maadili na itifaki ya chama. Hata hivyo, ieleweke, rufani inahusu kuvuliwa nafasi za uongozi, kusudio hilo haliwaondolei wajibu wa kujieleza kwa maandishi mbele ya Kamati Kuu kwa nini wasifukuzwe uanachama,” alisema Mnyika.

Thursday, December 12, 2013

DR. ASHA ROSE MIGIRO ALA KIAPO BUNGENI DODOMA LEO


PG4A9627
Mbunge wa Kuteuliwa , Dr. Asha Rose Migiro akiongozwa na Mpambe wa wa Bunge  na kusindindikizwa na badhi ya wabunge wa CCM kuingia Bungeni ili kuapishwa na Spika wa Bunge, Anne Makinda, Mjini Dodoma Desemba 12, 2013.
PG4A9630
Mbune wa Kuteuliwa , Dr. Asha Rose Migiro akiongozwa na Mpambe wa wa Bunge  na kusindindikizwa na badhi ya wabunge wa CCM kuingia Bungeni ili kuapishwa na Spika wa Bunge, Anne Makinda, Mjini Dodoma Desemba 12, 2013.

OPRAH WINFREY AELEZEA KWA NINI HANA WATOTO...!!!


Kwenye taarifa za hivi karibuni za Waandishi wa Hollywood, Oprah amefunguka juu ya kwa nini hana watoto na ukweli wa juu ya hali hiyo kutohusani na wanachohisi wengi kwamba hana uwezo wa kushika ujauzito huku akielezea kwa sababu kuu ni yeye kutaka kuwa mwanamke mwenye nguvu.

"Kama ningekuwa na watoto, watoto wangu wangenichukia. "Wangeishia kwenye hali ya kuniongelea kama ilivyo kwenye Oprah show; sababu kuna kitu katika maisha yangu kingeishia kuteseka na inawezekana kabisa wangekuwa wao. 
Gayle [King, rafiki wa karibu Winfrey ambaye ni mama wa watoto wawili] alikuwa ni aina ya mtoto ambaye, kwenye daraja la saba la darasa, alikuwa anaandika jina lake chini na majina ya watoto wake. 
Wakati alipokuwa na ndoto hizo za mchana, nilikuwa na ndoto za mchana juu vipi naweza kuwa Martin Luther King.

BASI LA BURUDANI LAPATA AJALI LEO HII MKOANI TANGA, WATU 12 WAPOTEZA MAISHA NA WENGINE KUJERUHIWA




Basi la Burudani baada ya ajali leo Wilaya ya Handeni, Tanga.

Basi la Burudani leo limepata ajali kijiji cha Kwaluguru Kata ya Kwedizinga  wilayani Handeni, Imeripotiwa mpaka sasa watu zaidi ya 12 wamefariki na majeruhi zaidi ya 55. Watu 4 wamepelekwa MOI na KCMC. Tuwaombee majeruhi.

Hospitali ya wilaya ya Korogwe.

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS DESEMBA 12, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.


.

Tuesday, December 10, 2013

'BABU SEYA, PAPII LAZIMA WATAACHIWA HURU TU'


Nguza Vicking ‘Babu Seya’ na Johnson Nguza ‘Papii Kocha’.
NGUZA Mbangu, mtoto mkubwa wa mwanamuziki mahiri wa muziki wa dansi anayetumikia kifungo cha maisha jela, Nguza Viking maarufu kama Babu Seya, amesema mzazi wake pamoja na mdogo wake, Papii, ni lazima wataachiwa huru hivi karibuni.

Mbangu, ambaye pia hufahamika kisanii kama Mashine, ambaye hivi sasa ni mwinjilisti, alitoa kauli hiyo hivi karibuni alipozungumza na gazeti la Uwazi, akisema kuwa kutolewa jela kwa ndugu zake hao, kutawafanya Watanzania kumsujudia Mungu kupitia tukio hilo.

“Amini nakuambia, Mungu amenipa maono, Babu Seya na Papii wako huru, watatoka tu, kinachosubiriwa ni muda tu ambao hauko mbali, ni lazima watatoka kwa sababu hawana hatia,” alisema Mbangu, ambaye pia alihukumiwa kifungo cha maisha jela kama mzazi wake, lakini akaachiwa wakati walipokata rufaa kwa mara ya kwanza mahakamani.

