Thursday, August 01, 2013

HII KALI: MWALIMU MKUU WA SHULE YA CHALINZE AHAMISHIA OFISI YAKE CHOONI...!!!


MWALIMU Mkuu wa Shule ya Msingi Chalinze Mzee, wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani, Elias Kapama, yuko katika wakati mgumu baada ya kuhamishia ofisi yake kwenye vyoo vya wanafunzi kutokana na jengo la ofisi yake kuharibika vibaya.

Hatua ya kuhamia chooni ilitokana na mkuu huyo kutawaliwa na hofu ya ubovu wa ofisi yake, hivyo kushindwa kufanya kazi zake kwa ufasaha unapotokea upepo au mvua.

Novemba 2012, Kapama alihamishia ofisi yake katika jengo la vyoo vya wanafunzi ambavyo havijaanza kutumika tangu ujenzi wake ukamilike mwaka 2011. Akizungumzia hali hiyo, Kapama alisema kuwa anajisikia vibaya kutumia chumba maalumu cha kubadilishia nguo cha wavulana katika choo hicho kutokana na kukosa msaada kutoka halmashauri ya wilaya hiyo.

MWANAUME AJIUA BAADA YA KUMUUA MKEWE KWA KUMCHOMA NA KISU, KISA NI WIVU WA MAPENZI...!!!


                                 Linah Keza enzi za uhai wake
Jamii ya wauganda huko Uingereza wameaamka na habari za kusikitisha baada ya mwenzao aliyejulikana kwa jina la David Kikaawa kumuua mke wake Linah Keza.

Inasemekana kuwa David alimuua mke wake mida ya alfajiri baada ya kuhisi kuwa mke wake anatembea nje ya ndoa..

David alienda kujificha baada ya kumchoma mke wake na kisu hadi kufa. Baadae nae maiti yake(David) ilikutwa kwenye club 791,inayomilikiwa na kaka yake. Alijiua baada ya kumuua mke wak.

Wawili hao walikua wanaishi  kaskazini mwa London,amebaki mtoto wao wa kike mwenye miaka mitatu 
 
           Kushoto ni David,mtoto wao na Linah
                            

LIST YA WASANII, PRODUCERS NA WATU WA MEDIA 166 WALIOALIKWA NA RAIS KIKWETE KUFUTURU IKULU LEO


JK mtu wa watu
1

HUYU NDIYE BINTI ALIEFARIKI KWA KISA KILICHOANZIA FACEBOOK, FAMILIA YAKE KUISHITAKI FACEBOOK?


7

Kampuni ya mtandao wa kijamii wa facebook imezungumza baada ya tukio la yule msichana aliejiua kutokana na kisa ambacho kilianzia facebook January 2013.
1
Kumbe Chanzo ni picha ambayo ilikua inamuonyesha mrembo huyu wa Italia Carolina akiwa amelewa, aliiweka kwenye page yake ya facebook ambapo mpenzi wake wa zamani kwa kushirikiana na marafiki walianza kumtolea maneno machafu Carolina, walimtukana hivyo yeye na mdogo wake wa kike wakaamua kuripoti facebook lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa.
Kwenye mji wa Italia wa Novarra ndio tukio lilitokea kupitia facebook na likaingia mpaka kwenye maisha ya Carolina ambapo bila yeye kujua, tukio liliendelea kuwa kubwa na kutishia kuwa kubwa kumshinda.

MWANAJESHI AMGONGA RAIA BAADA YA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI KATIKA MATAA YA KUONGOZEA MAGARI ENEO LA TAZARA DAR ES SALAAM



Gari lililomgonga raia likipita katika upande wa kulia zinakotokea gari za Buguruni,Ubungo,baada ya dereva kukiuka sheria za usalama barabarani.

 Raia aliyegongwa akiwa hoi baada ya kugongwa na dereva wa gari la Jeshi akipepewa na askari Jeshi.

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI AGOSTI 1, 2013

DSC 0051 066d6
DSC 0052 9dfcf

JUMA KASEJA APATA DILI KUBWA KONGO...!!!

Mlinda mlango wa Taifa Stars Juma Kaseja
NAHODHA wa timu ya soka ya taifa ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, Juma Kaseja amesema kwamba amefanya mazungumzo tu na wakala wa klabu ya St. Eloi Lupopo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), lakini bado hajaingia Mkataba na klabu hiyo ya Lubumbashi.

Akizungumza jana mchana, Kaseja amesema kwamba mtu aliyejitambulisha kwake kama wakala wa Lupopo alimfuata wakafanya mazungumzo na kufikia makubalino juu ya dau la usajili, mshahara na mambo mengine ya msingi.

Hata hivyo, kipa huyo namba moja Tanzania amesema kwamba baada ya mazungumzo hayo na maafikiano, wakala huyo amepeleka majibu Lupopo ambao wakiafiki ndipo masuala ya Mkataba yatafuatia.

MUSWADA WA SUALA LA KODI YA SIM CARD KURUDISHWA BUNGENI AGOSTI

Waziri wa Fedha, , Dk. William Mgimwa amenukuliwa kwenye magazeti ya NIPASHE na HabariLeo matoleo ya leo akisema kuwa Serikali sasa imekubali kuwa kodi mpya ya laini ya simu ni mgogoro na hivyo inakusudia kurejesha muswada wa sheria ulioazisha kodi hiyo wenye mkutano wa Bunge mwishoni mwa mwezi wa Agosti kwa mjadala zaidi na ufumbuzi kutoka kwa Wabunge.

Wiki iliyopita Rais Jakaya Kikwete alikutana na Wizara hiyo, Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia na wajumbe wa MOAT (Chama cha Wamiliki wa Kampuni za Simu -  TTCL, Airtel, Vodacom, Tigo na Zantel)  Ikulu kusikia pamoja na mambo mengine, kuondolewa kwa kodi ya simu kutakavyokwaza maendeleao ya sekta ya mawasiliano na kuwataka MOAT kutoa mapendekezo ya jinsi serikali itapata kiasi cha Sh. bilioni 178 zilizopangwa kupatikana katika bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha wa 2013/14 kutokana na kodi ya simu.

VYAKULA VYA MAFUTA NI CHANZO CHA KUKUKOSESHA USINGIZI

baga

Tumekuwa tukipokea maoni toka kwa watu wengi juu ya matatizo ya kukosa usingizi, ingawa kuna sababu nyingi zinazoweza kukufanya ukose usingizi kama magonjwa nk, ila mlo nao ni moja ya sababu hizo.Na moja ya vyakula hivi ni vile vyenye mafuta (fat) mengi kama burger, chipsi nk. Tafiti zinaonesha kuwa, vyakula hivi sio tu hukufanya uongezeke uzito bali pia huabiri mfumo wa kulala.

Tafiti zinaendelea kuwa, vyakula hivi vizito huamsha mfumo wa usagaji vyakula (digestion system) na kuifanya ianze kufanya kazi, hii hukupelekea mwili wako kuwa hai na pia hukufanya mara nyingi kujisikia kwenda haja hivyo kukukosesha usingizi. 
Hivyo basi epuka kula mlo wenye wanga mwingi wakati wa usiku au angalau kwa masaa mawili kabla ya kwenda kulala.

Wednesday, July 31, 2013

MWANASHERIA KUISHITAKI ISRAEL KWA KIFO CHA YESU KRISTO...!!

dola
Maajabu mengi sana hugundulika duniani kila siku , lakini kuna kila uwezekano kuwa ajabu lililoko kwenye story hii likawa ajabu la kipekee . Mwanasheria mmoja ambaye ni raia wa Kenya ameibuka na kuzishitaki serikali za Israel na Italia kwa kosa la kuhusika kwenye kifo cha Yesu Kristo .
Mwanasheria huyo Dola Indidis amefungua kesi hiyo kwenye mahakama ya dunia The Hague kule kule ambako rais wa taifa Lake (Kenya ) Mh Uhuru Kenyatta na Makamau wake William Ruto nao wana kesi ya kujibu .
Jesus-Christ-Wallpapers-3Mwanasheria huyo amesema kuwa lazima serikali za mataifa hayo ziwajibike kwa kitendo cha unyama alichofanyiwa mwanzilishi wa dini ya madhehebu ya Kikristo ambaye ni Yesu aliyesulubiwa msalabani pasipo kuwa na hatia yoyote ya kustahili adhabu hiyo . 

Dola Indidis amefungua shitaka hilo dhidi ya Mfalme wa uliokuwa Ufalme wa Roma Tiberio pamoja na watawala waliokuwa chini yake wakati huo wakiwemo Pontio Pilato na Mfalme Herode pamoja na viongozi wa kiyahudi wakiwemo mafarisayo na masadukayo ambayo kwa pamoja walikula njama ya kumuua Bwana Yesu .

FAHAMU KWANINI UNATAKIWA KUZIFANYA NDIZI KUWA SEHEMU YA MAISHA YAKO.


banana-amazing-fruit-and-cureNdizi ni tunda ambalo limezoeleka kwa watu wengi , linapatikana karibu kila mahali . Hata hivyo inawezekana ukawa hujafahamu umuhimu wa tunda hili mwilini mwako . Taarif aifuatayo itabadilisha mtazamo wako kwa tunda hili na utafahamu kwanini hupaswi kulichukulia poa hata siku moja .

Ndizi mbivu zina sukari zinazohitajika kwenye mwili wako , sukari hizi ni zile ambazo zinafahamika kwa majina ya kitaalamu ya Sucrose , Fructose na Glucose ambazo kwa pamoja zimechanganyikana na Fibre muhimu ambazo zinalifanya tunda hili kuwa chanzo muhimu cha nishati au nguvu inayohitajika mwilini mwako .