JIONEE PICHA ZAIDI YA 200 ZA IBADA YA KUMUOMBEA MANDELA INAVYOENDELEA IKIWAMO NA MARAIS NA VIONGOZI WALIOWASILI

Sombre occasion: Members of Nelson Mandela's family take their seats amid heavy rain ahead of his memorial service at the FNB Stadium in Soweto, near Johannesburg

Respect: Nelson Mandela is shown on a giant screen inside the stadium as thousands of South Africans and global dignitaries file into the ground

NORA AFUNGUKA KUHUSU RAY ADAI ALIMTONGOZA. MSIKILIZE HAPA..!!!

Muigizaji wa kike aliyefanya vizuri kupitia kundi la Kaole Sanaa Group, Nuru Nassoro aka Nora amedai kuwa amekuwa akifanyiwa fitina na muigizaji mwenzake Vicent Kigosi aka Ray kwa kuwa aliwahi kumtaka kimapenzi akamkataa.
  
Nora amefunguka kupitia kipindi cha Filamonata cha 100.5 Times Fm na kudai kuwa Ray amekuwa akimbania hata kwenye baadhi ya makampuni ambayo anapeleka kazi zake.
 
Mpaka kwenye kampuni ambayo nimepeleka kazi nimeshawahi kusikia wanasema, wakaniahidi sana mpaka nikawakubalia walichokuwa wanataka wao. Lakini yeye (Ray) alitanguliza movies zake, akasema ana movie zake sijui kitu gani..” amelalamika Nora.
 
Ameeleza kuwa Ray amewahi kumbania kufanya kazi na marehemu Kanumba, na hata Mtitu sababu ikiwa ile ile kumkataa kimapenzi.

WINNIE MANDELA NA GRACA MACHEL WAKUTANA MSIBANI, MARAIS ZAIDI YA 90 KUHUDHURIA MAZISHI.... R.I.P MANDELA


Marais zaidi ya 90 wa nchi mbalimbali duniani akiwemo Barack Obama wa Marekani ni miongoni mwa maelfu ya waliojitokeza Johannesburg South Africa kwenye uwanja wa soka wa FNB leo kumuaga Mzee Mandela anaetarajiwa kuzikwa Jumapili ijayo December 15 2013.
madiba 9
Serikali ya Afrika Kusini imeimarisha ulinzi kwa kutumia vikosi vyake vya jeshi vyenye ulinzi wa hali ya juu ambapo sniper team ni miongoni mwa wanaohusika na ulinzi kwenye eneo lote la kiwanja anakoagiwa Mzee Mandela huku helicopter pamoja na ndege za kijeshi zikipita angani mara kwa mara.

ANGALIA PICHA ZA BIRTHDAY PARTY YA NICK MINAJ, BONGE LA KEKI...!!!


First lady wa label ya YMCMB Nicki Minaj amesherehekea birthday yake ya kutimiza miaka 31 na mafanikio ya kujivunia kwenye kazi yake ya muziki ambapo party ilifanyika huko L.A na Restaurant nzima ilibadilika rangi yake na kuwa ya pink maalum kwa ajili ya party ya Minaj ambayo ilihudhuriwa na Lil Twist, Safaree boyfriend wa Nicki Minaj na watu wengine.
nicki-minaj-birthday-5nicki-minaj-birthday-3

YAFAHAMU MAAJABU 10 YA MSIBA WA MANDELA...!!!

RAIS wa zamani wa Afrika Kusini, Mzee Nelson Mandela, mweusi wa kwanza kushika wadhifa huo katika taifa lenye uwezo mkubwa kiuchumi na kijeshi barani Afrika, alifariki dunia Alhamisi iliyopita akiwa nyumbani kwake jijini Johannesburg.
Kifo chake kimeushtua ulimwengu na kwa mara ya kwanza katika historia, dunia nzima imesimama nyuma ya jemedari huyo, kila mmoja akionesha masikitiko yake. Wakati dunia ikisubiri mazishi yake ambayo pia yatavunja rekodi ya mazishi yote yaliyowahi kufanywa tokea kuumbwa kwa uso wa dunia hapo Desemba 15 mwaka huu, Uwazi limebaini maajabu kumi yanayoambatana na msiba huo.

AIR FORCE ONE KUBEBA MARAIS WATANO WA MAREKANI
AIR Force One ni ndege inayombeba Rais wa Marekani aliye madarakani na kumpeleka popote duniani. Lakini katika hali ya kushangaza, Idara ya Usalama ya Marekani imetoa ruhusa kwa marais wastaafu wakiwa na wake zao, kuandamana na Rais Barak Obama kuhudhuria mazishi ya shujaa huyo wa dunia.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...