Utafiti umeonyesha kuwa ndizi mbivu mbili zinatosha kukupa nishati ambayo utaitumia kwa mazoezi ya nguvu ya dakika 90 ambazo ni sawa na saa moja na nusu . Hii ndio sababu wanamichezo wengi hutumia ndizi mbivu kabla na baada ya mazoezi mazito na wakati mwingine kabla na baada ya mashindano katika mchezo husika .
Nishati si faida pekee inayokuja kwenye tunda la ndizi , tunda hili lina faida nyingine ambayo ni kuusaidia mwili wako kupambana na kujikinga na maradhi  kadhaa.

MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU MWAKA WA MASOMO 2013/2014 HAYA HAPA



Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Dr Shukuru kawambwa. 
---
Serikali imetangaza majina ya wanafunzi 18,754 waliochaguliwa kujiunga na vyuo vya ualimu vilivyo chini yake ikiwa ni ongezeko la wanafunzi 1,659 ikilinganishwa na 17,095 waliochaguliwa mwaka jana.

Kati ya wanafunzi hao, 11,806 wamechaguliwa kusomea ngazi ya cheti (Grade A) na 6,948 watasoma katika ngazi ya stashahada.Wanafunzi 363 wamechaguliwa kusoma elimu maalumu kwa ngazi ya cheti huku 57 wakisoma elimu hiyo kwa ngazi ya stashahada.
---

MAELEKEZO MUHIMU:

Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Mafunzo ya Ualimu mwaka wa masomo 2013/2014 wanatakiwa kuripoti katika Vyuo walivyopangiwa tarehe 15/08/2013.

ZIDANE AWAFUNGUKIA SPURS, AWATAKA WAMPE NAFASI YA KUCHEZA REAL MADRID KUTIMIZA NDOTO ZAKE



 Touch down: Gareth Bale arrives at Heathrow Airport from Hong Kong in the early hours  
Gareth Bale alipokuwa akiwasili uwanja wa  Heathrow akitokea Hong Kong  baada ya kupata majeruhi
Nothing to smile about: Bale, who may be subject of a world record £85m bid from Real Madrid, clearly has a lot on his mind on his return to London 
Hakuna tabasamu: Bale, anaweza kuwa mchezaji ghali zaidi duniani akimzidi Ronaldo kama dili la usajili wake wa pauni milioni 85 litakamilika kwenda Real Madridi, lakini wakati akiwasili London alionekana kuwa na mawazo mengi kichwani mwake.
Zidane alisisitiza kuwa : “Kama mchezaji ameonesha nia ya kujiunga na Madrid, basi Tottenham wampe ruksa ya kuzungumza na sisi. Nafasi ya kuichezea Real Madrid huwa inatokea mara moja katika maisha ya mchezaji na inaeleweka kuwa Gareth Bale hataki kukosa nafasi hii muhimu”.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO JULAI 31, 2013

DSC 0005 ea013
DSC 0006 f6d17

AFYA YA MANDELA YAZIDI KUIMARIKA

051 86464

RAIS mstaafu nchini Afrika Kusini , Nelson Mandela aliyelazwa hospitalini tangu tarehe nane mwezi Juni, anaonyesha dalili za afya yake kuimarika.

Hii ni kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa serikali. Hata hivyo Mandela mwenye umri wa miaka 95 angali hali mahututi ambayo inadhibitiwa na madaktari.

Rais Jacob Zuma amewataka watu kuendelea kumuombea Mandela na kuwashukuru wale waliotenda mema kwa niaba ya Mandela. (HM)

Mandela ambaye ni rais wa kwanza wa nchi hiyo kuchaguliwa kidemokrasia, anatazamiwa na wengi kama baba wa taifa.

Alifungwa jela miaka 27 baada ya kuanzisha vita dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi.
Anajulikana na ukoo wake kwa jina Madiba, na alichaguliwa kama rais wa Afrika Kusini mwaka 1994 baada ya wazungu kumaliza utawala wao na kisha akaondoka mamlakani baada ya miaka mitano ya kutawala nchi.

Katika taarifa yake, bwana Zuma alitoa wito kwa wafanyabiashara kuunga mkono mradi unaofadhiliwa na wakfu wa Mandela kujenga hospitali ya watoto.
"Madiba anapenda sana watoto, na anawatakia afya nzuri. Anatutaka tuhakikishe kuwa wanaishi maisha mazuri katika siku za baadaye,'' alisema Zuma.
Wakfu wa Mandela , ungependa kujenga hospitali yenye uwezo wa kuwashughulikia watoto 238 wa kulazwa pamoja na kuwatibu watoto kote nchini Afrika Kusini. Chanzo: bbcswahili

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...